00:00:07
Shule inaweza kuleta mkazo!00:00:10
00:00:10
Iwe unasomea shuleni00:00:11
00:00:12
au unasomea nyumbani.00:00:13
00:00:13
Hata wanafunzi bora00:00:15
00:00:15
huchoshwa na shule wakati mwingine.00:00:17
00:00:17
Na hata kuwa shuleni tu,00:00:19
00:00:19
hakumaanishi kwamba unanufaika na masomo.00:00:21
00:00:22
Kwa mfano,00:00:23
00:00:23
je, unakabiliana na wasiwasi00:00:25
00:00:25
au kushuka moyo?00:00:26
00:00:27
Au je, wewe huhisi00:00:29
00:00:29
umechoshwa na shule?00:00:30
00:00:31
Je, ni vigumu kwako00:00:32
00:00:32
kukaza fikira darasani?00:00:34
00:00:34
Je, familia yako00:00:36
00:00:36
inakutegemea uwasaidie kifedha?00:00:38
00:00:39
Au je, unahangaishwa na unyanyasaji00:00:41
00:00:41
au ukatili shuleni?00:00:43
00:00:44
Changamoto kama hizo00:00:45
00:00:46
zinaweza kukuvunja moyo.00:00:48
00:00:48
Huenda ukakosa kwenda darasani00:00:50
00:00:51
na ukaanguka mtihani.00:00:52
00:00:53
Kadiri hali yako shuleni00:00:55
00:00:55
inavyoendelea kuzorota,00:00:56
00:00:57
huenda ukashawishiwa kusikiliza00:00:58
00:00:58
hiyo sauti inayokuambia,00:01:00
00:01:00
“Acha shule.”00:01:01
00:01:03
Lakini,00:01:04
00:01:04
subiri kwanza!00:01:05
00:01:06
Biblia inasema kwamba, ‘mtu mwerevu00:01:08
00:01:08
hutafakari kila hatua00:01:10
00:01:10
anayochukua.’00:01:11
00:01:11
Kwa hiyo, kwanza,00:01:13
00:01:13
tafakari jinsi ambavyo shule00:01:15
00:01:15
inaweza kukusaidia.00:01:16
00:01:17
Elimu ina faida kubwa.00:01:19
00:01:19
Inakusaidia kujua mambo mengi.00:01:21
00:01:22
Lakini, cha muhimu zaidi,00:01:24
00:01:25
inauzoeza ubongo wako.00:01:26
00:01:32
Unaposoma masomo mbalimbali,00:01:34
00:01:35
unajua jinsi ya kujifunza00:01:37
00:01:37
na unapata stadi muhimu00:01:38
00:01:38
kama kusoma na kuandika,00:01:40
00:01:40
ambazo utahitaji maishani.00:01:42
00:01:44
Biblia inatuhimiza,00:01:45
00:01:45
‘tulinde hekima inayotumika00:01:48
00:01:48
na uwezo wa kufikiri.’00:01:49
00:01:50
Shule00:01:51
00:01:51
inakuwezesha kuboresha uwezo wako00:01:53
00:01:53
wa kutatua matatizo.00:01:54
00:01:59
Unajifunza mengi kujihusu00:02:01
00:02:01
na kuwahusu wengine.00:02:03
00:02:05
Hata hivyo,00:02:06
00:02:06
hilo halimaanishi kwamba00:02:07
00:02:07
changamoto zako zitatoweka ghafla,00:02:09
00:02:10
lakini shule inakuzoeza00:02:12
00:02:12
jinsi ya kushughulika nazo.00:02:14
00:02:14
Unajifunza jinsi ya kujidhibiti00:02:16
00:02:16
na jinsi ya 00:02:17
00:02:17
kutanguliza mambo muhimu.00:02:19
00:02:20
Unaweza kujifunza ustadi ambao00:02:22
00:02:22
utakuwezesha kupata kazi baadaye.00:02:24
00:02:27
Ukiamua kuacha shule,00:02:29
00:02:29
huenda itakuwa vigumu kwako00:02:31
00:02:31
kupata kazi.00:02:32
00:02:41
Kuwa na elimu00:02:42
00:02:42
kunakulinda pia.00:02:43
00:02:44
Ikiwa unajua mambo mengi,00:02:46
00:02:46
ni vigumu kwa watu kukulaghai.00:02:48
00:02:49
Hivyo, ikiwa unakabili00:02:51
00:02:51
wakati mgumu shuleni,00:02:53
00:02:53
usikate tamaa.00:02:54
00:02:55
Omba msaada.00:02:56
00:02:57
Unaweza kumwomba mzazi,00:02:58
00:02:59
rafiki mkomavu,00:03:00
00:03:00
au hata mwalimu.00:03:01
00:03:06
Katika maeneo ambayo sheria inaruhusu,00:03:08
00:03:09
baadhi ya wazazi wanaweza00:03:10
00:03:10
kuchagua watoto wasomee nyumbani.00:03:12
00:03:12
Popote unaposomea,00:03:14
00:03:14
tia bidii,00:03:15
00:03:15
kaza fikira,00:03:16
00:03:16
hadi utakapomaliza shule.00:03:18
00:03:19
Kula chakula chenye lishe,00:03:20
00:03:20
fanya mazoezi,00:03:22
00:03:22
na ulale vya kutosha.00:03:23
00:03:24
Mwili wako ukiwa na afya,00:03:26
00:03:26
ubongo wako unafanya kazi vizuri.00:03:28
00:03:29
Biblia inasema kwamba:00:03:30
00:03:30
“Kazi ngumu ina faida.”00:03:32
00:03:33
Ukimaliza shule,00:03:34
00:03:35
utanufaika sana.00:03:36
00:03:37
Shule inaweza kukusaidia00:03:39
00:03:39
kutambua na kukuza uwezo00:03:41
00:03:41
ambao hukujua unao.00:03:43
00:03:43
Inakuzoeza kufikiri na00:03:45
00:03:45
kutatua matatizo.00:03:46
00:03:46
Na inakutayarisha kutimiza majukumu00:03:49
00:03:49
ambayo utapata baadaye maishani.00:03:51
Je, Niache Shule?
-
Je, Niache Shule?
Shule inaweza kuleta mkazo!
Iwe unasomea shuleni
au unasomea nyumbani.
Hata wanafunzi bora
huchoshwa na shule wakati mwingine.
Na hata kuwa shuleni tu,
hakumaanishi kwamba unanufaika na masomo.
Kwa mfano,
je, unakabiliana na wasiwasi
au kushuka moyo?
Au je, wewe huhisi
umechoshwa na shule?
Je, ni vigumu kwako
kukaza fikira darasani?
Je, familia yako
inakutegemea uwasaidie kifedha?
Au je, unahangaishwa na unyanyasaji
au ukatili shuleni?
Changamoto kama hizo
zinaweza kukuvunja moyo.
Huenda ukakosa kwenda darasani
na ukaanguka mtihani.
Kadiri hali yako shuleni
inavyoendelea kuzorota,
huenda ukashawishiwa kusikiliza
hiyo sauti inayokuambia,
“Acha shule.”
Lakini,
subiri kwanza!
Biblia inasema kwamba, ‘mtu mwerevu
hutafakari kila hatua
anayochukua.’
Kwa hiyo, kwanza,
tafakari jinsi ambavyo shule
inaweza kukusaidia.
Elimu ina faida kubwa.
Inakusaidia kujua mambo mengi.
Lakini, cha muhimu zaidi,
inauzoeza ubongo wako.
Unaposoma masomo mbalimbali,
unajua jinsi ya kujifunza
na unapata stadi muhimu
kama kusoma na kuandika,
ambazo utahitaji maishani.
Biblia inatuhimiza,
‘tulinde hekima inayotumika
na uwezo wa kufikiri.’
Shule
inakuwezesha kuboresha uwezo wako
wa kutatua matatizo.
Unajifunza mengi kujihusu
na kuwahusu wengine.
Hata hivyo,
hilo halimaanishi kwamba
changamoto zako zitatoweka ghafla,
lakini shule inakuzoeza
jinsi ya kushughulika nazo.
Unajifunza jinsi ya kujidhibiti
na jinsi ya
kutanguliza mambo muhimu.
Unaweza kujifunza ustadi ambao
utakuwezesha kupata kazi baadaye.
Ukiamua kuacha shule,
huenda itakuwa vigumu kwako
kupata kazi.
Kuwa na elimu
kunakulinda pia.
Ikiwa unajua mambo mengi,
ni vigumu kwa watu kukulaghai.
Hivyo, ikiwa unakabili
wakati mgumu shuleni,
usikate tamaa.
Omba msaada.
Unaweza kumwomba mzazi,
rafiki mkomavu,
au hata mwalimu.
Katika maeneo ambayo sheria inaruhusu,
baadhi ya wazazi wanaweza
kuchagua watoto wasomee nyumbani.
Popote unaposomea,
tia bidii,
kaza fikira,
hadi utakapomaliza shule.
Kula chakula chenye lishe,
fanya mazoezi,
na ulale vya kutosha.
Mwili wako ukiwa na afya,
ubongo wako unafanya kazi vizuri.
Biblia inasema kwamba:
“Kazi ngumu ina faida.”
Ukimaliza shule,
utanufaika sana.
Shule inaweza kukusaidia
kutambua na kukuza uwezo
ambao hukujua unao.
Inakuzoeza kufikiri na
kutatua matatizo.
Na inakutayarisha kutimiza majukumu
ambayo utapata baadaye maishani.
-