JW subtitle extractor

Usiruhusu Maisha Yako Yaathiriwe na Sigara

Video Other languages Share text Share link Show times

Je, wewe huvuta sigara?
Je, unashawishika kuvuta sigara?
labda ili rafiki zako wakupende?
au ili ukabiliane na mkazo?
Au labda kwa sababu tu ya udadisi?
Vyovyote vile,
unapaswa kujua
madhara ya kuvuta sigara.
Kwenye Waroma 12:1,
Biblia inakuambia utumie
‘nguvu zako za kufikiri.’
Kwa hiyo, badala tu ya kuufuata umati,
tumia akili na ufanye uamuzi mzuri.
Kampuni za tumbaku
hutumia mabilioni ya dola
kujaribu kuwasadikisha watu wavute sigara.
Na watu wengi hunaswa
bila kufikiria madhara.
Kwa mfano,
kuvuta sigara kunaweza
kudhuru afya yako
na mwonekano wako pia.
Biblia inasema
“tujisafishe kila unajisi wa mwili na roho.”
Lakini kuvuta sigara kunamchafua mtu!
Watu wanaovuta sigara
wanaweza kufa kutokana na kansa,
mshtuko wa moyo,
na magonjwa mengine.
Je, unajua kuvuta sigara
hakukudhuru wewe peke yako?
Wale wanaokuzunguka
huathiriwa sana na moshi wa sigara yako.
Vipi kuhusu sigara za kielektroni?
Je, ni salama zaidi?
La hasha!
Watu wengi walidai kwamba
sigara hizo za kielektroni ni salama zaidi,
lakini zimehusianishwa na vifo vingi
na maelfu ya watu waliozitumia
wamekuwa wagonjwa.
Na unaweza kuwa mraibu
kama tu wanaovuta sigara za kawaida.
Unafikiri nani anafaidika unapozitumia?
Kwa hiyo, utafanya nini
mtu akikualika uvute sigara?
Mwambie tu: “Hapana.
Mimi sivuti sigara.”
Asipokuelewa, mwambie,
“Nilichunguza madhara ya sigara,
nikaamua sitavuta.”
Lakini vipi ikiwa tayari umekuwa mraibu?
Huenda ukahisi wewe
ni mfungwa wa zoea hilo.
Lakini unaweza kujinasua.
Kwanza, ikiwa wewe huvuta sigara,
omba msaada,
ikiwezekana, kutoka kwa mtu ambaye
amefaulu kuacha zoea hilo.
Pili, waepuke watu na maeneo
ambayo yanakutamanisha.
Na jambo lingine moja—
Sali.
Ukisali kwa bidii
kila unapopata tamaa ya kuvuta sigara,
utashinda zoea hilo
kwa msaada wa Mungu.
Zaburi 18:29 inatuambia hivi:
“Kwa nguvu za Mungu
ninaweza kuupanda ukuta.”
Naam, hata ikiwa unapambana na uraibu,
unaweza kushinda pambano hilo.
Shinda kishawishi cha kutumia
aina yoyote ya tumbaku.
Utakuwa na afya nzuri zaidi,
furaha zaidi,
na utapumua vizuri zaidi,
kwa kuwa maisha yako
hayaathiriwi na sigara.