00:00:01
Je, ulikuwa unatumaini janga hili00:00:03
00:00:03
lingekuwa limekwisha kufikia sasa?00:00:05
00:00:05
Nafikiri sote tulitamani hivyo.00:00:07
00:00:07
Katika maeneo fulani00:00:08
00:00:08
idadi ya wanaoambukizwa iko chini.00:00:11
00:00:11
Hata hivyo, katika maeneo
mengine ya ulimwengu00:00:14
00:00:14
aina mpya zinazoambukizwa
kwa kasi zinajitokeza00:00:17
00:00:17
na ugonjwa huu unaenea00:00:19
00:00:19
kuliko hapo awali.00:00:20
00:00:21
Hicho ni kikumbusho muhimu kwamba00:00:23
00:00:23
janga hili la ugonjwa
wa corona halijakwisha.00:00:27
00:00:28
Tunalia pamoja na wanaolia. 00:00:30
00:00:30
Na tunasali hasa kwa ajili ya00:00:33
00:00:33
ndugu na dada zetu00:00:34
00:00:34
walio Amerika Kusini na Afrika00:00:37
00:00:37
ambapo kumekuwa na idadi00:00:38
00:00:38
kubwa sana ya maambukizi00:00:40
00:00:40
katika majuma ya karibuni.00:00:42
00:00:42
Katika maeneo mengine ya ulimwengu00:00:45
00:00:45
chanjo imepunguza kasi00:00:47
00:00:47
ya kuenea kwa ugonjwa huu.00:00:49
00:00:49
Tunafanya yote ili00:00:51
00:00:51
kuwasaidia wanabetheli na00:00:53
00:00:53
watumishi wengine wakati wote
wapate chanjo,00:00:56
00:00:56
ikiwa wangependa.00:00:58
00:00:58
Tunafurahi kutangaza kwamba00:01:00
00:01:00
zaidi ya nusu ya00:01:01
00:01:01
familia ya Betheli
ya ulimwenguni pote,00:01:04
00:01:04
tayari wamepata
chanjo kufikia sasa. 00:01:06
00:01:07
Hapa nchini Marekani00:01:08
00:01:08
zaidi ya 98% ya wanabetheli00:01:12
00:01:12
wamechagua kupewa chanjo.00:01:13
00:01:14
Sheria za Jimbo la New York00:01:17
00:01:17
sasa zinawaruhusu
watu waliopata chanjo00:01:20
00:01:20
kushiriki katika utendaji
mwingi zaidi.00:01:23
00:01:24
Kupatana na miongozo hiyo ya serikali,00:01:26
00:01:26
tumefaulu kuanza kurudia tena00:01:29
00:01:29
baadhi ya utendaji00:01:30
00:01:30
humu ndani Betheli.00:01:31
00:01:32
Familia ya Betheli ilifurahi sana00:01:35
00:01:35
kwamba sheria za serikali00:01:37
00:01:37
ziliruhusu wale waliopewa chanjo00:01:39
00:01:39
kukusanyika pamoja.00:01:41
00:01:41
Hilo lilimaanisha tunaweza00:01:43
00:01:43
kukusanyika ili kula kwa pamoja00:01:45
00:01:45
kwenye chumba cha kulia chakula00:01:46
00:01:46
na pia kwa ajili ya Funzo
la Mnara wa Mlinzi.00:01:50
00:01:52
Ilikuwa pindi yenye kufurahisha sana00:01:54
00:01:54
tulipokutana tena00:01:56
00:01:56
kwa ajili ya Funzo
la Mnara wa Mlinzi.00:01:58
00:01:58
Bila shaka, uamuzi wa kutiwa chanjo00:02:01
00:02:01
ni wa kibinafsi.00:02:02
00:02:03
Mkristo anapaswa kufikiria00:02:05
00:02:05
mambo gani anapofanya uamuzi huo?00:02:07
00:02:08
Jambo la kwanza,00:02:09
00:02:09
tukiwa Mashahidi wa Yehova00:02:12
00:02:12
hatuna msimamo wa kidini
unaopinga chanjo.00:02:17
00:02:17
Jambo la pili,00:02:18
00:02:18
tuko katikati ya00:02:20
00:02:20
janga la ulimwenguni pote.00:02:21
00:02:21
Kufikia Julai 9,00:02:23
00:02:23
zaidi ya ndugu na dada 19,00000:02:26
00:02:26
wamekufa kwa sababu ya
ugonjwa wa corona. 00:02:29
00:02:30
Jambo la tatu,00:02:31
00:02:32
katika nchi fulani00:02:33
00:02:33
wenye mamlaka wametunga sheria00:02:36
00:02:36
zinazotaka raia wao wote
watiwe chanjo.00:02:39
00:02:40
Katika nchi nyingine00:02:42
00:02:42
wenye mamlaka hawajatunga sheria00:02:45
00:02:45
lakini wanawatia moyo sana00:02:47
00:02:47
raia wao watiwe chanjo.00:02:49
00:02:50
Kila moja wetu lazima00:02:52
00:02:52
apime mambo yote hayo00:02:54
00:02:54
anapofanya uamuzi wake00:02:55
00:02:55
kuhusu kutiwa chanjo.00:02:57
00:02:58
endeleeni kuchukua tahadhari00:03:01
00:03:01
kwa kutegemea hali00:03:02
00:03:02
zilivyo katika eneo lenu.00:03:04
00:03:04
Hasa ikiwa una matatizo ya afya,00:03:07
00:03:07
au umri wako umesonga. 00:03:09
00:03:09
Endelea kujifahamisha na00:03:11
00:03:11
habari zinazotoka kwa00:03:12
00:03:12
wataalamu wa afya,00:03:14
00:03:14
na uwe mwangalifu.00:03:15
00:03:15
Katika ripoti hii ningependa00:03:17
00:03:17
kuzungumza nanyi
wenye umri mkubwa. 00:03:20
00:03:20
Mimi mwenyewe nina umri mkubwa. 00:03:22
00:03:22
Hivi karibuni nitakuwa na00:03:24
00:03:24
umri wa miaka 87,00:03:26
00:03:26
nilipokuwa na umri wa miaka 20 au 3000:03:29
00:03:29
sikuwahi kuwazia00:03:31
00:03:31
kwamba bado ningekuwepo
nigonge 87.00:03:35
00:03:35
Huenda baadhi yenu mnahisi hivyo pia.00:03:37
00:03:37
Lakini ndio hawa sisi,00:03:39
00:03:39
na kama tu Mhubiri 12 inavyosema:00:03:43
00:03:43
“siku za taabu” zimekuja 00:03:46
00:03:46
Miili yetu imeanza kuchoka00:03:49
00:03:49
sisi si vijana tena.00:03:51
00:03:52
Hatuwezi kuona
wala kusikia vizuri,00:03:55
00:03:56
tuna matatizo ya afya aina nyingi00:03:59
00:04:00
na wakati wa janga hili00:04:01
00:04:01
tumelazimika kukaa ndani00:04:03
00:04:03
ya nyumba zetu00:04:05
00:04:05
kwa muda mrefu00:04:06
00:04:06
kuliko tulivyofikiri tungekaa.00:04:08
00:04:09
Na huenda labda00:04:10
00:04:10
mmoja au wawili00:04:12
00:04:12
kati yetu amehisi kwamba00:04:13
00:04:13
Yehova ametutupilia mbali,00:04:16
00:04:16
kwamba hapendezwi tena na wazee00:04:19
00:04:19
baada ya kuona
kwamba ujana wetu umeondoka.00:04:22
00:04:24
Tunajua kwamba atatunza00:04:26
00:04:26
na kwamba tutapata uzima wa milele00:04:29
00:04:29
lakini sasa hivi00:04:31
00:04:31
tunahisi ni kana kwamba00:04:33
00:04:33
tumeachwa peke yetu.00:04:35
00:04:36
Ningependa kuwakumbusha00:04:38
00:04:38
jambo fulani lililo katika Biblia.00:04:40
00:04:41
Inaonekana kwamba00:04:42
00:04:42
pindi fulani Daudi00:04:44
00:04:44
alihisi Yehova alikuwa amemwacha.00:04:47
00:04:47
Hiyo ndiyo sababu alisema maneno00:04:49
00:04:49
ambayo yameandikwa00:04:51
00:04:51
katika Zaburi 71:900:04:54
00:04:55
“Usinitupe wakati wa uzee,00:04:57
00:04:58
usiniache ninapoishiwa na nguvu.”00:05:01
00:05:02
Lakini tunajua kwamba00:05:04
00:05:04
Yesu alimtaja Daudi00:05:05
00:05:05
katika mafundisho yake00:05:07
00:05:07
kwa sababu miaka mingi baadaye,00:05:09
00:05:09
baada ya kifo cha Daudi00:05:10
00:05:10
Kristo alizungumza kuhusu Daudi.00:05:13
00:05:13
Kwa hiyo, Yehova00:05:14
00:05:14
hakumtupa Daudi kamwe,00:05:16
00:05:16
hilo ni hakika.00:05:18
00:05:18
Na atamkumbuka Daudi00:05:20
00:05:20
kwa njia kubwa zaidi
kwenye ufufuo.00:05:23
00:05:23
Naye hajamtupilia mbali00:05:25
00:05:25
yeyote kati yetu pia.00:05:27
00:05:27
Hata ingawa pindi fulani huenda00:05:29
00:05:29
tukahisi amefanya hivyo.00:05:31
00:05:32
Unajuaje hilo?00:05:34
00:05:34
Wewe binafsi unajuaje00:05:37
00:05:37
kwamba Yehova hajakutupilia mbali?00:05:39
00:05:40
Acheni tufikirie hilo.00:05:42
00:05:43
Wangapi kati yenu00:05:44
00:05:44
mnajua Methusela alikuwa
na umri gani alipokufa?00:05:48
00:05:49
Huenda ulijifunza hilo00:05:50
00:05:50
miaka mingi sana iliyopita.00:05:52
00:05:52
Unajua jibu.00:05:54
00:05:54
Alikuwa mzee sana00:05:56
00:05:56
ndiye mzee zaidi00:05:58
00:05:58
kati ya watu wasio wakamilifu.00:06:00
00:06:00
Wangapi kati yenu00:06:02
00:06:02
mnajua Noa alikuwa na umri gani00:06:04
00:06:04
alipoanza kazi ya kujenga safina?00:06:07
00:06:07
Alikuwa na umri wa00:06:09
00:06:09
zaidi ya miaka 50000:06:12
00:06:12
Hilo linatuonyesha00:06:14
00:06:14
Yehova anatukumbuka00:06:16
00:06:16
hata tunapozeeka.00:06:18
00:06:18
Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo00:06:20
00:06:20
yanatueleza pia kumhusu00:06:22
00:06:22
nabii wa kike, Ana.00:06:23
00:06:23
ambaye alikuwa na00:06:25
00:06:25
umri wa miaka 8400:06:26
00:06:26
Tunajuaje alikuwa na miaka 84?00:06:29
00:06:29
Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu00:06:32
00:06:32
Ikiwa Yehova hangetaka tujue umri wake,00:06:35
00:06:35
asingeruhusu iandikwe humo, sivyo?00:06:38
00:06:39
Je, hilo halitufundishi jambo fulani?00:06:42
00:06:42
Yehova anaangalia sana umri.00:06:45
00:06:46
Naye anapendezwa
sana nasi tuliozeeka.00:06:49
00:06:49
Zaburi ya 9000:06:51
00:06:51
inasema mambo waziwazi00:06:53
00:06:53
kwamba wanadamu
wasio wakamilifu00:06:55
00:06:55
huishi kufikia
miaka 70 au 80.00:06:58
00:06:58
Na licha ya hayo,00:07:00
00:07:00
miaka hiyo imejaa taabu00:07:02
00:07:03
Kwa hiyo Yehova alihakikisha00:07:05
00:07:05
mambo yote hayo00:07:06
00:07:06
yameandikwa ili tujue00:07:08
00:07:08
kwamba yeye00:07:09
00:07:09
hajatutupa mbali,00:07:12
00:07:12
kwamba anatukumbuka sisi.00:07:15
00:07:16
Tunajivunia ninyi nyote.00:07:19
00:07:19
Wengi wenu mmejifunza00:07:21
00:07:21
jinsi ya kutumia Zoom,00:07:22
00:07:22
kuwasha mic na kuizima,00:07:25
00:07:25
mimi bado najifunza kutumia Zoom.00:07:27
00:07:27
Mmejifunza kutumia simu00:07:30
00:07:30
na kuandika barua00:07:31
00:07:31
na inapendeza kuona mmejifunza00:07:33
00:07:33
kwa muda mfupi sana.00:07:34
00:07:35
Ni wazi Yehova00:07:36
00:07:36
amekuwa pamoja nanyi00:07:37
00:07:37
naye amewapa nguvu.00:07:39
00:07:39
Hivyo ndivyo anavyoahidi00:07:41
00:07:41
kwenye Zaburi 29:11:00:07:46
00:07:46
“Yehova atawapa nguvu watu wake.00:07:49
00:07:49
Yehova atawabariki00:07:50
00:07:50
watu wake kwa amani.”00:07:52
00:07:52
Wakati wa janga hili lote,00:07:55
00:07:55
tumeona uthibitisho kwamba Yehova00:07:57
00:07:57
anaendelea kutupatia nguvu00:07:59
00:07:59
na kutubariki kwa amani.00:08:02
00:08:02
Hiyo ndiyo sababu00:08:03
00:08:03
hakuna jambo lolote lililozuia00:08:05
00:08:05
kazi ya Ufalme isiendelee.00:08:07
00:08:07
Mfano mzuri ni kazi yetu ya00:08:09
00:08:09
ujenzi wa kitheokrasi.00:08:11
00:08:12
Huenda mkajiuliza00:08:14
00:08:14
jinsi janga hili
linavyoathiri kazi ya ujenzi00:08:17
00:08:17
inayoendelea ulimwenguni pote.00:08:19
00:08:19
Na pia kazi inayofanywa00:08:21
00:08:21
ili kudumisha Majumba00:08:22
00:08:22
yetu yote ya Ufalme.00:08:24
00:08:24
Je, kila kitu kilisimama tu ghafla?00:08:27
00:08:28
Kwa kweli,00:08:29
00:08:29
ugonjwa huu ulipotokea00:08:31
00:08:31
mara ya kwanza00:08:32
00:08:32
tulisimamisha ujenzi00:08:34
00:08:34
uliokuwa tu unaanza00:08:35
00:08:35
na kazi fulani za ukarabati00:08:37
00:08:37
ili watumishi wa ujenzi00:08:39
00:08:39
waweze kukaa ndani kwa muda.00:08:42
00:08:42
Hangaiko letu la kwanza
lilikuwa usalama00:08:45
00:08:45
wa maelfu ya wajitoleaji00:08:47
00:08:47
wanaofanya kazi wakati wote00:08:49
00:08:49
na Idara ya Usanifu-Majengo na Ujenzi.00:08:52
00:08:52
Bila shaka,
wengi kati ya wafanyakazi hao00:08:54
00:08:54
wanafanya kazi mbali sana00:08:57
00:08:57
na watu wao
familia na marafiki.00:08:59
00:08:59
Kwa hiyo, haijawa rahisi kwao
kukaa ndani.00:09:03
00:09:03
Ni nini ambacho kimewasaidia00:09:05
00:09:05
kukabiliana na upweke00:09:07
00:09:07
na kutengwa kwa muda mrefu?00:09:09
00:09:10
Sikiliza maelezo
yao katika video ifuatayo:00:09:13
00:09:15
Akina ndugu walinifanyia00:09:16
00:09:16
ziara za uchungaji mara nyingi00:09:18
00:09:18
kwa kupitia mtandao.00:09:19
00:09:19
Wakati wa ziara hizo
waliniuliza jinsi hali yangu00:09:23
00:09:23
ilivyokuwa kimwili, kihisia, na kiroho.00:09:28
00:09:28
Ninathamini sana kwamba00:09:30
00:09:30
walikuwa wakinifikiria.00:09:32
00:09:32
Na walichagua maandiko00:09:34
00:09:34
hususa ya Biblia ili kunisomea.00:09:36
00:09:37
Wakati wa janga hili00:09:39
00:09:39
nilipewa mgawo00:09:40
00:09:40
wa kusimamia kikundi cha utumishi.00:09:42
00:09:42
Na hilo lilinipa00:09:43
00:09:43
nafasi nyingi zaidi00:09:45
00:09:45
za kuwasaidia00:09:46
00:09:46
wahubiri wapya kudumisha00:09:48
00:09:48
mazoea mazuri00:09:49
00:09:49
ya kujifunza Biblia kibinafsi00:09:51
00:09:51
na pia kuwazoeza akina ndugu00:09:53
00:09:53
kufikia mapendeleo zaidi00:09:55
00:09:55
Kwa sasa siwezi kutembelea00:09:56
00:09:56
familia yangu kule Ulaya00:09:58
00:09:58
lakini ninawasiliana nao00:10:00
00:10:00
na kuwaeleza mambo00:10:00
00:10:00
yenye kutia moyo.00:10:02
00:10:02
Pia ninapenda kuwasaidia00:10:03
00:10:03
vijana katika huduma00:10:05
00:10:05
si rahisi kwao kuhubiri00:10:07
00:10:07
wakati wa janga hili.00:10:08
00:10:08
Lakini kuhubiri pamoja00:10:10
00:10:10
kunatuchochea sisi sote.00:10:12
00:10:12
Na kwa kutoa
nilipata baraka za Yehova.00:10:15
00:10:15
Kwa mfano, ndugu na dada00:10:17
00:10:17
wamekuwa wakinijulia mimi hali00:10:18
00:10:18
pamoja na mume wangu00:10:20
00:10:20
Na wametutegemza kihisia00:10:21
00:10:21
muda huo ambao00:10:22
00:10:22
tumehitaji kukaa ndani.00:10:23
00:10:23
Bila wao kujua ujumbe wao00:10:26
00:10:26
na simu wanazotupigia00:10:27
00:10:27
zimefanya hali ikawa rahisi kwetu.00:10:30
00:10:31
Je, uliona ni nini kilichowasaidia00:10:33
00:10:33
kudumisha mtazamo unaofaa?00:10:35
00:10:36
Ziara za uchungaji00:10:37
00:10:37
zenye kutia moyo00:10:39
00:10:39
na kuendelea kuwa na00:10:40
00:10:40
shughuli nyingi
katika utendaji wa kiroho.00:10:42
00:10:42
Kwa hiyo, hata ingawa00:10:43
00:10:43
hawangeweza kufanya mengi00:10:45
00:10:45
katika miradi ya ujenzi00:10:46
00:10:46
katika ofisi za tawi00:10:47
00:10:47
au ya Majumba ya Ufalme.00:10:49
00:10:49
Wangeweza kujenga hali yao ya kiroho00:10:52
00:10:52
na kuwatia moyo wengine00:10:54
00:10:54
na hilo hasa ndilo jambo walilofanya.00:10:57
00:10:58
Kumbuka, tulisema mapema00:11:00
00:11:00
kwamba tulilazimika00:11:02
00:11:02
kuacha kufanya kazi nyingi00:11:04
00:11:04
za ujenzi kwa muda00:11:05
00:11:05
kwa sababu ya ugonjwa huu00:11:07
00:11:07
Je, hilo linamaanisha
kwamba kila kitu kilisimama?00:11:10
00:11:11
La hasha!00:11:12
00:11:12
Tulifaulu kushughulikia00:11:15
00:11:15
miradi kadhaa ya
ujenzi wa ofisi za tawi.00:11:17
00:11:18
Mfano mmoja ni ujenzi wa00:11:20
00:11:20
ofisi ya tawi ya Argentina.00:11:22
00:11:23
Mradi huo ulicheleweshwa00:11:25
00:11:25
katika njia nyingi00:11:26
00:11:26
kwa sababu ya janga hili00:11:28
00:11:28
kwa msaada wa Yehova,00:11:29
00:11:29
ndugu zetu waliweza kushughulikia00:11:31
00:11:31
changamoto hizo00:11:33
00:11:33
kwa kutumia wanakandarasi.00:11:35
00:11:35
Na sasa familia ya Betheli00:11:37
00:11:37
imeanza kuhamia makao mapya00:11:39
00:11:39
wakichukua tahadhari zote00:11:41
00:11:41
za kujilinda na COVID-19.00:11:44
00:11:44
Wote watakuwa
wamemaliza kuhamia00:11:47
00:11:47
katika majuma machache yanayokuja.00:11:49
00:11:50
Lakini vikundi vyetu vingine00:11:52
00:11:53
vya Usanifu-Majengo na Ujenzi00:11:55
00:11:55
vimefauluje kuendelea na kazi?00:11:57
00:11:58
Acheni tusikie kutoka kwa baadhi yao.00:12:01
00:12:02
Dawati la Mazoezi la Idara
ya Ulimwenguni Pote00:12:05
00:12:05
ya Usanifu-Majengo na Ujenzi00:12:07
00:12:07
liliona umuhimu wa00:12:08
00:12:08
kuwazoeza wote wanaoshiriki00:12:10
00:12:10
katika miradi ya ujenzi00:12:11
00:12:11
na udumishaji ya kitheokrasi00:12:13
00:12:13
kuhusu kudumisha usalama.00:12:15
00:12:15
Kwa sababu hiyo,00:12:16
00:12:16
mtaala wa mazoezi00:12:17
00:12:17
kuhusu usalama00:12:18
00:12:18
kwa ajili ya wasimamizi wote00:12:20
00:12:20
ilifanywa ulimwenguni pote.00:12:22
00:12:22
Ndugu 7500 hivi walishiriki00:12:24
00:12:24
kupitia video00:12:25
00:12:25
iliyounganishwa kwenye mtandao00:12:27
00:12:27
Ndugu mmoja kutoka00:12:28
00:12:28
Ubelgiji alisema hivi:00:12:30
00:12:30
“Sasa ninatambua kwamba00:12:31
00:12:31
kudumisha usalama00:12:32
00:12:32
ni sehemu ya hali yangu ya kiroho00:12:34
00:12:35
Huku Afrika,00:12:36
00:12:36
janga hili limetusaidia kuona umuhimu00:12:38
00:12:38
wa kutayarisha Majumba yetu00:12:40
00:12:40
ili kushughulikia usalama00:12:42
00:12:42
wa afya ya ndugu zetu.00:12:43
00:12:43
Tumezingatia umuhimu wa kuwa na00:12:46
00:12:46
sehemu za kunawa mikono,00:12:47
00:12:47
kupunguza maeneo ambayo 00:12:49
00:12:49
watu wanaweza kugusa00:12:50
00:12:50
na mahitaji mengine00:12:51
00:12:51
yanayohusiana na usafi yanashughulikiwa.00:12:54
00:12:55
Idara za Usanifu-Majengo na Ujenzi00:12:58
00:12:58
zinafanya kazi nyingi kujitayarisha00:13:00
00:13:00
kwa ajili ya miradi ya ujenzi wakati ujao 00:13:03
00:13:03
na kufanya udumishaji00:13:04
00:13:04
na ukarabati wa Majumba ya Ufalme.00:13:07
00:13:08
Na katika maeneo00:13:09
00:13:09
ambayo hali zimeruhusu00:13:11
00:13:11
ofisi fulani za tawi00:13:12
00:13:12
zimeweza kuanza miradi mipya00:13:14
00:13:14
ya ujenzi00:13:15
00:13:15
kwa kutumia watumishi00:13:16
00:13:16
wachache sana wa ujenzi.00:13:19
00:13:19
tunawashukuru sana ninyi nyote00:13:21
00:13:21
wajitoleaji wa ujenzi00:13:23
00:13:24
ambao mnaendelea00:13:25
00:13:25
kujitoa kwa ukarimu sana00:13:27
00:13:27
na kufanya kazi kwa bidii00:13:29
00:13:29
katika miradi ya ujenzi00:13:31
00:13:31
na udumishaji wa00:13:32
00:13:32
Majumba yenu ya Ufalme.00:13:34
00:13:34
Basi, mambo yote00:13:35
00:13:35
haya yanatuonyesha nini?00:13:37
00:13:38
Gari la Yehova halijasimama,00:13:40
00:13:41
na sisi sote00:13:42
00:13:43
vijana kwa wazee00:13:45
00:13:45
tunataka kwenda
sambamba na gari hilo00:13:48
00:13:48
kadiri siku zinavyosonga.00:13:50
00:13:50
Tutaendelea nyakati zote00:13:52
00:13:52
kuchukua tahadhari00:13:54
00:13:54
ili kuonyesha heshima kwa uhai00:13:56
00:13:56
huku tukiendelea na kazi ya Ufalme.00:13:59
00:14:00
Hatujui janga hili litakwisha00:14:03
00:14:03
wakati gani hasa,00:14:04
00:14:05
lakini tunajua hili00:14:07
00:14:08
Yehova ataendelea kutoa mwongozo00:14:12
00:14:12
tunaohitaji ili kukabiliana nao.00:14:15
00:14:17
Tungependa mjue kwamba00:14:18
00:14:18
tunawapenda sana00:14:20
00:14:20
na tunasali Yehova abariki00:14:22
00:14:22
yote mnayofanya00:14:24
00:14:24
mnapoendelea kumtumikia00:14:26
00:14:26
kwa uaminifu.00:14:27
00:14:27
Kutoka kwenye Makao Makuu00:14:29
00:14:29
ya Ulimwenguni Pote
ya Mashahidi wa Yehova00:14:32
00:14:32
hii ni
JW Broadcasting®.00:14:35
Ripoti ya 6 ya Baraza Linaloongoza la 2021
-
Ripoti ya 6 ya Baraza Linaloongoza la 2021
Je, ulikuwa unatumaini janga hili
lingekuwa limekwisha kufikia sasa?
Nafikiri sote tulitamani hivyo.
Katika maeneo fulani
idadi ya wanaoambukizwa iko chini.
Hata hivyo, katika maeneo
mengine ya ulimwengu
aina mpya zinazoambukizwa
kwa kasi zinajitokeza
na ugonjwa huu unaenea
kuliko hapo awali.
Hicho ni kikumbusho muhimu kwamba
janga hili la ugonjwa
wa corona halijakwisha.
Tunalia pamoja na wanaolia.
Na tunasali hasa kwa ajili ya
ndugu na dada zetu
walio Amerika Kusini na Afrika
ambapo kumekuwa na idadi
kubwa sana ya maambukizi
katika majuma ya karibuni.
Katika maeneo mengine ya ulimwengu
chanjo imepunguza kasi
ya kuenea kwa ugonjwa huu.
Tunafanya yote ili
kuwasaidia wanabetheli na
watumishi wengine wakati wote
wapate chanjo,
ikiwa wangependa.
Tunafurahi kutangaza kwamba
zaidi ya nusu ya
familia ya Betheli
ya ulimwenguni pote,
tayari wamepata
chanjo kufikia sasa.
Hapa nchini Marekani
zaidi ya 98% ya wanabetheli
wamechagua kupewa chanjo.
Sheria za Jimbo la New York
sasa zinawaruhusu
watu waliopata chanjo
kushiriki katika utendaji
mwingi zaidi.
Kupatana na miongozo hiyo ya serikali,
tumefaulu kuanza kurudia tena
baadhi ya utendaji
humu ndani Betheli.
Familia ya Betheli ilifurahi sana
kwamba sheria za serikali
ziliruhusu wale waliopewa chanjo
kukusanyika pamoja.
Hilo lilimaanisha tunaweza
kukusanyika ili kula kwa pamoja
kwenye chumba cha kulia chakula
na pia kwa ajili ya Funzo
la <i>Mnara wa Mlinzi.</i>
Ilikuwa pindi yenye kufurahisha sana
tulipokutana tena
kwa ajili ya Funzo
la <i>Mnara wa Mlinzi.</i>
Bila shaka, uamuzi wa kutiwa chanjo
ni wa kibinafsi.
Mkristo anapaswa kufikiria
mambo gani anapofanya uamuzi huo?
Jambo la kwanza,
tukiwa Mashahidi wa Yehova
hatuna msimamo wa kidini
unaopinga chanjo.
Jambo la pili,
tuko katikati ya
janga la ulimwenguni pote.
Kufikia Julai 9,
zaidi ya ndugu na dada 19,000
wamekufa kwa sababu ya
ugonjwa wa corona.
Jambo la tatu,
katika nchi fulani
wenye mamlaka wametunga sheria
zinazotaka raia wao wote
watiwe chanjo.
Katika nchi nyingine
wenye mamlaka hawajatunga sheria
lakini wanawatia moyo sana
raia wao watiwe chanjo.
Kila moja wetu lazima
apime mambo yote hayo
anapofanya uamuzi wake
kuhusu kutiwa chanjo.
endeleeni kuchukua tahadhari
kwa kutegemea hali
zilivyo katika eneo lenu.
Hasa ikiwa una matatizo ya afya,
au umri wako umesonga.
Endelea kujifahamisha na
habari zinazotoka kwa
wataalamu wa afya,
na uwe mwangalifu.
Katika ripoti hii ningependa
kuzungumza nanyi
wenye umri mkubwa.
Mimi mwenyewe nina umri mkubwa.
Hivi karibuni nitakuwa na
umri wa miaka 87,
nilipokuwa na umri wa miaka 20 au 30
sikuwahi kuwazia
kwamba bado ningekuwepo
nigonge 87.
Huenda baadhi yenu mnahisi hivyo pia.
Lakini ndio hawa sisi,
na kama tu Mhubiri 12 inavyosema:
“siku za taabu” zimekuja
Miili yetu imeanza kuchoka
sisi si vijana tena.
Hatuwezi kuona
wala kusikia vizuri,
tuna matatizo ya afya aina nyingi
na wakati wa janga hili
tumelazimika kukaa ndani
ya nyumba zetu
kwa muda mrefu
kuliko tulivyofikiri tungekaa.
Na huenda labda
mmoja au wawili
kati yetu amehisi kwamba
Yehova ametutupilia mbali,
kwamba hapendezwi tena na wazee
baada ya kuona
kwamba ujana wetu umeondoka.
Tunajua kwamba atatunza
na kwamba tutapata uzima wa milele
lakini sasa hivi
tunahisi ni kana kwamba
tumeachwa peke yetu.
Ningependa kuwakumbusha
jambo fulani lililo katika Biblia.
Inaonekana kwamba
pindi fulani Daudi
alihisi Yehova alikuwa amemwacha.
Hiyo ndiyo sababu alisema maneno
ambayo yameandikwa
katika Zaburi 71:9
“Usinitupe wakati wa uzee,
usiniache ninapoishiwa na nguvu.”
Lakini tunajua kwamba
Yesu alimtaja Daudi
katika mafundisho yake
kwa sababu miaka mingi baadaye,
baada ya kifo cha Daudi
Kristo alizungumza kuhusu Daudi.
Kwa hiyo, Yehova
hakumtupa Daudi kamwe,
hilo ni hakika.
Na atamkumbuka Daudi
kwa njia kubwa zaidi
kwenye ufufuo.
Naye hajamtupilia mbali
yeyote kati yetu pia.
Hata ingawa pindi fulani huenda
tukahisi amefanya hivyo.
Unajuaje hilo?
Wewe binafsi unajuaje
kwamba Yehova hajakutupilia mbali?
Acheni tufikirie hilo.
Wangapi kati yenu
mnajua Methusela alikuwa
na umri gani alipokufa?
Huenda ulijifunza hilo
miaka mingi sana iliyopita.
Unajua jibu.
Alikuwa mzee sana
ndiye mzee zaidi
kati ya watu wasio wakamilifu.
Wangapi kati yenu
mnajua Noa alikuwa na umri gani
alipoanza kazi ya kujenga safina?
Alikuwa na umri wa
zaidi ya miaka 500
Hilo linatuonyesha
Yehova anatukumbuka
hata tunapozeeka.
Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo
yanatueleza pia kumhusu
nabii wa kike, Ana.
ambaye alikuwa na
umri wa miaka 84
Tunajuaje alikuwa na miaka 84?
Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu
Ikiwa Yehova hangetaka tujue umri wake,
asingeruhusu iandikwe humo, sivyo?
Je, hilo halitufundishi jambo fulani?
Yehova anaangalia sana umri.
Naye anapendezwa
sana nasi tuliozeeka.
Zaburi ya 90
inasema mambo waziwazi
kwamba wanadamu
wasio wakamilifu
huishi kufikia
miaka 70 au 80.
Na licha ya hayo,
miaka hiyo imejaa taabu
Kwa hiyo Yehova alihakikisha
mambo yote hayo
yameandikwa ili tujue
kwamba yeye
hajatutupa mbali,
kwamba anatukumbuka sisi.
Tunajivunia ninyi nyote.
Wengi wenu mmejifunza
jinsi ya kutumia <i>Zoom</i>,
kuwasha <i>mic</i> na kuizima,
mimi bado najifunza kutumia <i>Zoom</i>.
Mmejifunza kutumia simu
na kuandika barua
na inapendeza kuona mmejifunza
kwa muda mfupi sana.
Ni wazi Yehova
amekuwa pamoja nanyi
naye amewapa nguvu.
Hivyo ndivyo anavyoahidi
kwenye Zaburi 29:11:
“Yehova atawapa nguvu watu wake.
Yehova atawabariki
watu wake kwa amani.”
Wakati wa janga hili lote,
tumeona uthibitisho kwamba Yehova
anaendelea kutupatia nguvu
na kutubariki kwa amani.
Hiyo ndiyo sababu
hakuna jambo lolote lililozuia
kazi ya Ufalme isiendelee.
Mfano mzuri ni kazi yetu ya
ujenzi wa kitheokrasi.
Huenda mkajiuliza
jinsi janga hili
linavyoathiri kazi ya ujenzi
inayoendelea ulimwenguni pote.
Na pia kazi inayofanywa
ili kudumisha Majumba
yetu yote ya Ufalme.
Je, kila kitu kilisimama tu ghafla?
Kwa kweli,
ugonjwa huu ulipotokea
mara ya kwanza
tulisimamisha ujenzi
uliokuwa tu unaanza
na kazi fulani za ukarabati
ili watumishi wa ujenzi
waweze kukaa ndani kwa muda.
Hangaiko letu la kwanza
lilikuwa usalama
wa maelfu ya wajitoleaji
wanaofanya kazi wakati wote
na Idara ya Usanifu-Majengo na Ujenzi.
Bila shaka,
wengi kati ya wafanyakazi hao
wanafanya kazi mbali sana
na watu wao
familia na marafiki.
Kwa hiyo, haijawa rahisi kwao
kukaa ndani.
Ni nini ambacho kimewasaidia
kukabiliana na upweke
na kutengwa kwa muda mrefu?
Sikiliza maelezo
yao katika video ifuatayo:
Akina ndugu walinifanyia
ziara za uchungaji mara nyingi
kwa kupitia mtandao.
Wakati wa ziara hizo
waliniuliza jinsi hali yangu
ilivyokuwa kimwili, kihisia, na kiroho.
Ninathamini sana kwamba
walikuwa wakinifikiria.
Na walichagua maandiko
hususa ya Biblia ili kunisomea.
Wakati wa janga hili
nilipewa mgawo
wa kusimamia kikundi cha utumishi.
Na hilo lilinipa
nafasi nyingi zaidi
za kuwasaidia
wahubiri wapya kudumisha
mazoea mazuri
ya kujifunza Biblia kibinafsi
na pia kuwazoeza akina ndugu
kufikia mapendeleo zaidi
Kwa sasa siwezi kutembelea
familia yangu kule Ulaya
lakini ninawasiliana nao
na kuwaeleza mambo
yenye kutia moyo.
Pia ninapenda kuwasaidia
vijana katika huduma
si rahisi kwao kuhubiri
wakati wa janga hili.
Lakini kuhubiri pamoja
kunatuchochea sisi sote.
Na kwa kutoa
nilipata baraka za Yehova.
Kwa mfano, ndugu na dada
wamekuwa wakinijulia mimi hali
pamoja na mume wangu
Na wametutegemza kihisia
muda huo ambao
tumehitaji kukaa ndani.
Bila wao kujua ujumbe wao
na simu wanazotupigia
zimefanya hali ikawa rahisi kwetu.
Je, uliona ni nini kilichowasaidia
kudumisha mtazamo unaofaa?
Ziara za uchungaji
zenye kutia moyo
na kuendelea kuwa na
shughuli nyingi
katika utendaji wa kiroho.
Kwa hiyo, hata ingawa
hawangeweza kufanya mengi
katika miradi ya ujenzi
katika ofisi za tawi
au ya Majumba ya Ufalme.
Wangeweza kujenga hali yao ya kiroho
na kuwatia moyo wengine
na hilo hasa ndilo jambo walilofanya.
Kumbuka, tulisema mapema
kwamba tulilazimika
kuacha kufanya kazi nyingi
za ujenzi kwa muda
kwa sababu ya ugonjwa huu
Je, hilo linamaanisha
kwamba kila kitu kilisimama?
La hasha!
Tulifaulu kushughulikia
miradi kadhaa ya
ujenzi wa ofisi za tawi.
Mfano mmoja ni ujenzi wa
ofisi ya tawi ya Argentina.
Mradi huo ulicheleweshwa
katika njia nyingi
kwa sababu ya janga hili
kwa msaada wa Yehova,
ndugu zetu waliweza kushughulikia
changamoto hizo
kwa kutumia wanakandarasi.
Na sasa familia ya Betheli
imeanza kuhamia makao mapya
wakichukua tahadhari zote
za kujilinda na COVID-19.
Wote watakuwa
wamemaliza kuhamia
katika majuma machache yanayokuja.
Lakini vikundi vyetu vingine
vya Usanifu-Majengo na Ujenzi
vimefauluje kuendelea na kazi?
Acheni tusikie kutoka kwa baadhi yao.
Dawati la Mazoezi la Idara
ya Ulimwenguni Pote
ya Usanifu-Majengo na Ujenzi
liliona umuhimu wa
kuwazoeza wote wanaoshiriki
katika miradi ya ujenzi
na udumishaji ya kitheokrasi
kuhusu kudumisha usalama.
Kwa sababu hiyo,
mtaala wa mazoezi
kuhusu usalama
kwa ajili ya wasimamizi wote
ilifanywa ulimwenguni pote.
Ndugu 7500 hivi walishiriki
kupitia video
iliyounganishwa kwenye mtandao
Ndugu mmoja kutoka
Ubelgiji alisema hivi:
“Sasa ninatambua kwamba
kudumisha usalama
ni sehemu ya hali yangu ya kiroho
Huku Afrika,
janga hili limetusaidia kuona umuhimu
wa kutayarisha Majumba yetu
ili kushughulikia usalama
wa afya ya ndugu zetu.
Tumezingatia umuhimu wa kuwa na
sehemu za kunawa mikono,
kupunguza maeneo ambayo
watu wanaweza kugusa
na mahitaji mengine
yanayohusiana na usafi yanashughulikiwa.
Idara za Usanifu-Majengo na Ujenzi
zinafanya kazi nyingi kujitayarisha
kwa ajili ya miradi ya ujenzi wakati ujao
na kufanya udumishaji
na ukarabati wa Majumba ya Ufalme.
Na katika maeneo
ambayo hali zimeruhusu
ofisi fulani za tawi
zimeweza kuanza miradi mipya
ya ujenzi
kwa kutumia watumishi
wachache sana wa ujenzi.
tunawashukuru sana ninyi nyote
wajitoleaji wa ujenzi
ambao mnaendelea
kujitoa kwa ukarimu sana
na kufanya kazi kwa bidii
katika miradi ya ujenzi
na udumishaji wa
Majumba yenu ya Ufalme.
Basi, mambo yote
haya yanatuonyesha nini?
Gari la Yehova halijasimama,
na sisi sote
vijana kwa wazee
tunataka kwenda
sambamba na gari hilo
kadiri siku zinavyosonga.
Tutaendelea nyakati zote
kuchukua tahadhari
ili kuonyesha heshima kwa uhai
huku tukiendelea na kazi ya Ufalme.
Hatujui janga hili litakwisha
wakati gani hasa,
lakini tunajua hili
Yehova ataendelea kutoa mwongozo
tunaohitaji ili kukabiliana nao.
Tungependa mjue kwamba
tunawapenda sana
na tunasali Yehova abariki
yote mnayofanya
mnapoendelea kumtumikia
kwa uaminifu.
Kutoka kwenye Makao Makuu
ya Ulimwenguni Pote
ya Mashahidi wa Yehova
hii ni
JW Broadcasting®.
-