JW subtitle extractor

Ripoti ya 2 ya Baraza Linaloongoza ya 2020

Video Other languages Share text Share link Show times

Habari zenu nyote!
Nawaletea salamu changamfu
kutoka kwa Baraza linaloongoza
na familia ya betheli ya Marekani.
Tungependa mjue kwamba
tunawapenda sana nyinyi nyote
na tunawafikiria sana,
na kila siku tunasali
kwa ajili ya kila mmoja wenu.
Tunajua kwamba ugonjwa huu
wa corona unazidi
kuwaathiri hatua kwa hatua.
Hamwezi kuenda kazini.
Hamwezi kuenda shuleni.
Hamwezi kuenda kwenye
Jumba la Ufalme au
kuhubiri nyumba kwa nyumba.
Baadhi yenu mmepoteza kazi
na hamjui sasa jinsi
mtakavyolisha familia zenu.
Baadhi yenu mna watu wa familia
wanaoishi mbali.
Hakuna mtu mwingine nyumbani.
Na mna wasiwasi kuwahusu.
Na kwa kusikitisha,
baadhi yenu mmewapoteza
wapendwa wenu katika kifo
kutokana na ugonjwa huu.
Tungependa mjue
tunahuzunika sana pamoja nanyi.
Poleni sana kwa msiba uliowapata.
Kwa kweli, hizi ni nyakati
zenye mkazo sana,
lakini ni muhimu
kukumbuka jambo moja:
Hakuna rafiki ya Yehova
ambaye yuko peke yake.
Kupitia roho yake takatifu
Yehova anaweza kutusaidia,
kututegemeza hata
ikiwa tuko wenyewe nyumbani.
Njia nyingine ambayo
Yehova anatusaidia
ni kupitia wachungaji wanaotujali.
Na hilo linapatana na
ahadi ambayo yeye mwenyewe alitoa.
Tutapenda kusoma Yeremia 23,
mstari wa nne
na utaona jinsi unabii huu
unavyotimizwa leo.
Nitasoma tu sehemu ya mstari huu.
Yehova aliahidi kwamba
atawaweka “wachungaji
ambao kwa kweli watawachunga.”
Na sehemu ya mwisho ya
mstari huu inasema
“Hakuna yeyote atakayekosekana.”
Je, umeona jinsi wazee leo
wanavyotimiza unabii huu?
Kwa mfano, fikiria kuhusu kazi yote
ambayo wazee wanafanya ili
kuhakikisha kwamba
hatukosi chakula cha kiroho.
Wamefanya mipango tuunganishwe
kwa ajili ya mikutano ya kutaniko,
wanatufanyia ziara za uchungaji kwa
kutuunganisha kupitia intaneti,
wanapanga mikutano ya
utumishi wa shambani
na wanahakikisha tuna maeneo ya
kuhubiri kupitia simu
au kuandika barua.
Mbali na hilo wachungaji hao
wanahangaikia pia hali yetu ya kimwili.
Kwa hiyo mara kwa mara
huenda wakatujulia hali
kuhakikisha ikiwa tuna chakula,
dawa au mahitaji mengine ya msingi.
Wanapofanya hivyo usiaibike,
wajulishe wazee unachohitaji:
Wanaweza pia kukupatia mapendekezo
yanayofaa ya jinsi ya kulinda afya yako.
Kama unavyoweza kuwazia,
ugonjwa huu ulipotokea.
Wazee walikuwa na maswali mengi.
Hawajawahi kukabiliana na
jambo kama hili tena.
Sasa ghafla
walihitaji kufanya mambo ambayo
hawakuwa wamewahi kufanya kama vile:
kufungua akaunti
kwa ajili ya mawasiliano ya video,
kujifunza kutumia programu
kama vile Skype® au Zoom.
Na kujifunza jinsi ya
kuunganisha kutaniko zima
kwa ajili ya mikutano
kwenye mtandao.
Ndugu hao wamefanya kazi kubwa sana,
na tungependa kuwapongeza
kwa kazi nzuri sana wanayofanya.
Wazee wameuliza maswali mengi sana,
lakini kupitia tengenezo lake,
Yehova ameandaa mwongozo waliohitaji,
jambo lililoonwa kutoka Kanada
litatusaidia kuona hilo.
Acheni tuone video inayoonyesha
Ndugu Warren Shewfelt,
mshiriki wa Halmashauri ya Tawi ya Kanada,
anaeeleza kilichotokea nchini humo.
Ili kujikinga na
maambukizi ya ugonjwa wa corona.
Baraza moja la wazee
la kutaniko lililo karibu na ofisi ya tawi
lilikutana hivi karibuni
ili kufanya maandalizi kuhusu mikutano,
walikuwa na maswali mengi,
walihitaji usawaziko kati ya
hali ya kiroho ya akina ndugu
na amri ya serikali ya kuepuka kukusanyika.
Walisali kwa Yehova ili kupata mwongozo
lakini
mkutano ulipoendelea
bado hawakujua jambo la kufanya.
Kisha ndugu mmoja akaona kwenye
kifaa chake cha kielektroni,
barua kutoka kwenye ofisi ya tawi
kwa ajili ya wazee.
Walipoisoma ilijibu maswali yao yote
na mengine ambayo hawakutarajia
waliona hilo kuwa jibu la Yehova
kwa sala yao.
Lakini sasa
walikuwa na muda usiozidi
saa 24 kuandaa
mkutano wao wa kwanza kabisa
kupitia video.
Walisali
na kufuata mwongozo huo
hatua kwa hatua
na kesho yake,
kutaniko lote liliungana
kufanya mkutano
kupitia video.
Hudhurio lilikuwa zaidi ya asilimia 100,
na moja wapo ya familia iliyohudhuria
iliwaandikia hivi wazee:
“Tunashukuru sana
kwa jitihada zote za
kuandaa chakula hiki muhimu cha kiroho
ndilo jambo ambalo tulihitaji.
Asanteni.”
Simulizi hilo linatia moyo sana!
Asante, Warren.
Tunathamini sana.
Unajua jambo hilo linanikumbusha
kile ambalo nabii Isaya alitabiri
kwenye Isaya 65:24:
“Hata kabla hawajaita,
nitajibu,
wakiwa bado wanasema,
nitasikia.”
Mara nyingi tunapofikiria
kuhusu wazee wanaotujali,
tunawakumbuka
waangalizi wetu wa mzunguko
kwa sababu msiba unapotokea,
wao ndio huunganisha
ofisi ya tawi na makutaniko.
Hilo linanikumbusha jambo
ambalo mimi na mke wangu tuliona
mwaka wa 2010.
Nilipewa mgawo wa
kufanya ziara ya uchungaji nchini Haiti
siku 10 tu baada ya
tetemeko kubwa la ardhi
kusababisha vifo vya
mamia ya maelfu ya watu.
Kwa kusikitisha
ndugu 154 walikufa pia.
Nilikutana na waangalizi
wa mzunguko nchini humo,
na niligundua kwamba baadhi yao
walikuwa wamepoteza watu wa familia zao.
Lakini walikuwa wakiwaokoa wengine,
hata hawakuwa wamepata nafasi ya
kuomboleza kwa ajili
ya watu wao wenyewe.
Bado walikuwa wakitafuta
waliookoka tetemeko hilo.
Unakumbuka Yehova alisema nini?
“Nitawaweka wachungaji
ambao kwa kweli watawachunga.
Hakuna yeyote atakayekosekana.”
Na wachungaji hao nchini Haiti
walihakikisha kwamba
hakuna ndugu au dada
aliyekosekana.
Je, ulijua kwamba
waangalizi wetu wa makutaniko
bado wanaendelea
kuyatembelea makutaniko
wakati wa ugonjwa huu?
Hilo linawezekanaje?
Katika ripoti hii ya
video yenye kutia moyo
Ndugu Paul Echon,
mshiriki wa Halmashauri ya
Tawi ya Filipino,
anaeleza jinsi hata makutaniko
ya mbali yanashughulikiwa.
Simulizi hili linapendeza.
Acheni tutazame.
Mwangalizi mmoja wa mzunguko
nchini Ufilipino
aliandika kwamba alitumia
programu ya Zoom
kufanyia ziara
katika makutaniko mawili ya
mbali zaidi katika mzunguko wake.
Kwa kawaida safari ya
kwenda kwenye visiwa hivyo
kwa kutumia mashua ndogo huchukua
kati ya saa tano na nane,
ikitegemea hali za bahari
na mawimbi ya Pasifiki.
Kwa sababu ya mlipuko wa
ugonjwa wa corona
vizuizi viliwekwa kwa ajili ya
kwenda kwenye visiwa vya
Patnanungan na Jomalig.
Mwangalizi wa mzunguko na mke wake,
walisali kwa bidii kwa Yehova
wakimwomba afungue njia
ili watembelee kutaniko
majuma mawili ya mwisho ya Machi.
Baada ya siku chache
walipokea barua kutoka ofisi ya tawi,
kuhusu njia mbalimbali za
kufanya ziara makutanikoni,
njia moja ilikuwa kufanya
ziara wakiwa mbali
kwa kuunganishwa kupitia intaneti.
Mara moja mwangalizi wa mzunguko
akawajulisha wazee
na wakafanya majaribio ya
njia yao mpya ya mawasiliano.
Alifanikiwa kufanya ziara hizo!
Na akina ndugu na dada
walishukuru sana
na walihisi jinsi Yehova alivyowapenda.
Akizungumzia jambo aliloona
mwangalizi huyo alisema:
“Ni wazi kwamba ugonjwa wa corona
hauwezi kumzuia
Mungu wetu Mweza Yote, Yehova,
kuwatia moyo watumishi wake leo.
Tumeazimia kuliko
wakati mwingine wowote,
kuwatia moyo na kuwasaidia
akina ndugu
waendelea kumtegemea
Yehova kabisa,
kama inavyotajwa kwenye Zaburi 91:2:
“Wewe ni kimbilio langu na
ngome yangu.”
Unakumbuka tulichosoma kwenye
Yeremia 23:4?
“hakuna yeyote atakayekosekana.”
Yehova anajua mahali
kondoo wake wote wapo
na anafanya mipango ili watunzwe.
Asante sana Paul.
Tafadhali wape salamu changamfu
ndugu zetu nchini Filipino.
Tunawapenda wote sana.
Kwa hiyo, tungependa kukumbuka nini
kutokana na mazungumzo hayo?
Mambo mawili: Kwanza,
tunaamini kwamba Yehova ataendelea
kuongoza tengenezo lake muda wote.
Na imeimarisha imani
kuona nyakati nyingine
tengenezo limekuwa hatua moja au mbili,
mbele ya wenye mamlaka
katika kutoa mwongozo unaolinda kundi.
Kwa hiyo, jambo la kwanza:
Yehova ataendelea kuliandalia
tengenezo lake mwongozo
Pili.
Anatumia njia gani kuhakikisha hilo?
Ameandaa wachungaji
wenye upendo kutoa mwelekezo huo.
Nao wanasimamiwa na yule aliyesema:
“Mimi ndiye mchungaji mwema;
mchungaji mwema huutoa uhai wake
kwa ajili ya kondoo.”
Ndugu na dada,
tunaomba mjitunze sana.
Msifanye mzaha.
Tiini miongozo
inayotolewa na “wenye mamlaka.”
Hapa Betheli tunafuata kikamili
mwongozo uliotolewa.
Kwa hiyo wenye mamlaka
wakiagiza usitoke nyumbani,
kaa nyumbani.
Epuka kuwakaribia watu wengine.
Halafu hakikisha unasikiliza habari
lakini si kupita kiasi,
utavunjika moyo ukitazama kupita kiasi.
Unakumbuka haya ni majira gani?
Majira ya ukumbusho.
Kwa hiyo ni nini ambacho
hasa kinapaswa
kuwa akilini mwetu wakati huu?
Zawadi yenye thamani ya fidia,
upendo wa Yehova Mungu
na upendo wa Kristo Yesu.
Mambo hayo ndio yanayopaswa
kutawala mawazo yetu.
Na unapojihisi mpweke
au una mkazo
rudia maneno yenye kutia moyo
yanayopatikana kwenye Waebrania 13:5:
“Sitakuacha wala kukutupa kamwe.”
“Sitakuacha wala kukutupa kamwe.”
Tafadhali
pokeeni upendo wetu mchangamfu,
tunasali kwa ajli yenu.
Kutoka kwenye makao makuu
ya ulimwenguni pote,
hii ni JW Broadcasting®.