JW subtitle extractor

Ripoti ya 5 ya Baraza Linaloongoza ya 2024

Video Other languages Share text Share link Show times

Karibuni!
Tangu ripoti iliyopita,
tumefanya makusanyiko matano zaidi ya pekee.
Makusanyiko hayo
yalifanyika katika maeneo yafuatayo:
Prague, kwenye Jamhuri ya Cheki;
Helsinki, Finland;
Budapest, Hungary;
Reykjavik, Iceland;
na Zurich, Switzerland.
Wajumbe kutoka nchi zaidi ya 30,
walihudhuria,
ni shangwe kubwa kuona upendo na umoja
miongoni mwa watu wa Mungu.
Jumla ya ndugu na dada zetu 578
walibatizwa katika makusanyiko hayo.
Katika kusanyiko la pekee lililofanyika Iceland,
Biblia Takatifu Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
ilitolewa katika Kiiceland.
Chakuka kingi cha kiroho katika makusanyiko ya mwaka huu
kinaburudisha na kutuimarisha,
ili tuendelee kutangaza habari njema.
Tunapofikiria kuhusu huduma,
tunafikiria kuhusu mwaka wa utumishi
ulio karibu sana kuanza.
Huenda unakumbuka kwamba kuanzia Septemba 1,
tutakuwa na kampeni kubwa ya ulimwenguni pote
ya kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Ni vizuri kwetu kuanza matayarisho sasa.
Wakati wa kampeni,
tutaanzisha mafunzo ya Biblia kwa watu wengi iwezekanavyo
kwa kutumia Broshua
Furahia Maisha Milele!
Katika mwezi huo,
mapainia wasaidizi watakuwa na fursa
ya kuchagua,
ikiwa watatimiza takwa la saa 15
au saa 30.
Kwa nini usitumie dakika chache juma hili
kupanga ratiba zako za mwezi wa Septemba?
Kupitia Sala
tafakari ikiwa unaweza kupanua utumishi wako mwezi huo.
Pia, tuna jambo la pekee
ambalo tungependa kushiriki nanyi.
Jumapili Julai 28,
tulifikia kilele kipya
inapohusu kazi ya kutafsiri Biblia.
Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
sasa inapatikana ikiwa nzima au kwa sehemu
katika lugha 300.
Inastaajabisha sana.
Kuna mambo mengi yenye kustaajabisha
yanayotokea katika tengenezo la Yehova.
Lakini sasa katika sehemu inayobaki
ya ripoti yetu,
ningependa kuzungumzia pamoja nanyi
mada hii muhimu.
Kuendelea kukazia fikira Ufalme wa Mungu,
kuwa ndiyo suluhisho pekee
la matatizo ya wanadamu.
Kweli hiyo muhimu
inatusaidia kutounga mkono upande wowote,
inapohusu siasa za ulimwengu huu.
Kusanyiko la eneo la mwaka huu
linatusaidia kukumbuka jambo hilo.
Wakati wa kusanyiko
tulifurahia drama ya kwanza
ya Habari Njema Kulingana na Yesu.
Ilitukumbusha jinsi kutokea kwa Masihi
kulivyokuwa habari njema.
Kwa kuwa Yesu alizaliwa duniani,
ahadi zote za Mungu,
zitatimizwa kupitia kwake.
Ahadi hizo zinatia ndani nini?
Kwamba suluhisho pekee la matatizo ya wanadamu,
Ufalme wa Mungu,
utaongozwa na Yesu
akiwa Mfalme.
Yesu Kristo ni Mfalme wa aina gani?
Isaya 9:6, 7
ina unabii unaomfafanua Yesu kwa njia hii:
Kwa maana mtoto amezaliwa kwetu,
Tumepewa mwana
na utawala utakaa juu ya bega lake.
Jina lake litakuwa Mshauri wa Ajabu,
Mungu Mwenye Nguvu,
Baba wa Milele,
Mkuu wa Amani.
Kwa wingi wa utawala wake na amani,
hakutakuwa na mwisho,
kwenye kiti cha ufalme cha Daudi
na juu ya ufalme wake
ili kuuimarisha kabisa na kuutegemeza
kupitia haki na uadilifu,
kuanzia sasa mpaka milele.
Bidii ya Yehova wa majeshi
itafanya hayo.
Mistari hii
inatuonyesha kwamba utawala wa Yesu
utaleta amani,
haki,
na uadilifu.
Na utawala wake
utadumu milele.
Jambo lenye kupendeza sana.
Tunashukuru kujua kwamba
tayari Ufalme wa Mungu umenza kutawala mbinguni,
tayari umekuwa suluhisho halisi na la kudumu,
kwa matatizo yote
ya jamii ya wanadamu.
Lakini tunahitaji kuwa waangalifu
ili tusisahau jambo hilo.
Kwa nini?
Kwa sababu wakati tunaoishi,
inafanya iwe vigumu sana kwetu
kukazia Ufalme wa Mungu
kuwa suluhisho halisi
kwa matatizo yetu yote.
Kuna mambo mengi yanayoleta migawanyiko ulimwenguni leo.
Vurugu na vita
vinaendelea katika maeneo mbalimbali,
ulimwengu unajitahidi sana
kuwashinikiza watu
waunge mkono upande fulani wa kisiasa
na hata uchaguzi.
Kwa ujumla
inakadiriwa kwamba
mabilioni ya watu,
karibu nusu ya watu wote duniani,
wanaishi katika nchi
ambazo kumekuwa
ama kutakuwa na uchaguzi mwaka huu.
Tumeona pia,
ongezeko la sherehe za kizalendo na kitaifa,
kutia ndani kwenye maeneo ya shule.
Hata michezo
imesababisha migawanyiko mbalimbali ya kitaifa.
Tunasikia mambo hayo
kupitia vyombo vya habari kila siku.
Ulimwengu leo
unakabili matizo mabaya hata zaidi.
Na wanadamu wasio wakamilifu
wamejaribu kutatua matizo hayo
kwa njia mbalimbali.
Lakini tukiwa Mashahidi wa Yehova,
tunapaswa kuwa na mtazamo gani
kuhusu maoni hayo?
Kwa kweli hatujihusishi kwa vyovyote na siasa.
Tunakumbuka maneno ya Yesu
kwenye Yohana 18:36 aliposema:
“Ufalme wangu
si sehemu ya ulimwengu huu.”
Badala yake
tunashikamana na Ufalme wa Mungu
kwa moyo wote
na hatujihusishi
na siasa za ulimwengu huu.
Ni kweli kwamba
Waroma 13:1, 2 inaonyesha
kwamba mamlaka zilizopo
zimewekwa na Mungu
katika vyeo vyao vya kadiri.
Kwa hiyo tunashukuru kwa kazi ambazo serikali zinafanya
na tunaheshimu mamlaka yao.
Hilo linapatana na maneno ya Yesu
yaliyorekodiwa katika Mathayo 22:21,
aliposema: “Basi mlipeni Kaisari
vitu vya Kaisari,
na Mungu vitu vya Mungu.”
Tunapowaheshimu wale walio na nafasi
ya kuwa na mamlaka katika serikali,
hatujihusishi katika masuala au mijadala ya kisiasa.
hata iwe maoni ya upande fulani
yanaonekana kuwa sawa.
Tunaendelea kuutafuta kwanza Ufalme wa Mungu
na uadilifu wake.
Tunajua kwamba hilo ndilo suluhisho la kweli.
Hivyo hatuungi mkono ulimwengu huu
kwa njia yoyote hata kupitia mawazo yetu.
Hatuungi mkono mgombea,
chama cha kisiasa,
au mtu fulani.
Hata ikiwa wao wanaunga mkono
au kufanya mambo yatakayotunufaisha.
Tunakazia fikira suluhisho la kweli.
Ufalme wa Mungu
chini ya Uongozi wa Yesu Kristo.
Ni nini kitatusaidia kuepuka kuunga mkono
upande wowote?
Tutazungumzia njia mbili kwa ufupi.
Kwanza tunapaswa kufikiria zaidi kuhusu suluhisho,
kuliko tatizo
na pili kutumia muda mwingi zaidi
kuzungumza kuhusu suluhisho
kuliko tatizo.
Tuzungumzie njia ya kwanza.
Ni nini kitatusaidia kutumia muda mwingi
kufikiria kuhusu suluhisho
badala ya tatizo?
Kusoma Biblia kila siku
na kutafakari.
Kufanya hivyo kutatusaidia kudumisha
na kuimarisha tumaini letu.
Na tunalinda mioyo yetu
kwa kupunguza wakati tunaotumia kusoma
au kusikiliza habari
au kutumia mitandao ya kijamii,
mambo yanayoweza kutuhangaisha, kutuvunja moyo
au hata kutuchosha.
Njia ya pili ya kutusaidia tusiunge mkono upande wowote
ni kutumia muda mwingi
kuzungumza kuhusu suluhisho
kuliko tatizo.
Si ni kweli kwamba
usemi wetu unafunua kile kilicho moyoni mwetu,
ikiwa tunaanza kuwaeleza wengine
jinsi tunavyohisi kuhusu uchaguzi,
vita, au mambo mengine ya kisiasa?
Je, hilo halitaonyesha kwamba
tumeanza kuunga mkono upande fulani?
Kwa kweli hiyo itakuwa ishara ya onyo kwetu.
Usemi wetu unaweza kuonyesha kwamba,
tunahitaji kujichunguza ikiwa hatuungi
mkono upande wowote.
Njia bora ya kuzungumza kuhusu suluhisho,
ni kuhubiri kuhusu habari njema ya Ufalme wa Mungu.
Hilo litatusaidia
kudumisha utimilifu wetu.
Tuna uhakika kwamba
Yehova ataondoa ukosefu wote wa haki
tunaokabili.
Kuhubiri kunatusaidai kuendelea kukumbuka tumaini letu.
Tumaini ni nanga
inayotuimarisha tunapokabili nyakati ngumu.
Inatuzuia tusiende mbali zaidi na Yehova,
au na tengenezo lake.
Ikiwa tutaendelea kufanya mambo yote hayo,
hatutaunga mkono upande wowote
inapohusu siasa za ulimwengu huu.
Na tutakazia fikira
kwenye suluhisho la kweli,
Ufalme wa Mungu.
Baraza Linaloongoza linashiriki nasi vikumbusho hivyo muhimu,
kwa kuwa Shetani mtawala wa ulimwengu huu
anawashinikiza
watu wa Yehova kuliko wakati mwingine wowote.
Shetani angependa tuunge mkono
mambo ya ulimwengu huu,
tukifanya hivyo
tutaacha kuwa washikamanifu kwa Yehova.
Hata tunaweza kujipata wenyewe,
tukianza kumpinga Yehova
na Ufalme wake.
Na matokeo?
tunaweza kutenda
kana kwamba Shetani ndiye mwenye suluhisho
la matatizo yetu.
Hatutaki tupatwe na jambo kama hilo.
Kwa hiyo ndugu na dada wapendwa
ni lazima tusali kwa Yehova
ili atusaidie kuimarisha imani yetu.
Ili kutusaidia kukazia fikira suluhisho la kweli,
jiwekee lengo
la kuwa na funzo la kibinafsi,
au ibada ya familia
kuhusu kutounga mkono upande wowote.
Fikiria mambo haya machache.
Kwenye kitabu,
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo,
unaweza kupitia habari kuhusu “Serikali.”
Ili kupata chapisho hili kwenye JW Library,
fungua JW Library,
kisha Machapisho,
kisha Vitabu.
Njia nyingine,
ni kupitia tena makala ya Mnara wa Mlinzi ya Oktoba 2023,
yenye kichwa, “Je Uko Tayari Kutii?”
Au kutazama
JW Broadcasting ya Machi 2019.
Ina mapendekezo mazuri
ya kutusaidia kutounga mkono
upande wowote.
Ili kuipata kwenye JW Library,
fungua JW Library, kisha video,
JW Broadcasting,
kisha fungua programu za kila mwezi,
au kwenye jw.org,
tafuta broadcasting ya Machi 2019.
Ikiwa utaandika
“Kutounga Mkono Upande Wowote” kwenye jw.org
utapata video na makala nyingi
zinazoweza kukusaidia.
Tunaweza kuwa na uhakika
kwamba moyo wa Yehova unashangilia,
kuona mamilioni ya watu kutoka mataifa yote,
wakiungana ili kumwabudu yeye,
hawaungi mkono upande wowote,
na kutangaza suluhisho la kweli
kwa matatizo ya wanadamu,
habari njema ya Ufalme wa Mungu.
Ndugu na dada
tafadhali kumbukeni,
tunawapenda sana ninyi nyote.
Kutoka Makao Makuu
ya Ulimwenguni Pote
ya Mashahidi wa Yehova,
hii ni JW Broadcasting.