JW subtitle extractor

Mungu Anasikilizaka Sala Zote?

Video Other languages Share text Share link Show times

Biblia inasema
Mungu ni “Musikiaji wa sala.”
Anaweza hata
kusikia sala ya kimya-kimya.
Ile inawezekana je?
Yeye njo aliumbaka kila kitu.
Anajua namna akili ya mwanadamu inatumikaka.
Yeye njo aliumbaka akili yetu.
Kwa hiyo,
anaweza kujua mambo yenye iko mu akili yako
na kusikia sala yako ya kimya-kimya.
Hata uishi wapi,
Yehova Mungu anakuhangaikia.
Hata useme luga gani,
anaisikiaka.
Lakini,
Mungu anasikilizaka sala zote?
Tukamate mufano:
Mukubwa wa kazi anaona mufanyakazi iko anaiba.
Anamuuliza,
lakini mufanyakazi anakatala kwanza na
kisha anaanza kujitetea-tetea.
Hata kama mukubwa wa kazi amesikia namna mufanyakazi iko anajitetea-tetea
na kusema uongo,
haitike.
Vilevile,
Mungu haitikake sala zote.
Kwa mufano,
itakuwa je kama mutu anaomba juu ya mambo yake mwenyewe tu?
Itakuwa je kama mutu anatendea bibi yake mubaya,
kisha anaomba Mungu amubariki?
Itakuwa je kama maaskari fulani wanasali Mungu awasaidie washinde maadui wao,
na kumbe maadui wao wako wanasali pia vile?
Pale Mungu atasikiliza nani?
Mungu
hasikilizake sala ya mutu mwenye anafanyaka mambo ya mubaya.
Lakini,
hata kama umefanya mambo ya mubaya,
Mungu atasikiliza sala yako kama unataka kabisa kuwa rafiki yake,
unatafuta akuongoze,
na kumuomba akusamehe.
Mungu
anasikilizaka sala ya mutu mwenye iko anajikaza kumufurahisha.
Lakini unapaswa kusali namna gani?
Utapata faida gani kama unamukaribia Mungu?
Majibu ya ile maulizo
iko mu somo ya 12 ya broshua
Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
Unaweza kuichukua
ku jw.org.
Mashahidi wa Yehova
watafurahi kujifunza Biblia na weye.
Omba funzo la Biblia ku jw.org,
na Shahidi wa eneo yenu
atakutembelea ili mujifunze Biblia,
mahali
na saa unapenda.