JW subtitle extractor

Ripoti ya 2 ya Baraza Linaloongoza ya 2021

Video Other languages Share text Share link Show times

Katika ripoti hii,
ningependa kuzungumza nanyi
kuhusu jambo muhimu sana kwangu
Betheli
Nilipojifunza kweli nilipokuwa tineja
nilijiwekea mradi wa kwenda Betheli
baada ya kubatizwa
nilifanya upainia kwa miaka miwili
kisha nikaja Betheli.
Na sasa nimekuwa hapa kwa miaka 36.
Kwa hiyo, ninafurahi kuwaeleza
jinsi mambo yalivyo Betheli sasa hivi
na jinsi familia
ya ulimwenguni pote ya Betheli
inavyokabiliana na ugonjwa huu wa corona.
Bila shaka, utatiwa moyo kujua
ni nini kinachowasaidia
kuwa na shangwe katika utumishi wao.
Wengi wenu mmeshukuru
mkisema kwamba
licha ya ugonjwa huu wa corona
bado tumeendelea kupata chakula cha kiroho.
Hilo linatia ndani mikutano ya kila juma,
makala za habari kwenye jw.org
machapisho mapya,
JW Broadcasting kila mwezi,
programu za kusanyiko
na mambo mengi zaidi.
Yote hayo yamewezekana
kwa sababu familia yetu ya Betheli
imeonyesha roho ya utayari na
kuendelea kufanya kazi kwa bidii
chini ya hali ngumu za sasa.
Ulimwenguni pote familia ya Betheli
haijatoka nje
wengine sasa
kwa karibu mwaka mmoja hivi.
Wanabetheli wetu wamedhabihu nafasi za
kuwa pamoja
na watu wa familia na marafiki.
Na wamefanya hivyo kwa
roho ya ushirikiano na utayari.
Kwa nini?
Kwa sababu wanampenda
Yehova na Yesu
na kwa sababu wanakupenda wewe.
Wanataka kushughulikia mahitaji
ya ndugu na dada ulimwenguni pote.
Wao wamejidhabihu sana
lakini tunajua kwamba
ninyi pia mmejidhabihu
ambao mna familia
na marafiki walio Betheli.
kwa sababu hamjaweza kuwa nao
kihalisi katika nyakati hizi ngumu.
Kwa njia fulani,
mmechangia katika kazi hiyo
kwa kuwasaidia washiriki wa familia yenu
walio Betheli
ili waendelee kukaa huko
na wakazie fikira kazi yao.
Utegemezo wenu
umekuwa zawadi nzuri sana.
Bila shaka,
mwanzoni ni
watu wachache waliofikiri
hali hii itaendelea
kwa muda mrefu kadiri hii.
Katika video ifuatayo,
utaona baadhi ya wanabetheli wetu
wamekuwa wakifanya mambo gani
ili kudumisha shangwe yao
na kuhakikisha kazi ya Ufalme
inaendelea bila kukatizwa.
Mambo matatu ninayokosa zaidi
ni kusafiri,
kucheza michezo,
na chakula ninachopenda zaidi.
Ninakosa sana familia yangu.
Kwa kuwa hapa ninaishi peke yangu,
jambo ninalokosa zaidi ni
kuwa pamoja na akina ndugu na dada.
Hatuwezi kuwasiliana sana
kama tulivyofanya zamani.
Zaidi ya yote,
ninawakosa wapwa zangu wawili wakike
ninawapenda sana watoto hao.
Nimekosa sana kuwakumbatia
akina-dada na watoto kutanikoni.
Ni kana kwamba kila kitu
kilibadilika usiku mmoja kwa ghafla.
Akina-ndugu waliokuwa wakija Betheli
kutusaidia kurekodi
hawangeweza kufanya hivyo tena.
kwa hiyo kazi iliongezeka sana.
Hasa kwa ajili ya kusanyiko la eneo.
Tulikuwa na kazi nyingi
kuliko wakati mwingine.
Kabla tu ugonjwa huu kuanza
nilihamishiwa katika ofisi nyingine ya tawi.
Hilo lilimaanisha kujifunza utamaduni mpya
na kuanza tena kutafuta marafiki wapya.
Nilihisi sasa sina
kazi nyingi kama zamani
au kazi nyingi
kama ambavyo ningependa kuwa nazo.
Na lazima nikubali
nyakati nyingine
mimi huhisi kwamba
sasa sina thamani sana
kama ilivyokuwa zamani.
Baba yangu alihitaji kulazwa hospitalini
kwa sababu alikuwa mgonjwa sana.
Nilihisi sijiwezi na nikahisi nina hatia
kwa sababu nisingeweza
kufanya nilichotamani yaani
kuwa pamoja na familia yangu.
Kwa kuwa nyumba tunayoishi
iko katikati ya jiji
hatuwezi kutoka nje.
Unapokuwa mpweke
na ni kana kwamba
umejifungia ndani ya kuta nne,
unaweza kushuka moyo vibaya sana.
Ninapenda kufikiria
mfano wa Biblia wa Yosefu
hakukazia fikira mambo yasiyofaa
ya hali yake
bali sikuzote
alikazia fikira kutimiza kazi aliyopewa
kwa njia bora zaidi.
Biblia imenisaidia sana
ninatafakari maandiko ya Biblia
kama Zaburi 94:18 na 19 inayosema:
“Upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova,
uliendelea kunitegemeza
Mahangaiko yaliponilemea,
Ulinifariji na kunibembeleza.”
Mimi hutafakari kuhusu paradiso
na kujiona nikiwa na mama yangu
na dada yangu Carol,
tukitembea ufuoni na kuona jua likitua
tutaweza kuishi milele pamoja.
Mimi hufanya mazoezi kila siku
na pia ninaungana na kutaniko
kwa ajili ya kazi ya kuhubiri.
Kuongeza muda ninaotumia
katika kazi ya kuhubiri
kumenisaidia kukazia fikira
kuwasaidia wengine.
Upainia msaidizi umekuwa kama
dirisha linaloniwezesha kuona nje.
Marafiki na watu wa familia wakiniuliza
ninaendeleaje ninawaambia niko sawa.
Hatujaribu kuwaonyesha wengine
kwamba kila kitu kiko sawa
kana kwamba hatuna shida
lakini tunakazia fikira
mambo yanayotia moyo.
Mimi na mke wangu huwa
tunawaambia watulie kwa sababu
hapa Betheli wanatutunza vizuri sana.
Lakini wanajua kwamba hali si rahisi
na kila mara ninapowaona wakitabasamu
tunapozungumza kupitia video
ni kana kwamba wananikumbatia.
Tunaona kwamba inatusaidia
tunapofanya mambo yanayofaa
na wazazi wetu.
Kwa mfano, tunaungana nao
na kusoma andiko la siku pamoja.
Kuwa Betheli wakati wa ugonjwa huu
wa corona ni pendeleo kubwa
kwa sababu inanipa nafasi ya
kuwatia moyo wengine
walio hapa Betheli ambao
wanakabili hali ngumu
na pia ndugu na dada ambao
hawako Betheli
ambao hawajalindwa kama sisi.
Kuwa Betheli kunanifanya
nihisi nina deni kwa Yehova
amekuwa akitutunza kiroho,
kihisia, na kimwili.
Kutumikia hapa Betheli
kama wengine tayari walivyosema
ndiyo njia ya kuhakikisha akina ndugu
wanapata kile wanachohitaji.
Si eti tu, ninatumikia Betheli
bali ninafanya hivyo katika wakati
muhimu zaidi katika historia.
Ninajionea mambo yote
haya moja kwa moja.
Hilo linafanya dhabihu
yoyote ninayotoa kwa ajili ya
pendeleo hili kuwa yenye thamani.
Tunawashukuru sana Wanabetheli wote
pamoja na familia zao
na makutaniko yao
kwa ajili ya dhabihu zote wanazofanya
ili kutegemeza kazi ya Ufalme.
Tunaendelea kuwakumbuka
ninyi ndugu na dada wapendwa
katika sala zetu.
Kama ulivyoona katika video,
Wanabetheli wanakabiliana na mahangaiko
kama wewe tu wakati wa
kipindi cha ugonjwa huu.
Ni kawaida kuwa na hisia kama zao.
Tunajua kwamba majaribu tunayokabili
yatakwisha siku moja.
Lakini kwa sasa,
tunaendelea kukumbwa na hisia
za kawaida za kibinadamu
basi tutafanya nini ili kukabiliana nazo?
Kwanza, uwe mnyoofu
unapozungumza na Yehova
na umweleze waziwazi
unachokabiliana nacho.
Daudi aliposali kwa
Yehova alipokabili hali ngumu
alisema hivi kwenye Zaburi 142:2:
“Ninamwaga mahangaiko yangu mbele zake,
mbele zake ninaeleza taabu yangu.”
Sisi tunaweza kufanya hivyo pia.
Mmiminie Yehova wasiwasi
na mahangaiko yako.
Anaahidi atatusaidia kukabiliana nayo
ikiwa tuna imani.
Basi omba imani kila siku.
Mbali na hilo,
kumbuka kwamba matatizo
tunayokabili leo ni ya muda tu.
Siku za mwisho zilikuwa na mwanzo
na hatimaye zitafikia mwisho.
Ugonjwa huu ulikuwa na mwanzo
na hatimaye ugonjwa huu utafikia mwisho.
Mtume Paulo alisema majaribu
kama haya ni ya “muda mfupi” tu.
Na muda huo unazidi kupungua
kadiri tunavyokaribia
mwisho wa mfumo huu wa mambo.
Kwenye 2 Wakorintho 4:17 na 18
alisema hivi:
“Kwa maana ingawa dhiki ni ya muda mfupi
na ni nyepesi,
inatokeza kwa ajili yetu utukufu ulio mkuu
na bora zaidi na zaidi,
na wa milele.
huku tukikaza macho yetu,
si juu ya vitu vinavyoonekana,
bali juu ya vitu visivyoonekana.
Kwa maana vitu vinavyoonekana
ni vya muda,
lakini vitu visivyoonekana ni vya milele.”
Maneno hayo yaliyoongozwa na roho
yaliwanufaisha Wakristo wa mapema
na yanaweza kuwanufaisha
watu wa Mungu leo.
Tunawapongeza sana kwa
kuvumilia kwa uaminifu
na kwa kuendelea kuwa na
kazi nyingi katika utumishi wa Yehova.
Kupitia jitihada zenu pamoja na
nguvu za roho takatifu ya Yehova
kazi ya Ufalme imezidi kusonga mbele
na inaedelea kupanuka
katika njia yenye kusisimua sana.
Mfano mmoja,
ni wa mradi wa ujenzi kwenye
makao makuu kule Ramapo, New York
uliotangazwa kwenye mkutano wa
kila mwaka wa 2019.
Je, umekuwa ukijiuliza jinsi
mradi wa Ramapo ulivyoathiriwa
kwa sababu ya ugonjwa wa corona?
Tunafurahi kushiriki nanyi
ripoti hii inayoonyesha
jinsi ambavyo kazi imekuwa ikiendelea.
Katika JW Broadcasting
ya Januari 2020
ndugu zetu ulimwenguni pote
walitangaziwa kwamba
Baraza Linaloongoza
limeona ni mapenzi ya Yehova
na idhini imetolewa
kwa ajili ya kuanza ujenzi
wa majengo yatakayotumiwa
kurekodi sauti na video
katika eneo la Ramapo.
Hata hivyo, miezi mitatu baadaye
ugonjwa mbaya sana wa virusi vya corona
ulisimamisha mipango yote
ambayo taasisi kubwa
na hata mataifa yalitaka kutekeleza.
Mradi wa Ramapo uliathiriwaje?
Je, ulikuwa wakati unaofaa
kwa tengenezo la Yehova
kuanza mradi huo mkubwa?
Tunapopitia matukio ya 2020
Angalia uone
si tu Yehova alivyotuongoza na kutubariki
Bali pia,
jinsi ambavyo maneno ambayo
Ayubu alimwambia Yehova yalivyotimizwa.
kwamba “hakuna jambo lolote unalokusudia
lisilowezekana kwako.”
Kwa kipindi fulani hapa New York
ujenzi wowote usio wa lazima ulisimamishwa.
Hata hivyo,
kulingana na muda na ratiba tuliopanga
Halmashauri ya Mji wa Ramapo
ilianza kupanga mikutano yake kupitia
Zoom.
Hilo lilimaanisha kwamba
ijapokuwa hali zilianza kuwa mbaya
ulimwenguni pote
bado tuliweza kufikia lengo letu
Julai 8, 2020
tulipofanya mkutano wetu wa
kwanza na halmashauri ya mji.
Tumejionea waziwazi
baraka za Yehova katika vikao
vyote tulivyofanya nao.
Lengo la pili
tulilofikia na la muhimu zaidi
ni lile la Desemba 9, 2020.
Jiji lilipoidhinisha
hati zetu za ujenzi.
Sawa na mwanafunzi anayepewa
kazi ya kufanya
ili aweze kufaulu mtihani
tunajua taarifa tunazopaswa kuwapa
halmashauri ya jiji
ili tupate kibali cha ujenzi.
Tutaanza lini?
Kwa sasa tunatarajia
mwishoni mwa 2021.
Miezi hiyo itakuwa mapema zaidi
ya mipango ya awali tuliyofanya
hata kabla ya ugonjwa wa corona.
Ni kama Ayubu alivyosema
lolote analokusudia Yehova linawezekana.
Tangu Aprili 2019,
Halmashauri ya Mradi wa Ujenzi
ilipowekwa rasmi
kumekuwa na maendeleo makubwa
katika uchoraji wa eneo
na majengo ya kwanza yatakayojengwa.
Mambo muhimu ambayo tumejifunza
kupitia miradi mikubwa
ambayo tumefanya
imeboresha miongozo
inayotolewa na
Idara ya Usanifu-Majengo na Ujenzi
ya Ulimwenguni Pote
iliyo chini ya usimamizi
wa Halmashauri ya Utangazaji.
Eneo la Ramapo
lina ukubwa wa ekari 249.
Majengo yako futi 160
kutoka kwenye barabara ya Sterling Mine.
Unapotoka barabara ya Sterling Mine
utakutana na kituo cha wageni
kinachoweza kupokea
wageni zaidi ya 1,200 kwa siku
Jengo la studio
pamoja na maeneo yake ya kuigizia
ndiyo sehemu kuu ya eneo hilo
na karibu na studio
kuna karakana.
Katika upande wa pili wa mwinuko
kuna eneo la nyuma
ambalo litatumiwa kurekodi video.
Karibu na studio
kuna ofisi,
mapokezi,
na jengo ambalo watu wanaweza kukutania.
Jengo hilo
linaweza kutumiwa
kwa ajili ya makusanyiko
na linaweza kuwa na wahudhuriaji 1,300.
Pia, linaweza kutumiwa
kama chumba cha kulia
kwa ajili ya watu 1,200
au kwa ajili ya kazi nyingine.
Upande wa magharibi
kuna majengo ya makazi ambamo
wajitoleaji 1,290 wataishi.
Utafiti na jitihada nyingi zimefanywa
ili kuona njia bora
ya kutumia nishati katika eneo hilo.
Jambo hilo lilifanya tuamue kutumia umeme
kama chanzo kikuu
cha nishati kwenye eneo hilo.
Mabomba yaliyopitishwa chini ya studio
na katika majengo mengine
yatatumiwa kuleta joto
katika eneo lote.
Vifaa ya kutokeza umeme
kupitia jua
vyenye urefu wa mita 11,000 za mraba
vitatokeza umeme
na umeme huo utahifadhiwa
katika betri kubwa
inayoweza kutumiwa itakapohitajika.
Matokeo ni kwamba
tutaweza kutokeza
umeme wetu wenyewe
kwa kiasi kikubwa
tuihifadhi,
halafu baadaye tunaweza kuitumia
mahali popote itakapohitajika.
Wengi wetu ambao tumekuwa
tukifanya kazi ofisini
tumezoea kufanya kazi
tukiwa nyumbani wakati huu wa janga.
Je, hilo litafikiriwa
wakati wa mradi wa Ramapo?
Kwa kweli, hatujui mambo yatakuwaje
kuhusiana na namna ofisi zitakavyokuwa.
Hivyo, jambo kuu ni kubuni ofisi ambazo
matumizi yake yanaweza kubadilishwa.
Jengo limegawanya katika ofisi zilizo
na urefu wa futi 10 kwa 15.
Kila ofisi ina paa lenye taa
pamoja na mashine ya
kuleta joto na ubaridi.
Nyaya za kompyuta na umeme zimepitishwa
chini ya sakafu iliyoinuliwa
ili kurahisisha marekebisho yatakapohitajiwa.
Kuna kuta zinazoweza kuondolewa
kwa urahisi kwanzia juu hadi chini.
Tunaweza kugeuza sehemu ndogo ikawa ofisi
au chumba kidogo cha mkutano.
Au zinaweza kuondolewa
na kuwa chumba kikubwa cha mkutano.
Au eneo hilo lililo wazi linaweza
kutumiwa na wafanya kazi kadhaa.
Kwa kuongezea, kwa kuwa
kuta hizi hazihitaji udumishaji mwingi,
mabadiliko yanaweza kufanywa
wakati wowote.
Kabla au baada ya
kuhamia katika eneo hilo.
Ikitegemea na mahitaji ya ofisi
ya wakati huo.
Kwa kutumia vioo vilivyopo tayari
na kuta zinazoweza kuondolewa
zilizotengenezwa kwa kioo
ofisi zinapata mwangaza wa kutosha.
Majengo kumi ya makazi
yamejengwa mengine kuelekea kaskazini
mengine kuelekea kusini.
Ili vyumba vyote
viweze kupata jua la asubuhi
au la mchana.
Yamejengwa kuzunguka mabwawa
yaliyo katika eneo hilo.
Baada ya kufanya utafiti,
tuliamua kutumia njia nyingine ya ujenzi.
Yaani kujenga kwa kutumia mbao zaidi.
Hatujawahi kufanya jambo kama hilo,
katika mradi mkubwa kama huu.
Mbao zenyewe
zinaunganishwa pamoja
ili kutokeza ukuta
ambao utakuwa msingi wa jengo.
Hii ni mbinu inayotumiwa sana siku hizi
iliiyo imara
na salama.
Hiyo inamaanisha nguzo,
mihimili na sakafu
zinaweza kutayarishwa mapema.
Na hivyo ujenzi
ukamalizika upesi.
Na mbali na kuokoa pesa,
kuokoa wakati,
na kutunza mazingira.
Majengo haya yatakuwa
yenye kuvutia sana.
Kwa kuwa miradi mingi
ya kurekodi video na sauti
itafanywa katika eneo hili la Ramapo.
Vyumba 50 vya makazi
vitajengwa katikati ya eneo hili
na vitakuwa kama vyumba vya hoteli
ili wale watakaoishi kwam muda mfupi
iwe wanakuja kwa ajili ya kurekodi video
au ni wageni
waweze kuishi kwa starehe.
Kama ilivyotajwa tayari
wengi wanafanya kazi kutoka nyumbani
hata wengine wanafurahia
kufanya hivyo.
Je, tutaendelea kufanya hivyo wakati ujao?
Hatuwezi kusema.
Hata hivyo,
vyumba vingi
vitakuwa na chumba cha ziada
kitakachokuwa na dirisha
na chumba hiho kinaweza
kutumiwa kama stoo
au ofisi ya nyumbani.
Ripoti zijazo
zitazungumzia hasa jengo kuu.
Jengo lenye studio za
kurekodia video na sauti.
Ingawa ndio itakua studio
kubwa zaidi tuliyowahi kujenga
jambo kuu ni kwamba
itaunganisha kazi zinazofanywa
katika maeneo mbalimbali
na ndugu na dada wanaofanya
kazi hii kwa bidii,
sasa watakuwa pamoja.
Licha ya changamoto nyingi
mwaka wa 2020,
mradi wa Ramapo
umeendelea vizuri.
Tunaposubiri mambo ya wakati ujao
tunatazamia kwa hamu kuona
jinsi ambavyo
‘hakuna jambo lolote ambalo Yehova
amekusudia litakaloshindwa kutimia.”
Maendeleo hayo yenye kustaajabisha
ya mradi wa Ramapo
licha ya hali ngumu kama za sasa
yanatukumbusha maneno ya Zaburi 127:1
“Yehova asipoijenga nyumba,
wale wanaoijenga
wanafanya kazi ngumu ya bure.”
Hakuna shaka kwamba Yehova
anatusaidia kuijenga nyumba
kule Ramapo.
Huenda umetambua kwamba video hiyo
imetaja kutakuwa na ripoti nyingine
basi unaweza kutazamia kwamba
kutakuwa na ripoti nyingine
kuhusu mradi wa Ramapo.
Tunapotafakari yote ambayo
yametimizwa mwaka uliopita.
Ni wazi kwamba Yehova anabariki
roho ya kujidhabihu ya familia yote
ya ulimwenguni pote ya Betheli.
Wao ni kama wale wanaofafanuliwa
kwenye Zaburi 110:3 inayosema:
“Watu wako
watajitoa kwa hiari.”
Kwa kweli ndugu na dada hao wanajitoa
kwa hiari kwa Yehova
siku baada ya siku.
Kwa hiyo tafadhali
endelea kusali kwa ajili ya familia ya Betheli
na kwa ajili ya mradi wa Ramapo.
Tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea
kubariki kazi yake ya bidii
na uvumilivu wako wakati wa ugonjwa huu
iwe unatumikia Betheli
au shambani.
Na tunajua kwamba
utakuwa na bidii sana wakati wa kampeni
ya kuwaalika watu wengi
kadiri iwezekanavyo
kwenye hotuba ya pekee
na kwenye Ukumbusho wa Kifo cha Kristo.
Tunaendelea kusali
kwamba Yehova aendelee kuwaongoza
na kuwaimarisha katika siku zinazokuja
kutoka kwenye
Makao Makuu ya Ulimwenguni Pote
ya Mashahidi wa Yehova
Hii ni JW Broadcasting®.