JW subtitle extractor

Ripoti ya 1 ya Baraza Linaloongoza ya 2022

Video Other languages Share text Share link Show times

Akina ndugu na dada
karibuni kwenye ripoti hii.
aina ya ugonjwa wa corona
inayoitwa Omicron
imeenea haraka sana
ulimwenguni kote.
Idadi ya walioambukizwa
imeongezeka sana.
Tunasikitika kuripoti,
kwamba kufikia
Ijumaa Januari 21,
akina ndugu
26,813
wamekufa kutokana na
COVID-19.
Lakini kumekuwa na
mambo yenye kutia moyo.
Kwa wale ambao wamepata chanjo,
aina ya Omicron
haijawa na makali sana.
Na hawakuhitaji kulazwa,
wala hawajafa.
Kwa mfano,
huenda mmesikia taarifa za habari
kwamba kuna mlipuko mkubwa
wa Omicron nchini Puerto Riko.
Huenda pia mnajua kwamba
nchini Puerto Riko
watu wengi sana wamepata chanjo.
Ingawa akina ndugu
551 waliripotiwa kuwa
waliambukizwa hivi karibuni,
ni ndugu watatu tu waliokufa.
Na tumejulishwa hasa
ni kwa sababu wote,
walikuwa na matatizo mengine mabaya
ya afya.
Tunasikitishwa yeyote anapokufa.
Kwa hiyo tunafurahi
kwamba wengi hawakufa.
Tunahuzunika pamoja na
wale ambao
wamewapoteza wapendwa wao.
Tafadhali endeleeni
kuwa waangalifu.
Janga hili halijakwisha.
Na tunahitaji kuendelea
kuchukua hatua zinazofaa ili
kulinda uhai wetu,
na afya zetu.
Mbali na janga hili,
hali zinazoendelea katika ulimwengu,
zimekuwa zikitufanya tutafakari.
Tunajionea msiba mmoja
wa asili
baada ya mwingine,
na tunasikia
kuhusu vitisho vya vita.
Mfalme wa kaskazini na
mfalme wa kusini
wanaendelea kusukumana
Tunaposikia mambo hayo yote,
yakitokea ulimwenguni,
tunakumbushwa kwamba,
ni muhimu sana kwamba
tuendelee kukesha.
Tunahitaji kuendelea
kuwa macho kiroho.
Na tusianze kusinzia
au kukengeushwa.
Kwa nini?
Kwa sababu tunaishi wakati
mgumu zaidi katika
historia ya wanadamu.
Yesu alijua kwamba
siku za mwisho zingetokeza hali
ambazo zingefanya iwe vigumu
kwetu kuendelea
kuwa karibu na Yehova.
Kutokana na upendo mwingi
ambao alikuwa nao,
aliwahimiza hivi wafuasi wake,
kama ilivyorekodiwa kwenye
Luka 21:34-36
“Lakini jiangalieni wenyewe,
ili mioyo yenye isilemewe kamwe
na kula
na kunywa kupita kiasi
na mahangaiko ya maisha,
na siku ile iwakute ghafula
kama mtego.
Kwa maana itakuja
juu ya wale wote
wanaoishi juu ya uso wa dunia.
Basi, endeleeni kukesha
siku zote mkiomba dua
ili mfanikiwe kuponyoka
mambo yote hayo
ambayo lazima yatukie
na kusimama mbele ya
mwana wa binadamu.”
Tunasikia mara nyingi
ripoti zenye kutia moyo.
Kwamba nyinyi ndugu na dada
mnaendelea kufanya kazi kwa bidii
ili kuendelea kukesha.
Na kuendelea kuwa na mengi
ya kufanya
katika utumishi wa Yehova.
Mnafanya mengi katika
huduma yenu,
kuandika barua,
kupiga simu,
na kutafuta nafasi
za kushiriki habari njema,
kwa njia isiyo rasmi.
Na wengi wenu mlifaulu
kufanya upainia msaidizi
wakati wa kampeni iliyopita.
Kuendelea kuwa na
mengi ya kufanya katika
utumishi wa
Yehova ni ulinzi kwetu.
Lakini mengi zaidi yanahitajika
ili kulinda mioyo yetu.
Ni muhimu sana kwetu sote
kuendelea kukesha.
Kuwa macho
kuhusu mambo
yanayoweza kuhatarisha
hali yetu ya kiroho.
Baadhi ya hatari hizo ni zipi?
Yesu alitaja mambo kama vile,
kula na kunywa kupita kiasi,
na mahangaiko ya maisha.
Ni katika njia zipi
mambo hayo
yanaweza kufanya mioyo yetu
ianze kulemewa?
Kwanza,
acheni tuzungumzie jambo moja,
ambalo linasababisha mahangaiko.
Kujitenga na wengine.
Bila shaka hatujawahi
kuhisi kwamba tumetengwa na wengine
kama wakati wa janga hili.
Ni kweli,
tunahitaji kujitenga na wengine
kwa njia ya kimwili.
ili kuepuka kueneza
ugonwa wa Covid-19.
Lakini tusipokuwa waangalifu,
tunaweza kuanza kujitenga,
katika njia nyingine pia.
Labda nyakati nyingine tunahisi
tumechoshwa kutumia Zoom.
Na huenda hata tukataka
kujitenga kwa njia hiyo.
Hatari ni nini?
Methali 18:1 inasema:
“Yeyote anayejitenga na wengine,
anafuatia tamaa zake
mwenyewe za kichoyo.
Hukataa hekima yote inayotumika.
Jitihada zinahitajika
ili kuwasiliana na ndugu zetu kupitia simu,
kupitia video iliyounganishwa mtandaoni,
au hata kupitia barua-pepe
au ujumbe wa simu.
Lakini jinsi tunavyohisi kwamba
tumetiwa moyo
baada ya kufanya hivyo,
kunafanya jitihada yetu
iwe yenye manufaa sana.
Mara nyingi,
tunapata mengi zaidi,
kuliko tulichotoa.
Kama Yesu alivyosema,
kwenye Matendo 20:35:
“Kuna furaha zaidi katika kutoa
kuliko ilivyo katika kupokea.”
Makala kwenye Jw.org
yenye kichwa,
“Nikabilianeje na upweke?”
ilitaja jambo lenye kupendeza
chini ya kichwa kidogo,
“Sitawisha urafiki na watu.”
Marafiki wanaweza kukusaidia
kuona mambo kwa njia tofauti
na kukuletea shangwe
hata katika hali ambazo
inakuwa vigumu
kuzungumza nao uso kwa uso.
Ikiwa huwezi kutoka nyumbani,
unaweza kuwasiliana nao
kwa njia ya video
au kwa kuwapigia simu,
ili kuimarisha urafiki wenu,
au kujenga urafiki na watu wapya.
Tunawahitaji ndugu na dada zetu,
nao wanatuhitaji pia.
Ili kupata marafiki,
tunahitaji kuwa marafiki.
Basi uwe rafiki!
Je, unaweza
kuwasiliana na mtu juma hili?
Labda unaweza kufikiria kuhusu
rafiki ambaye hamjaweza kuzungumza
kwa muda fulani.
Shangwe utakayopata
kwa kuzungumza na rafiki
bila shaka itatuliza
baadhi ya mahangaiko yako
Tunasubiri kwa hamu
kurudi kwenye majumba ya ufalme
na majumba ya kusanyiko.
Na kuwa tena na
makusanyiko yetu ya eneo
ya pekee,
na hata makusanyiko ya kimataifa.
Kwa sasa,
tunafurahi kwamba kuna njia nyingine
ya kufurahia programu hizo,
kama vile Zoom,
JW Stream,
na katika visa fulani,
tv na redio.
Bila shaka,
makutaniko fulani yanatumia Zoom
kwa ajili ya mikutano yao.
Je, haipendezi kuona
nyuso za ndugu na dada zetu?
Tunafurahi kuweza
kuwaona wakitoa maelezo,
na wakiimba kutoka moyoni.
Hilo pia linatusaidia kushinda hisia
za kwamba tumetengwa.
Ukiwasha kamera yako tu
na kutabasamu
au hata tu kupunga mkono,
unaweza kuwatia moyo sana wengine.
Tunaweza kujiwekea lengo
la kuingia mapema kwenye mkutano,
na vilevile kubaki muda mrefu
baada ya mkutano.
Tunaweza kufurahia
ushirika na wengine
kwenye breakout rooms.
Ndugu na dada,
hizo ni baadhi ya
njia zinazofaa ambazo
tunaweza kushinda hisia
za kuwa tumetengwa,
na mahangaiko ambayo
kutengwa na wengine
kunaweza kutokeza moyoni mwetu.
Hatari nyingine ambayo Yesu alitaja,
ni kunywa kupita kiasi
Bila shaka hakuna kosa lolote
kunywa kileo kwa kiasi.
Maandiko yanafafanua divai
kuwa zawadi kutoka kwa Mungu,
iliyokusudiwa kuufanya moyo ushangilie.
Lakini tahadhari inahitajika.
Kwa nini?
Kumbuka,
Yesu alionya moja kwa moja,
kwamba mioyo yetu inaweza kulemewa,
na kunywa kupita kiasi.
Ripoti ulimwenguni zinaonyesha
kwamba watu wengi wameongeza
kiasi cha kileo wanachotumia
wakati wa janga hili.
Makala yenye kichwa:
“Jinsi ya kudhibiti matumizi
ya kileo,”
iliyo kwenye jw.org,
inasema hivi:
“Watu fulani huhisi kwamba
wanahitaji kunywa kileo zaidi
wanapokuwa na mkazo,
wanapohisi upweke,
au wanapohisi kuwa wamechoka
kwa sababu hawana lolote la kufanya.”
Je, siku hizi
unakunywa kiasi kikubwa
kuliko hapo awali?
Ikiwa ndivyo,
unaweza kufanya nini
ili kuhakikisha kwamba
hunywi kupita kiasi au
kwamba wewe si mraibu wa kileo?
Hata ikiwa mtu hatalewa,
kunywa kwa njia isiyo ya kiasi
kunaweza kutokeza hatari za kiroho.
Isaya 5:11 inasema:
“Ole wao wanaoamka asubuhi
na mapema ili wanywe kileo.
wanaokawia hadi giza linapoingia jioni
mpaka divai inapowawasha.”
Kwa nini wawe na ole?
Ona madhara ya kiroho wanayopata
kwenye sehemu ya pili ya
mstari wa 12.
“Hawafikirii utendaji wa Yehova,
wala hawaioni kazi ya mikono yake.”
Kunywa bila kiasi,
kunaweza kufanya mioyo yetu ilemewe
hivi kwamba
tuanze kupuuza mambo ya kiroho.
Kunaweza kufanya tupunguze mwendo
katika mbio za uzima,
au hata tuache kukimbia kabisa.
Si ajabu kwamba
Yesu alizungumzia jambo hilo
alipozungumzia uhitaji
wa kuendelea kuwa macho kiroho.
Kwa nini usipitie tena
makala hiyo iliyo kwenye jw.org?
Inataja mambo matano,
yatakayokusaidia kudhibiti
matumizi ya kileo.
Ni jambo gani lingine linaloweza
kuhatarisha hali yetu ya kiroho?
Matumizi mabaya ya
mitandao ya kijamii.
Kumekuwa na wasiwasi mwingi
kutoka kwa serikali
na hata kwa madaktari wengi
kuhusu jinsi mitandao ya kijamii
inavyoathiri afya ya kiakili
na ya kihisia ya watu.
Muhimu hata zaidi,
ni madhara ya kiroho inayoleta.
Habari zilizomo,
watu wanaohusika,
na muda unaotumiwa,
unaweza kumfanya mtu awe mraibu.
Ndugu na dada,
mkiamua kuruhusu familia yenu
itumie mitandao ya kijamii,
iweni waangalifu.
Hakikisha kwamba
una ushirika mzuri pamoja na wale
walio na mazoea mazuri ya kiroho,
iwe ni kwenye mtandao
au uso kwa uso.
Video ya vibonzo kwenye ubao,
yenye kichwa,
“Tumia mitandao ya kijamii
kwa hekima,”
ina vikumbusho vinavyofaa
vya jinsi ya kuwa na usawaziko,
na kuwa na tahadhari
tunapotumia mitandao ya kijamii.
Ni changamoto gani ya mwisho,
ambayo tungependa kuzungumzia?
Kutounga mkono upande wowote.
Kwa kuwa kuna hali nyingi sana
zenye kutatanisha ulimwenguni,
na pia tishio la vita
katika nchi mbalimbali,
tunapaswa kuwa waangalifu
kwamba mioyo yetu
isianze kuunga mkono upande wowote
katika masuala hayo.
Imesikitisha sana kuona
hatua za kulinda afya ya watu,
kama vile kuvaa barakoa,
kunawa mikono,
kukaa umbali
unaofaa kutoka kwa wengine,
na chanjo,
yakianza kubishaniwa,
hata na wanasiasa.
Baadhi ya ndugu na dada zetu,
wameathiriwa na maoni ya kisiasa,
ya watu katika jamii zao.
Wengine wameingia kwenye intaneti,
na wameathiriwa sana na
tovuti zinazoonekana kuwa rasmi,
zilizojaa propaganda
nyingi
sana ya kisiasa.
Ndugu na dada tafadhali,
iweni waangalifu.
Kwa kuwa tu jambo fulani
linatokea katika
tovuti fulani inayoonekana kuwa rasmi,
haimanishi ni la kweli.
Tunapaswa kujilinda dhidi ya
roho ya ulimwengu,
na kutounga mkono upande wowote.
Maneno ya Yesu yanafaa sana.
“Jiangalieni wenyewe
ili mioyo yenu isilemewe kamwe.”
Acheni tuendelee kukazia fikira
Ufalme wa Mungu,
kuwa ndio suluhisho pekee,
la matatizo ya ulimwengu huu.
Nini ambacho kimesaidia familia fulani,
kuendelea kuwa macho?
Acheni tuone
tunapotazama video ifuatayo.
Wakati wa janga hili,
ilikuwa vigumu sana
kudumisha ratiba nzuri
na ilikuwa rahisi sana
kusitawisha mazoea mabaya.
Tulipokuwa tumejitenga,
nilitumia kompyuta
kwa muda mwingi zaidi.
Na hilo lilivuruga
ratiba yangu ya kulala.
Nilihitaji kurekebisha hali,
kwa sababu
ni rahisi kutokeza mazoea mabaya
lakini ni vigumu kuyaacha.
Kwa hiyo nilijaribu
kujitibu kwa njia fulani,
kwa kuacha kutazama tv,
na kuibadili na kitu
chenye manufaa zaidi,
yaani, kituo chetu cha tv,
Jw Broadcasting.
Nilipokuwa nikitazama tv
kwa muda mwingi,
nilisikia mambo mengi yasiyofaa
kuhusu chanjo.
Kwa hiyo niliogopa sana.
Kwa sababu ya
shinikizo ambalo nilipata
kutoka kwa vyombo vya habari,
niliepuka kupata chanjo
kwa muda fulani.
Mara nyingi sana tulisali ili
tupate mwongozo wa Yehova.
Ripoti za Baraza Linaloongoza
zilikuja kwa wakati
na kutusaidia kufanya uamuzi mzuri.
Janga hili lilipoanza,
nilikuwa na wakati mwingi
kwa hiyo,
wakati wote nilikuwa nikitumia
mitandao ya kijamii
au teknolojia nyingine.
Ibada ya familia
ilikuwa nafasi nzuri
kwetu kuzungumza
kuhusu mitandao ya kijamii.
Na kutusaidia
kupata maoni ya Yehova,
jinsi ya kuitumia kwa usawaziko,
ingawa hatutaiacha kabisa,
tuhakikishe kwamba haitatudhibiti.
Ilichukua muda,
lakini hatimaye nilifuta akaunti yangu
ya mtandao wa kijamii.
Na nikaanza kujiwekea muda,
wa kutumia programu nyingine
zilizokuwa zikiniibia muda.
Familia yetu iliamua
kuanza kutumia muda mwingi zaidi pamoja.
Tulipiga muziki na kucheza dansi,
tulicheza michezo ya mezani,
na kwenda matembezi msituni.
Hilo lilitusaidia
kupunguza muda tunaotumia
kwenye mitandao ya kijamii
Niliamua kuwa na
mengi zaidi ya kufanya,
kwa hiyo
nilifanya mambo yenye kufurahisha
kama vile kushona
na pia kulima.
Niliona kuna faida kubwa
kukaa karibu na kutaniko
kupitia Zoom.
Hata ingawa si rahisi kwangu
kutumia Zoom,
Kutumia muda mwingi na watu
wanaokabili mambo yaleyale,
kama mimi,
kulinisaidia sana.
Tungeweza kuzungumza
kuhusu mambo tunayokabili
na kutiana moyo.
Tulipanga michezo fulani ya Biblia,
kupitia Zoom.
Nilifurahia kuungana na wengine
katika kutaniko
kwa ajili ya mambo tuliyokuwa
tumepanga kufanya pamoja.
Kwa mfano,
tuliwahoji baadhi ya wale
ambao wamekuwa
kutanikoni kwa muda mrefu.
Na ilipendeza
kusikia mambo waliyojionea
na kuwa na uhusiano
wa karibu zaidi nao.
Wakati wa janga hili,
niliwasiliana na wengine,
ama kwa kuwapigia simu
kuwaandikia kadi,
au ujumbe wa simu
au kuwapelekea kitu tu mlangoni kwao.
Hilo lilinisaidia
kujihisi nikiwa karibu zaidi
na akina ndugu na dada.
Ripoti za Baraza Linaloongoza
zimetusaidia sana.
Zilitusaidia kuendelea kukazia fikira
utendaji wetu wote,
Tukiwa wazazi,
zimetusaidia kutoa mwongozo wa wazi.
Kwa hiyo tunahisi tumeongozwa
wakati wote wa janga hili.
Na wakati huohuo
tukatiwa moyo pia.
Pia nimejionea Yehova akijibu
sala zangu za kibinafsi
na kuona jinsi anavyotutegemeza,
wakati wa kipindi hiki kigumu.
Kwa sababu sidhani ikiwa
yeyote angeweza kukabiliana
na hali za janga hili,
bila msaada wa Yehova.
Tunajivunia familia hizo
kwa kuendelea kujilinda
dhidi ya hatari za kiroho.
Je, uliona jinsi walivyoshinda hisia
za kwamba wametengwa na wengine?
Waliwasiliana
na wengine kwa ukawaida.
Walitumia video
iliyounganishwa kwenye mtandao
ili kuwa karibu na kutaniko,
na marafiki wao.
Je, uliona jinsi walivyoshughulikia
matumizi ya mitandao ya kijamii?
Walizungumzia hilo wakiwa familia.
Na wakaamua ama
kupunguza muda waliotumia,
au kuepuka kutumia kabisa.
Pia wameongeza muda
ambao wanatumia wakiwa pamoja,
kutia ndani kufurahia
utendaji fulani nje ya nyumba.
Na walishugulikiaje jaribu
la kutounga mkono upande wowote?
Walisali kwa Yehova.
Na wakategemea habari
zinazotoka kwa
mtumwa mwaminifu na mwenye busara,
walipokuwa wakifanya
maamuzi yao ya kibinafsi.
Hivi karibuni,
siku ya Yehova
itakuja juu ya dunia yote.
Ni muhimu
kwamba tuendelee kukesha.
Huu si wakati
wa kuanza kusinzia kiroho
au kukengeushwa.
Kumbuka maneno ya Yesu kwenye
Luka 21:36:
“Basi endeleeni kukesha
sikuzote mkiomba dua
ili mfanikiwe kuponyoka
mambo yote hayo
ambayo lazima yatukie
na kusimama mbele
ya mwana wa binadamu.”
Tukiendelea kutoa dua
kwa unyoofu kwa Yehova
na tukiendelea kutumia
mwongozo unaofaa tunaopata,
bila shaka tutafanikiwa.
Kutoka kwenye
Makao Makuu ya Ulimwenguni Pote
ya Mashahidi wa Yehova,
hii ni JW Broadcasting!