JW subtitle extractor

Mungu Anakubali Dini Zote?

Video Other languages Share text Share link Show times

Watu mingi wanaamini kama dini zote ni za muzuri,
zote ziko sawa barabara,
na zinapeleka tu ku uzima wa milele.
Lakini ile ni kweli?
Mungu anakubali dini zote?
Biblia nayo inafananisha dini na barabara mbili:
Moya ni ya mukubwa na inajaa watu.
Ingine ni ya kidogo na muko watu kidogo.
Ni barabara ya kidogo tu njo inafananisha dini ya kweli,
na inapeleka ku uzima wa milele.
Tutajua je kama tuko mu barabara ya muzuri?
Kwa mufano unapotea.
Unauliza watu wakuonyeshe njia.
Wa kwanza, anakuambia uende mashariki.
Wa pili, anakuambia uende mangaribi.
Wa mwisho iko na karte na anakuonyesha kama unapaswa kuenda kaskazini.
Utafuata mawazo ya nani?
Biblia iko sawa vile karte, yenye inatupeleka ku uzima wa milele.
Sasa, juu ya nini kuko mafundisho yenye inapingana?
Kwa mufano,
dini mingi zinafundishaka kama nafsi ya mutu haikufake, inaendaka ishi milele fasi fulani.
Wengine wanaamini kama mutu anazaliwaka mu mwili ingine.
Ile ni mufano moya tu ya kuonyesha namna mafundisho ya dini inapingana.
Tunaweza kusema kama dini zote zinafundishaka kweli?
Karte yenye inatuongoza, ni kusema, Biblia, inasema wafu hawajue kitu.
Mungu atawafufua, na wenye haki wataishi milele ku dunia.
Mambo yenye Biblia inasema juu ya kifo iko wazi.
Kwa hiyo, mambo yenye inasema juu ya mwenendo iko pia wazi.
Tunaweza kuwa mu dini fulani, lakini kama mwenendo wetu unachukiza Mungu, hatakubali ibada yetu.
Biblia inasema kama watu mingi leo watakuwa
“wenye hawajizuie,
wakali,
wenye hapendi wema.”
Inasema pia kama Wakristo wa kweli watakuwa wenye amani,
wenye kusema maneno ya muzuri
na kutenda mambo ya muzuri.
Biblia haiseme kama dini zote zinapendeza Mungu,
lakini inasema kama kuko dini moya tu ya kweli.
Dini ya kweli inasaidia mutu akuwe rafiki ya Mungu
na inapeleka ku uzima wa milele.
Pengine unajiuliza,
‘Namna gani ninaweza kujua dini ya kweli?’
Ile ulizo na maulizo ingine inajibiwa mu somo ya 10 ya broshua Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
Unaweza kuichukua ku jw.org.
Mashahidi wa Yehova watafurahia kujifunza Biblia na weye.
Omba funzo la Biblia ku jw.org,
na Shahidi wa eneo yenu atakutembelea ili mujifunze Biblia,
mahali na saa unapenda.