JW subtitle extractor

Je, Ni Kazi ya Ubuni? Ubongo wa Kindi wa Aktiki

Video Other languages Share text Share link Show times

Kindi wa Aktiki anaweza kulala
kwa miezi saba wakati wa
marija ya baridi kali ya kila mwaka.
Usingizi huo
ni tofauti sana na usingizi wa kawaida.
Kwa kawaida usingizi hupumzisha ubongo
Lakini inaonekana
usingizi wa kindi huyu
huudhuru ubongo wake.
Kindi anapoanza kulala,
anapumua polepole
na mapigo ya moyo yanapungua
na mwili wake mdogo huingia baridi
kufikia kiwango cha kuganda.
Damu yake huanza
kuzunguka polepole sana
na kunyima ubongo wake
oksijeni na virutubisho inavyohitaji.
Kadiri siku zinavyopita
chembe za ubongo zinazoitwa
nuroni hupungua
na maelfu au hata mamilioni
ya viunganishi
vinavyofanyiza kumbukumbu yake
huanza kupotea.
Protini hushikamana na
kujishikiza kwenye nuroni
nayo hufanya kindi apoteze
kumbukumbu zaidi.
Kwa njia fulani,
ubongo wake huanza kufanana
na ule ulioathiriwa na
ugonjwa wa Alzheimer’s.
Halafu jambo
lenye kustaajabisha hutokea.
Baada ya kila majuma mawili,
mwili wake hutetemeka sana
hadi unafikia
kiwango cha joto cha kawaida,
joto hilo hudumu kwa
saa 15 hivi.
Katika muda huo,
ubongo wake huondoa
protini zilizoshikana
na kujenga upya nuroni zilizopungua
na hivyo kuurudishia ubongo
uwezo wake kamili
katika muda wa saa mbili tu.
Jambo hilo hujirudia
katika miezi yake saba ya usingizi
Kiasi cha virutubisho na oksijeni
kinachoufikia ubongo hupungua
halafu kinaongezeka tena
baada ya kila majuma mawili
hadi atakapotoka nje
tena wakati wa majira ya masika
akiwa mzima kabisa.
Na si hilo tu.
Wanasayansi wanafikiria kwamba
viunganishi vya zamani vya nuroni
vina uwezo wa kurudia hali yake haraka.
Hivyo ubongo wa kindi
unarudia hali yake ya kawaida,
na pia kumbukumbu zake zinarudi.
Watafiti wanaamini kwamba
uelewaji huu
utawasaidia kuelewa vizuri zaidi
jinsi ya kutibu
magonjwa ya ubongo wa mwanadamu.
Una maoni gani?
Je, ubongo wa kindi wa aktiki
wenye uwezo wa kujifanyiza upya
ulijitokeza wenyewe?
Au je, ni kazi ya ubuni?