00:00:09
Kila mtu
huhuzunika mara kwa mara.00:00:11
00:00:15
Vipi wewe?00:00:16
00:00:19
Huenda ukajua sababu ya kuhuzunika;00:00:22
00:00:26
nyakati nyingine, huenda usijue.00:00:28
00:00:33
Hata ikiwa hujui sababu,00:00:34
00:00:34
unaweza kufanya
nini ili uache kuhuzunika?00:00:38
00:00:39
Kwanza, tafuta mtu
wa kuzungumza naye,00:00:41
00:00:41
iwe ni mzazi
au rafiki wa karibu.00:00:44
00:00:45
Alipokuwa akiteseka sana,00:00:47
00:00:47
Ayubu, mwanamume mwaminifu00:00:49
00:00:49
anayetajwa katika Biblia alisema hivi:00:00:52
00:00:52
“Nitasema waziwazi
katika mateso yangu makali!”00:00:55
00:00:55
Mtu mwingine
anapojua hali unayokabili,00:00:58
00:00:58
anaweza kukushushia kamba00:00:59
00:00:59
ya kutoka kwenye shimo hilo.00:01:01
00:01:03
Jambo lingine unaloweza kufanya ni,00:01:06
00:01:06
Andika mawazo yako!00:01:08
00:01:11
Kwenye Methali 3:21,00:01:13
00:01:13
Biblia inatuambia ‘tulinde hekima
inayotumika na uwezo wa kufikiri.’00:01:18
00:01:22
Kuandika kuhusu hisia zako00:01:24
00:01:24
kunaweza kukusaidia kufanya hivyo.00:01:26
00:01:26
Baada ya kuziandika00:01:28
00:01:28
unaweza kuelewa
kwa nini umehuzunika,00:01:30
00:01:30
na hivyo kupunguza huzuni yako.00:01:33
00:01:37
Pendekezo la tatu:00:01:39
00:01:39
Biblia inasema kwamba
ukisali kuhusu mahangaiko yako,00:01:42
00:01:42
‘amani ya Mungu
inayozidi uelewaji wote00:01:45
00:01:45
italinda moyo
wako na mawazo yako.’00:01:48
00:01:48
Kwa hiyo, usikose kusali.00:01:51
00:01:52
Jambo lingine litakalokusaidia sana00:01:54
00:01:54
ni kusoma Biblia00:01:56
00:01:56
hasa kitabu cha Zaburi.00:01:58
00:01:59
Kujaza mawazo
yanayofaa akilini mwako00:02:02
00:02:02
kutoka katika Biblia
kutakusaidia ujihisi vizuri.00:02:06
00:02:06
Lakini vipi ikiwa
bado unaendelea kuhuzunika?00:02:09
00:02:11
Vipi ikiwa hufurahii mambo yote00:02:12
00:02:12
uliyokuwa ukifurahia zamani?00:02:15
00:02:16
Vipi ikiwa huna hamu ya kula,00:02:18
00:02:20
unashindwa kulala,00:02:22
00:02:23
na unajihisi kuwa
hufai hata kidogo?00:02:26
00:02:27
Hisia hizo zikiendelea,00:02:29
00:02:30
zungumza na wazazi
wako kuhusu kumwona daktari.00:02:33
00:02:34
Daktari anaweza
kukusaidia kutambua00:02:36
00:02:36
ikiwa una
tatizo la afya kama vile,00:02:39
00:02:39
kushuka moyo.00:02:40
00:02:42
Ikiwa una tatizo la kushuka moyo,00:02:43
00:02:43
huna sababu ya kuaibika.00:02:46
00:02:46
Watu wengi wamepata
nafuu baada ya kupata matibabu00:02:50
00:02:50
huenda hawakufikiri
wangewahi kuhisi hivyo.00:02:53
00:02:54
Kwa hiyo, iwe huzuni yako00:02:57
00:02:57
inatokana na kushuka moyo au la,00:02:59
00:02:59
kwa msaada na jitihada,00:03:01
00:03:01
unaweza kutoka
katika shimo refu la huzuni.00:03:04
00:03:08
Kumbuka, hisia za huzuni00:03:11
00:03:11
ni za muda; zitapita.00:03:13
00:03:13
Na ukijifunza
kukabiliana nazo sasa,00:03:16
00:03:16
utakuwa tayari kuzishughulikia00:03:17
00:03:17
utakapokuwa mtu mzima.00:03:20
00:03:20
Unaposhughulikia
hali siku baada ya siku,00:03:23
00:03:23
na kutegemea msaada wa wazazi00:03:25
00:03:25
na marafiki wanaotegemeka,00:03:27
00:03:28
utaacha kuhuzunika
na kuanza kuchangamka.00:03:33
Acha Kuhuzunika, Changamka!
-
Acha Kuhuzunika, Changamka!
Kila mtu
huhuzunika mara kwa mara.
Vipi wewe?
Huenda ukajua sababu ya kuhuzunika;
nyakati nyingine, huenda usijue.
Hata ikiwa hujui sababu,
unaweza kufanya
nini ili uache kuhuzunika?
Kwanza, tafuta mtu
wa kuzungumza naye,
iwe ni mzazi
au rafiki wa karibu.
Alipokuwa akiteseka sana,
Ayubu, mwanamume mwaminifu
anayetajwa katika Biblia alisema hivi:
“Nitasema waziwazi
katika mateso yangu makali!”
Mtu mwingine
anapojua hali unayokabili,
anaweza kukushushia kamba
ya kutoka kwenye shimo hilo.
Jambo lingine unaloweza kufanya ni,
Andika mawazo yako!
Kwenye Methali 3:21,
Biblia inatuambia ‘tulinde hekima
inayotumika na uwezo wa kufikiri.’
Kuandika kuhusu hisia zako
kunaweza kukusaidia kufanya hivyo.
Baada ya kuziandika
unaweza kuelewa
kwa nini umehuzunika,
na hivyo kupunguza huzuni yako.
Pendekezo la tatu:
Biblia inasema kwamba
ukisali kuhusu mahangaiko yako,
‘amani ya Mungu
inayozidi uelewaji wote
italinda moyo
wako na mawazo yako.’
Kwa hiyo, usikose kusali.
Jambo lingine litakalokusaidia sana
ni kusoma Biblia
hasa kitabu cha Zaburi.
Kujaza mawazo
yanayofaa akilini mwako
kutoka katika Biblia
kutakusaidia ujihisi vizuri.
Lakini vipi ikiwa
bado unaendelea kuhuzunika?
Vipi ikiwa hufurahii mambo yote
uliyokuwa ukifurahia zamani?
Vipi ikiwa huna hamu ya kula,
unashindwa kulala,
na unajihisi kuwa
hufai hata kidogo?
Hisia hizo zikiendelea,
zungumza na wazazi
wako kuhusu kumwona daktari.
Daktari anaweza
kukusaidia kutambua
ikiwa una
tatizo la afya kama vile,
kushuka moyo.
Ikiwa una tatizo la kushuka moyo,
huna sababu ya kuaibika.
Watu wengi wamepata
nafuu baada ya kupata matibabu
huenda hawakufikiri
wangewahi kuhisi hivyo.
Kwa hiyo, iwe huzuni yako
inatokana na kushuka moyo au la,
kwa msaada na jitihada,
unaweza kutoka
katika shimo refu la huzuni.
Kumbuka, hisia za huzuni
ni za muda; zitapita.
Na ukijifunza
kukabiliana nazo sasa,
utakuwa tayari kuzishughulikia
utakapokuwa mtu mzima.
Unaposhughulikia
hali siku baada ya siku,
na kutegemea msaada wa wazazi
na marafiki wanaotegemeka,
utaacha kuhuzunika
na kuanza kuchangamka.
-