JW subtitle extractor

Je, Mungu Husikiliza Sala Zote?

Video Other languages Share text Share link Show times

Biblia inasema Mungu
ndiye “Msikiaji wa sala.”
Hata anaweza kusikia
sala unayosema kimyakimya.
Hilo linawezekanaje?
Akiwa Msikiaji wa sala,
yeye pia ndiye Muumba wa uhai.
Anaelewa jinsi akili ya
mwanadamu inavyofanya kazi.
Yeye ndiye aliyeiumba.
Kwa hiyo, anaweza
kusoma mawazo akilini mwako
na kusikiliza
sala unazosema kimyakimya.
Yehova Mungu anapendezwa
nawe popote pale unapoishi.
Anaelewa lugha
yoyote unayozungumza.
Lakini je, anakubali
na kusikiliza sala zote?
Mwazie meneja
anayemwona mfanyakazi akiiba.
Meneja anapomwendea,
kwanza mfanyakazi
anajaribu kusema uwongo,
halafu anajaribu kutetea
sababu yake ya kufanya hivyo.
Ingawa meneja anamsikia
akisema uwongo na kujitetea,
anakataa kuukubali.
Kwa njia hiyo pia,
Mungu hakubali sala zote.
Kwa mfano,
vipi ikiwa mtu
anatoa sala kwa ubinafsi?
Vipi ikiwa mwanamume
anamtendea vibaya mke wake,
halafu kesho yake
anamwomba Mungu ambariki?
Namna gani askari wakisali
Mungu awasaidie
kuwaangamiza maadui wao,
na wakati huohuo
askari wa jeshi pinzani
wanaomba jambo hilohilo?
Je, Mungu atakubali sala kama hizo?
Ni wazi kwamba Mungu hapendezwi
na sala zinazopingana
na kanuni zake za maadili.
Kwa upande mwingine,
Mungu yuko tayari kukubali sala zako,
hata ikiwa umefanya mambo mabaya,
ikiwa kwa unyoofu unataka kumkaribia
na unatafuta hekima na msamaha wake.
Mungu husikiliza sala za wale
wanaojitahidi kufanya
mambo yanayompendeza.
Lakini tunapaswa kusali jinsi gani?
Utafaidika jinsi gani kwa kumkaribia Mungu?
Maswali hayo yanajibiwa
katika somo la 12 la broshua
Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
Unaweza kuipakua kwenye jw.org/sw.
Mashahidi wa Yehova
watafurahi kujifunza Biblia pamoja nawe.
Jaza ombi la kujifunza Biblia
linalopatikana kwenye mtandao,
na mmoja wa Mashahidi wa Yehova
atakutembelea wakati
na mahali panapokufaa.