JW subtitle extractor

Ripoti ya 8 ya Baraza Linaloongoza ya 2023

Video Other languages Share text Share link Show times

Karibuni ndugu na dada wapendwa
kwenye ripoti yetu.
Tungependa kuanza
na ripoti fupi
kuhusu baadhi ya misiba ya asili,
ambayo imeendelea kuwaathiri ndugu zetu
hivi karibuni.
Mwezi wa Septemba
Ndugu zetu nchini Ugiriki
walikabili mvua kubwa
na mafuriko makubwa.
Mwezi wa Oktoba
ndugu zetu nchini Mexico
walikumbwa na kimbunga kikubwa sana
ambacho kilisababisha uharibifu mkubwa sana.
Na mwezi wa Novemba
ndugu zetu nchini Filipino
walikabili tetemeko la ardhi
lenye kipimo cha 6.7.
Kwa kusikitisha
tetemeko hilo la ardhi
lilisababisha kifo cha dada mmoja
na pia ndugu na dada zetu 10
walijeruhiwa.
Tunaendelea kusali
kwa ajili ya wale walioathiriwa
na majanga mbalimbali
yanayoendelea ulimwenguni pote.
Lakini pia tunawashukuru ninyi nyote
kwa utegemezo wenu
na sala zenu.
Baadhi yenu mnafanya kazi kwa bidii
ya kutoa msaada
na wengi zaidi kati yenu
mnatoa michango kwa ukarimu,
na michango hiyo
inatusaidia kuwaandalia ndugu na dada
mahitaji yao ya lazima
na pia kuwasaidia kujenga upya nyumba zao
na Majumba yao ya Ufalme.
Tunashukuru sana
kwa msaada wenu.
Kwa niaba ya Baraza Linaloongoza tunasema
asanteni.
Lakini kuanzia hapa katika ripoti hii,
acheni tuzungumzie kichwa
“Tunajipendekeza
Kuwa Wahudumu wa Mungu”
kichwa hicho kinategemea 2 Wakorintho 6:4
Ambapo mtume Paulo alisema
“katika kila njia
tunajipendekeza kuwa wahudumu
wa Mungu.”
Hilo linamaanisha nini?
Habari za utafiti katika Biblia ya kiingereza
zinasema; “Kitenzi cha Kigiriki kinachotafsiriwa
tunajipendekeza,
kinatoa wazo la
tunajithibitisha
au tunajionyesha wenyewe kuwa.”
Lakini
tunajionyeshaje wenyewe
kuwa wahudumu
wa Mungu wa kweli?
Njia moja muhimu
ni kupitia
mwonekano wetu.
Sisi sote tungependa sifa zimwendee
Mungu wetu tunayempenda
na tunayemwabudu.
Tunawezaje kufanya hivyo?
Kwa kufuata kanuni za Biblia.
Kwa mfano,
fikiria kanuni hii,
inayotajwa kwenye 1 Timotheo 2:9, 10
“Vivyo hivyo,
wanawake wanapaswa kujipamba
kwa mavazi yanayofaa,
kwa kiasi
na utimamu wa akili.
Si kwa mitindo ya kusuka nywele,
dhahabu,
lulu au mavazi ya bei ghali sana,
bali
kwa njia inayowafaa wanawake
wanaokiri kwamba
wanamtumikia Mungu,
yaani,
kupitia matendo mema.”
Ingawa shauri hilo limeelekezwa
kwa wanawake Wakristo,
kanuni hiyo inatumika vilevile kwa wanaume
kama tu kwa wanawake.
Kwa hiyo njia moja
sisi sote
tunaweza kujipendekeza
kuwa wahudumu wa Mungu
ni kwa kuhakikisha kwamba,
mwonekano wetu,
unafaa,
ni wenye kiasi,
unaoonyesha utimamu wa akili.
Lakini je, hilo linamaanisha kwamba
Mashahidi wote wa Yehova
wanafanya maamuzi yaleyale?
Je, tunapaswa,
kuvaa sare?
Au je tunapaswa kujipamba
na kuvaa kwa mtindo uleule mmoja?
Bila shaka la.
Kuna zaidi ya Mashahidi wa Yehova
milioni nane ulimwenguni pote.
Nasi tumetoka
katika tamaduni mbalimbali,
Yehova amevuta
mamilioni ya watu hao wote,
naye anapenda
unamna-namna.
Lakini sasa tuulize,
namna gani kuhusu kufuga
ndevu?
Je inafaa kwa ndugu
kufanya hivyo?
Ili kutusaidia kujibu swali hilo
acheni tutazame video ifuatayo,
ambayo itazungumzia
historia ya ndevu,
miongoni mwa watu wa Yehova.
Katika nyakati za kale,
lilikuwa jambo la kawaida kwa wanaume
kufuga ndevu.
Zoea hilo liliendelea
miongoni mwa Waisraeli.
Mwanamume Mwisraeli
angenyoa ndevu wakati tu alipoaibishwa,
au alipokuwa akiomboleza.
Kwa mfano,
mfalme wa Amoni
alipowaaibisha watumishi wa Daudi
kwa kunyoa ndevu zao,
Daudi alilinda heshima yao
kwa kuwaambia hivi:
“Kaeni Yeriko
mpaka ndevu zenu zitakapoota,
kisha mrudi.”
Karne nyingi baadaye,
nabii Ezekieli alinyoa ndevu
na nywele za kichwa chake
ili kuonyesha msiba mkubwa na huzuni
ambayo jiji la Yerusalemu lingekabili.
Namna gani Yesu,
kwa kuwa alikuwa Mwisraeli,
je, yeye pia alifuga ndevu?
Kwa miaka kadhaa
kwa kutegemea maoni ya waakiolojia fulani,
mara nyingi machapisho yetu
yalionyesha picha za Yesu
akiwa amenyoa ndevu.
Hata hivyo,
katika mwaka wa 1968,
Mnara wa Mlinzi
lilichunguza uthibitisho unaoaminika zaidi,
kutoka kwenye vyanzo vya kihistoria
na kwenye Maandiko.
Hakuna Injili yoyote iliyoonyesha kwamba
mwonekano wa Yesu
ulitofautiana na wa watu wengine.
Alifanya jambo
lililokuwa la kawaida
miongoni mwa wanaume Wayahudi wakati huo,
alifuga ndevu.
Tangu wakati huo,
video zetu na picha katika machapisho yetu,
zimemuonyesha Yesu
akiwa na ndevu zilizotunzwa vizuri.
Kufikia wakati ambapo
kutaniko la Kikristo lilianzishwa,
lilikuwa jambo la kawaida
kwa Waroma kunyoa ndevu.
Je, Wakristo Wayahudi
walitarajiwa kunyoa ndevu?
Au je, Wakristo wa mataifa
walitarajiwa kufuga ndevu
ili waweze kufanana
na ndugu zao Wayahudi?
Haionekani hivyo.
Kwa kuwa Maandiko
hayawaagizi waabudu wa kweli wafuge ndevu
wala kuzinyoa,
huo ulikuwa uamuzi
wa kibinafsi.
Katika miaka ya mwisho-mwisho
ya karne ya 19 na
mwanzoni mwa karne ya 20,
lilikuwa jambo la kawaida kufuga ndevu
hata miongoni mwa wanafunzi wa Biblia.
Kama picha hizi waangalizi wasafirio
walioitwa Mapilgrimu zinavyoonyesha.
Ndugu Russel pia,
alifuga ndevu.
Mhariri mmoja wa gazeti la habari alimwita,
mhudumu aliyekuwa nadhifu.
Mhariri huyo alisema:
“Sijawahi kufikiri kwamba alikuwa tofauti
na maelfu ya wahubiri wengine.
Ndevu zake nyeupe,
nyororo zinamfanya aonekane
kama mzee wa ukoo,
kama baba,
zinakufanya uwe na uhakika naye.”
Muda mfupi
baada ya Vita vya Kwanza vya Ulimwengu,
lilianza tena kuwa jambo la kawaida
kunyoa ndevu.
Mwaka wa 1919
picha hii ya mapilgrimu ilipopigwa,
wengi kati yao
hawakuwa na ndevu.
Ingawa machapisho yetu
hayakusema mengi kuhusu hilo wakati huo,
ni ndugu wachache sana
waliofuga ndevu.
Katika nchi nyingi
kuanzia mwaka wa 1960,
ndevu zililihusianishwa
na wale waliopinga mamlaka iliyowekwa.
kwa sababu hiyo
wanaume wengi walichagua kunyoa ndevu,
iwe walikuwa Mashahidi
au hawakuwa Mashahidi.
Kwa sababu ya maoni yasiyofaa
yaliyohusianishwa na kufuga ndevu,
ndugu wengi walifuga ndevu
hawakuwekwa kuwa watumishi wa huduma,
wazee,
au kupewa majukumu mengine.
Katika nchi fulani
kadiri ambavyo muda ulivyopita,
ndevu zikaja kuwa jambo la kawaida
na hazikuhusianishwa na uasi.
Katika maeneo hayo,
baadhi ya akina ndugu waliokuwa na ndevu,
waliwekwa rasmi
kuwa watumishi wa huduma na wazee.
Katika nyakati za karibuni,
limekuwa jambo la kawaida
katika nchi nyingi kufuga ndevu.
Kwa hiyo, tunapaswa kumwonaje
ndugu anayechagua kufuga ndevu leo?
Video hiyo imemalizia
kwa swali, lenye kuchochea fikira.
Tunapaswa kumwonaje,
ndugu anayechagua
kufuga ndevu leo?
Baraza Linaloongoza, limeniomba
nisome tangazo lifuatalo.
“Ofisi kadhaa za tawi, ulimwenguni
zimetuandikia,
zikionyesha kwamba,
bado kuna maswali mengi yanayoulizwa,
kuhusu ikiwa
ni sawa au la
kwa ndugu aliyewekwa rasmi
kufuga ndevu.
Baada ya kufikiria jambo hilo kwa sala,
Baraza Linaloongoza
limeona kwamba kuna uhitaji
wa kuweka wazi jambo hili.
Baraza Linaloongoza
halipingi kwamba
akina ndugu wanaweza kufuga ndevu.
Kwa nini?
Kwa sababu Maandiko
hayashutumu kufuga ndevu.
” Mbali na hilo
kadiri ambavyo muda umepita,
tumeona kwamba
katika nchi nyingi,
inakubalika kwa wanaume,
walio na mamlaka katika biashara,
au hata serikalini,
kufuga ndevu.
Kwa hiyo
ikiwa ndugu atachagua kufuga ndevu,
huo ni uamuzi
wa kibinafsi.
Sifa za kustahili kwa ndugu
kutumikia akiwa mzee au mtumishi wa huduma,
zinategemea
hali yake ya kiroho,
bali hazitegemei ikiwa anaamua
kufuga ndevu.
Mwongozo huo pia unatumika,
kwa watumishi wa wakati wote
walio Betheli,
na wale walio shambani,
kutia ndani mapainia wa pekee,
wamishonari,
na waangalizi wa mzunguko.
Kupatana na andiko la Waroma 14:4,
wazee
wala Mkristo mwingine yeyote,
hawapaswi kumhukumu
ndugu anayeamua
kufuga ndevu.
Tunaamini kwamba maelezo haya
yatatusaidia tuendelee kujilinda,
dhidi ya chochote
ambacho kinaweza kusababisha migawanyiko
miongoni mwa watu wa Yehova.
Huo ndio mwisho wa tangazo
la Baraza Linaloongoza.
Hata hivyo, mwongozo huu
huenda ukaibua maswali.
Kwa mfano swali moja:
Kwa nini Baraza linaloongoza
linatoa mwongozo huu
wakati huu?
Kama ilivyoandikwa kwenye 1 Wakorintho 7:31,
mtume Paulo aliongozwa na roho kuandika:
“tamasha ya ulimwengu huu
inabadilika.”
Habari za utafiti za mstari huo
zinaonyesha kwamba huenda Paulo,
alikuwa akirejelea
jinsi maonyesho
yanavyobadilika upesi,
katika jumba la maonyesho.
Waigizaji
wakipanda na kutoka
kwenye jukwaa upesi.
Kupatana na kanuni ya maneno hayo ya Paulo
yaliyoongozwa na roho,
mitindo ya kujipamba
imebadilika kadiri ambavyo miaka imepita.
Kwa mfano,
wanaume wengi zaidi
walio na madaraka,
wanafuga ndevu
na bado wanaonekana
kuwa wana mwonekano
wenye kuheshimika.
Swali lingine:
Tunapaswa kuwa na maoni gani
kuhusu ndugu anayeamua
kufuga ndevu?
Tunapaswa kutumia shauri la Yesu,
linalopatikana kwenye Yohana 7:24.
“Acheni kuhukumu,
kwa kutazama sura ya nje tu.”
Kama tulivyoona katika video,
mitindo ya kujipamba ilibadilika
kadiri muda ulivyopita.
Si kwamba
mabadiliko haya yote yalikuwa mabaya.
Kwa mfano,
huenda hakuna yeyote kati yetu
ambaye angependa kuvalia na kujipamba
kama watu walivyofanya,
katika nyakati za Biblia,
au pia huenda tusingependa
kujipamba na kuvalia
kama walivyofanya karne moja iliyopita,
kwa kweli
wengi hupenda kufuata mitindo
ambayo inafaa leo,
si ile ya makumi ya miaka iliyopita.
Kwa kweli si vibaya kuvalia au kujipamba
kama vile ambavyo watu wengi
katika jamii yetu wanavyofanya leo.
Maadamu,
mtindo huo tunaoiga
hauvunji kanuni
za Biblia.
Sikuzote tungependa kuhakikisha
mwonekano wetu,
unaonekana safi,
ni wenye kiasi
na wenye utimamu wa akili.
Swali lingine;
tunawezaje kuendeleza umoja
baada ya kupata mwelekezo huu?
Baada ya kutazama programu hii,
huenda baadhi wakalazimika
kukabiliana na hisia kali sana.
Kwa mfano,
huenda baadhi
wakahisi kwamba
wameshinda
na kusema kwamba
hayo ndiyo yamekuwa maoni yangu
kwa muda mrefu.
Hilo linathibitisha
mimi nilikuwa sahihi
muda wote huo.
Huenda wengine wakahisi,
wamevunjika moyo
labda watasema,
kwa miaka yote hiyo
nilitii mwongozo kuhusu kujipamba,
lakini sasa
nimekatishwa tamaa.
Je, kuna maoni yoyote
yaliyo sawa kati ya hayo mawili?
Hapana,
Ona kile ambacho mtume Paulo
aliongozwa na roho kuandika
kwenye 1 Wakorintho 1:10.
“Sasa ninawahimiza ninyi akina ndugu,
kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo,
kwamba nyote mseme
kwa upatano.
Na kwamba kusiwe na migawanyiko
kati yenu,
bali kwamba muunganishwe
kabisa
katika akili ileile
na njia ileile ya kufikiri.”
Kanuni hiyo inatumakaje hapa?
Ikiwa
tumekuwa tukiendeleza
maoni yetu wenyewe
ya kibinafsi
kuhusu hili,
yanayopingana na mwongozo wa tengenezo,
je tumekuwa tukiendeleza umoja?
Je, tumekuwa tukisaidia undugu wetu
kuunganishwa
katika njia ileile ya kufikiri?
Ni wazi la.
Wowote
ambao wamefanya hivyo
wanahitaji kubadili kufikiri
na mtazamo wao.
Kwa upande mwingine
ikiwa miaka yote tumekuwa tukiunga mkono
mwongozo wa tengenezo kwa ushikamanifu,
je, tuna sababu yoyote ya kimaandiko
kujutia
kwamba tulifanya hivyo?
Bila shaka la.
Yehova anathamini sana
utumishi wetu mshikamanifu,
pia, anathamini utayari wetu
wa unyenyekevu,
wa kutii na kujitiisha
kwa mwongozo tunaopata
kutoka kwa tengenezo la Mungu.
Katika karne ya kwanza W.K.
baadhi ya Wakristo waliruhusu
suala la kutahiriwa,
lisababishe
migawanyiko.
Lakini roho takatifu iliongoza
Baraza Linaloongoza,
litatue suala hilo
na kuendeleza umoja.
Vivyo hivyo,
Baraza Linaloongoza leo
linajitahidi kuendeleza umoja.
Tusingependa kamwe
suala kuhusu kufuga ndevu,
lisababishe migawanyiko
miongoni mwetu.
Sisi sote tunahitaji kukumbuka
kwamba sehemu ya kidunia
ya tengenezo la Yehova
inajitahidi sikuzote kujipatanisha
na sehemu ya kimbingu
na kwenda sambamba nayo.
Je, unakumbuka katika maono ya Ezekieli
gari la kimbingu linasonga kwa kasi kadiri gani,
kama radi inayowakawaka.
Mtu yeyote anayejaribu
kutangulia gari hilo
na kulazimisha mabadiliko
kabla ya wakati,
au
kubaki nyuma
akisitasita
kuunga mkono mabadiliko
ambayo yametoka kwa mtumwa mwaminifu,
haendi sambamba
na tengenezo la Yehova.
Kwa kumalizia,
je, hatushukuru
kwa mwongozo huo wenye usawaziko
kuhusu kufuga ndevu?
Yehova ametuonyesha heshima,
amempa kila ndugu uhuru
wa kuchagua ikiwa
atafuga ndevu au la.
Tuna uhakika kwamba
ninyi nyote mmeazimia
kwenda sambamba
na kubadili maoni yenu inavyohitajika,
na kuendelea kumtumikia Yehova
kwa ushikamanifu,
mkiendeleza upendo
na umoja miongoni mwa ndugu
na dada zenu.
Kutoka kwenye Makao Makuu
ya Ulimwenguni Pote ya Mashahidi wa Yehova,
hii
ni JW Broadcasting