JW subtitle extractor

Yehova Mungu Atakusaidia

Video Other languages Share text Share link Show times

Papa, weye ni siku gani?
Mashahidi wa Yehova walitutembelea hakuyapita miaka mingi.
Rachel njo alianzaka kujifunza.
Kisha, siye wote tukaanza kujifunza.
Kwa mara ya kwanza, tulivumbula mambo yenye Biblia inafundisha kabisa.
Bila kukawia, tukaanza kuhubiri.
Karibu familia yote ikaanza kuhubiri.
Nilijua kama ilikuwa kweli, lakini niliwaza sitaweza kufanya mambo yenye Yehova anataka.
Toka kule!
Watu wataona je kama minajiendesha mubaya?
Na Yehova ataona je?
Tafazali, unichunge kidogo! Sawa, hakuna shida. Sawa
Ben, muzee mwenye upendo,
Ni je?
alielewa kama nilikuwa na shida fulani.
Alitafuta namna ya kunisaidia.
Aliniuliza, “Nini njo ilifanya umupende Yehova?”
Nilimupenda Yehova wakati nilitambua kama haiko mukali na hatuombake mambo ya mingi, ni Baba mwenye upendo.
Ben aliitika na akaniambia, “Wakati tunafanya yetu yote ili kumutumikia Yehova, naye anatusaidia.”
Aliniambia Yehova anajua mipaka yetu na hatuombe ukamilifu.
Siku zote iko tayari kutusaidia juu anataka tuweze.
Kisha alinisomea Isaya 41:10: “Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe.
Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako.
Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia,
Nisaidie!
nitakushika kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa haki.”
Haiko lazima nikuwe mukamilifu juu nimutumikie Yehova.
Napaswa tu kumupenda na kumutumainia, naye atanisaidia.