JW subtitle extractor

Ripoti ya 6 ya Baraza Linaloongoza ya 2022

Video Other languages Share text Share link Show times

Karibuni ninyi nyote.
Katika programu hii
tutawajulisha
andiko la mwaka wa 2023.
Kwa hiyo
usibanduke.
Lakini kwanza
tungependa kuwapa habari za karibuni.
Bila shaka sisi sote tulifurahia
kusanyiko la eneo
la “Fuatilia Amani.”
Je, hiyo haikuwa programu ya pekee?
Ilikuwa yenye kufaa sana.
Na ilisisimua sana kusikia tangazo
kwamba tunapanga kufanya makusanyiko ya
2023 ana kwa ana.
Baada ya miaka mitatu
itapendeza sana
kukutana na ndugu na dada zetu
ana kwa ana kusanyikoni.
Inasisimua pia,
kwamba tutaanza tena
huduma ya nyumba kwa nyumba,
kuanzia Septemba 1,
wakati hasa wa kuanza kampeni
ya ulimwenguni pote
ya kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Ninahakika malaika pia watasisimka,
kwa sababu,
itawapa fursa za kutusaidia
katika huduma yetu.
Tunasali Yehova abariki jitihada zetu
za kuanzisha mafunzo ya Biblia
na watu wengi
iwezekanavyo.
Limekuwa jambo lenye
kuburudisha sana
kurudia utendaji
mmoja baada ya mwingine
wa kitheokrasi.
Tunashukuru
kwa mwongozo mzuri
ambao Yehova anaandaa.
Unaimarisha imani yetu kwake.
Na uhakika wetu
katika tengenezo lake.
Ni tofauti kubwa
na ulimwengu.
Watu leo wanahangaika
kwa sababu hawajui
wamtumaini nani.
Wana mashaka
ikiwa watu
wanaowategemea
kama vile wanasiasa,
wanasayansi,
wafanyabiashara
ikiwa kweli wanawatakia mema.
Wanajiuliza,
je, kweli watu hawa wananijali
au wanahangaikia tu faida zao?
Namna gani viongozi wa dini?
Tayari watu wengi
wameacha kuwaheshimu.
Kwa hiyo haishangazi kwamba
wana mashaka
kuhusu kitabu ambacho
viongozi hao wanadai kuwakilisha
yaani Biblia.
Tunawezaje kuwasaidia watu wawe
na uhakikaa uleule ambao tunao
katika neno la Mungu?
Tuzungumzie sababu tatu
kwa nini tunaweza kuiamini Biblia.
(1) Usahihi wake,
(2) Utimizo wa unabii wa Biblia,
na (3) Nguvu za Biblia
za kubadili maisha.
Kwanza
usahihi wa Biblia
Biblia
ilikamilishwa miaka 2,000 iliyopita.
Na kufikia sasa,
maandishi ya awali ya Biblia
hayajagunduliwa kufikia leo.
Kile kilichogunduliwa
ni nakala za maandishi hayo.
Inaeleweka
watu fulani wanajiuliza
Biblia iliponakiliwa
tena na tena,
huenda ujumbe wake ulibadilishwa.
Baada ya uhamisho wa Babiloni,
kikundi cha wataalamu
kilifanya kazi kubwa
kutokeza nakala
za maandiko ya kiebrania,
na walichukua kazi hiyo
kwa uzito sana.
Walionakili baada yao
walifanya kazi
kwa umakini mkubwa pia
hivi kwamba walihesabu
si maneno tu,
bali pia herufi walizonakili
ili kuhakikisha hakuna kinachobadilishwa.
Licha ya hayo,
kwa sababu ya
kutokamilika kwa wanadamu,
kasoro ndogo sana
ziliingia katika maandishi hayo.
Wasomi katika siku zetu
wana njia za kutambua kasoro hizo.
Wanafanyaje hivyo?
Tutoe mfano.
Tuseme wanaume100
wanapewa kazi ya kunakili
ukurasa mmoja.
Na mmoja wao,
anaingiza kasoro ndogo kwenye ukurasa wake.
Njia moja ya kutambua kasoro hiyo
ni kulinganisha nakala yake
na zile nyingine 99.
Vivyohivyo,
kwa kulinganisha hati kadhaa za Biblia,
wasomi wamefaulu kutambua kasoro
au kitu kilichokosa kuandikwa
katika nakala.
Kasoro hizo,
zinaweza kurekebishwa.
Hivyo,
tunaweza kuwa na uhakika
kwamba, Biblia za kisasa
zinawasilisha kwa usahihi
ujumbe wa Mungu kwa wanadamu.
Wanaume hao walionakili hati za Biblia
walifanya kazi kwa umakini gani?
Hati ya zamani zaidi
iliyonakiliwa ya maandiko ya kiebrania,
ni ya mwaka wa 1008 au 1009
wakati wa kawaida.
Inaitwa Kodeksi ya Leningrad.
Hivi karibuni,
hati fulani za Biblia
na vipande vyake vimegunduliwa,
ambavyo ni vya miaka 1000 mapema,
kabla ya Kodeksi ya Leningrad.
Huenda tukafikiri,
kwa kuwa hati hizo zilinakiliwa
na kunakiliwa tena,
katika kipindi cha miaka 1000,
kungekuwa na tofauti kubwa
katika maandishi ya Kodeksi ya Leningrad
na hati hizo za zamani zaidi.
Sivyo ilivyo.
Wasomi wamelinganisha
nakala hizo za zamani
na za karibuni zaidi,
na wamegundua kwamba
ujumbe wa Mungu kwa wanandamu
umehifadhiwa
kwa usahihi.
Wakristo wa mapema,
walinakili kwa bidii maandiko ya kigiriki,
ambayo walitumia mikutanoni
na katika huduma.
Wasomi ambao wamelinganisha
nakala za hati hizo,
wamefikia mkataa
kwamba Biblia zetu zina ujumbe,
ambao waandishi wa awali waliandika.
Bila shaka,
ni Yehova
aliyehakikisha ujumbe wake kwa wanadamu
unahifadhiwa kwa usahihi.
Tunakumbushwa
maneno ya
Isaya 40:8:
“Neno la Mungu wetu
linadumu milele.”
Huenda
baadhi ya watu wakasema
kwa kuwa tu Biblia imehifadhiwa,
si uthibitisho kwamba
imeongozwa na roho ya Mungu.
Wazo muhimu,
basi tuchunguze uthibitisho kwamba
Biblia imeongozwa na roho ya Mungu.
Biblia ina unabii mwingi sana
ambao tayari umetimizwa.
Mfano mmoja ni
unabii wa Danieli kuhusu serikali kuu ya ulimwengu ya
Uingereza na Marekani.
Tusome unabii huo,
unaopatikana katika
Danieli 2:41-43,
unaweza kuona maandishi kwenye skrini yako.
Danieli 2:41-43
“Na kama tu ulivyoona
kwamba nyayo na vidole vya miguu kwa sehemu
vilikuwa vya udongo wa mfinyanzi
na kwa sehemu vilikuwa vya chuma,
ufalme huo utagawanyika,
lakini ugumu fulani wa chuma utakuwa ndani yake,
kama tu ulivyoona chuma
kikiwa kimechanganyika
na udongo laini wa mfinyanzi.
Na kama vile vidole vyake vya miguu
vilikuwa kwa sehemu vya chuma
na kwa sehemu vya
udongo wa mfinyanzi,
ndivyo ufalme huo utakavyokuwa
na nguvu kwa sehemu
na kuwa dhaifu kwa sehemu.
Kama tu ulivyoona chuma
kikiwa kimechanganyika
na udongo laini wa mfinyanzi,
sehemu hizo zitachanganyika na wanadamu;
lakini hazitashikamana na wanadamu,
kama tu chuma
kisivyochanganyika na
udongo wa mfinyanzi.”
Kulingana na unabii huo,
kwa sehemu
Marekani na Uingereza
zingekuwa na nguvu,
na dhaifu.
Walionyesha nguvu zao,
waliposhinda vita vya kwanza vya ulimwengu
na vya pili.
Lakini nguvu hizo zimedhoofishwa,
si na maadui wao,
bali na raia wao,
raia wanang’ang’ania haki zao,
kupitia miungano ya wafanyakazi
na kampeni za kutetea haki
na uhuru.
Hivi karibuni
mtaalamu mmoja wa
siasa za ulimwengu
alisema hivi:
“Hakuna taifa lingine
la kidemokrasia lililoendelea kiviwanda,
lililogawanyika zaidi kisiasa,
au lisilo na uwezo wa kutenda kisiasa
kama Marekani ilivyo leo.”
Namna gani sehemu
ile nyingine ya muungano huo
Uingereza?
Wamegawanyika sana
kuhusiana na ushirikiano
wanaopaswa kuwa nao
na Muungano wa Ulaya.
Kwa hiyo,
serikali kuu ya ulimwengu
ya Uingereza na Marekani,
haijawa na uwezo
wa kufanya maamuzi ya uhakika.
Kuona unabii huu na mwingine mwingi ukitimia,
kunaimarisha imani yetu
kwamba Yehova
atatimiza ahadi zake zote.
Wimbo namba 63 unasema,
Mungu wetu wa kweli
hutimiza ahadi.
Sababu ya tatu
kwa nini tunaweza
kuitumaini Biblia,
tuone jinsi kufuata ushauri wa Biblia,
kulivyomsaidia mhalifu mkatili
tutakayemuita Jack.
Jack alipokuwa gerezani
akisubiri hukumu ya kifo itekelezwe,
alijulikana sana
kuwa hatari zaidi
kati ya wafungwa waliohukumiwa kunyongwa.
Siku moja,
Jack aliketi kusikiliza
funzo la Biblia.
Alivutiwa na upendo,
na fadhili ya akina ndugu
waliokuwa wakiongoza funzo hilo.
Kwa hiyo akaomba ajifunze.
Alipotumia mambo aliyojifunza
mwenendo wake
na utu wake, ulianza kubadilika.
Baada ya muda
akabatizwa.
Na katika kipindi
alichokuwa gerezani,
aliwasaidia wafungwa wengine wanne
kupata kweli
Siku ya hukumu yake kutekelezwa,
wakili wake alisema:
“Jack
ni mtu tofauti na yule
niliyejua miaka ishirini iliyopita.
Mafundisho ya Mashahidi wa Yehova
yamebadili maisha yake.”
Sisi tunajua,
Biblia ndio inayobadili maisha.
Jean,
ni mtu mwingine
ambaye maisha yake
yalibadilika kabisa,
kwa kutumia kanuni za Biblia.
Alilelewa katika
nchi moja ya Afrika.
Vita vya
wenyewe kwa wenyewe vilipolipuka,
alijiunga na jeshi.
Na baadaye alikimbilia nchi jirani
ambako alikutana na
Mashahidi wa Yehova.
Anasema:
“Nilijifunza
kwamba, wafuasi wa dini ya kweli
hawajihusishi katika siasa.
na hawana mgawanyiko.
Badala yake
wanapendana.”
Jean anasema:
“nilikuwa nimetoa
maisha yangu kuilinda nchi.
Lakini nilipojifunza kweli za Biblia,
nilichochewa kutoa
maisha yangu kwa Yehova.”
Jean
alibadilika
kabisa.
Badala ya kupigana
na watu wenye malezi tofauti,
sasa anashiriki ujumbe wa Biblia
na watu wote anaokutana nao.
Kwa kuwa ushauri wa Biblia
unafanya kazi kwa njia nzuri,
na kuwasaidia watu
wenye malezi mengi tofauti,
ni uthibitisho wenye nguvu,
kwamba tunaweza
kutumaini neno la Mungu.
Kwa hiyo,
tumechunguza mambo matatu rahisi,
ambayo tunaweza kutumia
kuwasadikisha watu,
kwa nini wawe na uhakika
katika neno la Mungu.
Unakumbuka mambo hayo?
(1) ujumbe wa Biblia
umehifadhiwa
kwa usahihi.
(2) Unabii ulioandikwa zamani
unatimia leo.
(3) Na Biblia
inabadili
maisha.
Hali za ulimwengu
zinapozidi kuwa mbaya,
imani yetu katika kweli
itatahiniwa.
Huenda watu wakajaribu
kupanda mashaka akalini mwetu,
labda kwa kutufanya tuwe na shaka
ikiwa Biblia inasema kweli.
Lakini tukisadiki
kwamba siku zote
Biblia inasema kweli,
tutaweza kupinga
mashambulizi kama hayo
dhidi ya imani yetu.
Kweli ya Biblia
hutuimarisha.
Inatupa kusudi
na mwelekeo wa
wazi maishani.
Naam
inatupa tumaini zuri
kwa ajili ya wakati ujao.
Mwandikaji wa Zaburi 119
alisadiki kabisa kwamba neno la Mungu,
ni mwongozo unaotegemeka.
Hatujui mwandikaji huyo alikuwa nani,
lakini tunajua
alithamini neno la Mungu.
Ili kutukumbusha
jinsi kweli ya Biblia
ilivyo muhimu kwetu,
Baraza Linaloongoza limechagua
andiko la mwaka wa
2023,
litegemee Zaburi ya 119.
Uko tayari?
Ndilo hili,
Andiko la mwaka wa
2023
“Kiini hasa cha neno lako ni kweli,”
“Kiini hasa cha neno lako ni kweli,”
—Zaburi 119:160.
Tukiwa na mawazo hayo
itapendeza sana kushiriki
katika kampeni ya kuwasaidia watu
ulimwenguni pote
wenye mioyo myeupe,
kujifunza kweli zenye thamani
za Neno la Mungu.
Yehova na atubariki sote
tunaposhiriki kampeni hiyo.
Kutoka kwenye makao makuu
ya Mashahidi wa Yehova
hii
ni JW Broadcasting.