JW subtitle extractor

Ripoti ya 6 ya Baraza Linaloongoza la 2021

Video Other languages Share text Share link Show times

Je, ulikuwa unatumaini janga hili
lingekuwa limekwisha kufikia sasa?
Nafikiri sote tulitamani hivyo.
Katika maeneo fulani
idadi ya wanaoambukizwa iko chini.
Hata hivyo, katika maeneo
mengine ya ulimwengu
aina mpya zinazoambukizwa
kwa kasi zinajitokeza
na ugonjwa huu unaenea
kuliko hapo awali.
Hicho ni kikumbusho muhimu kwamba
janga hili la ugonjwa
wa corona halijakwisha.
Tunalia pamoja na wanaolia.
Na tunasali hasa kwa ajili ya
ndugu na dada zetu
walio Amerika Kusini na Afrika
ambapo kumekuwa na idadi
kubwa sana ya maambukizi
katika majuma ya karibuni.
Katika maeneo mengine ya ulimwengu
chanjo imepunguza kasi
ya kuenea kwa ugonjwa huu.
Tunafanya yote ili
kuwasaidia wanabetheli na
watumishi wengine wakati wote
wapate chanjo,
ikiwa wangependa.
Tunafurahi kutangaza kwamba
zaidi ya nusu ya
familia ya Betheli
ya ulimwenguni pote,
tayari wamepata
chanjo kufikia sasa.
Hapa nchini Marekani
zaidi ya 98% ya wanabetheli
wamechagua kupewa chanjo.
Sheria za Jimbo la New York
sasa zinawaruhusu
watu waliopata chanjo
kushiriki katika utendaji
mwingi zaidi.
Kupatana na miongozo hiyo ya serikali,
tumefaulu kuanza kurudia tena
baadhi ya utendaji
humu ndani Betheli.
Familia ya Betheli ilifurahi sana
kwamba sheria za serikali
ziliruhusu wale waliopewa chanjo
kukusanyika pamoja.
Hilo lilimaanisha tunaweza
kukusanyika ili kula kwa pamoja
kwenye chumba cha kulia chakula
na pia kwa ajili ya Funzo
la Mnara wa Mlinzi.
Ilikuwa pindi yenye kufurahisha sana
tulipokutana tena
kwa ajili ya Funzo
la Mnara wa Mlinzi.
Bila shaka, uamuzi wa kutiwa chanjo
ni wa kibinafsi.
Mkristo anapaswa kufikiria
mambo gani anapofanya uamuzi huo?
Jambo la kwanza,
tukiwa Mashahidi wa Yehova
hatuna msimamo wa kidini
unaopinga chanjo.
Jambo la pili,
tuko katikati ya
janga la ulimwenguni pote.
Kufikia Julai 9,
zaidi ya ndugu na dada 19,000
wamekufa kwa sababu ya
ugonjwa wa corona.
Jambo la tatu,
katika nchi fulani
wenye mamlaka wametunga sheria
zinazotaka raia wao wote
watiwe chanjo.
Katika nchi nyingine
wenye mamlaka hawajatunga sheria
lakini wanawatia moyo sana
raia wao watiwe chanjo.
Kila moja wetu lazima
apime mambo yote hayo
anapofanya uamuzi wake
kuhusu kutiwa chanjo.
endeleeni kuchukua tahadhari
kwa kutegemea hali
zilivyo katika eneo lenu.
Hasa ikiwa una matatizo ya afya,
au umri wako umesonga.
Endelea kujifahamisha na
habari zinazotoka kwa
wataalamu wa afya,
na uwe mwangalifu.
Katika ripoti hii ningependa
kuzungumza nanyi
wenye umri mkubwa.
Mimi mwenyewe nina umri mkubwa.
Hivi karibuni nitakuwa na
umri wa miaka 87,
nilipokuwa na umri wa miaka 20 au 30
sikuwahi kuwazia
kwamba bado ningekuwepo
nigonge 87.
Huenda baadhi yenu mnahisi hivyo pia.
Lakini ndio hawa sisi,
na kama tu Mhubiri 12 inavyosema:
“siku za taabu” zimekuja
Miili yetu imeanza kuchoka
sisi si vijana tena.
Hatuwezi kuona
wala kusikia vizuri,
tuna matatizo ya afya aina nyingi
na wakati wa janga hili
tumelazimika kukaa ndani
ya nyumba zetu
kwa muda mrefu
kuliko tulivyofikiri tungekaa.
Na huenda labda
mmoja au wawili
kati yetu amehisi kwamba
Yehova ametutupilia mbali,
kwamba hapendezwi tena na wazee
baada ya kuona
kwamba ujana wetu umeondoka.
Tunajua kwamba atatunza
na kwamba tutapata uzima wa milele
lakini sasa hivi
tunahisi ni kana kwamba
tumeachwa peke yetu.
Ningependa kuwakumbusha
jambo fulani lililo katika Biblia.
Inaonekana kwamba
pindi fulani Daudi
alihisi Yehova alikuwa amemwacha.
Hiyo ndiyo sababu alisema maneno
ambayo yameandikwa
katika Zaburi 71:9
“Usinitupe wakati wa uzee,
usiniache ninapoishiwa na nguvu.”
Lakini tunajua kwamba
Yesu alimtaja Daudi
katika mafundisho yake
kwa sababu miaka mingi baadaye,
baada ya kifo cha Daudi
Kristo alizungumza kuhusu Daudi.
Kwa hiyo, Yehova
hakumtupa Daudi kamwe,
hilo ni hakika.
Na atamkumbuka Daudi
kwa njia kubwa zaidi
kwenye ufufuo.
Naye hajamtupilia mbali
yeyote kati yetu pia.
Hata ingawa pindi fulani huenda
tukahisi amefanya hivyo.
Unajuaje hilo?
Wewe binafsi unajuaje
kwamba Yehova hajakutupilia mbali?
Acheni tufikirie hilo.
Wangapi kati yenu
mnajua Methusela alikuwa
na umri gani alipokufa?
Huenda ulijifunza hilo
miaka mingi sana iliyopita.
Unajua jibu.
Alikuwa mzee sana
ndiye mzee zaidi
kati ya watu wasio wakamilifu.
Wangapi kati yenu
mnajua Noa alikuwa na umri gani
alipoanza kazi ya kujenga safina?
Alikuwa na umri wa
zaidi ya miaka 500
Hilo linatuonyesha
Yehova anatukumbuka
hata tunapozeeka.
Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo
yanatueleza pia kumhusu
nabii wa kike, Ana.
ambaye alikuwa na
umri wa miaka 84
Tunajuaje alikuwa na miaka 84?
Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu
Ikiwa Yehova hangetaka tujue umri wake,
asingeruhusu iandikwe humo, sivyo?
Je, hilo halitufundishi jambo fulani?
Yehova anaangalia sana umri.
Naye anapendezwa
sana nasi tuliozeeka.
Zaburi ya 90
inasema mambo waziwazi
kwamba wanadamu
wasio wakamilifu
huishi kufikia
miaka 70 au 80.
Na licha ya hayo,
miaka hiyo imejaa taabu
Kwa hiyo Yehova alihakikisha
mambo yote hayo
yameandikwa ili tujue
kwamba yeye
hajatutupa mbali,
kwamba anatukumbuka sisi.
Tunajivunia ninyi nyote.
Wengi wenu mmejifunza
jinsi ya kutumia Zoom,
kuwasha mic na kuizima,
mimi bado najifunza kutumia Zoom.
Mmejifunza kutumia simu
na kuandika barua
na inapendeza kuona mmejifunza
kwa muda mfupi sana.
Ni wazi Yehova
amekuwa pamoja nanyi
naye amewapa nguvu.
Hivyo ndivyo anavyoahidi
kwenye Zaburi 29:11:
“Yehova atawapa nguvu watu wake.
Yehova atawabariki
watu wake kwa amani.”
Wakati wa janga hili lote,
tumeona uthibitisho kwamba Yehova
anaendelea kutupatia nguvu
na kutubariki kwa amani.
Hiyo ndiyo sababu
hakuna jambo lolote lililozuia
kazi ya Ufalme isiendelee.
Mfano mzuri ni kazi yetu ya
ujenzi wa kitheokrasi.
Huenda mkajiuliza
jinsi janga hili
linavyoathiri kazi ya ujenzi
inayoendelea ulimwenguni pote.
Na pia kazi inayofanywa
ili kudumisha Majumba
yetu yote ya Ufalme.
Je, kila kitu kilisimama tu ghafla?
Kwa kweli,
ugonjwa huu ulipotokea
mara ya kwanza
tulisimamisha ujenzi
uliokuwa tu unaanza
na kazi fulani za ukarabati
ili watumishi wa ujenzi
waweze kukaa ndani kwa muda.
Hangaiko letu la kwanza
lilikuwa usalama
wa maelfu ya wajitoleaji
wanaofanya kazi wakati wote
na Idara ya Usanifu-Majengo na Ujenzi.
Bila shaka,
wengi kati ya wafanyakazi hao
wanafanya kazi mbali sana
na watu wao
familia na marafiki.
Kwa hiyo, haijawa rahisi kwao
kukaa ndani.
Ni nini ambacho kimewasaidia
kukabiliana na upweke
na kutengwa kwa muda mrefu?
Sikiliza maelezo
yao katika video ifuatayo:
Akina ndugu walinifanyia
ziara za uchungaji mara nyingi
kwa kupitia mtandao.
Wakati wa ziara hizo
waliniuliza jinsi hali yangu
ilivyokuwa kimwili, kihisia, na kiroho.
Ninathamini sana kwamba
walikuwa wakinifikiria.
Na walichagua maandiko
hususa ya Biblia ili kunisomea.
Wakati wa janga hili
nilipewa mgawo
wa kusimamia kikundi cha utumishi.
Na hilo lilinipa
nafasi nyingi zaidi
za kuwasaidia
wahubiri wapya kudumisha
mazoea mazuri
ya kujifunza Biblia kibinafsi
na pia kuwazoeza akina ndugu
kufikia mapendeleo zaidi
Kwa sasa siwezi kutembelea
familia yangu kule Ulaya
lakini ninawasiliana nao
na kuwaeleza mambo
yenye kutia moyo.
Pia ninapenda kuwasaidia
vijana katika huduma
si rahisi kwao kuhubiri
wakati wa janga hili.
Lakini kuhubiri pamoja
kunatuchochea sisi sote.
Na kwa kutoa
nilipata baraka za Yehova.
Kwa mfano, ndugu na dada
wamekuwa wakinijulia mimi hali
pamoja na mume wangu
Na wametutegemza kihisia
muda huo ambao
tumehitaji kukaa ndani.
Bila wao kujua ujumbe wao
na simu wanazotupigia
zimefanya hali ikawa rahisi kwetu.
Je, uliona ni nini kilichowasaidia
kudumisha mtazamo unaofaa?
Ziara za uchungaji
zenye kutia moyo
na kuendelea kuwa na
shughuli nyingi
katika utendaji wa kiroho.
Kwa hiyo, hata ingawa
hawangeweza kufanya mengi
katika miradi ya ujenzi
katika ofisi za tawi
au ya Majumba ya Ufalme.
Wangeweza kujenga hali yao ya kiroho
na kuwatia moyo wengine
na hilo hasa ndilo jambo walilofanya.
Kumbuka, tulisema mapema
kwamba tulilazimika
kuacha kufanya kazi nyingi
za ujenzi kwa muda
kwa sababu ya ugonjwa huu
Je, hilo linamaanisha
kwamba kila kitu kilisimama?
La hasha!
Tulifaulu kushughulikia
miradi kadhaa ya
ujenzi wa ofisi za tawi.
Mfano mmoja ni ujenzi wa
ofisi ya tawi ya Argentina.
Mradi huo ulicheleweshwa
katika njia nyingi
kwa sababu ya janga hili
kwa msaada wa Yehova,
ndugu zetu waliweza kushughulikia
changamoto hizo
kwa kutumia wanakandarasi.
Na sasa familia ya Betheli
imeanza kuhamia makao mapya
wakichukua tahadhari zote
za kujilinda na COVID-19.
Wote watakuwa
wamemaliza kuhamia
katika majuma machache yanayokuja.
Lakini vikundi vyetu vingine
vya Usanifu-Majengo na Ujenzi
vimefauluje kuendelea na kazi?
Acheni tusikie kutoka kwa baadhi yao.
Dawati la Mazoezi la Idara
ya Ulimwenguni Pote
ya Usanifu-Majengo na Ujenzi
liliona umuhimu wa
kuwazoeza wote wanaoshiriki
katika miradi ya ujenzi
na udumishaji ya kitheokrasi
kuhusu kudumisha usalama.
Kwa sababu hiyo,
mtaala wa mazoezi
kuhusu usalama
kwa ajili ya wasimamizi wote
ilifanywa ulimwenguni pote.
Ndugu 7500 hivi walishiriki
kupitia video
iliyounganishwa kwenye mtandao
Ndugu mmoja kutoka
Ubelgiji alisema hivi:
“Sasa ninatambua kwamba
kudumisha usalama
ni sehemu ya hali yangu ya kiroho
Huku Afrika,
janga hili limetusaidia kuona umuhimu
wa kutayarisha Majumba yetu
ili kushughulikia usalama
wa afya ya ndugu zetu.
Tumezingatia umuhimu wa kuwa na
sehemu za kunawa mikono,
kupunguza maeneo ambayo
watu wanaweza kugusa
na mahitaji mengine
yanayohusiana na usafi yanashughulikiwa.
Idara za Usanifu-Majengo na Ujenzi
zinafanya kazi nyingi kujitayarisha
kwa ajili ya miradi ya ujenzi wakati ujao
na kufanya udumishaji
na ukarabati wa Majumba ya Ufalme.
Na katika maeneo
ambayo hali zimeruhusu
ofisi fulani za tawi
zimeweza kuanza miradi mipya
ya ujenzi
kwa kutumia watumishi
wachache sana wa ujenzi.
tunawashukuru sana ninyi nyote
wajitoleaji wa ujenzi
ambao mnaendelea
kujitoa kwa ukarimu sana
na kufanya kazi kwa bidii
katika miradi ya ujenzi
na udumishaji wa
Majumba yenu ya Ufalme.
Basi, mambo yote
haya yanatuonyesha nini?
Gari la Yehova halijasimama,
na sisi sote
vijana kwa wazee
tunataka kwenda
sambamba na gari hilo
kadiri siku zinavyosonga.
Tutaendelea nyakati zote
kuchukua tahadhari
ili kuonyesha heshima kwa uhai
huku tukiendelea na kazi ya Ufalme.
Hatujui janga hili litakwisha
wakati gani hasa,
lakini tunajua hili
Yehova ataendelea kutoa mwongozo
tunaohitaji ili kukabiliana nao.
Tungependa mjue kwamba
tunawapenda sana
na tunasali Yehova abariki
yote mnayofanya
mnapoendelea kumtumikia
kwa uaminifu.
Kutoka kwenye Makao Makuu
ya Ulimwenguni Pote
ya Mashahidi wa Yehova
hii ni
JW Broadcasting®.