JW subtitle extractor

Ripoti ya 8 ya Baraza Linaloongoza ya 2021

Video Other languages Share text Share link Show times

Ndugu wapendwa,
akina dada,
watoto waaminifu,
na marafiki wapendwa,
ni furaha kubwa kuwa
pamoja nanyi kwa ajili ya
ripoti hii.
Tuna mambo mengi
sana mazuri ya
kuwaeleza kutia ndani
ripoti kuhusu jinsi ambavyo
tumeshughulikia misiba
ya asili
na mwishoni mwa ripoti hii
tutafurahi sana
kuwajulisha andiko
la mwaka lenye kujenga sana
kwa ajili ya mwaka wa 2022.
Hata hivyo,
ningependa kuanza
kwa kueleza mambo
fulani muhimu kuhusu
chanjo
ya COVID-19.
Kwa sababu
tunawapenda sana
na kwa sababu hili
ni suala linaloweza
kuokoa uhai
tumeamua kuwaeleza
mambo tunayofahamu
kuhusu hili.
Kuanzia Juni 1,
nchini Marekani
wahubiri 1,407
wamelazwa hospitalini
kwa sababu ya COVID-19
au dalili zake.
Kati yao
zaidi ya asilimia 99
hawakuwa wamepata
chanjo kamili.
Kwa kusikitisha katika
kipindi hicho hicho
nchini Marekani,
ndugu 486
walikufa kutokana
na ugonjwa wa COVID-19.
Kati yao,
zaidi ya asilimia 99
hawakuwa wamepata
chanjo kamili.
Na habari tulizopata
waliokufa ambao walikuwa
wamepata chanjo kamili
walikuwa na matatizo mengine
mabaya sana ya afya.
Takwimu hizo
ni zenye kuchochea
fikira sana.
Tunaweza pia kuwajulisha
kwamba kati ya
Wanabetheli 22,000
na watumishi wa wakati wote
wa pekee, 44,000
walio shambani
ambao wamepewa chanjo,
tumejulishwa kwamba
ni 4 tu kati yao
ambao walipata matatizo fulani
yanayohusiana
na chanjo hiyo.
Lakini kwa kupendeza
imeripotiwa kwamba
afya yao iko salama
na kwamba wanaendelea
kupata nafuu.
Tunawajulisha habari hizi zote
ili mzifikirie kwa makini
mnapofanya uamuzi
wenu wenyewe
kuhusiana na kupata
chanjo.
Tunahisi lisingekuwa
jambo lenye upendo
ikiwa tungewanyima
habari zote hizi muhimu.
Kama andiko la
Methali 3:27 linavyosema:
“Usiwanyime mema
wale unaopaswa kuwatendea mema.”
Tunajua inaweza kuwa vigumu
kufanya uamuzi wa hekima
kunapokuwa na maoni tofauti-tofauti.
Na ripoti zinazopingana
zinazotolewa katika ulimwengu.
Na huenda hilo
likafanya iwe vigumu
kujua uamini nini.
Lakini takwimu tulizotaja
zimekusanywa
na ndugu zetu.
Kwa hiyo tunaweza
kuamini takwimu hizo.
Tunatumaini
zitakuwa na manufaa kwenu.
Tunatambua kwamba
huo si uchunguzi
uliofanywa na wanasayansi
lakini tunaweza kuwajulisha
kile ambacho
ndugu zetu wameona.
Na kwa sababu tuna habari hizo
tungependa nyinyi pia mjue
tunachojua sisi.
Bila shaka, lazima pia
tuzingatie mwongozo
unaotolewa na wenye mamlaka.
Katika nchi fulani,
serikali zimeanza kutoa sheria
kwamba raia wao wote
wanapaswa kupata chanjo.
Katika maeneo mengi
wanachochewa sana.
Sisi tunatendaje tunapopata
mwongozo huo?
Kitabu “Dumu Katika Upendo
wa Mungu”
kimetaja jambo muhimu.
Kiliposema hivi:
“Leo, Yehova ameruhusu serikali
ziwe na mamlaka fulani
nasi tunapaswa kuziheshimu
zinafanya mipango
katika nchi na jamii
ili shughuli ziendeshwe
kwa njia inayofaa
na watu wapate
huduma za lazima.
Wakristo wanatii agizo lililo
katika Waroma 13:1-7.
Tunaheshimu
‘mamlaka zilizo kubwa’
na kutii sheria za nchi
au jamii tunamoishi.”
Huenda sheria hizo zikaathiri
familia yetu,
biashara yetu,
au mali zetu.
Mbali na hilo,
habari za utafiti
kwenye Waroma 13:5
zinasema hivi:
“Mkristo hujitiisha
kwa serikali za wanadamu
wakati amri inayotolewa
haipingi sheria za Mungu.”
Basi hilo ni jambo
lingine muhimu sana
ambalo kila mmoja wetu
anapaswa kufikiria kwa uzito
na kupitia sala
anapofanya uamuzi.
Kwa kuwa sasa,
zaidi ya asilimia 99 ya
familia ya betheli ya Marekani
imepata chanjo kamili.
Tumefaulu kuruhusu
utendaji mwingi zaidi
ndani ya Betheli
kupatana na maagizo
ya jimbo la New York.
Hilo liliwezesha familia ya Betheli
kula mlo pamoja na
wahitimu wa Gileadi
halafu Septemba 11,
kukawa na kuhitimu
kwa shule ya Gileadi.
Wageni kutoka nje ya Betheli
hawakuruhusiwa kuwepo
kwenye matukio hayo.
Pia,
Wanabetheli ambao wamepata
chanjo kamili nchini Marekani
walipewa ruhusa
ya kuchukua
Muda wa Kibinafsi
ili kuwatembelea
watu wa familia
na marafiki.
Wakizingatia miongozo ya
kujilinda na covid-19
wanapokuwa nje ya Betheli.
Kwa kweli,
kufikia Septemba 24,
zaidi Wanabetheli 3,975
ambao wamepata chanjo kamili,
nchini Marekani,
wameweza kusafiri
katika miezi ya Agosti
na Septemba.
Baada ya kurudi Betheli
wanaweka katika aina
ya karantini
ambayo si kufungiwa kabisa
na siku chache baadaye
wanapimwa ikiwa wana COVID-19.
Kati ya hao 3,975
walioambukizwa
ni wanne tu kati yao.
Wawili
waliambukizwa kwa
kadiri ndogo eneo waliloenda
na walipata nafuu
kabla ya kurudi Betheli.
Wale wengine wawili
ambao waligunduliwa
kuwa wameambukizwa
baada ya kurudi,
walilkuwa na dalili ndogo tu
ambazo zilikwisha upesi.
Wote wanne
sasa wamepata nafuu kabisa.
Tunafurahi kuripoti
kwamba mpango huo utaanza
kutumika kwa ajili
ya Wanabetheli
katika ofisi nyingi za tawi
ulimwenguni pote.
Tunaweza kufanya hivyo
katika ofisi za tawi
ambapo asilimia 90 ya
familia ya Betheli
wamepewa chanjo kamili.
Ofisi hizo za tawi
zimeanza kurudia
ratiba ya utendaji
wa kawaida.
Sasa, tuna ripoti fupi
kuhusu jinsi ndugu zetu
wanavyoendelea
baada ya misiba ya asili
iliiyotokea karibuni nchini Haiti,
na pia,
nchini Marekani.
Kama ilivyoripotiwa
kwenye Habari za JW,
tetemeko la ardhi lenye
kipimo cha 7.2
liliikumba Haiti
Jumamosi, Agosti 14.
Kwa kusikitisha,
Mashahidi watatu walikufa
kutokana na tetemeko hilo.
Tunasikitika pamoja na
familia za hao waliokufa.
Ofisi ya tawi ilitoa
ripoti hii hivi karibuni
kuhusu jitihada
za kutoa msaada.
Tetemeko hilo liliharibu
kabisa angalau
nyumba 130 za akina ndugu,
na likaharibu kwa kadiri fulani
nyumba nyingine 250.
Jumatatu, Agosti 16,
siku mbili baada ya tetemeko
matarubai yalifika
kwa ajili ya akina ndugu
kabla tu ya mvua kubwa
zilizosababishwa na
Kimbunga Grace kumwagika.
Tangu wakati huo
tumesambaza bidhaa
zenye uzito wa zaidi ya tani 3
na pia tukawasambazia
ndugu zetu tani 28 za chakula,
mahema,
matarubai,
blanketi,
magodoro,
mifumo ya kuchuja maji,
na pia tochi na chaja
zinazotumia nguvu
za jua zimesambazwa.
Isitoshe wajitoleaji
wanafanya kazi kwa bidii
ili kukagua
na kutathmini
nyumba za ndugu zetu.
Ingawa ndugu wa eneo hilo
wana hali ngumu ya kiuchumi
ndugu hao walio katika
mji mkuu wa Port-au-Prince
wametoa kwa ukarimu
mchango wa tani
nyingi za chakula.
Marekani ilikumbwa
na kimbunga Ida
nacho kilikuwa
kimbunga kikubwa sana
kilichofika Pwani
Agosti 29.
Kimbunga hicho kiliathiri
eneo linaloitwa Gulf Coast
hadi kaskazini-mashariki
mwa Marekani.
Ofisi ya tawi inaripoti
kwamba kufikia Septemba 20,
ndugu zetu 2,788
ambao walilazimika kuhama
hawajaweza kurudi
nyumbani kwao.
Inakadiriwa kwamba
itachukua majuma kadhaa
kabla ya umeme kurudishwa
katika maeneo fulani.
Kimbunga hicho kiliharibu
nyumba 1,800 za ndugu zetu
na kubomoa kabisa
nyumba nyingine 28.
Mbali na hilo,
Majumba 58 ya Ufalme
na Majumba manne ya Kusanyiko
yaliharibiwa.
Chini ya mwelekezo wa
waangalizi wa mzunguko
upesi ndugu na dada
walianza kuimarisha
mamia ya nyumba
zilizoharibiwa na
kimbunga hicho.
Halmashauri mbili za Kutoa Msaada
zinaandaa matarubai
vifaa,
chakula,
maji,
jenereta
wakati ambapo bidhaa hizo
hazipatikani katika eneo.
Utendaji wote huo unafanywa
kwa kuzingatia
miongozo inayofaa ya usalama
na pia kupata na miongozo
ya kujilinda na COVID-19.
Tunashukuru sana
kwa kazi yote ngumu
ambayo nyinyi ndugu
mnaotoa msaada mnafanya
kutia ndani
nyinyi nyote ambao
mmetoa michango ya kifedha.
Asanteni sana
kwa ukarimu wenu
na fadhili mlizoonyesha.
Lakini sasa acheni tuzungumzie
andiko la mwaka wa 2022.
Janga hili lilipoanza
hatukujua kwamba bado
lingekuwa likiendelea
zaidi ya mwaka mmoja na
nusu baadaye.
Limeathiri uchumi
wa nchi nyingi sana.
Kwa sababu hiyo
watu
kutia ndani ndugu na
dada zetu wengi
wamekosa vitu vingi
vya kimwili.
Baadhi yao
wana vitu vichache sana
kutia ndani
ukosefu wa chakula.
Hilo linatukumbusha kuhusu
Daudi aliyekuwa mwaminifu
nyakati za kale.
Ingawa si ugonjwa mbaya
uliokuwa ukimsumbua,
bali alikuwa akikimbia
na kujificha asipatikane na
Mfalme Sauli mwenye wivu,
ambaye alikusudia kumuua Daudi
na wale waliokuwa
pamoja naye.
Walikuwa na vitu vichache,
walikula chakula kidogo sana,
naye Daudi alipoteza
makao yake kwa muda.
Wakijificha katika mapango
kule nyikani.
Ingawa alikuwa na vitu
vichache sana
vya kimwili,
ni katika pindi hiyo
ambapo Daudi aliandika
Zaburi yenye kupendeza,
kwenye Zaburi ya 34.
Je, alikengeushwa
kutoka kwenye ibada yake
kwa Yehova?
Je, alijisikitikia
na kuvunjika moyo
wakati wa kipindi
hicho kigumu?
Acheni tusome
mistari michache,
Kwenye Zaburi 34.
Tuone Daudi alikuwaje
inapohusu mtazamo wake.
Zaburi 34:1
“Nitamsifu Yehova
nyakati zote,
sifa yake
itakuwa midomoni mwangu
daima.”
Kisha, katika mstari wa 3
aliwatia moyo wengine
wajiunge naye
kumsifu Yehova.
Msatari wa 3, Daudi alisema:
“Mtukuzeni Yehova
pamoja nami,
na tulikweze jina lake
pamoja.”
Huo ulikuwa
mtazamo mzuri sana.
Licha ya hali ngumu
ambazo alikuwa akikabili
wakati huo.
Ninyi ndugu na dada
wengi sana
mnakabili hali ngumu kiuchumi.
Katika kipindi hiki
cha janga hili
na huenda mna wasiwasi.
Lakini Baraza Linaloongoza
lilitaka nishiriki nanyi
hasa, mstari wa 10
wa Zaburi 34,
mstari wa 10 unasema:
“Hata wanasimba wenye nguvu
wamelemewa na njaa,
lakini wale wanaomtafuta Yehova
hawatakosa chochote chema.”
Sehemu ya mwisho ya andiko hilo
ndio andiko la mwaka wa 2022.
Wale wanaomtafuta Yehova
hawatakosa chochote chema.
Zaburi 34:10
Ni wazi, kutokana na
kile ambacho
tumekuwa tukizungumzia,
Daudi hakuwa akirejelea
kuwa na wingi wa
vitu vya kimwili.
Tunakumbuka Zaburi ya 23
ambapo Daudi alisema
kitu kama hicho.
Hapo alisema:
“Yehova ni Mchungaji wangu.
Sitakosa chochote.”
Sehemu inayosalia
ya Zaburi hiyo
inaonyesha baraka za kiroho.
Hata ingawa
kwa kweli alisema
nikinukuu:
“Katika bonde lenye
kivuli kizito.”
Katika Zaburi hiyo yote
anataja baraka
za kiroho ambazo alifurahia.
Alimalizia kwa kusema hivi
kwenye Zaburi 23:6:
“Nami nitakaa katika
nyumba ya Yehova
siku zangu zote.”
Na hiyo ndiyo sala
ya watumishi wote
waaminifu wa Yehova
katika nyakati hizi ngumu.
Ndugu wapendwa,
ugonjwa wa corona
siyo pigo kubwa zaidi
ambalo limewapata wanadamu,
na halitakuwa la mwisho.
Tunapaswa kutarajia
hali ziwe mbaya hata zaidi.
Kadiri siku hizi za mwisho
zinavyozidi kusonga
kufikia mwisho.
Hali ngumu za kiuchumi
na majaribu mengine
yatakuja
na kuondoka.
Lakini kama mtunga Zaburi
tunaweza kukubali
kwamba andiko la
mwaka wa 2022
litathibitika kuwa kweli.
Hasa kwa njia ya kiroho.
Kama Zaburi 34:10 inavyosema:
“Wale wanaomtafuta Yehova
hawatakosa chochote chema.”
Ndugu na dada wapendwa,
tunawapenda
sana
nyinyi nyote
kutoka moyoni.
Kutoka kwenye Makao Makuu
ya Ulimwenguni Pote
ya Mashahidi wa Yehova
Hii ni JW Broadcasting®!