JW subtitle extractor

Ripoti ya 8 ya Baraza Linaloongoza ya 2020

Video Other languages Share text Share link Show times

“Endeleeni kukesha.”
Hivyo ndivyo Yesu
aliwaambia wanafunzi wake
baada ya kusimulia mambo
yatakayotokea katika siku za mwisho.
Wewe umekuwa ukiendelea
kukesha kwa muda gani?
Bila shaka sasa tunakabili
nyakati za hatari
zilizo ngumu kushughulika nazo.
Hizi ndizo hali ambazo
tunakuwa tukihubiri
kuzihusu kwa miaka mingi.
Katika ripoti hii,
acheni tuchunguze baadhi ya unabii
ambao tunaona ukitimia mbele yetu
sasa hivi.
Na tuzungumzie
jinsi kampeni ya Novemba
ya kutangaza
kuhusu Ufalme wa Mungu
inavyofaa kabisa wakati huu.
Kwanza,
fikiria kuhusu ishara
ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake.
Kwenye Luka 21:11,
Yesu alisema kwamba
tungeona “magonjwa
na upungufu wa chakula”
“katika sehemu mbalimbali.”
Sasa hivi
tunajionea sehemu hiyo ya ishara
ambayo Yesu alitoa
ikitimia kwa njia kubwa sana.
Unabii wa pili ambao tutachunguza
unapatikana katika Danieli sura ya 2.
Hapo tunasoma kuhusu
sanamu kubwa sana
inayowakilisha falme za wanadamu
ambazo zingefuatana
kuanzia milki ya Babiloni
hadi leo.
Vidole vya miguu
kwenye sehemu ya chini
ya sanamu hiyo
viliwakilisha serikali kuu ya ulimwengu
ya Uingereza na Marekani.
Na Danieli anatuambia
vilikuwa kwa sehemu vya chuma
na kwa sehemu vya
udongo wa mfinyanzi.
Je, unakumbuka mchanganyiko huo
wa udongo wa mfinyanzi
na chuma unawakilisha nini?
Udongo unafananisha
watu wanaotawaliwa na
serkali hiyo kuu ya ulimwengu
ya Uingereza na Marekani
ambao wanapinga utawala huo
na kudhoofisha uwezo wa
serikali hiyo kutumia nguvu
zake kikamili kama chuma.
Danieli 2:43 inasema:
‘sehemu hizo mbili
hazitashikamana.’
Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 2012
lilitoa uthibitisho wa wazi
wa chuma na udongo wa mfinyanzi
liliposema hivi:
“maoni ya kisiasa yanayopingana
na matokeo ya uchaguzi yanayokaribiana
na ambayo hayaonyeshi wazi mshindi
yamedhoofisha uwezo
wa hata viongozi maarufu,
hivi kwamba
hawana mamlaka ya
kutekeleza sera zao.”
Je, hukubali kwamba
tunajionea ukweli wa hilo sasa
kuliko miaka minane iliyopita
wakati ambapo gazeti hilo lilichapishwa.
Tafakari kutimizwa
kwa unabii wa Biblia ambao
tunaona sasa hivi
kunaweza kuimarisha
imani yetu sana.
Katika mahojiano yafuatayo
Ndugu Richard Kelsey
ambaye alibatizwa mwaka wa 1941
anasimulia ni mambo gani
ambayo yamemsaidia
kuendelea kukesha
kwa karibu miaka 80 sasa.
Nilibatizwa Juni 1941
huko Des Moines, Iowa,
wakati uleule kama Peggy,
na tulibatizwa katika tangi
la kunyweshea farasi.
Hiyo ilikuwa muda mfupi kabla ya
kusanyiko la kimataifa
kule St. Louis, Missouri.
Sisi vijana na watoto
tuliambiwa sote tuketi
kwenye safu zilizokuwa
mbele tu ya jukwaa.
Na Ndugu Rutherford alitoa hotuba
“Watoto wa Mfalme.”
Na wakati wa hotuba hiyo
mwishoni alisema:
“’Kuna kitabu kipya,
kitabu cha Watoto
nanyi mtapata nakala yenu
bila malipo.’
Hilo lilinichochea sana
nilipokisoma baadaye
nilichochewa hata zaidi
kumtumikia Yehova.
Nilianza upainia Septemba 1948,
lakini tayari nilikuwa painia msaidizi
na bila shaka
hilo lilinisaidia kuwa na hamu
ya kushiriki katika
utumishi wa wakati wote.
Tunaona hali za ulimwengu
zikiendelea kuwa mbaya
na hilo linaweza kutuogopesha
na wenye umri mkubwa
ambao ni waaminifu
wanaweza kuanza kuvunjika moyo
baada ya miaka mingi
basi ni muhimu sana kuwa na
uhusiano wa karibu pamoja na Yehova.
Tunatazamia wakati ambapo
Ufalme wake utatatua
matatizo yetu yote.
Vijana watatambua
kwamba wenye umri mkubwa
wanadumisha uaminifu wao
na hilo litawachochea
kuiga imani yao.
Na bila shaka
hilo linampendeza Yehova.
Tuliposikia kwamba kutakuwa
na kampeni ya pekee,
mimi na mke wangu Peggy,
tulijiandikisha kuwa mapainia wasaidizi.
Tumekuwa tukihubiri
kuhusu Ufalme wa Mungu
kwa miaka mingi
na sasa kuna kampeni ya pekee
ya kutangaza hasa kuhusu ujumbe huo
Ufalme wa Mungu.
HIlo litakuwa jambo la pekee
katika miaka yetu
mingi ya utumishi kwa Yehova.
Kama tu Ndugu Kelsey
Je, uhakika wako katika
ahadi za Yehova umeimarishwa
kwa sababu ya kuona
mambo yanayotukia leo?
Watu ulimwenguni pote wanatambua
kwamba si jambo la kawaida
kuwa na ugonjwa wa kuenea,
upungufu wa chakula,
misukosuko ya kijamii,
matetemeko ya ardhi
na majanga mengine,
yote yakitokea wakati ule ule.
Kuona utimizo wa unabii wa Biblia
kunaimarisha uhakika wetu kwamba
unabii mwingine
wote utatimia.
Unabii unaoahidi kuleta
kitulizo cha kudumu
kwa matatizo tunayokabiliana nayo.
Kwa mfano,
kama Danieli 2:44 inavyotuambia,
hivi karibuni Ufalme wa Mungu
utakuwa ndio serikali pekee
inayotawala dunia yote milele.
Je, haisisimui kwamba
licha ya hali hizi ngumu
tunashiriki katika kampeni ya pekee
inayowaelekeza watu
kwenye suluhisho la pekee
na ambalo ni halisi kabisa
yaani Ufalme wa Mungu.
Baadhi ya watu
ambao wakati fulani
walishirikiana na
tengenezo la Yehova.
Pia, wanatambua utimizo
wa unabii wa Biblia,
na sasa wamechochewa kurudi.
Ikiwa wewe ni asiyetenda
au umetengwa na ushirika
Tunakutia moyo
uzungumze na wazee wa kutaniko
lililo katika eneo lako.
Watafurahi sana kukusaidia.
Ikiwa ungependa nakala ya gazeti hili,
tafadhali nenda kwenye tovuti yetu
jw.org/sw
na uipakue
au umwombe mmoja wa
Mashahidi wa Yehova nakala.
Siku chache tu
baada ya kampeni hii ya
Novemba kuanza,
dada nchini Ufaransa
alipigiwa simu na mfanyabiashara fulani.
Acheni tumsikilize Ndugu Bruno Faure
akieleza jinsi dada huyo
alivyotumia nafasi hiyo
kutangaza kuhusu Ufalme.
Dada yetu alipigiwa simu
na mmoja wa wafanya biashara
wanaotumia simu kuuza bidhaa.
Alimsikiliza mfanyabiashara huyo
kisha badala tu ya kukata simu hiyo,
dada huyo alimuuliza
mwanamke huyo maoni yake
kuhusu hali za ulimwengu.
Baada ya mwanamke huyo kujibu,
dada yetu aliongezea kwamba
hali hizo zote
tayari zilishatabiriwa na Yesu.
Na kwamba hivi karibuni ukombozi
utakuja kupitia Ufalme wa Mungu.
Mwanamke huyo alipendezwa sana
na akasema atampigia
dada huyo baadaye
akiwa na mume wake
baada ya kazi
ili waendeleze mazungumzo hayo.
Basi baadaye siku hiyo,
mwanamke huyo na mume wake
walipiga simu
kama walivyoahidi.
walikuwa na mazungumzo mazuri
yanayotegemea Mnara wa Mlinzi, Na. 2
tunalotoa katika kampeni yetu.
Na wakafanya mpango
kuzungumza tena siku inayofuata.
Kwa kupendeza siku inayofuata
wenzi hao wa ndoa walikuwa tayari
na nakala yao ya Biblia.
Walisema kwamba
baada ya kusoma kwa makini
Mnara huo wa Mlinzi
waliguswa
na andiko la Yohana 17:3
na wakatambua umuhimu wa
kujifunza Biblia.
Walisema kwamba wao
wamezaliwa nchini Kamerun
na walipata nafasi ya
kufahamiana na Mashahidi wa Yehova
walipokuwa nchini humo.
walipotembelea tovuti ya jw.org
waliguswa sana kuona habari ikipatikana
katika lugha yao ya mama.
Sasa walisema wangependa
kuhudhuria mikutano
na kuendeleza
mazungumzo hayo ya Biblia.
Kwa hiyo mipango inafanywa
ili kufuatilia upendezi.
Ni wazi jitihada zenye bidii
za ndugu zetu nchi Ufaransa
na ulimwenguni pote
zinatokeza ushahidi mkubwa sana.
Watu wengi wanashangazwa sana
kuona jinsi mambo yamebadilika haraka
katika mwaka wa 2020.
Miezi michache tu iliyopita
maisha yalikuwa tofauti sana,
hilo ni somo zuri sana kwetu
na jinsi mambo yanavyoweza
kubadilika upesi sana wakati ujao.
Baada ya Yesu kusema
“endeleeni kukesha”
kwenye Mathayo 24:42,
hebu ona
jinsi alivyoonyesha kwamba
mambo hayo yatatokea
kwa mfuatano wa haraka
na jinsi tunavyopaswa kutenda.
Mathayo 24:42-44 inasema:
“Kwa hiyo,
endeleeni kukesha
kwa sababu hamjui
Bwana wenu atakuja siku gani.
Lakini jueni jambo hili:
Ikiwa mwenye nyumba angejua
mwizi atakuja katika kesha gani,
angekaa macho
na hangeruhusu nyumba yake ivunjwe.
Kwa hiyo
ninyi pia
iweni tayari,
kwa sababu Mwana wa binadamu
atakuja saa
msiyotazamia.”
Je, hali zinazobadilika upesi
katika ulimwengu
hazijakuonyesha umuhimu
wa kuendelea kuwa tayari?
Badala ya kuruhusu
vikengeusha fikira
vitufanye tuache kuwa macho kiroho,
sasa kuliko wakati mwingine
tunahitaji kusali,
kujifunza,
kuhudhuria mikutano
na kuwa watendaji katika huduma.
Tunawashukuru nyote
ambao mmefanya kazi kwa bidii
katika kampeni hii
ya kutangaza kuhusu Ufalme.
Ikiwa bado hujashiriki
katika kampeni hii,
tafadhali usikose.
Ni pendeleo kubwa sana kwetu
kutangaza kuhusu Ufalme,
suluhisho
la matatizo yote ya wanadamu!
Kufanya hivyo kutatusaidia
‘kuendelea kukesha’
na kuendelea ‘kuwa tayari.’
Muwe na uhakika kwamba
tunaendelea kusali kwa ajili yenu
na kwamba tunawapenda sana.
Kutoka kwenye Makao Makuu
ya Mashahidi wa Yehova,
Hii ni JW Broadcasting.