JW subtitle extractor

Ripoti ya 7 ya Baraza Linaloongoza ya 2023

Video Other languages Share text Share link Show times

Karibuni
kuna mambo yenye kusisimua
ambayo tutawaambia katika ripoti hii
nina hakika utatiwa moyo sana.
Mwezi huu
tumetimiza miaka 10
tangu kutolewa kwa
tafsiri ya ulimwengu mpya iliyorekebishwa
kwenye mkutano wa kila mwaka wa 2013.
Programu hiyo ya kihistoria
ilipeperushwa katika nchi 31
na watu zaidi ya milioni 1.4 walihudhuria
uso kwa uso au kupitia mtandao.
Sasa tafsiri ya ulimwengu mpya
inapatikana ikiwa nzima katika lugha 158
lakini tukihesabu pia
lugha ambazo zina tafsiri kamili
ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo
au ambazo zina vitabu vichache tu
vya Maandiko hayo,
Jumla ya Biblia hiyo inafikia
lugha 279.
Tafsiri hiyo iliyorekebishwa
imetusaidia sana katika huduma yetu.
Sasa baraza linaloongoza
limeidhinisha kifaa kingine kiongezwe
ili kutusaidia kupata upesi
ujumbe wenye nguvu wa Biblia.
Sote tunaamini kwamba
Neno la Mungu lina nguvu
za kutupatia faraja na mwongozo.
Kwa sababu hiyo
tuna maandiko tunayoyapenda sana
ambayo tunatumia tena na tena.
Hata hivyo,
je, kuna pindi unakumbuka tu
sehemu ya andiko
lakini hujui utalipata wapi?
Jambo hilo hutukia kwangu.
Au je labda ungependa kumfariji mtu
kwa kutumia andiko ambalo
halisikii kwa ukawaida sana.
Ikiwa ndivyo
basi utafurahi kujua kwamba
kifaa kipya kinatolewa sasa.
Kichwa chake ni
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo.
Chapisho hili
linafanana katika njia mbalimbali
na kitabu kilichotolewa mwaka wa 1965.
Kitabu “Make Sure of All Things;
Hold First to What Is Fine.”
Ukurasa wenye kichwa cha kitabu hicho
ulikifafanua kuwa
“mkusanyo wa Maandiko Matakatifu
uliopangwa chini ya vichwa
mia na ishirini na tatu.”
Kusudi lake lilikuwa nini?
Ukurasa wa kichwa ulisema
“kitabu hiki
kinaweza kutumiwa kukusadikisha
mafundisho ya Biblia
kuhusu habari hizi ni ya kweli
na pia kuwajibu wale wanaopinga imani yako.”
Kitabu Make Sure
kilipendwa sana.
Sikiliza wahubiri wawili
walipenda nini kukihusu.
Ninapenda kitabu hiki.
Kina orodha yenye kina
ya Maandiko
kuhusu vichwa kama vile malaika,
kazi
na kimenisaidia kuelewa
na kutambua kanuni muhimu za Biblia.
Kitabu Make Sure kilipotolewa
tulikuwa tukifanya upania
katika eneo ambalo
watu wanazungumzia mambo ya Biblia.
Nakumbuka pindi moja
mwanamke alizusha
kuhusu mfano wa tajiri na Lazaro
basi tukafungua kitabu Make Sure
chini ya moto wa mateso
na tukamsaidia kuelewa.
Nilikuwa kwenye jeshi la wanahewa
nilipopata kweli
kitabu hiki kilinisaidia
kuelewa wazi zaidi
habari kuhusiana na vita,
kutounga mkono upande wowote,
na urafiki na ulimwengu.
Bado nina nakala yangu.
Kilikuwa kifaa cha ufundishaji cha wakati huo
nasi mapainia hatungetaka nyumbani
bila kuwa nacho.
Kama tu kitabu Make Sure
ambacho sasa hakichapishwi tena,
kitabu hiki kipya
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
ni mkusanyo wa Maandiko
kuhusu vichwa zaidi ya 100.
Lengo la chapisho hili jipya
ni kutusaidia
ni kutimiza tunachoambiwa
kwenye 2 Timotheo 2:15,
yaani,
kulitumia sawasawa Neno la kweli.
Acheni tuzungumzie mambo fulani muhimu
ya kitabu hiki kipya.
kwa kutumia JW Library.
Kitabu Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
ambacho tutakiita
Scl
kinatusaidia kupata mistari
na masimulizi ya Biblia kwa urahisi
kutusaidia kukabiliana na changamoto
na kuwatia moyo wengine
hakiorodheshi maandiko yote
kuhusu kichwa fulani,
badala yake
kinaorodhesha habari mbalimbali
chini ya kikundi kikuu.
Ili kupata kichwa fulani,
Tumia kisanduku cha tafuta
kwenye JW Library
au ubofye kikundi kikuu.
Scl
imepangwa katika vikundi 7 vikuu.
Changamoto,
mwenendo,
kutaniko,
maisha ya kila siku,
familia,
hali ya kiroho,
na sifa.
Chagua kikundi kikuu,
halafu chunguza vichwa vilivyoorodheshwa.
Ikiwa huna uhakika
kichwa unachotafuta
kitakuwa chini ya kikundi gani kikuu
bofya zote.
Vichwa vingi vikuu
vitakuwa na sehemu hizi
chini ya kila kichwa,
utaona vichwa vidogo kadhaa,
vyenye wino mzito.
Maandiko yaliyotajwa
yanaunga mkono maelezo
au kujibu swali lililoulizwa
katika visa fulani.
Kuna mistari iliyoandikwa
tazama pia
au masimulizi ya Biblia yanayohusika.
Kitabu Scl
kinaweza kutumiwaje
tofauti na kitabu Make Sure
kilichokusudiwa hasa
kutumiwa katika huduma ya shambani.
Scl imetayarishwa,
kutusaidia kukabiliana
na changamoto tunazopata
tukiwa Wakristo wa kweli.
Wazee
mtaona kwamba kitabu hiki kipya
ni kifaa chenye thamani
kwa ajili ya ziara za uchungaji
na pia, mnapotayarisha hotuba.
Vichwa vya familia
huenda ikafaa kutumia habari zilizomo
wakati wa vipindi vyenu vya ibada ya familia.
Na wahubiri wote kutanikoni
mnaweza kutumia habari zilizomo
si tu kwa ajili ya miradi yenu
ya funzo la kibinafsi.
Bali pia,
kuwasaidia wanafunzi wenu wa Biblia kujifunza
na kutumia kanuni za Biblia
wanapofanya maamuzi.
Scl
kimeidhinishwa kutolewa
katika lugha zaidi ya 300.
Utapataje nakala yako
na swali muhimu zaidi
utapata lini nakala yako.
Tunafurahi kukujulisha
kwamba Scl
sasa inapatikana kwenye JW Library
na baadaye utapata nakala iliyochapishwa.
Scl pia,
itapatikana kwa muda
kwenye sehemu ya nini kipya.
Na utaweza pia kuipata
unapobofya sehemu ya maktaba
kwenye sehemu ya chini ya skrini yako
kisha ubofye vitabu.
Katika lugha fulani
kitabu hicho kitapatikana wakati uleule
na cha Kiingereza
na lugha zingine zitafuata baadaye.
Baraza linaloongoza lina imani
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo,
kitatusaidia sote
kufanya kama 2 Timotheo 3:17 inavyosema
tutatumia Neno la Mungu
kuwa na uwezo kamili
na kuwa na vifaa kamili
kwa ajili ya kila kazi njema.
Hilo ni muhimu sana sasa.
Tunapozama zaidi
katika siku za mwisho.
Je umewahi kuwa na woga
katika miaka kadhaa iliyopita.
Kuogopa utakuwa mgonjwa.
Kuogopa utapoteza kazi.
Kuogopa kwamba
hutaweza kuilisha familia yako.
Labda umekabili msiba fulani wa asili.
Mateso
au vita.
Huenda unahisi kwa muda mrefu sana
umeishi ukiwa na woga.
Ikiwa ndivyo,
Hilo linamaanisha nini?
Je, kuogopa kunamaanisha huna imani.
La hasha.
Wanaume waaminifu wa kale,
pindi fulani waliogopa.
Kwa mfano mfikirie Daudi.
Mfalme sauli
alitaka kumuua Daudi,
kwa sababu hiyo
Daudi asingekuwa salama nchini Israeli
kwa hiyo akaamua kukimbilia eneo lingine.
Alienda wapi?
Alienda Ghathi
huko ndiko Goliathi alizaliwa.
Unaweza kuwazia
hakuna mtu aliyempenda Daudi huko.
Kwa sababu hiyo,
Biblia inasema kwamba
Daudi akamwogopa sana
mfalme Akishi wa Gathi.
Katika kipindi hicho hatari sana
maishani mwa Daudi,
ndipo alipotunga zaburi 56.
Tuchunguze mistari kadhaa
tukianza na mstari wa kwanza.
“Nionyeshe kibali Ee Mungu
kwa sababu mwanadamu
anayeweza kufa ananishambulia.”
Ni muhimu kukumbuka hilo.
Hata mtawala aonekane
kuwa mwenye nguvu kadiri gani
bado yeye ni mwanadamu anayeweza kufa.
Anahitaji chakula na maji
ili aendelee kuishi.
Yehova anachohitaji kufanya ni
kumnyang’anya vitu hivyo.
Na mtu huyo anakufa.
Sasa tazama mstari wa 8.
Daudi anasema.
“Unafuatia kutangatanga kwangu.”
Popote pale Daudi alipoenda,
Yehova angeweza kumwona.
Kisha anaendelea kusema:
“Yakusanye machozi yangu
Katika kiriba chako cha ngozi.
Je, hayajaandikwa katika kitabu chako?”
Daudi aliyekuwa shujaa jasiri,
hakuaibika kusema
alitoa machozi pindi fulani,
kwamba pindi fulani aliogopa,
Hata hivyo,
Daudi hakuruhusu alemewe na huzuni.
Alikuwa na uhakika
kwamba Yehova alitambua machozi yake.
Na kwamba Yehova alielewa
sababu iliyomfanya Daudi alie.
Ni kana kwamba machozi yake
yaliandikwa katika kitabu
Daudi alikuwa na uhakika kwamba
siku moja kitabu hicho kingefunguliwa.
Na Yehova angewalipa kisasi.
wanaume waliomfanya alie.
Je, haipendezi kujua kwamba Yehova
hakosi kuona machozi tunayomwaga?
Unaokabili hali tata sana,
Sali.
Ikiwa kuna jambo unaloweza kufanya
sali upate hekima.
Ikiwa huwezi kufanya chochote,
sali upate amani.
Hali mbaya inapotokea,
inatufanya tuogope
lakini kumbuka
tuna silaha ya siri
ni silaha yenye nguvu.
Sala.
Tukimmwagia Yehova moyo wetu,
Yeye atatusikiliza
naye atatusaidia.
Hilo linaturudisha kwenye mstari wa 3.
Ni maneno rahisi
lakini ni yenye maana sana.
Ninapoogopa,
ninakutumaini wewe.
Ni maneno yanayofaa
yanaonyesha pindi fulani sote tunaogopa.
Lakini mstari huo
unatuambia jambo la kufanya
tumtumaini Yehova.
Mwaka ujao
tutakuwa na nafasi nyingi
za kutafakari andiko hilo
kwa sababu limechaguliwa
na Baraza Linaloongoza
kuwa andiko la mwaka wa 2024
tulirudie
Zaburi 56:3.
“Ninapoogopa ninakutumaini wewe.”
Kutoka kwenye Makao Makuu
ya Ulimwenguni Pote ya Mashahidi wa Yehova
hii ni JW Broadcasting.