JW subtitle extractor

Rafika Morris: Nilitaka Kupigania Haki

Video Other languages Share text Share link Show times

Tulilelewa Kusini mwa Marekani
kulipokuwa na ubaguzi wa rangi.
Watu weusi na weupe
hawangekaa pamoja.
Si hilo tu,
kulikuwa na ishara
ambazo zilionyesha mahali
ulipopaswa kuwa.
Sikuelewa kwa nini
hatukuwa na amani
Senti hamsini.
Naam bwana.
Asante bwana.
Nyanya, yeye ni mvulana tu,
kwa nini unamwita bwana?
Kaa kimya.
Unapaswa kujua wewe ni nani.
Tuliporudi kwenye gari,
nilimwambia
Unajua nini?
Kamwe sitaaibikia rangi yangu.
Nyanya yangu alijua
kwamba niliipenda Biblia
kwa sababu nilipokuwa mdogo
sikuzote niliisoma.
Lakini sikuelewa.
Kwenye sala niliuliza
Kwa nini tuko tofauti?
Kwa nini hatuwezi kuishi pamoja?
Nilikutana na kikundi fulani,
nilitaka sana kujiunga na kikundi hiki.
Walijihusisha na siasa.
Walisema, tunapigania haki.
Waliposema neno haki
niliwaza,
kwa kweli ningependa kujiunga nao.
Niwe sehemu ya kitu
kinacholeta mabadiliko
na kuunganisha watu, sivyo?
Hilo ndilo lililokuwa lengo langu.
Tulianza kupinga ukatili wa polisi,
na ninafikiri hilo ndilo watu
wengi walitaka sana.
Nilipenda baadhi ya
mambo waliyokuwa wakifanya.
Lakini kila siku walitufanyisha
mazoezi ya kijeshi.
Tulijifunza kutumia
silaha na vitu kama hivyo.
Basi nikafikiri,
sipendi kuwa hapa.
sikutarajia itakuwa hivyo.
Basi nikaanza kumrudia Mungu.
Kusoma Biblia.
Kwa sababu niligundua kwamba,
mambo ninayofanya hayabadili chochote.
Nilikuwa nikisoma Biblia ya
King James Version.
Basi nilikuwa nikiisoma,
nikiisoma, nikiisoma,
lakini sikuielewa.
Tulitembelea Jamaica
tukapata Biblia hii,
Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.
Nilianza kuisoma.
Na ilieleweka vizuri sana.
Haikuwa na lugha ya zamani.
Nilishangaa, nikajiambia
hii ndiyo Biblia ninayoitaka.
Siku moja wanawake
wawili walibisha mlango
sikujua kwamba wao ni
Mashahidi wa Yehova.
Nilichoona ni Biblia.
Nikauliza, Mliipata wapi Biblia hii?
Wakasema, Sawa tutakuleta moja.
Na kweli wakaleta.
Basi wakaniletea Biblia.
Lakini sikujua kwamba wao
wangenifundisha Biblia.
Mara ya kwanza nilipohudhuria
kusanyiko la Mashahidi wa Yehova
kulikuwa na watu elfu kumi hivi.
Nilipoingia ndani na kuona
watu wa rangi mbalimbali
ni kana kwamba Yehova
alikuwa ananiambia
Rafika, kumbuka ulikuwa unaniuliza
kama inawezekana kwa watu wa
jamii mbalimbali
kuungana na kuwa kitu kimoja.
Ona mimi sina ubaguzi.
Wote wana amani wameungana.
Nilijihisi vizuri sana moyoni.
Naam, ningependa kushirikiana na
tengenezo hili.
Ninawaona watu wote kuwa sawa.
Ninaweza kuhubiri na
kuwa na urafiki na mtu yeyote.
Sasa kwa kuwa ninajua
Biblia inafundisha nini hasa
nina maisha mazuri sana
kwa sababu ninajua kwamba
Mungu tu ndiye anayeweza
kuleta amani kupitia Ufalme wake.
Kama vile Yehova
ameunganisha watu wake
ningependa watu wote
waunganishwe na kumjua Yehova
kama vile ninavyomjua.
Yehova alijibu sala yangu.