JW subtitle extractor

Ripoti ya 2 ya Baraza Linaloongoza ya 2022

Video Other languages Share text Share link Show times

Karibuni!
Tuna habari nyingi za kuwapa.
Ni wazi,
akili za kila mtu ulimwenguni
zinafikiria mambo yanayotokea Urusi
na Ukrainia.
Tukiwa watu wa Yehova,
hatushangazwi na matukio hayo.
Tunatambua vizuri
kwamba Urusi na
mataifa yanayounga mkono
wanatimiza jukumu lililotabiriwa
kwenye Danieli 11
la kuwa “mfalme wa kaskazini.”
Baraza Linaloongoza lilipotaja
jambo hilo kwa mara ya kwanza
kwenye mkutano wa kila mwaka wa 2018.
Tulitaja kwamba tayari,
mfalme wa kaskazini alikuwa amemiliki
eneo la Krimea.
Unaposoma Danieli 11
Haishangazi kuona kwamba
mfalme wa kaskazini
anapendezwa kumiliki
maeneo mengine pia.
Bila shaka,
huu ndio wakati wa
kuendelea kukesha
kila wakati
na kudumisha
msimamo wa
kutounga mkono upande wowote.
Kufikia Februari 28,
hakuna ripoti ya vifo
bali kuna mmoja kati ya ndugu zetu
ambaye alijeruhiwa.
Nyumba nyingi za ndugu
zetu zimeharibiwa,
maelfu ya akina ndugu wamekimbia
kutoka maeneo yenye vita.
Tunaendelea wakati wote
kusali kwa ajili yenu
ndugu mlio nchini Ukrainia
na nchini Urusi.
Wakati huo huo,
tunafanya yote tuwezayo
ili kuhakikisha kwamba mtapata
chakula chenu cha kiroho
na vilevile mahitaji mengine maishani.
Kuhusu mambo ya kisheria,
katika juma la Februari 21,
tulipata maamuzi
matatu muhimu mahakamani.
Februari 22,
mahakama katika Ust-Abakan
iliamua kumwachilia huru
Dada Valentina Baranovskaya
mwenye umri wa miaka 70.
Dada Baranovskaya
amekuwa gerezani kwa miezi 12 iliyopita.
Mwendesha-mashtaka anaweza
kukata rufaa kabla ya Machi 4.
Ikiwa hatakata rufaa,
basi dada yetu ataachiliwa
Machi tarehe 5.
Tafadhali,
endeleeni kumkumbuka Dada Baranovskaya
katika sala zenu.
Februari 22, 2022,
Mahakama ya Ulaya ya
Haki za Kibinadamu
ilifanya maamuzi mawili muhimu
kuhusu ndugu zetu nchini Urusi.
Kesi hizo zilihusu
upekuzi uliofanywa na polisi
kisha ndugu zetu wakazuiliwa
kuanzia 2010 hadi 2012.
Mahakama ilitoa
uamuzi unaotuunga mkono
na ikaagiza serikali ilipe
ndugu na dada 15 waliohusika
katika kesi hizo.
Kwa ujumla,
serikali ya Urusi inapaswa kulipa
karibu euro 100,000.
Mahakama hiyo ilisema kwamba
kazi ya kuhubiri
ya Mashahidi wa Yehova
ni haki ya msingi
ambayo hakuna
serikali inapaswa kuingilia.
Katika nchi nyingi,
idadi ya wanaoambukizwa
COVID-19 inapungua.
Baadhi ya serikali
zimeanza kupunguza
au hata kuondoa kabisa vizuizi.
Tunatumaini kwamba
hali zitaturuhusu tuanze tena
kushiriki utendaji mwingi
zaidi wa kitheokrasi.
Hata hivyo,
bado tungependa
kuendelea kuwa waangalifu.
Baraza Linaloongoza
limeaagiza Halmashauri za Tawi
zichunguze hali kwa uangilifu
katika hila sehemu ya eneo lao.
Kila Halmashauri ya Tawi
inaweza kuanza kutumia
programu mpya iliyoanzishwa
ya kukutana uso kwa uso
ikiwa hilo linaweza
kufanywa kwa usalama.
Je, itawezekana
kwa kutaniko lenu
kukutana pamoja
kwa ajili ya ukumbusho mwaka huu?
Tunasubiri tuone.
Vyovyote vile,
hii ni nafasi nzuri ya kila mmoja wetu
kufikiria jinsi tunavyoona
mikutano ya kutaniko.
Ikiwa tunaweza kurudi
kwenye Jumba la Ufalme
Je, nitakuwa tayari kufanya hivyo?
Fikiria mambo tunayozungumza
na wanafunzi wetu wa Biblia
kuhusu umuhimu wa
kuhudhuria mikutano
katika somo la 10
la kitabu Furahia Maisha Milele!
Hapo inasema:
Jitihada inahitajika
ili kuhudhuria mikutano
Fikiria hali ilivyokuwa
katika familia ya Yesu.
Kila mwaka,
walitembea kwa siku kadhaa
umbali wa kilomita 100 hivi
kwenye eneo lenye milima
kutoka Nazareti hadi Yerusalemu
ili kwenda hekaluni.
Kisha kitabu kinauliza swali hili:
Kwa nini huenda ukahitaji kujitahidi
ili uhudhurie mikutano?
Hakuna shaka swali hilo linalohitaji
mtu ajichunguze
limewachochea wanafunzi
fulani wa Biblia
kuhudhuria mikutano.
Lakini huenda hilo likawa
swali ambalo sisi sote
tukahitaji kujiuliza.
Kuanza kurudia tena mikutano
kwenye Jumba la Ufalme
kutahitaji jitihada.
Lakini
bila shaka lazima tufikirie baraka
zinazotokana na kukutana pamoja
na kuwa na ushirika na ndugu
na dada zetu.
Tunaweza kuwazia
jinsi Yosefu na Maria
na watoto wao
walivyofurahia kuwepo pale Yerusalemu
wakati ambapo jiji lilikuwa
limejaa waabudu wenzao wa Yehova.
Bila shaka,
shangwe ya kuwepo hapo
iliwasaidia Yosefu na Maria
kutambua kwamba
jitihada waliyofanya
ilifaa.
Vivyo hivyo,
shangwe yetu ya kuwa
kwenye Jumba la Ufalme
pamoja na ndugu na dada zetu
itazidi kwa mbali
changamoto zozote za kuwepo pale.
Hadi tutakaporudi
kwenye Jumba la Ufalme
tunathamini sana jitihada zote
ambazo nyinyi ndugu
na dada mnafanya
za kuhudhuria mkutano kwenye zoom.
Kwa kujiunga mapema
ma kuendelea kubaki baadaye
Tunapata nafasi zaidi
za kufanya kile kinachotajwa
kwenye Waebrania 10:24,25:
“Na acheni tufikiriane
ili kuchocheana katika upendo
na matendo mazuri,
bila kuacha kukutana pamoja,
kama wengine walivyo na desturi,
bali tutiane moyo,
na kufanya hivyo zaidi
kwa kadiri mnavyoona
siku ile ikikaribia.”
Tunaweza kupata
shangwe ya kutoa
tunapowatia moyo
ndugu na dada zetu kwa bidii
na kuwachochea katika upendo
na matendo mazuri.
Basi,
kwa nini tunatia jitihada zote hizo?
Kwa nini tunatia bidii sana
kudumisha hali yetu ya kiroho
na pia kuwatia moyo wengine?
Kwa sababu tunataka
kudumisha uhusiano wetu
na Yehova
ukiwa wenye nguvu
na wakati huo huo
tuchukue msimamo thabiti
dhidi ya adui yetu mkuu,
Shetani Ibilisi.
Kumbuka onyo
linalotajwa kwenye 1 Petro 5:8
Mstari huo unasema:
“Tunzeni akili zenu,
iweni waangalifu!
Adui yenu, Ibilisi,
anatembea huku na huku
kama simba anayenguruma,
akitafuta kummeza mtu.”
Ingawa Ibilisi hasababishi
matatizo yetu yote,
sikuzote anatafuta
nafasi ya kuyatumia.
Angependa kutumia mkazo
na pia upweke
kwa sababu ya janga hili
ili kudhoofisha imani yetu.
Au tu kutukengeusha
kupitia propaganda zake.
Ni nini kinachoweza kutusaidia?
Ona jinsi mstari wa 9 unavyosema:
“Lakini chukueni
msimamo dhidi yake,
mkiwa imara katika imani,
mkijua kwamba
mateso yaleyale yanaupata
ushirika mzima
wa ndugu zenu
ulimwenguni.”
Kwa ufupi,
watumishi wote
wa Yehova ulimwenguni
wanakabili shambulizi lilelile.
Ingawa huenda
changamoto zetu zikatofautiana
popote pale tulipo duniani
tunashambuliwa.
Lakini unapotafakari
mambo ambayo ndugu na dada zetu
maeneo mengine wanakabili
huenda ukawa na maoni tofauti
kuhusu hali unazokabili.
Kwa mfano,
wafikirie ndugu zetu
ambao wanakabili misiba ya asili
au mateso.
Kufikia sasa
katika mwaka huu wa utumishi
ndugu zetu wamekumbwa na zaidi
ya misiba ya asili 120.
Fikiria mifano kadhaa.
Desemba,
Kimbunga Rai
kinachojulikana kama Odette,
kilipiga nchi ya Filipino.
Kwa kusikitisha,
wahubiri wanne walikufa,
wengine wakajeruhiwa,
na zaidi ya 2,000
wakalazimika kuhama makwao.
Halafu wazia pia,
zaidi ya nyumba 1,700
za ndugu zetu
zilipata uharibifu fulani
au zikabomolewa kabisa.
Kisha mwezi Januari,
Kimbunga Ana
kilipiga eneo la
kusini-mashariki ya Africa.
Kwa kusikitisha,
ndugu mmoja alipoteza
mke wake na watoto wake wawili.
Ndugu watatu
na mtoto mmoja walijeruhiwa,
zaidi ya 2,000
wakalazimika kuhama makwao
na zaidi ya nyumba 400
za ndugu zetu
zilipata uharibifu fulani
au zikabomolewa kabisa.
Na Februari 15,
mvua kubwa
na maporomoko ya ardhi
yalitokea kule Brazili.
Kwa kusikitisha,
ndugu mmoja na
mtoto wake mwenye umri
wa miaka miwili
walisombwa na
poromoko hilo la ardhi.
Baba alipona,
lakini akajeruhiwa vibaya.
Kwa kusikitisha,
mwana wake alikufa.
Kwa kusikitisha pia
ndugu mwingine alikufa.
Tunaendelea kusali
kwa ajili ya wote ambao
wamewapoteza wapendwa wao.
Au ambao
wameathriwa na misiba
hiyo ya karibuni.
Mbali na misiba hiyo ya asili,
ndugu zetu wanakabili
pia msukosuko wa kisiasa.
Katika Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo
ndugu na dada zetu
katika maeneo mbalimbali,
wamelazimika kukumbia
kutoka kwenye vijiji
na mashamba yao.
Hata hivyo,
kwa msaada wa Yehova
tumefaulu kuwaandalia zaidi ya
tani 81 za chakula
ili kuwa saidia zaidi ya watu 19,600!
Tunathamini sana msaada wote
ambao mnawatolea ndugu na dada zetu
wanaokabili misiba hiyo.
Sala zenu
pamoja na
michango yenu ya ukarimu
inasaidia kwa njia kubwa sana.
Asanteni!
Licha ya misiba yote hiyo,
Ndugu na dada zetu
wanaendelea kuwa imara
katika imani.
Acheni tusikie jinsi
baadhi nchini Kongo,
Ufilipino,
na katika eneo la Karibea
wanahisi kuhusu msaada waliopata.
Ninamshukuru sana Yehova
kwa msaada wa kimwili
ambao amenipa
ili kunisaidia kurudia maisha yangu.
Kwa maoni yangu,
ninaona haitoshi tu
kusema asante
ili kushukuru
kwa msaada wote ambao nimepata.
kwa kuwa mimi ni mmoja
kati wale ambao nyumba
zao ziliharibika
na nimerekebishiwa.
Akina ndugu walitusaidia sana.
Licha ya hali ngumu
ambazo zilitokezwa
na Kimbunga Odette,
Yehova hakutuacha.
Altusaidia.
Siku iliyofuata,
akina ndugu waliwasiana nasi,
na wakatuletea chakula,
na hata wakatusaidia
kurekebisha nyumba yetu.
Tunamshukuru sana
Yehova kwa msaada
na kwa kutuandalia
mahitaji yetu yote
ili tuweze kuendelea vizuri
na maisha yetu!
Ninamshukuru sana Yehova
na tengenezo lake
kwa upendo wote
ambao ametuonyesha
wakati huu ambao tuliathiriwa na
mlipuko wa mlima wa volkano.
Hata hatujui tuseme nini
ili kuonyesha shukurani zetu.
Ni kana kwamba Yehova
ametushika mkono
akatutunza,
na kutuambia:
“Msiogope.
Nitawasaidia.”
Kwa kweli, tunashukuru sana.
Asanteni sana kwa
kutujengea nyumba hii
kwa sababu nyumba yetu
ilichomeka.
Na nyinyi watumishi wa Yehova
ninataka kuwaambia
asanteni,
asanteni,
asanteni sana.
Niliondoka nikiwa tu
na nguo nilizokuwa nimevaa.
Nikikumbuka hali
ambayo tuliacha nyumba yetu
na sasa kurudi kuona
kazi yote ambayo
akina ndugu walitufanyia
haata sijui nitumie maneno gani
kuelezea hisia zangu.
Ninawapenda na kuwashukuru
kila mmoja wenu
kwa yote mliyotufanyia.
Hamwezi kuelewa kinachomaanisha
kujua kwamba
hatukuwa tumeachwa peke yetu.
Tulijionea kabisa mkono wa Yehova
na upendo wake,
tulihisi Yehova akitusaidia kabisa.
Tunashukuru sana
kuona baraka za Yehova.
Changamoto nyingine
ambayo ndugu na dada zetu
wanakabili ni mateso.
Fikiria kwa mfano,
Dada Anna Safronova.
Januari 25,
Anna mwenye umri wa miaka 56,
alihukumiwa kifungo
cha miaka sita gerezani.
Hiyo ndiyo hukumu ndefu
na kali zaidi
kuwahi kupewa dada nchini Urusi
tangu marufuku ya mwaka 2017.
Mahakama ilimfunga
licha ya kwamba yeye
ndiye anayemtunza mama yake
mwenye umri wa miaka 81.
Familia za wale ambao wamefungwa
zinakabili hali gani?
Yehova anawasaidiaje?
Acheni tutazame mahojiano
yafuatayo kutoka Urusi.
Majaribu na changamoto zetu
zilianza Juni 12, 2018.
Wakati ambapo wenye mamlaka
walifanya upekuzi nyumbani kwetu.
Kisha hatukumwona Aleksey
kwa miezi 11
kwa sababu
alikuwa amefungwa mahabusu.
Hakimu alimhukumu
kifungo cha miaka mitatu na nusu
gerezani.
Kisha jambo lingine
baya lililotokea
ni wakati ambapo nyumba yetu
iliteketea usiku.
Oktobab mwaka wa 2020,
Mimi na watoto wangu
tukaambukizwa COVID
na muda mfupi uliopita
tuliambukizwa tena
ugonjwa wa COVID
kwa mara ya pili.
Ninaishi na binti yangu Anna.
Julai 2021,
nyumba yetu ilifanyiwa upekuzi
na Januari 25, 2022,
mahakama ikamhukumu
miaka sita gerezani.
Hata sikupewa nafasi
ya kumwaga binti yangu.
Baba yangu amefungwa gerezani
kwa mwaka mmoja na nsusu.
Januari mwaka huu,
alihukumiwa kifungo
cha miaka saba gerezani.
Pamoja na yote hayo,
mwishoni mwa mwaka uliopita,
mama yangu alikufa ghafla
kutokana ugonjwa wa COVID.
Kukabiliana na
jaraibu moja ni vigumu
lakini yanapokuja mawili
kwa wakati mmoja,
yaani, eti siwezi kuwaona watu
wawili ninaowapenda sana.
Ninasali kwa Yehova
na ninahisi kwamba ananipa
amani moyoni.
Na ananisaidia niwe mtulivu
na sina wasiwasi mwingi sana.
Marafiki huwa wanakuja
wananisaidia kufanya usafi,
wanaenda kunifanyia ununuzi,
tunazungumza,
na katika yote hayo
ninauona mkono wa Yehova
akinisaidia na kunitegemeza.
Yehova alituimarisha
tena na tena kupitia Neno lake.
Na aliwatumia akina ndugu
kwa mfano, rafiki zetu
walitutumia ujumbe wa simu
wakinukuu maandiko niliyohitaji
ili kunipa nguvu.
Hilo lilikuwa jibu la sala zangu.
Ilikuwa siku ya kukumbuka harusi
ya wazazi wangu na siku nzima,
ni kana kwamba tulikuwa
tukiletewa zawadi,
maua,
vifurushi.
Ni kana kwamba siku hiyo yote
nyumba ilijaa maua.
Ni kana kwamba Yehova
alikuwa akisema kwa sauti,
“Ninawapenda,
nipo pamoja nanyi,
sitawaacha!”
Kisha Sasha akaniambia,
“Mama,
ikiwa Baba angekuwa huru
ungekuwa na ua moja tu!”
Unakumbuka ile pindi
ambayo uliogopa
kusema kwa sauti:
“Baba, Nakupenda!
Uwe imara.
Yehova anakupenda!”?
Lakini bado ulijipa ujasiri
na tukasali pia.
Kisha aliandika barua
akisema kwamba
alilia kwa shangwe
kwa sababu alisikia sauti yangu
imani yangu iliimarishwa
nilianza kusoma Biblia
kila siku.
Pia, nimechukua
hatua kubwa kumwelekea Yehova
nilijiweka wakfu kwake
na kubatizwa.
Mara nyingi,
nilikumbuka wazo kwamba
Yehova mara nyingi anatukumbatia
akitumia mikono ya mtu mwingine.
Katika miaka ambayo imepita
tulihisi Yehova
akitukumbatia mara nyingi.
Sikuzote Yehova
anabadili magumu kuwa baraka.
Kulikuwa na moto,
tukapoteza makao yetu.
Lakini sasa tuna nyumba mpya,
ambayo ni bora hata
kuliko ya kwanza.
Nina hakika tutafaulu kukabiliana
na chochote kitakachotupata.
Jambo kuu ni kuwa karibu na Yehova.
Tunajivunia sana
wote ambao
wanasimama imara katika imani
licha ya mateso.
Tunakumbushwa
Maneno ya 2 Wakorintho 4:9:
“Tunateswa,
lakini hatuachwi bila msaada;
tunaangushwa chini,
lakini hatuangamizwi.”
Yehova hatawahi kuwaacha
watumishi wake waaminifu.
Kama ambavyo tumekumbushwa
katika ripoti hii,
ndugu na dada zetu ulimwenguni pote
wanaendelea kusimama
imara katika imani
licha ya mashambulizi ya kijeshi,
janga la ulimwenguni pote,
misiba ya asili,
na mateso.
Ndugu na dada,
kama 1 Petro 5:8 inavyosema:
“Tunzeni akili zenu,
iweni waangalifu!”
Adui yetu,
Shetani Ibilisi,
ameujaza ulimwengu huu
propaganda yake ya kishetani.
Iweni waangalifu!
Chukueni msimamo dhidi yake.
Kadiri ulimwengu unavyozidi
kuzingatia utaifa,
na kugawanyika
hatutavunja msimamo wetu
wa kutounga mkono
upande wowote.
Tutaendelea kuwa na umoja,
na kuwa washikamanifu
kwa Ufalme wa Mungu
na kuonyeshana
upendo miongoni mwetu.
Endelea kusikiliza
sauti ya yule mchungaji mwema,
Yesu Kristo,
na sauti kutoka kwa
mfereji uliowekwa rasmi,
mtumwa mwaminifu
na mwenye busara.
Mungu wetu mweza yote,
Yehova yupo pamoja nasi.
Na undugu wa ulimwenguni pote
unatuunga mkono,
hata iwe tutakabili majaribu gani,
tuna kila kitu tunachohitaji
ili kuendelea kuwa waaminifu
kwa Yehova.
Ndugu na dada wapendwa,
tunawapenda sana
nyinyi nyote.
Kutoka kwenye
makao makuu ya ulimwenguni pote
ya Mashahidi wa Yehova,
Hii ni JW Broadcasting®.