JW subtitle extractor

Ripoti ya 3 ya Baraza Linaloongoza ya 2024

Video Other languages Share text Share link Show times

Karibuni kwenye ripoti yetu,
katika ripoti hii
tutachunguza kanuni za Biblia
zinazotuongoza tunapofanya maamuzi
kuhusu mavazi na mapambo.
Lakini kwanza,
tupate habari kuhusu jitihada za kutoa msaada
baada ya misiba ya karibuni.
Kusini-mashariki mwa Afrika
baadhi ya nchi kama vile Malawi,
Msumbiji,
na Zimbabwe,
zimekumbwa na ukame mbaya sana.
Ofisi ya tawi ya Zimbabwe
inakadiria kwamba wahubiri 13,500,
wanahitaji msaada wa mahitaji ya msingi.
Mbali na hilo
baadhi ya ndugu zetu nchini Malawi
walikabili mafuriko
ambayo yaliharibu nyumba zao
pamoja na chakula
walichokuwa wamehifadhi.
Mwishoni mwa mwezi wa Aprili,
Ndugu Gage Fleegle alitembelea Malawi
na Zimbabwe,
ili kuwatia moyo ndugu na dada hao.
Ili kuandaa msaada
baada ya misiba hiyo ya karibuni,
Baraza Linaloongoza lilituma pesa
ili ndugu zetu wapate chakula,
kama vile mahindi,
maharage,
samaki waliokaushwa
na mafuta ya kupikia.
Huenda unakumbuka kwamba mwezi Januari,
tetemeko lenye kipimo cha 7.6,
lilitokea nchini Japani.
Nyumba 600, za ndugu zetu
zilipata uharibifu fulani,
na nyumba nane zikaharibiwa kabisa.
Majumba 13 ya Ufalme, yaliharibiwa pia.
Tangu wakati huo
serikali imejitahidi kurekebisha miundombinu.
Ofisi ya tawi inajitahidi sana kuwasaidia ndugu zetu
kurekebisha na kujenga upya nyumba zao.
Aprili 3,
Taiwan ilikumbwa na tetemeko kubwa zaidi
la ardhi kwa miaka 25 iliyopita.
Lilisababisha ving’ola vya tsunami
kupigwa nchini Japani na Filipino.
Tunafurahi kwamba hakuna yeyote
kati ya ndugu zetu
aliyekufa au kujeruhiwa.
Na pia, hakuna nyumba iliyopata uharibufu mkubwa.
Hata hivyo, Majumba 20 ya Ufalme,
na ofisi ya tafsiri ya lugha ya Amis,
zilipata uharibifu mdogo.
Ukarabati unaendelea.
Licha ya hali ngumu ambazo zimetokezwa na misiba hiyo,
ndugu na dada zetu wamejitolea upesi
kusaidia katika jitihada za kutoa msaada.
Na tunawashukuru sana ninyi nyote kwa sala zenu
pamoja na michango yenu ya ukarimu
inayofanya kazi hiyo ya kutoa msaada iwezekane.
Hivi karibuni
video yenye kusisimua,
itatolewa kwenye tovuti yetu.
Ni video kuhusu hati ya Biblia
ambayo watu walifikiri ilikuwa imeharibiwa.
Hati hiyo ni tafsiri ya Kiingereza
ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo,
ambamo jina Yehova
linapatikana zaidi ya mara 200.
Acheni tutazame kionjo cha video yenye Kichwa
Tafsiri ya Biblia Iliyopotea Yapatikana.
Kazi ya kutafsiri ilipingwa sana katika karne ya 19,
na viongozi wa kisiasa na wa kidini.
katika kipindi hicho,
ulipaswa kuwa mwangalifu sana
ulipowaeleza wengine maoni yako.
Wenye mamlaka hawakufurahishwa na jitihada zake,
za kujaribu kujifunza kuhusu kweli.
Ikiwa unaamini kwamba
Biblia ni mkusanyo wa maandishi matakatifu,
ni wazi hutafurahi
ikiwa utaona kuna makosa katika tafsiri zilizopo.
kazi yetu haikuwa kukisia,
kazi yetu ilikuwa kuuliza maswali
yatakayotusaidia kupata habari kamili.
Tafsiri hiyo ilifanywa na wasomi halisi
ambao walijua vizuri Kiebrania na Kigiriki.
Tuliamini kwamba tafsiri hii
ilikuwa imepotea kabisa.
kwa kweli inavutia sana.
na watu wengi wanahitaji kujua habari hizi.
Tuna uhakika kwamba
mtafurahi kutazama video nzima,
kuhusu ugunduzi huu wenye kusisimua.
Hivi karibuni,
tumefurahia ripoti kuhusu mavazi na mapambo.
Zimehusu akina ndugu kufuga ndevu,
akina dada kuvaa suruali
na pia kuhusu akina ndugu kuvaa koti na tai.
Tunashukuru,
kwamba Yehova anatuamini kuhusu mambo hayo.
Hata hivyo, maswali yamezuka.
Kwanza kabisa,
je, mabadiliko hayo kuhusu mavazi na mapambo
yanamaanisha kwamba
tunashusha viwango vyetu?
Bila shaka la,
Yehova anastahili tumwabudu kwa staha
na heshima kubwa.
Mabadiliko hayo hayapaswi kupunguza
kina cha uthamini wetu wa kumtumikia Yehova.
Mabadiliko hayo
yanaonyesha tu kwamba tunatambua kuwa
mitindo hubadilika.
Na kwamba maoni kuhusu mavazi yanayokubalika
na yanayoheshimika
kwa ajili ya matukio mbalimbali hubadilika.
Kwa mfano,
je, unakumbuka picha hizi
kwenye ripoti ya nane
ya Baraza Linaloongoza ya 2023.
Hatuwezi kutarajia kwamba
watu wavalie
kama ilivyokuwa katika nyakati za Biblia,
wala tusingetarajia
watu wavalie kama ilivyokuwa
miaka miamoja iliyopita,
nyakati hubadilika.
Maoni kuhusu mavazi na mapambo yanayoheshimika,
hubadilika kadiri wakati unavyopita.
Mabadiliko yaliyotangazwa katika ripoti za karibuni,
yanazingatia hilo.
Swali lingine linalozuka kuhusu mwongozo huu mpya ni:
Tutafanya nini ili kuhakikisha
bado tunaonyesha heshima kwa Yehova na ibada yake,
kuhusiana na kufuga ndevu,
kuvaa suruali au kutovalia tai?
Kama tu ilivyo na mavazi na mapambo mengine,
kuna mitindo mingi mbalimbali.
Tuchunguze kanuni tatu
zilizo katika Neno la Mungu.
Unafahamu kanuni hizi
na unampenda Yehova.
Tunajua kwamba kanuni hizi ni muhimu kwako.
Basi acheni tuone jinsi mistari hiyo
inavyoweza kutuongoza,
tunapofanya maamuzi
kuhusu mavazi na mapambo.
Kwanza, tuchunguze 1 Timotheo 2:9, 10.
Inasema:
“Vivyo hivyo, wanawake wanapaswa kujipamba kwa mavazi yanayofaa,
kwa kiasi na utimamu wa akili,
si kwa mitindo ya kusuka nywele,
dhahabu, lulu, au mavazi ya bei ghali sana,
bali kwa njia inayowafaa wanawake wanaokiri
kwamba wanamtumikia Mungu,
yaani, kupitia matendo mema.”
Kulingana na mistari tuliyosoma,
ni nini kinachoamua
tunavyovalia na kujipamba?
Ulimwenguni watu huchagua mavazi
kwa kutegemea tu mapendezi yao.
Lakini tukiwa Wakristo
kuna mambo mengine ya kufikiria.
Sisi tunakiri kwamba tunamtumikia Mungu.
Sisi tukiwa Wakristo tunataka mavazi
na mapambo yetu
yamletee Yehova utukufu.
Kwa hiyo, tunachagua mitindo inayofaa,
yenye kiasi,
na inayoonyesha tuna utimamu wa akili.
Hasa tunapoenda kwenye Jumba la Ufalme
au katika huduma.
Maneno haya yanamaanisha nini?
Tuangalie baadhi ya habari za utafiti
kwenye Biblia ya Kiingereza.
Biblia hiyo inafafanua
mavazi yanayofaa kwa njia hii:
Au yenye kuheshimika.
Katika muktadha huu
neno la Kigiriki linatokeza wazo la mavazi
yenye staha na yanayofaa.
Mavazi hayo
yangemfaa mtu aliyekiri
kuwa mhudumu wa Mungu.
Ikiwa mavazi yetu yanaonyesha sehemu za mwili
au yanabana,
je kweli yanafaa,
ni yenye staha au heshima?
Je, mavazi haya yangefaa kuvaliwa
tunapomwabudu Yehova?
Nina hakika ungekubali kuwa
yasingefaa.
Hilo linamaanisha kwamba
tunapaswa kuchunguza kwa uangalifu tutavaa nini,
hasa tunapomwabudu Yehova.
Ikiwa tuna mavazi ya starehe,
je, yangefaa kuvalia
tunapomwabudu Yehova mikutanoni,
au tunapokuwa katika huduma?
La hasha,
mavazi hayo yasingefaa.
Bila shaka
najua unakubali kwamba
maoni yetu kuhusu kinachofaa,
yanategemea tukio,
kwa mfano, kuna mavazi ambayo yanafaa
tunapoenda kwenye ufuo wa bahari
au tafrija.
Na kuna mavazi yanayofaa tunapohudhuria harusi,
na pia kuna mavazi yanayofaa
tunaposhiriki katika ibada kwenye Jumba la Ufalme,
au katika huduma.
Jambo kuu ni nini?
Licha ya kwamba mitindo na nyakati hubadilika,
ni muhimu kwetu kutambua kwamba
kuna viwango fulani vya mavazi
ambavyo vinapaswa kuamuliwa,
kwa kutegemea tukio.
Hilo ndilo wazo
sote tungependa kuzingatia.
Turudi kwenye habari za utafiti.
Inamaanisha nini kuvalia kwa kiasi?
Habari za utafiti zinasema,
katika muktadha huu,
kiasi kinatia ndani kuzingatia dhamiri ya mtu binafsi,
na pia hisia na maoni ya wengine.
Mkristo mwenye kiasi
ataepuka kuvalia kwa njia
inayoamsha tamaa mbaya,
inayowafanya wengine wamwelekezee fikira
kwa njia isiyofaa,
au ambayo huenda ikashtua
na kuwakwaza wengine.
Kwa hiyo tunapofanya maamuzi
tunafikiria jinsi engine watakavyoathiriwa,
yaani ndugu na dada zetu,
na pia wengine katika jamii.
Kwa kweli hatutakuwa tukionyesha kiasi,
ikiwa mavazi yetu
yataonekana kuwa ya ajabu,
au yenye kupita kiasi.
Hatutaki watu watuelekezee fikira kwa njia isiyofaa
au kuwakengeusha wengine
kupitia mavazi na mapambo yetu.
Tungependa watu wamkazie fikira Yehova
na ujumbe wa Ufalme tunaotangaza.
Turudi tena kwenye habari za utafiti,
maneno utimamu wa akili
yanamaanisha nini?
Habari za utafiti zinasema yanamaanisha
kufanya maamuzi mazuri.
Busara,
sifa hii inatufanya tusionekane tumevalia kizembe,
au shagalabagala.
Tutoe mfano,
wazia umealikwa kwenye tafrija rasmi
na maofisa wa serikali,
utavaliaje,
je, utavalia mavazi ya kulala,
au ya kwenda kwenye ufuo wa bahari?
Bila shaka la!
Sote tungependa kuvalia
kwa njia inayoonyesha heshima kwa tukio hilo,
na kwa wale watakaokuwepo.
Namna gani, basi tunapomwabudu Yehova
kwenye mikutano,
au tunaposhiriki katika huduma?
Acheni tufikirie kanuni ya pili ya Biblia,
inapatikana kwenye 2 Wakorintho 6:3, 4.
“Hatutoi sababu yoyote ya kukwaza,
ili kosa lolote lisipatikane katika huduma yetu;
bali katika kila njia
tunajipendekeza
kuwa wahudumu wa Mungu.”
Ni muhimu kwetu kuchunguza
jinsi mavazi na mapambo yetu
yatakavyoathiri maoni ya wengine kuhusu huduma yetu
na Mungu tunayemwabudu.
Kwa kweli
watu hujenga picha kuhusu kweli
iwe nzuri au mbaya,
kwa kutegemea mwonekano wetu.
Tunaweza kujiuliza hivi,
katika eneo letu,
je, majirani wataniona kuwa mmoja wa wahudumu wa Mungu
ikiwa nitavalia au kujipamba kwa njia fulani?
Je, wataona tofauti kati ya watu wa Yehova
na wale ambao hawamtumikii Mungu?
Tuchunguze kanuni ya tatu.
Inapatikana kwenye 1 Yohana 2:15-17.
“Msiupende ulimwengu
au vitu vilivyo katika ulimwengu.
Yeyote akiupenda ulimwengu,
kumpenda Baba hakumo ndani yake,
kwa sababu kila kitu katika ulimwengu,
tamaa ya mwili na tamaa ya macho,
na mtu kujionyesha mali zake maishani,
hakitokani na Baba
bali hutokana na ulimwengu.
Zaidi ya hayo,
ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake,
lakini yule anayefanya mapenzi ya Mungu,
anadumu milele.”
Mistari hii inatukumbusha kwamba
mavazi na mapambo yetu
hayapaswi kuonyesha tunaupenda ulimwengu.
Mitindo hubadilika kadiri miaka inavyopita,
na kuna mitindo mingi ambayo haiwakwazi
na kuwashtua watu wengi.
Machapisho yetu yamesema kwamba
hatupaswi kuwa wa kwanza kukimbilia mtindo fulani,
au wa mwisho kuachana na wa zamani.
Lakini sote tunatambua kuna mitindo mingi
ambayo hatungependa kuikumbatia,
hasa ile isiyo ya kiasi
inayochochea hisia za ngono,
isiyo na heshima na ya kizembe.
Na tunahitaji pia kuzingatia
si tu aina ya vazi lenyewe,
lakini pia kuhakikisha kuwa vazi hilo halitubani,
tusingependa kumwonyesha Yehova kwamba
hatumuheshimu
na viwango vyake vya uadilifu.
Tumechunguza viwango vitatu vya Biblia
vinavyoweza kutusaidia
kufanya maamuzi yanayofaa
kuhusu mavazi.
Kanuni hizo pia zinahusika
kuhusiana na mitindo ya nywele,
ndevu, na mambo mengine yote
yanayohusiana na mavazi na mapambo.
Yanatusaidia kuamua urefu
na mtindo wa nywele zetu,
akina ndugu hutumia kanuni hizo
kuamua jinsi ya kutunza ndevu zao
ili zionekane nadhifu na zenye kupendeza.
Je, hatushukuru
kwamba Yehova ametupatia kanuni hizo
katika Neno lake?
Inafaa kwamba tuzichunguze
kwa kuzingatia mabadiliko yaliyofanywa karibuni.
Tufanye nini kingine
kwa kuzingatia vikumbusho hivi?
Sali kuvihusu.
Mwombe Yehova akusaidie kuona
ikiwa unahitaji kufanya mabadiliko.
Mwombe rafiki mkomavu kiroho
akupe maoni yake,
nanyi vichwa vya familia,
mwonyeshe mke wako na watoto wako
kwamba unawapenda
kwa kuwasaidia kutumia kanuni hizi.
Ndugu na dada
tunawapenda na kuwaheshimu sana.
Kutoka kwenye makao makuu
ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova
hii ni JW Broadcasting.