JW subtitle extractor

Ripoti ya 1 ya Baraza Linaloongoza ya 2024

Video Other languages Share text Share link Show times

Karibuni.
Tutazungumzia
umuhimu wa kujiwekea miradi ya kibinafsi
katika huduma.
Lakini kwanza
acheni tupate habari za karibuni.
Januari 01 mwaka huu,
tetemeko la ardhi lenye kipimo cha 7.6
liliikumba Japani.
Kwa kupendeza
hakuna yeyote kati ya ndugu zetu aliyekufa.
Hata hivyo,
zaidi ya nyumba 100 za ndugu zetu
zilipata uharibifu
na mbili ziliharibiwa kabisa.
Pia Majumba tisa ya Ufalme
yalipata uharibifu.
Upesi ofisi ya tawi ilifanya mipango
ya kupata mahali pa kulala
na mahitaji mengine
kwa ajili ya ndugu na dada.
Muda mfupi baada ya hapo
ofisi ya tawi iliweka rasmi
Halmashauri ya Kutoa Msaada
na ikawatuma wawakilishi wa ofisi ya tawi
kwenda kuwatembelea akina ndugu
katika maeneo yaliyoathiriwa.
Baada ya siku chache tu,
msaada zaidi ulipelekwa
kwenye makutaniko yaliyokuwa na uhitaji.
Katika kutaniko la Wajima
wazee hawakuweza kumpata dada mmoja.
Ili kumtafuta
mzee mmoja alitembea kwa saa nane,
akikwepa maporomoko ya ardhi
na nyufa zilizokuwa ardhini,
hadi alipohakikisha dada yetu yuko salama.
Makutaniko katika eneo hilo
kutia ndani yaliyoathiriwa kabisa,
yameendelea kufanya
mikutano tangu juma lile
tetemeko la ardhi lilitokea
Wengi kati ya wahubiri
wamehudhuria uso kwa uso
ili waweze kutiana moyo.
Tunaendelea kusali
kwa ajili ya ndugu na dada zetu nchini Japani
na katika nchi nyingine
zilizoathiriwa na misiba ya asili hivi karibuni.
Januari 1,
kituo cha wageni cha Patterson
kilifunguliwa rasmi kwa ajili ya matembezi!
Ujenzi ulianza mapema mwaka wa 2021
na ulikamilishwa Septemba 2023.
Utajionea mambo gani
utakapotembelea eneo hilo?
Acheni tuone!
Kituo cha wageni cha Patterson
kina maonyesho matatu
kutia ndani sehemu ya maonyesho ya sarafu.
Maonyesho ya kwanza utakayoona
yana kichwa
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema.”
Yanaonyesha mambo yaliyoonwa
ya wanaume, wanawake,
na hata watoto wa shule
walioshikamana na imani yao
inayotegemea Biblia
licha ya upinzani wa kisheria.
Maonyesho haya yanaonyesha
jinsi tengenezo la Yehova
lilivyowategemeza
walipokabili majaribu magumu.
Maonyesho ya sarafu za Biblia
yanaonyesha mkusanyo wa pekee
wa sarafu za awali zilizotumiwa
katika karne ya kwanza
na pia kuna maelezo kuhusu
Maandiko yanayoonyesha sarafu hizo
na umuhimu wake.
Maonyesho mengine yenye kichwa
“Wana Wako Wote Watafundishwa na Yehova,”
yanaonyesha baadhi ya programu za mazoezi
na shule ambazo zimetumiwa na tengenezo la Yehova
kutuzoeza kuwa wahudumu na walimu.
Tuna uhakika yatakuchochea kuona njia za ziada
unazoweza kutumia ili kufaidika
kutokana na elimu ambayo Yehova anatupatia.
Maonyesho ya pekee katika eneo hili
ni kijiji cha Biblia katika karne ya kwanza.
“Wanakijiji” watakukaribisha kwa uchangamfu
na wana hamu ya kukuonyesha
jinsi wanavyoishi
na kufanya kazi pamoja kama jamii.
Utajionea jinsi maisha yalivyokuwa
Yesu alipokuwa duniani.
Utapata nafasi ya kutembelea mashamba,
soko,
eneo la makazi,
sinagogi
na hata ufuo wa bahari.
Bila shaka maonyesho hayo mapya
yataongeza uthamini wako kwa Biblia
na kwa kile ambacho Yehova anatimiza
kupitia tengenezo lake leo.
Tunawakaribisha wote wanaoweza
waje wajionee
kituo kipya cha wageni cha Patterson.
Kituo cha wageni cha Patterson
ni chenye kustaajabisha!
Tunawashukuru wote waliofanya kazi kwenye mradi huo.
Sasa tunawakaribisha nyote mje mtembee
unaweza kuomba kutembelea
kupitia jw.org.
Sasa acheni tuzungumzie kuhusu
mabadiliko ya karibuni
kuhusu jinsi tunavyoripoti huduma yetu.
Tuone jinsi yanavyoathiri miradi yetu.
Kwenye mkutano wa kila mwaka
tulitangaziwa kuanzia Novemba
hatutakuwa tena tukitoa ripoti ya utumishi
yenye mambo mengi.
Mhh! Hilo lilikuwa badiliko kubwa sivyo?
Lakini ingawa tumebadili jinsi tunavyoripoti
hatujabadili maoni yetu
kuhusu huduma yenyewe, sivyo?
Tunawakazia fikira watu.
Tunawapenda watu,
na tunataka kuwasaidia.
Tuko tayari kuwaeleza habari njema
popote tunapowakuta.
Jumamosi asubuhi
huenda tukaenda nyumba kwa nyumba
kwa saa kadhaa.
Kisha tunaenda kufanya manunuzi.
Je wakati huu tunaacha kufanya kazi
eti kwa sababu hatuko katika mahubiri rasmi?
Sisi hatuna maoni hayo,
tunapoendelea na manunuzi
bado tunaangalia
tunaweza kushiriki na nani habari njema.
Tunaweza kuzungumza
na mtu aliyesimama kando yetu
tunapokuwa tukisubiri kulipa
au na muuza duka tunapomlipa.
Hatutazungumza sana.
Baada ya kusalimiana kwa uchangamfu kidogo
tunaweza tu kumtolea kadi ya mawasiliano
na kusema:
“Ninafikiri utafurahia tovuti hii,
ina makala zenye kupendeza
katika lugha zaidi ya 1000.”
Au baada ya kusema maneno fulani yanayofaa
unaweza kumtolea trakti
ikiwa muda unaruhusu
na mtu huyo anapendezwa,
tunaweza kusema mengi zaidi.
Kanuni hiyo inaweza kutumika
tunapokuwa tukimsubiri daktari,
kwenye uwanja wa ndege,
dukani, au katika usafiri wa umma.
Hili ni dokezo:
Kwa nini usibebe kadi kadhaa
au machapisho mengine
popote unapoenda?
Tumesema tuko tayari
kushiriki habari njema
popote tunapowapata watu.
Lakini vipi kuhusu watu ambao hatuwakuti,
wale ambao mara nyingi
hawapatikani nyumbani?
Je, umewahi kupita kwenye eneo
Jumamosi au Jumapili alasiri
na ukaona ya kwamba kuna gari katika kila nyumba?
Hata hivyo ulipopita hapo asubuhi
hakukuwa na mtu nyumbani.
Sijui ni watu wangapi kati ya hao
ambao wangekubali funzo la Biblia
ikiwa tungewajulisha.
Upendo wetu kuelekea watu
utatuchochea kuwaendea
wanapokuwa nyumbani.
Nakumbuka jioni moja
tulikuwa tukienda kula mlo kwenye mkahawa
pamoja na wenzi fulani wa ndoa.
Ndugu ndiye aliyekuwa akiendesha.
Tulipopita kwenye nyumba fulani,
alisimama akaegesha gari na kusema,
“Samahani sana,
lakini naona gari kwenye nyumba ile,
kwa majuma kadhaa
tumejaribu kumtafuta mtu huyu.
Hatutakaa sana.”
Yeye na mke wake wakashuka
wakaenda kwenye nyumba hiyo.
Hongera sana.
Sehemu nyingine ambapo jitihada inahitajika
ni kufuatilia upendezi.
Mhubiri anayehubiri kwenye kigari,
anazungumza na mtu anayependezwa
anayeomba kutembelewa.
Mtu huyo anaishi kwenye eneo lenu
na unakubali kwamba utamtembelea.
Jumamosi asubuhi unabisha mlango wake
nini kinatokea?
Najua unajua
mtu huyo hayupo nyumbani.
Je, tutainua mikono yetu na kusema,
“si nimejaribu?
La hasha!
Mtu huyo alionyesha anapendezwa
na tutaendelea kurudi hapo wakati mbalimbali
hadi tutakapompata.
Ingawa hatuandiki
ripoti ya utumishi yenye mambo mengi,
bado tunaweza kujiwekea miradi yetu wenyewe.
Baadhi ya miradi hiyo inaweza kuwa
kusikiliza kwa makini zaidi
mwenye nyumba anapozungumza
au kuonyesha upendezi wa kibinafsi zaidi.
Lengo lingine linaweza kuwa
kuhubiri eneo letu kikamili.
Kujiwekea miradi ya kibinafsi
kunapatana na ushauri ambao Paulo alitoa
kwenye Wagalatia 6:4.
Unaweza kufuatana kwenye skrini yako
tunaposoma.
Paulo aliandika:
“Lakini kila mmoja na achunguze matendo yake mwenyewe
kisha atakuwa na sababu ya kushangilia
kuhusiana na yeye mwenyewe.
Na si kwa kujilinganisha na mtu mwingine.”
Miradi ya kibinafsi
inaweza kutupatia kichocheo tunachohitaji
ili kushiriki katika kazi hii muhimu.
Acheni tusikie baadhi ya ndugu na dada
wanahisije kuhusu mabadiliko ya karibuni
na mambo wanayofanya
ili kupanua utendaji wao.
Mabadiliko haya yamenisaidia
kufurahia huduma hata zaidi
na kufanya wanafunzi.
Kwa kweli nimeyafurahia.
Ninahisi mabadiliko haya mapya
kuhusu kuripoti saa yamenisaidia
nisiwe na wasiwasi kuhusu wakati ninapoanza
na ninapomaliza utumishi
nipo utumishi wakati wote.
Kwanza kabisa nimebadili ratiba yangu
ninaenda kuhubiri
wakati watu wanapopatikana.
Hapo awali nilipoenda katika huduma
nilitarajia watu wanisikilize mimi,
lakini sasa ninataka kuwasikiliza wao.
Sasa sijali ninawaachia watu machapisho mangapi?
Nimeona umuhimu wa kuzungumza na watu
kila nafasi inapopatikana.
Lengo likiwa kufanya wanafunzi.
Hapo awali nilikuwa ninafurahi sana
ninapomwachia mtu kitu kutoka kwenye mfuko wangu.
Lakini sasa nina furaha
ninapomwachia mtu kitu kutoka moyoni mwangu.
Mabadiliko haya
yamenisaidia kukazia fikira jambo muhimu zaidi,
yaani, kufanya wanafunzi.
Ninapenda njia hii mpya ya kuhubiri
kwa sababu sasa sihitaji
kukariri utoaji fulani hususa.
Sasa ninazungumza na watu kwa njia ya kawaida
na wanafurahia mazungumzo ya Biblia.
Utendaji wetu hautegemei
idadi ya tunachoripoti
badala yake unachochewa
na upendo tulionao kwa watu.
Tumetambua kwamba
ndugu na dada katika mzunguko wetu
wamesikia sana
mbinu hii mpya katika huduma.
Hapo awali kulikuwa na mpangilio
wazo fulani kisha andiko
lakini sasa ni mazungumzo tu.
Awali nilikuwa na wasiwasi ningesema nini
na ningeelekezaje mazungumzo yenyewe
kwenye Biblia.
Lakini sasa ninatambua
jambo muhimu hata kuliko ninachosema.
Ni kwamba mwenye nyumba
ahisi kwamba ninamjali kikweli.
Kwa hiyo kama tu Yesu
alivyomwendea yule mwanamke kwenye kisima,
mimi hupenda kuwaendea watu
na kuzungumza nao kuhusu mbwa wao
na kuuliza ikiwa ninaweza
kugusa mbwa wao.
Hilo huanzisha mazungumzo
yenye kustarehesha
kisha ninawaachia kadi au kuwahubiria
na mara nyingi ninapoondoka
ninaona tayari wameanza kuingia kwenye tovuti yetu
kwa kutumia kadi niliyowaachia.
Nimetambua kwamba kutanikoni kwetu.
Tumeanza kuwa na utambuzi hata zaidi.
Kisha tunatumia mambo tulipotambua
kuanzisha mazungumzo.
Kwa kawaida mimi ni mkimya
na mwenye haya, kwa hiyo
mbinu hii mpya inayosema usizungumze sana,
nilipoisikia nilisema safi sana.
Hilo ni jambo mimi ninaweza kufanya vizuri.
Nimeipenda.
Ninajihisi nikiwa nimestarehe zaidi sasa
kwa sababu lengo letu ni kuanzisha mazungumzo
kwa hiyo ninakazia fikira kutayarisha mawazo
yanayotegemea mahitaji ya watu
katika eneo.
Nimesisimka sana
kuhusiana na mabadiliko katika kazi ya kuhubiri
kwa sababu
yanatutia moyo
tushiriki katika aina mbalimbali za utumishi,
kama vile mahubiri yasiyo rasmi.
Na hilo si rahisi kwangu.
Hata hivyo, ninahisi inachochewa na Yehova
na tengenezo lake nijaribu mbinu hizo mpya,
ninapojaribu kufikia mradi
wa kuwa painia wa kawaida.
Yametuchochea sana
kujaribu kupanua huduma yetu,
tungependa sasa kutoka
kwenda kuwasaidia watu
wamfahamu Yehova.
Niliona wengi kutanikoni
wakipata shangwe ya kufanya upainia.
Na mimi pia nilitaka kuhisi hivyo.
Kwa hiyo nina furaha sana
kuanza upainia wa kawaida
kuanzia mwezi huu.
Tukiwa wenzi wa ndoa
tungependa kuhudhuria
shule wenye za Injili wa ufalme
ili tujifunze njia mpya za kuwaonyesha watu kwamba tunawapenda.
Ninatamani sana kuanza kufanya upainia
kisha nihudhurie shule ya Waeneza Injili wa Ufalme
na niende popote ninapotumwa
kwa sababu naona nitafurahia sana.
Inapendeza sana
ninahitaji tu sasa kukazia fikira watu
na hilo ndilo lengo letu kuu.
Ndugu na dada tunawapenda sana
kwa sababu mnafanya yote mnayoweza
kulingana na hali zenu!
Yesu alisema hivi
kama inavyopatikana kwenye Yohana 14:15:
“Ikiwa mnanipenda
mtazishika amri zangu.”
Tunampenda Bwana wetu
na tunawapenda watu.
Kwa hiyo kwa shangwe tunatia amri
ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake:
“mnapoenda hubirini.”
Kutoka kwenye Makao Makuu
ya Ulimwenguni Pote ya Mashahidi wa Yehova
hii ni JW Broadcasting.