JW subtitle extractor

Ripoti ya 1 ya Baraza Linaloongoza ya 2021

Video Other languages Share text Share link Show times

Habari zenu nyote?
Katika ripoti hii,
Ningependa kuzungumzia kile
ambacho ninyi ndugu na dada mmetimiza
katika miezi michache iliyopita.
Lazima Yehova awe
anafurahishwa sana nanyi.
Utii wenu,
bidii yenu,
licha ya vizuizi vyote
hamjaacha kumpa Yehova kilicho bora.
Tofauti na hilo,
tunapokea ripoti kutoka nchi
moja baada ya nyingine
ya vilele vipya katika idadi ya wahubiri,
machapisho,
mapainia wa kawaida
mafunzo ya Biblia,
na hudhurio la mikutano.
Hongereni sana
ninyi watumishi waaminifu wa Yehova.
Bila shaka,
sisi sote tunatamani
kurudi kuhubiri nyumba kwa nyumba
na kufanya mahubiri ya hadharani.
Na ikiwa kwa sasa
tunaandika barua na pia
kuhubiri kupitia simu
huenda tukaanza kujihisi
hatutimizi mengi.
Ikiwa hivyo ndivyo unavyohisi
kumbuka kile ambacho tunaambiwa
kwenye Ufunuo 14:6.
Tafadhali fuatana nami
ninaposoma mstari huo.
Unasema
“Nami nikamwona malaika mwingine
akiruka katikati ya mbingu,
naye alikuwa na
habari njema ya milele
ili aitangaze kwa wale wanaokaa duniani
kwa kila taifa
na kabila
na lugha
na watu.”
Kwa hiyo malaika
au kikundi cha malaika
wanasimamia kazi ya kuhubiri.
Kwa hiyo ukitafakari
kwa sababu ya vizuizi vilivyopo
Huenda malaika wana
shughuli nyingi zaidi wakati huu
wakihakikisha ujumbe wa Ufalme
unawafikia watu wanaofaa.
Ikiwa sivyo,
ungeelezaje ongezeko lote tunaloona?
Unaandika barua na kuituma
anayeipokea anaisoma
lakini hapendezwi.
Umetimiza nini?
Umetoa ushahidi.
Na huenda huo ndio ushahidi
bora zaidi mtu huyo amewahi kupokea.
Watu wengine hawapatikani
nyumbani tunapowatembelea.
Au huenda hawafungui mlango.
Kwa hiyo hawajui tunaamini nini
hadi . . .
hadi wanapopokea barua yako.
Lakini namna gani mtu mwingine
katika nyumba hiyo anapopendezwa?
Malaika watahakikisha
mtu huyo anasoma barua hiyo.
Umewapa malaika nafasi
ya kutimiza kazi yao.
Au
unapiga simu kwenye namba isiyofaa
halafu kumbe ndio namba
uliyofaa kupiga.
Je, malaika walihusika
katika yeyote ya masimulizi yafuatayo:
Nitakuacha wewe uamue.
Dada mmoja kule Amerika Kusini
alikuwa akihubiri
kupitia simu na hakuwa akipata matokeo.
lakini hakukata tamaa.
Alipiga namba nyingine
na mwanamume akajibu,
Dada huyo alieleza kwamba alikuwa
akipiga simu ili
kuwatia moyo majirani wake
kwa sababu ya ugonjwa wa corona
na akasoma Yeremia 29:11
inayoonyesha kwamba Yehova
anatupatia “wakati ujao
na tumaini.”
Kisha mwanamume huyo akasema
“Hujapiga
simu hii kimakosa.
Umetumwa na Mungu.”
Alimwambia Dada huyo kwamba
alikuwa amepiga kwenye kituo cha redio
na kwamba alikuwa hewani wakati huo,
watu wengi sana walikuwa
wakimsikiliza akizungumza
na mada iliyokuwa ikizungumziwa
ni ugonjwa wa corona.
Upesi Dada huyo alisali apate nguvu
kisha
akashiriki Maandiko yenye kutia moyo
na wasikilizaji wote kwenye redio.
Na pia akawajulisha kuhusu tovuti yetu.
Mtangazaji aliandika Maandiko hayo
na akawatia moyo kwa uchangamfu
wasikilizaji watembelee tovuti hiyo.
Ajabu sana.
Sasa jiulize,
je dada yetu angepiga simu hiyo
ikiwa angejua mapema
kwamba angezungumza
na watu kwenye redio?
Dada mwingine nchini Marekani
alikuwa akinunua nguo kupitia simu
na alikuwa amesali kwa Yehova
ampe ujasiri wa kutoa ushahidi
baada ya kumaliza ununuzi.
Alitenda kupatana na sala yake.
Kwanza alimshukuru muuzaji huyo
kwa kuwa mwenye fadhili
kisha akamuuliza ikiwa
angemsomea andiko la Biblia.
Msichana huyo alikubali.
Kumbe
zamani alikuwa akijifunza Biblia
lakini akaacha kwa sababu
ya kuwa na mambo mengi maishani.
Walianza kujifunza
kitabu Biblia Inatufundisha
na msichana huyo
akahudhuria mikutano kupitia Zoom
Jumapili iliyofuata.
Namna gani simulizi hilo?
Ndugu nchini Japani
aliwaandikia barua
wanafunzi wenzake wa zamani 100.
Sasa wakiwa na miaka thelathini na kitu
wengi wao walikuwa
wanakabili matatizo kazini
na mahangaiko ya kuwalea watoto wao
kwa njia inayofaa.
Hotuba kuhusu maisha ya familia
ilipotolewa kutanikoni
29 kati yao walihudhuria.
Sasa
anajifunza na 18 kati yao.
Dada nchini Brazili
alimpigia mwanamke simu
kumbe simu ililia wakati
mwanamke huyo alikuwa karibu tu kujiua.
Alikuwa na matatizo mengi
lakini simu hiyo
ilimsadikisha kwamba
Mungu anapendezwa naye.
Alikubali funzo
na anafanya maendeleo makubwa.
Dada mwingine anayeishi
kwenye kisiwa kilicho chini ya
ofisi ya Tawi ya Ufaransa
alienda kumwona daktari.
Baada ya kuzungumzia
matatizo yake ya afya kwa muda
alimuuliza daktari yeye anaendeleaje.
Daktari alishtuka
alimwambia
ni mara chache wagonjwa wake
wanapendezwa naye kibinafsi.
Hilo
lilimfungulia njia dada yetu kutoa ushahidi.
Daktari huyo alisema hajawahi
kufungua mlango
Mashahidi walipomtembelea.
Walipomaliza mazungumzo
Daktari alimwambia Dada yetu atakaporudi
atampanga awe mwisho kabisa
ya wagonjwa wengine
ili waweze kuendeleza mazungumzo yao.
Dada mwenye umri wa miaka 80 anaishi
vijijini nchini Ufaransa
alimpigia simu mwanamke katika
kijiji cha mbali
wakazungumza kuhusu ile sala ya kielelezo.
Na hiyo,
ndiyo habari iliyomfaa mwanamke huyo.
Alisema kwamba alilelewa na watawa
lakini hakuwa ameilewa sala hiyo ya Bwana.
Funzo la Biblia linaongozwa kila juma
na mwanamke huyo
anahudhuria mikutano kupitia Zoom.
Masimulizi yote hayo
yanapatana kwa njia gani?
Mtu aliandika barua,
alipiga simu
au kuanzisha mazungumzo.
Ndugu na Dada walifanya walichoweza
na kuwapa malaika jambo la kufanyia kazi.
Kwa hiyo, wape malaika kazi!
Tumia nafasi zote kutoa
ushahidi kwa wanafunzi wenzako,
wataalamu wa afya,
wafanyabiashara,
na wauza duka.
Njia rahisi ya kuanzisha
mazungumzo ni kusema:
“Ningependa kukuambia kuhusu tovuti
ambayo mamilioni ya watu wameona
ina habari zenye kutia moyo.”
Kuhusu tovuti yetu
jitihada za pekee zinafanywa
ili kuandaa habari za karibuni zaidi
kwenye jw.org
Acheni tumsikilize Ndugu Herman van Selm
Msaidizi wa Halmashauri ya
Uandikaji anapotueleza.
Jambo la pekee lilitokea
Januari mwaka uliopita.
Ni jambo gani hilo?
Halmashauri ya Uandikaji
pamoja na Halmashauri ya Waratibu
ziliamua kwamba
ukurasa wa Mwanzo wa tovuti yetu
uwe na makala zinazoonyesha
matukio ya karibuni zaidi,
unase fikira za watazamaji
na kuandaa ufafanuzi
na ushauri kutoka katika Biblia.
Basi uamuzi huo
uliofanywa mwezi Januari
ulithibitikaje kuwa wa wakati unaofaa?
Kwa kweli,
miezi michache tu baadaye
ugonjwa wa corona ulianza.
Kwa hiyo mara moja idara ya uandikaji
ilianza kutayarisha makala
ambazo zingejibu maswali muhimu
yaliyokuwa yakiwahangaisha watu.
Hata hiyo,
changamoto ni kwamba
kutayarisha toleo moja la Amkeni!
au Mnara wa Mlinzi kunaweza kuchukua
zaidi ya miezi 18.
Kwa hiyo tulihitaji kutafuta njia
ya kutayarisha makala kwa ajili ya
ukurasa wa Mwanzo
kwa muda mfupi zaidi.
Kwa kupendeza,
kwa msaada wa Yehova
na kwa msaada wa ndugu na dada
katika idara mbalimbali
muda wote wa kutayarisha
na kutokeza makala moja mpya
kwa ajili ya ukurasa wa Mwanzo
umepunguzwa na kuwa majuma 5.
Tunafurahi sana kwamba
tayari kuna makala nyingi
ambazo zimetayatishwa
kwa ajili ya ukurasa wa Mwanzo
kuhusiana na ugonjwa wa corona.
Kati ya makala hizi sita,
unafikiri ni gani ambayo watu wengi
waliitembelea kwenye ukurasa wa Mwanzo?
Makala iliyotembelewa
na watu wengi zaidi ilikuwa na kichwa
“Biblia Inasema Nini Kuhusu Magonjwa ya Mlipuko?”
Basi hilo linatuonyesha nini?
Watu wanataka kujua
jinsi matukio ya karibuni
yanayohusiana na Biblia.
Na tovuti yetu inaeleza kwa njia ya wazi
jinsi hali za ulimwengu
zinavyotimiza unabii wa Biblia.
Hilo linafanya habari
zilizo katika tovuti yetu
ziwe tofauti na habari ambazo
watu wanaweza kupata
katika sehemu nyingine.
Pia, ndugu na dada
kutoka ulimwenguni pote
wanaona kwamba
makala hizo zinawasaidia.
Huu ni mfano mmoja
wa wenzi wa ndoa walio na watoto matineja.
Wakati tu sisi wazazi tunapohisi
hatujui jinsi ya kushughulika
na ugonjwa huu wa corona
na pia kutengwa, mkazo, na vurugu katika jamii
makala inatokea ambayo inatupa
mwongozo ulio wazi wa Maandiko
wa jinsi ya kushughulikia hali tunayokabili.
Tunashukuru sana kwamba
mtumwa mwaminifu
anatuandalia upesi sana
kile hasa ambacho tunahitaji.
Wengi wameeleza jinsi makala
zilizo kwenye ukurasa wa Mwanzo
zinavyowasaidia katika huduma
Haya ni baadhi ya maelezo yao:
Kutoka Hispania:
Vichwa vinavuta uangalifu,
lugha ni rahisi
lakini yenye nguvu.
Kutoka Benin:
Wahubiri wanavutiwa sana
na jinsi makala hizo
zinavyopatana na matukio ya sasa.
Uholanzi:
Zinawasaidia wahubiri kuendelea
kuwa na uchangamfu katika huduma
wakati wa ugonjwa huu wa corona.
Skandinavia:
Wahubiri huangalia ukurasa wa Mwanzo
kabla ya kuanza mahubiri ya simu.
Uingereza:
Ndicho kitu tulichohitaji zaidi
kwa ajili ya huduma tunayofanya sasa.
Mabadiliko haya ya karibuni
katika ukurasa wa Mwanzo
ni mfano wenye kuimarisha imani wa jinsi
mtumwa mwaminifu na mwenye busara
anavyoandaa chakula
kinachofaa
kwa wakati unaofaa.
Kwa kumalizia,
tungependa kuwapongeza tena
kwa kubadilikana na kwa bidii yenu
wakati wa ugonjwa huu wa corona.
Endeleeni kutia bidii ndugu na dada
na Yehova atawabariki sana.
Kutoka kwenye Makao Makuu
ya Ulimwenguni Pote
ya Mashahidi wa Yehova.
Hii ni JW Broadcasting®.