00:00:01
Karibuni ndugu na dada wapendwa00:00:04
00:00:05
kwenye ripoti yetu. 00:00:06
00:00:08
Tungependa kuanza00:00:09
00:00:09
na ripoti fupi00:00:10
00:00:11
kuhusu baadhi ya misiba ya asili,00:00:13
00:00:14
ambayo imeendelea kuwaathiri ndugu zetu00:00:17
00:00:17
hivi karibuni.00:00:18
00:00:19
Mwezi wa Septemba00:00:20
00:00:21
Ndugu zetu nchini Ugiriki00:00:23
00:00:23
walikabili mvua kubwa00:00:25
00:00:25
na mafuriko makubwa.00:00:26
00:00:28
Mwezi wa Oktoba00:00:29
00:00:29
ndugu zetu nchini Mexico00:00:31
00:00:32
walikumbwa na kimbunga kikubwa sana00:00:34
00:00:35
ambacho kilisababisha uharibifu mkubwa sana.00:00:38
00:00:39
Na mwezi wa Novemba00:00:40
00:00:41
ndugu zetu nchini Filipino00:00:43
00:00:43
walikabili tetemeko la ardhi00:00:45
00:00:45
lenye kipimo cha 6.7.00:00:47
00:00:48
Kwa kusikitisha00:00:50
00:00:50
tetemeko hilo la ardhi00:00:52
00:00:52
lilisababisha kifo cha dada mmoja00:00:55
00:00:55
na pia ndugu na dada zetu 1000:00:58
00:00:58
walijeruhiwa.00:00:59
00:01:00
Tunaendelea kusali00:01:02
00:01:02
kwa ajili ya wale walioathiriwa00:01:04
00:01:04
na majanga mbalimbali00:01:06
00:01:06
yanayoendelea ulimwenguni pote. 00:01:09
00:01:09
Lakini pia tunawashukuru ninyi nyote00:01:12
00:01:12
kwa utegemezo wenu00:01:14
00:01:14
na sala zenu.00:01:15
00:01:15
Baadhi yenu mnafanya kazi kwa bidii00:01:18
00:01:18
ya kutoa msaada00:01:19
00:01:20
na wengi zaidi kati yenu00:01:22
00:01:22
mnatoa michango kwa ukarimu,00:01:24
00:01:24
na michango hiyo00:01:25
00:01:26
inatusaidia kuwaandalia ndugu na dada00:01:28
00:01:28
mahitaji yao ya lazima00:01:30
00:01:30
na pia kuwasaidia kujenga upya nyumba zao00:01:33
00:01:33
na Majumba yao ya Ufalme.00:01:35
00:01:35
Tunashukuru sana00:01:37
00:01:37
kwa msaada wenu.00:01:39
00:01:39
Kwa niaba ya Baraza Linaloongoza tunasema00:01:42
00:01:42
asanteni. 00:01:44
00:01:46
Lakini kuanzia hapa katika ripoti hii,00:01:48
00:01:49
acheni tuzungumzie kichwa00:01:51
00:01:52
“Tunajipendekeza00:01:53
00:01:53
Kuwa Wahudumu wa Mungu”00:01:55
00:01:56
kichwa hicho kinategemea 2 Wakorintho 6:400:02:00
00:02:00
Ambapo mtume Paulo alisema00:02:02
00:02:03
“katika kila njia00:02:04
00:02:05
tunajipendekeza kuwa wahudumu00:02:08
00:02:08
wa Mungu.”00:02:08
00:02:10
Hilo linamaanisha nini? 00:02:12
00:02:13
Habari za utafiti katika Biblia ya kiingereza00:02:15
00:02:15
zinasema; “Kitenzi cha Kigiriki kinachotafsiriwa00:02:18
00:02:18
tunajipendekeza,00:02:20
00:02:20
kinatoa wazo la00:02:22
00:02:22
tunajithibitisha00:02:24
00:02:24
au tunajionyesha wenyewe kuwa.”00:02:27
00:02:28
Lakini00:02:29
00:02:29
tunajionyeshaje wenyewe00:02:31
00:02:31
kuwa wahudumu00:02:32
00:02:32
wa Mungu wa kweli?00:02:34
00:02:35
Njia moja muhimu00:02:36
00:02:37
ni kupitia00:02:38
00:02:38
mwonekano wetu.00:02:40
00:02:40
Sisi sote tungependa sifa zimwendee00:02:43
00:02:43
Mungu wetu tunayempenda00:02:45
00:02:45
na tunayemwabudu.00:02:47
00:02:47
Tunawezaje kufanya hivyo?00:02:49
00:02:49
Kwa kufuata kanuni za Biblia.00:02:52
00:02:52
Kwa mfano,00:02:52
00:02:53
fikiria kanuni hii,00:02:55
00:02:55
inayotajwa kwenye 1 Timotheo 2:9, 1000:03:01
00:03:02
“Vivyo hivyo,00:03:03
00:03:03
wanawake wanapaswa kujipamba00:03:06
00:03:06
kwa mavazi yanayofaa,00:03:08
00:03:09
kwa kiasi00:03:10
00:03:11
na utimamu wa akili.00:03:13
00:03:14
Si kwa mitindo ya kusuka nywele,00:03:16
00:03:16
dhahabu,00:03:17
00:03:17
lulu au mavazi ya bei ghali sana,00:03:21
00:03:21
bali00:03:22
00:03:22
kwa njia inayowafaa wanawake00:03:25
00:03:25
wanaokiri kwamba00:03:26
00:03:27
wanamtumikia Mungu,00:03:29
00:03:29
yaani,00:03:30
00:03:30
kupitia matendo mema.”00:03:32
00:03:34
Ingawa shauri hilo limeelekezwa00:03:37
00:03:37
kwa wanawake Wakristo,00:03:39
00:03:40
kanuni hiyo inatumika vilevile kwa wanaume00:03:43
00:03:43
kama tu kwa wanawake.00:03:44
00:03:45
Kwa hiyo njia moja00:03:47
00:03:47
sisi sote00:03:48
00:03:48
tunaweza kujipendekeza00:03:50
00:03:50
kuwa wahudumu wa Mungu00:03:52
00:03:53
ni kwa kuhakikisha kwamba,00:03:54
00:03:55
mwonekano wetu,00:03:57
00:03:57
unafaa,00:03:58
00:03:59
ni wenye kiasi,00:04:00
00:04:00
unaoonyesha utimamu wa akili. 00:04:03
00:04:05
Lakini je, hilo linamaanisha kwamba00:04:07
00:04:07
Mashahidi wote wa Yehova00:04:08
00:04:08
wanafanya maamuzi yaleyale?00:04:10
00:04:11
Je, tunapaswa,00:04:13
00:04:13
kuvaa sare?00:04:14
00:04:15
Au je tunapaswa kujipamba00:04:17
00:04:17
na kuvaa kwa mtindo uleule mmoja?00:04:20
00:04:21
Bila shaka la.00:04:23
00:04:23
Kuna zaidi ya Mashahidi wa Yehova00:04:26
00:04:26
milioni nane ulimwenguni pote.00:04:28
00:04:29
Nasi tumetoka00:04:30
00:04:30
katika tamaduni mbalimbali,00:04:32
00:04:33
Yehova amevuta00:04:35
00:04:35
mamilioni ya watu hao wote,00:04:37
00:04:37
naye anapenda00:04:39
00:04:39
unamna-namna. 00:04:41
00:04:43
Lakini sasa tuulize,00:04:44
00:04:45
namna gani kuhusu kufuga00:04:47
00:04:48
ndevu?00:04:48
00:04:49
Je inafaa kwa ndugu00:04:51
00:04:52
kufanya hivyo?00:04:52
00:04:54
Ili kutusaidia kujibu swali hilo00:04:56
00:04:56
acheni tutazame video ifuatayo,00:04:59
00:05:00
ambayo itazungumzia00:05:01
00:05:01
historia ya ndevu,00:05:03
00:05:04
miongoni mwa watu wa Yehova.00:05:06
00:05:10
Katika nyakati za kale,00:05:12
00:05:12
lilikuwa jambo la kawaida kwa wanaume00:05:14
00:05:14
kufuga ndevu.00:05:15
00:05:16
Zoea hilo liliendelea00:05:17
00:05:17
miongoni mwa Waisraeli.00:05:19
00:05:19
Mwanamume Mwisraeli00:05:21
00:05:21
angenyoa ndevu wakati tu alipoaibishwa,00:05:23
00:05:23
au alipokuwa akiomboleza.00:05:25
00:05:26
Kwa mfano,00:05:27
00:05:27
mfalme wa Amoni00:05:28
00:05:28
alipowaaibisha watumishi wa Daudi00:05:30
00:05:30
kwa kunyoa ndevu zao,00:05:32
00:05:32
Daudi alilinda heshima yao00:05:33
00:05:33
kwa kuwaambia hivi:00:05:35
00:05:35
“Kaeni Yeriko00:05:36
00:05:37
mpaka ndevu zenu zitakapoota,00:05:38
00:05:39
kisha mrudi.” 00:05:40
00:05:40
Karne nyingi baadaye,00:05:42
00:05:42
nabii Ezekieli alinyoa ndevu00:05:44
00:05:44
na nywele za kichwa chake00:05:45
00:05:45
ili kuonyesha msiba mkubwa na huzuni00:05:48
00:05:48
ambayo jiji la Yerusalemu lingekabili. 00:05:51
00:05:51
Namna gani Yesu,00:05:52
00:05:52
kwa kuwa alikuwa Mwisraeli,00:05:54
00:05:54
je, yeye pia alifuga ndevu?00:05:56
00:05:56
Kwa miaka kadhaa00:05:57
00:05:58
kwa kutegemea maoni ya waakiolojia fulani,00:06:00
00:06:00
mara nyingi machapisho yetu00:06:02
00:06:02
yalionyesha picha za Yesu00:06:03
00:06:03
akiwa amenyoa ndevu.00:06:04
00:06:05
Hata hivyo,00:06:06
00:06:06
katika mwaka wa 1968,00:06:08
00:06:08
Mnara wa Mlinzi00:06:09
00:06:09
lilichunguza uthibitisho unaoaminika zaidi,00:06:12
00:06:12
kutoka kwenye vyanzo vya kihistoria00:06:14
00:06:14
na kwenye Maandiko.00:06:15
00:06:16
Hakuna Injili yoyote iliyoonyesha kwamba00:06:18
00:06:18
mwonekano wa Yesu00:06:19
00:06:19
ulitofautiana na wa watu wengine.00:06:21
00:06:22
Alifanya jambo00:06:22
00:06:22
lililokuwa la kawaida00:06:23
00:06:23
miongoni mwa wanaume Wayahudi wakati huo,00:06:26
00:06:26
alifuga ndevu.00:06:27
00:06:28
Tangu wakati huo,00:06:29
00:06:29
video zetu na picha katika machapisho yetu,00:06:32
00:06:32
zimemuonyesha Yesu00:06:33
00:06:33
akiwa na ndevu zilizotunzwa vizuri. 00:06:36
00:06:37
Kufikia wakati ambapo00:06:39
00:06:39
kutaniko la Kikristo lilianzishwa,00:06:41
00:06:41
lilikuwa jambo la kawaida00:06:42
00:06:42
kwa Waroma kunyoa ndevu.00:06:44
00:06:44
Je, Wakristo Wayahudi00:06:46
00:06:46
walitarajiwa kunyoa ndevu?00:06:48
00:06:48
Au je, Wakristo wa mataifa00:06:50
00:06:50
walitarajiwa kufuga ndevu00:06:51
00:06:51
ili waweze kufanana00:06:53
00:06:53
na ndugu zao Wayahudi?00:06:54
00:06:54
Haionekani hivyo.00:06:56
00:06:56
Kwa kuwa Maandiko00:06:57
00:06:57
hayawaagizi waabudu wa kweli wafuge ndevu 00:07:00
00:07:00
wala kuzinyoa,00:07:01
00:07:02
huo ulikuwa uamuzi00:07:04
00:07:04
wa kibinafsi. 00:07:05
00:07:06
Katika miaka ya mwisho-mwisho00:07:07
00:07:07
ya karne ya 19 na00:07:08
00:07:08
mwanzoni mwa karne ya 20,00:07:10
00:07:10
lilikuwa jambo la kawaida kufuga ndevu00:07:12
00:07:12
hata miongoni mwa wanafunzi wa Biblia.00:07:14
00:07:14
Kama picha hizi waangalizi wasafirio00:07:16
00:07:16
walioitwa Mapilgrimu zinavyoonyesha.00:07:19
00:07:19
Ndugu Russel pia,00:07:20
00:07:20
alifuga ndevu.00:07:21
00:07:22
Mhariri mmoja wa gazeti la habari alimwita,00:07:24
00:07:25
mhudumu aliyekuwa nadhifu.00:07:26
00:07:26
Mhariri huyo alisema:00:07:28
00:07:28
“Sijawahi kufikiri kwamba alikuwa tofauti00:07:30
00:07:30
na maelfu ya wahubiri wengine.00:07:32
00:07:33
Ndevu zake nyeupe, 00:07:34
00:07:34
nyororo zinamfanya aonekane00:07:36
00:07:36
kama mzee wa ukoo,00:07:37
00:07:37
kama baba,00:07:38
00:07:38
zinakufanya uwe na uhakika naye.” 00:07:40
00:07:40
Muda mfupi00:07:41
00:07:41
baada ya Vita vya Kwanza vya Ulimwengu,00:07:43
00:07:43
lilianza tena kuwa jambo la kawaida00:07:45
00:07:45
kunyoa ndevu.00:07:46
00:07:46
Mwaka wa 191900:07:48
00:07:48
picha hii ya mapilgrimu ilipopigwa,00:07:50
00:07:50
wengi kati yao00:07:51
00:07:51
hawakuwa na ndevu.00:07:52
00:07:52
Ingawa machapisho yetu00:07:53
00:07:53
hayakusema mengi kuhusu hilo wakati huo,00:07:56
00:07:56
ni ndugu wachache sana00:07:57
00:07:57
waliofuga ndevu.00:07:59
00:07:59
Katika nchi nyingi00:08:00
00:08:00
kuanzia mwaka wa 1960,00:08:02
00:08:03
ndevu zililihusianishwa00:08:04
00:08:04
na wale waliopinga mamlaka iliyowekwa.00:08:06
00:08:07
kwa sababu hiyo00:08:08
00:08:08
wanaume wengi walichagua kunyoa ndevu,00:08:10
00:08:10
iwe walikuwa Mashahidi00:08:12
00:08:12
au hawakuwa Mashahidi.00:08:14
00:08:14
Kwa sababu ya maoni yasiyofaa00:08:16
00:08:16
yaliyohusianishwa na kufuga ndevu,00:08:18
00:08:18
ndugu wengi walifuga ndevu00:08:19
00:08:19
hawakuwekwa kuwa watumishi wa huduma,00:08:22
00:08:22
wazee,00:08:22
00:08:23
au kupewa majukumu mengine. 00:08:24
00:08:26
Katika nchi fulani00:08:27
00:08:27
kadiri ambavyo muda ulivyopita,00:08:29
00:08:29
ndevu zikaja kuwa jambo la kawaida00:08:31
00:08:31
na hazikuhusianishwa na uasi.00:08:33
00:08:33
Katika maeneo hayo,00:08:35
00:08:35
baadhi ya akina ndugu waliokuwa na ndevu,00:08:37
00:08:37
waliwekwa rasmi00:08:38
00:08:38
kuwa watumishi wa huduma na wazee.00:08:40
00:08:40
Katika nyakati za karibuni,00:08:42
00:08:42
limekuwa jambo la kawaida00:08:43
00:08:43
katika nchi nyingi kufuga ndevu.00:08:45
00:08:46
Kwa hiyo, tunapaswa kumwonaje00:08:47
00:08:47
ndugu anayechagua kufuga ndevu leo?00:08:50
00:08:54
Video hiyo imemalizia00:08:56
00:08:56
kwa swali, lenye kuchochea fikira.00:08:59
00:09:00
Tunapaswa kumwonaje,00:09:02
00:09:02
ndugu anayechagua00:09:04
00:09:04
kufuga ndevu leo? 00:09:05
00:09:07
Baraza Linaloongoza, limeniomba00:09:09
00:09:09
nisome tangazo lifuatalo.00:09:12
00:09:14
“Ofisi kadhaa za tawi, ulimwenguni00:09:16
00:09:16
zimetuandikia,00:09:18
00:09:18
zikionyesha kwamba,00:09:20
00:09:20
bado kuna maswali mengi yanayoulizwa,00:09:23
00:09:23
kuhusu ikiwa00:09:24
00:09:25
ni sawa au la00:09:26
00:09:26
kwa ndugu aliyewekwa rasmi00:09:29
00:09:29
kufuga ndevu.00:09:30
00:09:31
Baada ya kufikiria jambo hilo kwa sala,00:09:34
00:09:34
Baraza Linaloongoza00:09:36
00:09:36
limeona kwamba kuna uhitaji00:09:38
00:09:38
wa kuweka wazi jambo hili.00:09:40
00:09:41
Baraza Linaloongoza00:09:44
00:09:44
halipingi kwamba00:09:45
00:09:45
akina ndugu wanaweza kufuga ndevu.00:09:48
00:09:49
Kwa nini?00:09:49
00:09:50
Kwa sababu Maandiko00:09:52
00:09:52
hayashutumu kufuga ndevu.00:09:55
00:09:56
” Mbali na hilo00:09:57
00:09:58
kadiri ambavyo muda umepita,00:10:00
00:10:00
tumeona kwamba00:10:01
00:10:01
katika nchi nyingi,00:10:03
00:10:03
inakubalika kwa wanaume,00:10:05
00:10:05
walio na mamlaka katika biashara,00:10:08
00:10:08
au hata serikalini,00:10:10
00:10:11
kufuga ndevu.00:10:12
00:10:13
Kwa hiyo00:10:13
00:10:14
ikiwa ndugu atachagua kufuga ndevu,00:10:16
00:10:17
huo ni uamuzi00:10:19
00:10:19
wa kibinafsi.00:10:20
00:10:21
Sifa za kustahili kwa ndugu00:10:23
00:10:23
kutumikia akiwa mzee au mtumishi wa huduma,00:10:26
00:10:27
zinategemea00:10:28
00:10:29
hali yake ya kiroho,00:10:31
00:10:31
bali hazitegemei ikiwa anaamua00:10:34
00:10:34
kufuga ndevu.00:10:35
00:10:35
Mwongozo huo pia unatumika,00:10:37
00:10:37
kwa watumishi wa wakati wote00:10:40
00:10:40
walio Betheli,00:10:41
00:10:42
na wale walio shambani,00:10:43
00:10:43
kutia ndani mapainia wa pekee,00:10:46
00:10:46
wamishonari,00:10:47
00:10:47
na waangalizi wa mzunguko. 00:10:49
00:10:50
Kupatana na andiko la Waroma 14:4,00:10:54
00:10:54
wazee00:10:55
00:10:56
wala Mkristo mwingine yeyote,00:10:58
00:10:58
hawapaswi kumhukumu00:11:01
00:11:01
ndugu anayeamua00:11:03
00:11:03
kufuga ndevu.00:11:05
00:11:05
Tunaamini kwamba maelezo haya00:11:08
00:11:08
yatatusaidia tuendelee kujilinda,00:11:10
00:11:10
dhidi ya chochote00:11:12
00:11:12
ambacho kinaweza kusababisha migawanyiko00:11:15
00:11:15
miongoni mwa watu wa Yehova.00:11:17
00:11:18
Huo ndio mwisho wa tangazo00:11:19
00:11:20
la Baraza Linaloongoza. 00:11:21
00:11:24
Hata hivyo, mwongozo huu00:11:26
00:11:26
huenda ukaibua maswali.00:11:28
00:11:30
Kwa mfano swali moja:00:11:31
00:11:32
Kwa nini Baraza linaloongoza00:11:34
00:11:34
linatoa mwongozo huu00:11:36
00:11:36
wakati huu?00:11:37
00:11:38
Kama ilivyoandikwa kwenye 1 Wakorintho 7:31,00:11:42
00:11:42
mtume Paulo aliongozwa na roho kuandika:00:11:44
00:11:45
“tamasha ya ulimwengu huu00:11:47
00:11:47
inabadilika.”00:11:49
00:11:50
Habari za utafiti za mstari huo00:11:52
00:11:52
zinaonyesha kwamba huenda Paulo,00:11:55
00:11:55
alikuwa akirejelea00:11:56
00:11:56
jinsi maonyesho00:11:57
00:11:57
yanavyobadilika upesi,00:11:59
00:11:59
katika jumba la maonyesho.00:12:01
00:12:01
Waigizaji00:12:02
00:12:03
wakipanda na kutoka00:12:05
00:12:05
kwenye jukwaa upesi.00:12:07
00:12:08
Kupatana na kanuni ya maneno hayo ya Paulo00:12:11
00:12:11
yaliyoongozwa na roho,00:12:13
00:12:13
mitindo ya kujipamba00:12:14
00:12:14
imebadilika kadiri ambavyo miaka imepita.00:12:17
00:12:17
Kwa mfano,00:12:18
00:12:18
wanaume wengi zaidi00:12:20
00:12:20
walio na madaraka,00:12:21
00:12:22
wanafuga ndevu00:12:23
00:12:23
na bado wanaonekana00:12:25
00:12:26
kuwa wana mwonekano00:12:27
00:12:27
wenye kuheshimika. 00:12:28
00:12:30
Swali lingine:00:12:31
00:12:32
Tunapaswa kuwa na maoni gani00:12:34
00:12:35
kuhusu ndugu anayeamua00:12:36
00:12:37
kufuga ndevu?00:12:38
00:12:39
Tunapaswa kutumia shauri la Yesu,00:12:41
00:12:41
linalopatikana kwenye Yohana 7:24.00:12:45
00:12:45
“Acheni kuhukumu,00:12:46
00:12:46
kwa kutazama sura ya nje tu.”00:12:49
00:12:51
Kama tulivyoona katika video,00:12:53
00:12:53
mitindo ya kujipamba ilibadilika00:12:55
00:12:55
kadiri muda ulivyopita.00:12:56
00:12:58
Si kwamba00:12:58
00:12:58
mabadiliko haya yote yalikuwa mabaya.00:13:00
00:13:01
Kwa mfano,00:13:02
00:13:03
huenda hakuna yeyote kati yetu00:13:04
00:13:04
ambaye angependa kuvalia na kujipamba00:13:07
00:13:07
kama watu walivyofanya,00:13:08
00:13:08
katika nyakati za Biblia,00:13:09
00:13:10
au pia huenda tusingependa00:13:11
00:13:11
kujipamba na kuvalia00:13:12
00:13:12
kama walivyofanya karne moja iliyopita,00:13:15
00:13:15
kwa kweli00:13:16
00:13:16
wengi hupenda kufuata mitindo00:13:19
00:13:19
ambayo inafaa leo,00:13:22
00:13:22
si ile ya makumi ya miaka iliyopita.00:13:25
00:13:26
Kwa kweli si vibaya kuvalia au kujipamba00:13:29
00:13:29
kama vile ambavyo watu wengi00:13:32
00:13:32
katika jamii yetu wanavyofanya leo.00:13:34
00:13:35
Maadamu,00:13:36
00:13:36
mtindo huo tunaoiga00:13:38
00:13:39
hauvunji kanuni00:13:41
00:13:41
za Biblia.00:13:42
00:13:43
Sikuzote tungependa kuhakikisha00:13:46
00:13:46
mwonekano wetu,00:13:47
00:13:48
unaonekana safi,00:13:49
00:13:50
ni wenye kiasi00:13:52
00:13:52
na wenye utimamu wa akili.00:13:55
00:13:56
Swali lingine;00:13:57
00:13:58
tunawezaje kuendeleza umoja00:14:01
00:14:01
baada ya kupata mwelekezo huu?00:14:03
00:14:05
Baada ya kutazama programu hii,00:14:07
00:14:08
huenda baadhi wakalazimika00:14:10
00:14:11
kukabiliana na hisia kali sana.00:14:13
00:14:14
Kwa mfano,00:14:15
00:14:16
huenda baadhi00:14:17
00:14:17
wakahisi kwamba00:14:19
00:14:19
wameshinda00:14:20
00:14:20
na kusema kwamba00:14:22
00:14:22
hayo ndiyo yamekuwa maoni yangu00:14:25
00:14:25
kwa muda mrefu.00:14:27
00:14:27
Hilo linathibitisha00:14:29
00:14:29
mimi nilikuwa sahihi00:14:31
00:14:31
muda wote huo.00:14:33
00:14:34
Huenda wengine wakahisi,00:14:36
00:14:36
wamevunjika moyo00:14:38
00:14:38
labda watasema,00:14:40
00:14:40
kwa miaka yote hiyo00:14:42
00:14:42
nilitii mwongozo kuhusu kujipamba,00:14:45
00:14:45
lakini sasa00:14:46
00:14:47
nimekatishwa tamaa.00:14:48
00:14:50
Je, kuna maoni yoyote00:14:51
00:14:51
yaliyo sawa kati ya hayo mawili?00:14:53
00:14:53
Hapana, 00:14:54
00:14:55
Ona kile ambacho mtume Paulo00:14:57
00:14:57
aliongozwa na roho kuandika00:14:59
00:14:59
kwenye 1 Wakorintho 1:10.00:15:04
00:15:06
“Sasa ninawahimiza ninyi akina ndugu,00:15:09
00:15:09
kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo,00:15:12
00:15:12
kwamba nyote mseme00:15:14
00:15:15
kwa upatano.00:15:16
00:15:17
Na kwamba kusiwe na migawanyiko00:15:20
00:15:20
kati yenu,00:15:21
00:15:22
bali kwamba muunganishwe00:15:24
00:15:24
kabisa00:15:26
00:15:26
katika akili ileile00:15:28
00:15:28
na njia ileile ya kufikiri.” 00:15:30
00:15:32
Kanuni hiyo inatumakaje hapa?00:15:35
00:15:36
Ikiwa00:15:37
00:15:37
tumekuwa tukiendeleza00:15:39
00:15:39
maoni yetu wenyewe00:15:40
00:15:41
ya kibinafsi00:15:42
00:15:42
kuhusu hili,00:15:44
00:15:45
yanayopingana na mwongozo wa tengenezo,00:15:48
00:15:49
je tumekuwa tukiendeleza umoja?00:15:51
00:15:52
Je, tumekuwa tukisaidia undugu wetu00:15:55
00:15:55
kuunganishwa 00:15:56
00:15:56
katika njia ileile ya kufikiri?00:15:58
00:15:59
Ni wazi la.00:16:01
00:16:02
Wowote00:16:03
00:16:03
ambao wamefanya hivyo00:16:04
00:16:04
wanahitaji kubadili kufikiri00:16:06
00:16:07
na mtazamo wao.00:16:08
00:16:09
Kwa upande mwingine00:16:11
00:16:11
ikiwa miaka yote tumekuwa tukiunga mkono00:16:14
00:16:14
mwongozo wa tengenezo kwa ushikamanifu,00:16:17
00:16:17
je, tuna sababu yoyote ya kimaandiko00:16:20
00:16:20
kujutia00:16:21
00:16:21
kwamba tulifanya hivyo?00:16:22
00:16:23
Bila shaka la.00:16:24
00:16:25
Yehova anathamini sana00:16:27
00:16:27
utumishi wetu mshikamanifu,00:16:29
00:16:29
pia, anathamini utayari wetu00:16:32
00:16:32
wa unyenyekevu,00:16:33
00:16:33
wa kutii na kujitiisha00:16:35
00:16:35
kwa mwongozo tunaopata00:16:38
00:16:38
kutoka kwa tengenezo la Mungu. 00:16:40
00:16:42
Katika karne ya kwanza W.K.00:16:44
00:16:44
baadhi ya Wakristo waliruhusu00:16:47
00:16:47
suala la kutahiriwa,00:16:49
00:16:49
lisababishe00:16:50
00:16:50
migawanyiko.00:16:52
00:16:52
Lakini roho takatifu iliongoza00:16:55
00:16:55
Baraza Linaloongoza,00:16:56
00:16:57
litatue suala hilo00:16:59
00:16:59
na kuendeleza umoja.00:17:01
00:17:01
Vivyo hivyo,00:17:02
00:17:03
Baraza Linaloongoza leo00:17:04
00:17:05
linajitahidi kuendeleza umoja.00:17:07
00:17:08
Tusingependa kamwe00:17:10
00:17:10
suala kuhusu kufuga ndevu,00:17:12
00:17:13
lisababishe migawanyiko00:17:15
00:17:15
miongoni mwetu. 00:17:16
00:17:17
Sisi sote tunahitaji kukumbuka00:17:19
00:17:19
kwamba sehemu ya kidunia00:17:21
00:17:21
ya tengenezo la Yehova00:17:23
00:17:23
inajitahidi sikuzote kujipatanisha00:17:26
00:17:26
na sehemu ya kimbingu00:17:28
00:17:28
na kwenda sambamba nayo.00:17:30
00:17:31
Je, unakumbuka katika maono ya Ezekieli00:17:34
00:17:34
gari la kimbingu linasonga kwa kasi kadiri gani,00:17:37
00:17:37
kama radi inayowakawaka.00:17:40
00:17:41
Mtu yeyote anayejaribu00:17:43
00:17:44
kutangulia gari hilo00:17:45
00:17:46
na kulazimisha mabadiliko00:17:48
00:17:48
kabla ya wakati,00:17:49
00:17:50
au00:17:51
00:17:51
kubaki nyuma00:17:53
00:17:53
akisitasita00:17:54
00:17:54
kuunga mkono mabadiliko00:17:56
00:17:56
ambayo yametoka kwa mtumwa mwaminifu,00:17:59
00:17:59
haendi sambamba00:18:01
00:18:02
na tengenezo la Yehova. 00:18:04
00:18:06
Kwa kumalizia,00:18:07
00:18:08
je, hatushukuru00:18:10
00:18:10
kwa mwongozo huo wenye usawaziko00:18:13
00:18:13
kuhusu kufuga ndevu?00:18:14
00:18:15
Yehova ametuonyesha heshima,00:18:17
00:18:18
amempa kila ndugu uhuru00:18:20
00:18:20
wa kuchagua ikiwa00:18:22
00:18:23
atafuga ndevu au la.00:18:25
00:18:26
Tuna uhakika kwamba00:18:28
00:18:28
ninyi nyote mmeazimia00:18:30
00:18:31
kwenda sambamba00:18:32
00:18:32
na kubadili maoni yenu inavyohitajika,00:18:35
00:18:35
na kuendelea kumtumikia Yehova 00:18:38
00:18:38
kwa ushikamanifu,00:18:39
00:18:40
mkiendeleza upendo00:18:41
00:18:42
na umoja miongoni mwa ndugu00:18:46
00:18:46
na dada zenu. 00:18:47
00:18:48
Kutoka kwenye Makao Makuu00:18:50
00:18:50
ya Ulimwenguni Pote ya Mashahidi wa Yehova,00:18:52
00:18:53
hii00:18:53
00:18:54
ni JW Broadcasting00:18:56
Ripoti ya 8 ya Baraza Linaloongoza ya 2023
-
Ripoti ya 8 ya Baraza Linaloongoza ya 2023
Karibuni ndugu na dada wapendwa
kwenye ripoti yetu.
Tungependa kuanza
na ripoti fupi
kuhusu baadhi ya misiba ya asili,
ambayo imeendelea kuwaathiri ndugu zetu
hivi karibuni.
Mwezi wa Septemba
Ndugu zetu nchini Ugiriki
walikabili mvua kubwa
na mafuriko makubwa.
Mwezi wa Oktoba
ndugu zetu nchini Mexico
walikumbwa na kimbunga kikubwa sana
ambacho kilisababisha uharibifu mkubwa sana.
Na mwezi wa Novemba
ndugu zetu nchini Filipino
walikabili tetemeko la ardhi
lenye kipimo cha 6.7.
Kwa kusikitisha
tetemeko hilo la ardhi
lilisababisha kifo cha dada mmoja
na pia ndugu na dada zetu 10
walijeruhiwa.
Tunaendelea kusali
kwa ajili ya wale walioathiriwa
na majanga mbalimbali
yanayoendelea ulimwenguni pote.
Lakini pia tunawashukuru ninyi nyote
kwa utegemezo wenu
na sala zenu.
Baadhi yenu mnafanya kazi kwa bidii
ya kutoa msaada
na wengi zaidi kati yenu
mnatoa michango kwa ukarimu,
na michango hiyo
inatusaidia kuwaandalia ndugu na dada
mahitaji yao ya lazima
na pia kuwasaidia kujenga upya nyumba zao
na Majumba yao ya Ufalme.
Tunashukuru sana
kwa msaada wenu.
Kwa niaba ya Baraza Linaloongoza tunasema
asanteni.
Lakini kuanzia hapa katika ripoti hii,
acheni tuzungumzie kichwa
“Tunajipendekeza
Kuwa Wahudumu wa Mungu”
kichwa hicho kinategemea 2 Wakorintho 6:4
Ambapo mtume Paulo alisema
“katika kila njia
tunajipendekeza kuwa wahudumu
wa Mungu.”
Hilo linamaanisha nini?
Habari za utafiti katika Biblia ya kiingereza
zinasema; “Kitenzi cha Kigiriki kinachotafsiriwa
tunajipendekeza,
kinatoa wazo la
tunajithibitisha
au tunajionyesha wenyewe kuwa.”
Lakini
tunajionyeshaje wenyewe
kuwa wahudumu
wa Mungu wa kweli?
Njia moja muhimu
ni kupitia
mwonekano wetu.
Sisi sote tungependa sifa zimwendee
Mungu wetu tunayempenda
na tunayemwabudu.
Tunawezaje kufanya hivyo?
Kwa kufuata kanuni za Biblia.
Kwa mfano,
fikiria kanuni hii,
inayotajwa kwenye 1 Timotheo 2:9, 10
“Vivyo hivyo,
wanawake wanapaswa kujipamba
kwa mavazi yanayofaa,
kwa kiasi
na utimamu wa akili.
Si kwa mitindo ya kusuka nywele,
dhahabu,
lulu au mavazi ya bei ghali sana,
bali
kwa njia inayowafaa wanawake
wanaokiri kwamba
wanamtumikia Mungu,
yaani,
kupitia matendo mema.”
Ingawa shauri hilo limeelekezwa
kwa wanawake Wakristo,
kanuni hiyo inatumika vilevile kwa wanaume
kama tu kwa wanawake.
Kwa hiyo njia moja
sisi sote
tunaweza kujipendekeza
kuwa wahudumu wa Mungu
ni kwa kuhakikisha kwamba,
mwonekano wetu,
unafaa,
ni wenye kiasi,
unaoonyesha utimamu wa akili.
Lakini je, hilo linamaanisha kwamba
Mashahidi wote wa Yehova
wanafanya maamuzi yaleyale?
Je, tunapaswa,
kuvaa sare?
Au je tunapaswa kujipamba
na kuvaa kwa mtindo uleule mmoja?
Bila shaka la.
Kuna zaidi ya Mashahidi wa Yehova
milioni nane ulimwenguni pote.
Nasi tumetoka
katika tamaduni mbalimbali,
Yehova amevuta
mamilioni ya watu hao wote,
naye anapenda
unamna-namna.
Lakini sasa tuulize,
namna gani kuhusu kufuga
ndevu?
Je inafaa kwa ndugu
kufanya hivyo?
Ili kutusaidia kujibu swali hilo
acheni tutazame video ifuatayo,
ambayo itazungumzia
historia ya ndevu,
miongoni mwa watu wa Yehova.
Katika nyakati za kale,
lilikuwa jambo la kawaida kwa wanaume
kufuga ndevu.
Zoea hilo liliendelea
miongoni mwa Waisraeli.
Mwanamume Mwisraeli
angenyoa ndevu wakati tu alipoaibishwa,
au alipokuwa akiomboleza.
Kwa mfano,
mfalme wa Amoni
alipowaaibisha watumishi wa Daudi
kwa kunyoa ndevu zao,
Daudi alilinda heshima yao
kwa kuwaambia hivi:
“Kaeni Yeriko
mpaka ndevu zenu zitakapoota,
kisha mrudi.”
Karne nyingi baadaye,
nabii Ezekieli alinyoa ndevu
na nywele za kichwa chake
ili kuonyesha msiba mkubwa na huzuni
ambayo jiji la Yerusalemu lingekabili.
Namna gani Yesu,
kwa kuwa alikuwa Mwisraeli,
je, yeye pia alifuga ndevu?
Kwa miaka kadhaa
kwa kutegemea maoni ya waakiolojia fulani,
mara nyingi machapisho yetu
yalionyesha picha za Yesu
akiwa amenyoa ndevu.
Hata hivyo,
katika mwaka wa 1968,
Mnara wa Mlinzi
lilichunguza uthibitisho unaoaminika zaidi,
kutoka kwenye vyanzo vya kihistoria
na kwenye Maandiko.
Hakuna Injili yoyote iliyoonyesha kwamba
mwonekano wa Yesu
ulitofautiana na wa watu wengine.
Alifanya jambo
lililokuwa la kawaida
miongoni mwa wanaume Wayahudi wakati huo,
alifuga ndevu.
Tangu wakati huo,
video zetu na picha katika machapisho yetu,
zimemuonyesha Yesu
akiwa na ndevu zilizotunzwa vizuri.
Kufikia wakati ambapo
kutaniko la Kikristo lilianzishwa,
lilikuwa jambo la kawaida
kwa Waroma kunyoa ndevu.
Je, Wakristo Wayahudi
walitarajiwa kunyoa ndevu?
Au je, Wakristo wa mataifa
walitarajiwa kufuga ndevu
ili waweze kufanana
na ndugu zao Wayahudi?
Haionekani hivyo.
Kwa kuwa Maandiko
hayawaagizi waabudu wa kweli wafuge ndevu
wala kuzinyoa,
huo ulikuwa uamuzi
wa kibinafsi.
Katika miaka ya mwisho-mwisho
ya karne ya 19 na
mwanzoni mwa karne ya 20,
lilikuwa jambo la kawaida kufuga ndevu
hata miongoni mwa wanafunzi wa Biblia.
Kama picha hizi waangalizi wasafirio
walioitwa Mapilgrimu zinavyoonyesha.
Ndugu Russel pia,
alifuga ndevu.
Mhariri mmoja wa gazeti la habari alimwita,
mhudumu aliyekuwa nadhifu.
Mhariri huyo alisema:
“Sijawahi kufikiri kwamba alikuwa tofauti
na maelfu ya wahubiri wengine.
Ndevu zake nyeupe,
nyororo zinamfanya aonekane
kama mzee wa ukoo,
kama baba,
zinakufanya uwe na uhakika naye.”
Muda mfupi
baada ya Vita vya Kwanza vya Ulimwengu,
lilianza tena kuwa jambo la kawaida
kunyoa ndevu.
Mwaka wa 1919
picha hii ya mapilgrimu ilipopigwa,
wengi kati yao
hawakuwa na ndevu.
Ingawa machapisho yetu
hayakusema mengi kuhusu hilo wakati huo,
ni ndugu wachache sana
waliofuga ndevu.
Katika nchi nyingi
kuanzia mwaka wa 1960,
ndevu zililihusianishwa
na wale waliopinga mamlaka iliyowekwa.
kwa sababu hiyo
wanaume wengi walichagua kunyoa ndevu,
iwe walikuwa Mashahidi
au hawakuwa Mashahidi.
Kwa sababu ya maoni yasiyofaa
yaliyohusianishwa na kufuga ndevu,
ndugu wengi walifuga ndevu
hawakuwekwa kuwa watumishi wa huduma,
wazee,
au kupewa majukumu mengine.
Katika nchi fulani
kadiri ambavyo muda ulivyopita,
ndevu zikaja kuwa jambo la kawaida
na hazikuhusianishwa na uasi.
Katika maeneo hayo,
baadhi ya akina ndugu waliokuwa na ndevu,
waliwekwa rasmi
kuwa watumishi wa huduma na wazee.
Katika nyakati za karibuni,
limekuwa jambo la kawaida
katika nchi nyingi kufuga ndevu.
Kwa hiyo, tunapaswa kumwonaje
ndugu anayechagua kufuga ndevu leo?
Video hiyo imemalizia
kwa swali, lenye kuchochea fikira.
Tunapaswa kumwonaje,
ndugu anayechagua
kufuga ndevu leo?
Baraza Linaloongoza, limeniomba
nisome tangazo lifuatalo.
“Ofisi kadhaa za tawi, ulimwenguni
zimetuandikia,
zikionyesha kwamba,
bado kuna maswali mengi yanayoulizwa,
kuhusu ikiwa
ni sawa au la
kwa ndugu aliyewekwa rasmi
kufuga ndevu.
Baada ya kufikiria jambo hilo kwa sala,
Baraza Linaloongoza
limeona kwamba kuna uhitaji
wa kuweka wazi jambo hili.
Baraza Linaloongoza
halipingi kwamba
akina ndugu wanaweza kufuga ndevu.
Kwa nini?
Kwa sababu Maandiko
hayashutumu kufuga ndevu.
” Mbali na hilo
kadiri ambavyo muda umepita,
tumeona kwamba
katika nchi nyingi,
inakubalika kwa wanaume,
walio na mamlaka katika biashara,
au hata serikalini,
kufuga ndevu.
Kwa hiyo
ikiwa ndugu atachagua kufuga ndevu,
huo ni uamuzi
wa kibinafsi.
Sifa za kustahili kwa ndugu
kutumikia akiwa mzee au mtumishi wa huduma,
zinategemea
hali yake ya kiroho,
bali hazitegemei ikiwa anaamua
kufuga ndevu.
Mwongozo huo pia unatumika,
kwa watumishi wa wakati wote
walio Betheli,
na wale walio shambani,
kutia ndani mapainia wa pekee,
wamishonari,
na waangalizi wa mzunguko.
Kupatana na andiko la Waroma 14:4,
wazee
wala Mkristo mwingine yeyote,
hawapaswi kumhukumu
ndugu anayeamua
kufuga ndevu.
Tunaamini kwamba maelezo haya
yatatusaidia tuendelee kujilinda,
dhidi ya chochote
ambacho kinaweza kusababisha migawanyiko
miongoni mwa watu wa Yehova.
Huo ndio mwisho wa tangazo
la Baraza Linaloongoza.
Hata hivyo, mwongozo huu
huenda ukaibua maswali.
Kwa mfano swali moja:
Kwa nini Baraza linaloongoza
linatoa mwongozo huu
wakati huu?
Kama ilivyoandikwa kwenye 1 Wakorintho 7:31,
mtume Paulo aliongozwa na roho kuandika:
“tamasha ya ulimwengu huu
inabadilika.”
Habari za utafiti za mstari huo
zinaonyesha kwamba huenda Paulo,
alikuwa akirejelea
jinsi maonyesho
yanavyobadilika upesi,
katika jumba la maonyesho.
Waigizaji
wakipanda na kutoka
kwenye jukwaa upesi.
Kupatana na kanuni ya maneno hayo ya Paulo
yaliyoongozwa na roho,
mitindo ya kujipamba
imebadilika kadiri ambavyo miaka imepita.
Kwa mfano,
wanaume wengi zaidi
walio na madaraka,
wanafuga ndevu
na bado wanaonekana
kuwa wana mwonekano
wenye kuheshimika.
Swali lingine:
Tunapaswa kuwa na maoni gani
kuhusu ndugu anayeamua
kufuga ndevu?
Tunapaswa kutumia shauri la Yesu,
linalopatikana kwenye Yohana 7:24.
“Acheni kuhukumu,
kwa kutazama sura ya nje tu.”
Kama tulivyoona katika video,
mitindo ya kujipamba ilibadilika
kadiri muda ulivyopita.
Si kwamba
mabadiliko haya yote yalikuwa mabaya.
Kwa mfano,
huenda hakuna yeyote kati yetu
ambaye angependa kuvalia na kujipamba
kama watu walivyofanya,
katika nyakati za Biblia,
au pia huenda tusingependa
kujipamba na kuvalia
kama walivyofanya karne moja iliyopita,
kwa kweli
wengi hupenda kufuata mitindo
ambayo inafaa leo,
si ile ya makumi ya miaka iliyopita.
Kwa kweli si vibaya kuvalia au kujipamba
kama vile ambavyo watu wengi
katika jamii yetu wanavyofanya leo.
Maadamu,
mtindo huo tunaoiga
hauvunji kanuni
za Biblia.
Sikuzote tungependa kuhakikisha
mwonekano wetu,
unaonekana safi,
ni wenye kiasi
na wenye utimamu wa akili.
Swali lingine;
tunawezaje kuendeleza umoja
baada ya kupata mwelekezo huu?
Baada ya kutazama programu hii,
huenda baadhi wakalazimika
kukabiliana na hisia kali sana.
Kwa mfano,
huenda baadhi
wakahisi kwamba
wameshinda
na kusema kwamba
hayo ndiyo yamekuwa maoni yangu
kwa muda mrefu.
Hilo linathibitisha
mimi nilikuwa sahihi
muda wote huo.
Huenda wengine wakahisi,
wamevunjika moyo
labda watasema,
kwa miaka yote hiyo
nilitii mwongozo kuhusu kujipamba,
lakini sasa
nimekatishwa tamaa.
Je, kuna maoni yoyote
yaliyo sawa kati ya hayo mawili?
Hapana,
Ona kile ambacho mtume Paulo
aliongozwa na roho kuandika
kwenye 1 Wakorintho 1:10.
“Sasa ninawahimiza ninyi akina ndugu,
kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo,
kwamba nyote mseme
kwa upatano.
Na kwamba kusiwe na migawanyiko
kati yenu,
bali kwamba muunganishwe
kabisa
katika akili ileile
na njia ileile ya kufikiri.”
Kanuni hiyo inatumakaje hapa?
Ikiwa
tumekuwa tukiendeleza
maoni yetu wenyewe
ya kibinafsi
kuhusu hili,
yanayopingana na mwongozo wa tengenezo,
je tumekuwa tukiendeleza umoja?
Je, tumekuwa tukisaidia undugu wetu
kuunganishwa
katika njia ileile ya kufikiri?
Ni wazi la.
Wowote
ambao wamefanya hivyo
wanahitaji kubadili kufikiri
na mtazamo wao.
Kwa upande mwingine
ikiwa miaka yote tumekuwa tukiunga mkono
mwongozo wa tengenezo kwa ushikamanifu,
je, tuna sababu yoyote ya kimaandiko
kujutia
kwamba tulifanya hivyo?
Bila shaka la.
Yehova anathamini sana
utumishi wetu mshikamanifu,
pia, anathamini utayari wetu
wa unyenyekevu,
wa kutii na kujitiisha
kwa mwongozo tunaopata
kutoka kwa tengenezo la Mungu.
Katika karne ya kwanza W.K.
baadhi ya Wakristo waliruhusu
suala la kutahiriwa,
lisababishe
migawanyiko.
Lakini roho takatifu iliongoza
Baraza Linaloongoza,
litatue suala hilo
na kuendeleza umoja.
Vivyo hivyo,
Baraza Linaloongoza leo
linajitahidi kuendeleza umoja.
Tusingependa kamwe
suala kuhusu kufuga ndevu,
lisababishe migawanyiko
miongoni mwetu.
Sisi sote tunahitaji kukumbuka
kwamba sehemu ya kidunia
ya tengenezo la Yehova
inajitahidi sikuzote kujipatanisha
na sehemu ya kimbingu
na kwenda sambamba nayo.
Je, unakumbuka katika maono ya Ezekieli
gari la kimbingu linasonga kwa kasi kadiri gani,
kama radi inayowakawaka.
Mtu yeyote anayejaribu
kutangulia gari hilo
na kulazimisha mabadiliko
kabla ya wakati,
au
kubaki nyuma
akisitasita
kuunga mkono mabadiliko
ambayo yametoka kwa mtumwa mwaminifu,
haendi sambamba
na tengenezo la Yehova.
Kwa kumalizia,
je, hatushukuru
kwa mwongozo huo wenye usawaziko
kuhusu kufuga ndevu?
Yehova ametuonyesha heshima,
amempa kila ndugu uhuru
wa kuchagua ikiwa
atafuga ndevu au la.
Tuna uhakika kwamba
ninyi nyote mmeazimia
kwenda sambamba
na kubadili maoni yenu inavyohitajika,
na kuendelea kumtumikia Yehova
kwa ushikamanifu,
mkiendeleza upendo
na umoja miongoni mwa ndugu
na dada zenu.
Kutoka kwenye Makao Makuu
ya Ulimwenguni Pote ya Mashahidi wa Yehova,
hii
ni JW Broadcasting
-