JW subtitle extractor

Kusanyiko la Eneo la 2020 la “Shangilieni Sikuzote”!: Jumapili Asubuhi—Sehemu ya 1

Video Other languages Share text Share link Show times

Hamjambo ndugu na dada.
Video ya muziki itaanza
baada ya muda mfupi,
unapoitazama fikiria kuhusu
jinsi uaminifu wetu sasa
utakavyotuletea shangwe zaidi.
Kama una simu ya mkononi,
au kifaa kingine cha kielektroni,
weka kwenye mfumo ambao
hautawakengeusha wengine.
Sasa furahieni muziki.
Karibuni kwenye kipindi hiki,
cha kusanyiko letu la eneo.
Ni kipindi cha jumapili
asubuhi kwenye programu yetu.
Kichwa cha leo kinategemea
Zaburi 37:4
“Pata furaha tele katika Yehova,
naye atatosheleza
tamaa za moyo wako.”
Tafadhali simameni
tuimbe wimbo namba 22.
“Ufalme Umesimamishwa—Na Uje!”
Baada ya wimbo mnaweza
kusimamisha programu
na kutoa sala, sasa
tuimbe wimbo namba 22.
Tafadhali ketini
je, tunaweza kuwa na shangwe
tunapokabili majaribu makali.
Biblia inatuhakikishia
kwamba inawezekana.
Mufululizo ufuatao
wenye sehemu saba,
utaonyesha jinsi Yehova
anavyotusaidia
kila msemaji atamkaribisha
anayefuata,
kwanza
tumsikilize ndugu Kenneth flodin,
msaidizi wa Halmashauri ya Ufundishaji,
anapotoa hotuba ya kwanza,
yenye kichwa,
“Tunaweza kuwa na shangwe
licha ya dhiki.”
Asanteni kwa hotuba hizo nzuri.
Tunamshukuru Yehova
kwa kutuandalia kile tunachohitaji
ili kudumisha shangwe yetu.
Acheni tusimame
tuimbe wimbo namba tisa.
“Yehova Ni Mfalme Wetu!”
Tuimbe wimbo namba tisa.
Je, umetambua
kila hotuba katika
mfululizo huu
ina neno “licha ya?”
Neno “licha ya”
linaweza kumaanisha kutozuiwa
Basi shangwe yetu
haiwezi kuzuiwa
au kushindwa.
Tunaweza kuwa na shangwe
licha ya majaribu.
Lakini huenda hilo
lisieleweke mwanzoni,
kwa sababu mara nyingi
tunahusianisha shangwe
na kupokea zawadi
na sio majaribu.
Lakini huo ndio ukweli.
Tunaweza kuwa na shangwe
licha ya majaribu
kwa sababu ya zawadi
ambazo Yehova anatupatia.
Na tutachunguza zawadi tatu
katika mfululizo huu,
uhusiano wetu na Yehova,
undugu wetu wenye thamani,
na tumaini letu la wakati ujao.
Tafadhali
tufungue andiko la
Waroma 5:3-5,
tuone jinsi zawadi ya kwanza
inavyotajwa katika andiko hili.
Uhusiano wetu na Yehova.
Waroma 5:3-5 inasema
“Si hilo tu,
bali na tushangilie tukiwa katika dhiki
kwa kuwa tunajua kwamba dhiki
hutokeza uvumilivu;
nao uvumilivu,
hali yenye kukubaliwa”
kukubaliwa na nani?
Kukubaliwa na Yehova.
Mstari unasema,
“nayo hali yenye kukubaliwa,
tumaini,
nalo tumaini halikatishi tamaa”
kwa sababu ya uhusiano
wetu na Yehova
“kwa sababu upendo wa Mungu
umemiminwa ndani ya mioyo yetu
kupitia roho takatifu,
ambayo tulipewa.”
Tunapovumilia majaribu
tunahisi kibali cha Yehova.
na hilo linatusaidia kupata
shangwe licha ya magumu.
Tusome Waroma 8:38,39.
Paulo alikabili jaribu moja
baada ya jingine.
Lakini alikuwa na uhakika
kwamba hakuna jaribu
ambalo lingeweza kumzuia
au kumtenganisha na
upendo wa Yehova.
uhusiano wa kudumu.
Waroma 8:38, 39,
“Kwa maana
nimesadiki kwamba wala kifo
wala uzima wala malaika
wala serikali
wala mambo yaliyopo sasa
wala mambo yatakayokuja
wala nguvu
wala kimo wala kina
wala uumbaji mwingine wowote
havitaweza kututenga
na upendo wa Mungu
ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.”
Uhusiano wetu na Mungu
utatusaidia tunapokabili majaribu.
Tuzungumzie zawadi ya pili
kutoka kwa Yehova.
1 Petro 5:9.
Shetani hutumia majaribu
kutuvunja moyo.
Ona jinsi tunavyohimizwa
kwenye mstari wa 9.
“Lakini chukueni msimamo dhidi yake
mkiwa imara katika imani”
Ni nini kitatusaidia?
mkijua kwamba mateso
(yaani majaribu)
yaleyale yanaupata ushirika mzima
wa ndugu zenu ulimwenguni.
Naam,
tunahisi msaada na utegemezo
kutoka kwa ndugu zetu,
hasa kwa kipindi cha miezi sita iliyopita,
Waroma 12:12
inataja zawadi ya tatu inayotusaidia
kuvumilia majaribu.
Waroma 12:12
inasema hivi waziwazi
“Shangilieni katika tumaini.”
Kisha unasema,
“vumilieni chini ya dhiki.
Dumuni katika sala.”
Hivyo, uhusiano wetu na Yehova,
undugu wetu,
na tumaini letu,
hutusaidia kukabiliana na hali hizi.
Huenda hali zikatofautiana,
kwa mfano
huenda ndugu aliyefungwa gerezani
akashindwa kuwasiliana
na ndugu wengine.
Nini humwimarisha?
Ni uhusiano wake pamoja na Yehova.
Kumbuka kisa cha ndugu Harold King
kwenye JW broadcasting
alifungwa kifungo cha upweke
kwa miaka minne na nusu
gerezani huko China.
Je, kweli alikuwa peke yake?
Wenye mamlaka walifikiri hivyo.
Lakini akiwa hapo kifungoni,
alikuwa na rafiki bora zaidi.
Katika video hiyo alisema hivi,
“Nilikuwa na uhusiano mzuri
pamoja na Yehova.
Ninampenda sana.
Alikuwa mtu halisi
hakuwa mtu wa kuwaziwa.”
Ndugu King alidumisha shangwe
licha ya hali hiyo
kwa sababu alikuwa na uhusiano
wa karibu pamoja na Yehova.
Fikiria mfano mwingine.
Huenda ndugu au dada
aliyeshuka moyo,
akapambana kudumisha
uhusiano wa karibu pamoja na Mungu.
Kuna zawadi nyingine
kutoka kwa Yehova
inayoweza kumsaidia.
Ndugu na dada wanaweza kumsaidia.
Ni kama mtu aliye na
matatizo ya kupumua,
yuko hai
lakini anapambana
kuendelea kupumua.
Kisha, madaktari wanakuja kumsaidia,
anapata nafuu
na kuanza kupumua tena vizuri.
Ndugu zetu wanaweza kutusaidia
tunaposhuka moyo au
tunapopambana na
majaribu mengine.
tumaini linaweza kutusaidiaje
kuwa na shangwe
licha ya majaribu?
Mfano mwingine,
baadhi yetu tuna wazazi waliozeeka
na wenye matatizo ya afya.
Huenda hilo likawa jaribu kwetu,
hali hiyo inaweza kulinganishwa
na rafiki yetu anapopata aksidenti,
kisha analazwa hospitalini,
na hawezi kufanya chochote.
Kisha daktari anakuja na kusema
atapona kabisa.
Hilo linatupatia tumaini.
Ndivyo ilivyo na wazazi
wetu waliozeeka.
Kwa sababu tuna tumaini hakika
kuhusu wakati ujao,
ni kama Yehova anatuambia
watapona kabisa.
Naam, tumaini hutusaidia
kuwa na shangwe,
hata tukabili majaribu ya aina gani,
tunaweza kuwa na uhakika kwamba
mojawapo ya zawadi hizo
itatusaidia kudumisha shangwe.
Tufungue andiko la Waroma sura ya 8,
Waroma 8:35, 37.
Katika mfululizo huu
tutachunguza kila jaribu linalotajwa
katika mstari wa 35.
Tuone majaribu hayo
Waroma 8:35,
“Ni nani atakayetutenga
na upendo wa Kristo?
Je, ni dhiki au taabu
au mateso au njaa
au uchi au hatari
au upanga?”
Hayo ni mambo 7.
Sasa mstari wa 37.
“Badala yake,
katika mambo haya yote
tunatoka tukiwa tumeshinda kabisa
kupitia yule aliyetupenda.”
Kila hotuba katika mfululizo huu
itakuwa na video ya ndugu
au dada ambaye amekabili
jaribu fulani,
jaribu kali sana.
Vilevile tutachunguza
zawadi zilizowasaidia
kuendelea kuwa na shangwe
licha ya majaribu.
tuchunguze jaribu la kwanza ambalo
Paulo alitaja-dhiki.
Dhiki
hurejelea mateso
yanayosababishwa
na hali fulani ngumu.
Kwa mfano
ugonjwa mbaya.
Tusome
2 Wakorintho sura ya 12
12 mstari wa 7,8.
Hali hii ilimsumbua sana Paulo
hivi kwamba aliita mwiba katika mwili.
Mstari wa 7 na 8,
“Ili nisijiinue mno,
nilipewa mwiba katika mwili,
malaika wa Shetani,
aendelee kunipiga kofi,
ili nisijiinue kupita kiasi.
Mara tatu nilimwomba Bwana
kuhusu jambo hili,
kwamba aniondolee.”
Mwiba katika mwili.
Bila shaka
huu ulikuwa ugonjwa.
uliendelea kumpiga kofi.
Ni jambo lililoendelea.
Haikuwa homa au mafua ya kawaida
ambayo huisha baada ya wiki.
Hilo lilikuwa jaribu lililoendelea,
lilikuwa tatizo la kudumu
na kulingana na Maandiko,
inawezekana kwamba
lilikuwa tatizo kubwa la macho.
Jambo hilo lilimhangaisha sana Paulo.
Hata alisali mara tatu
kwamba mwiba huo uondolewe.
“Uniondolee mwiba huu.”
Vipi miwani?
watu hawakuwa na
miwani siku hizo,
wala hangefanyiwa upasuaji wa macho.
Basi hii ilikuwa dhiki ya kuendelea,
na kumbuka kwamba
kupitia roho takatifu,
pindi kadhaa
Paulo mwenyewe alikuwa
amewaponya watu magonjwa yao.
Labda aliwaza,
zawadi hii ya roho takatifu iko wapi?
Ninahitaji kuponywa.
Ni nini kilichomsaidia
Paulo kuwa na shangwe
licha ya dhiki yake?
Ni uhusiano wake wa karibu
pamoja na Yehova.
Tusome 2 Wakorintho 12:9.
Katika mstari huu
Yehova anamwambia Paulo,
hutaponywa kimuujiza.
Mstari wa 9
“Lakini akaniambia:
‘Fadhili zangu zisizostahiliwa
zinakutosha,
kwa kuwa nguvu zangu zinakamilika
katika udhaifu.’”
Yehova anasema hutaponywa,
lakini nitakupa nguvu za
kuendelea licha ya dhiki hiyo.
Ona uhusiano wa karibu ambao
Paulo alikuwa nao pamoja na Yehova
katika sehemu ya mwisho
ya mstari huu
“Kwa furaha zaidi,
basi, nitajisifu kuhusu udhaifu wangu,
ili nguvu za Kristo
zibaki juu yangu kama hema.”
Alipata shangwe kutokana na
nguvu za Yehova.
Mstari wa 10
‘Basi ninapendezwa
au tunaweza kusema ninashangilia katika
udhaifu, na matusi,
na nyakati za uhitaji,
na mateso na shida,
kwa ajili ya Kristo.
Kwa maana ninapokuwa dhaifu,
ndipo ninapokuwa na nguvu.”
sasa
tungependa kuona video
kuhusu mfano mmoja wa dhiki.
Ni nini ambacho kilimsaidia
ndugu huyu na mke wake
wawe na shangwe
licha ya kukabili ugonjwa mbaya?
Kwa miaka 45
nimetumikia nikiwa painia,
mwangalizi wa mzunguko,
na sasa ninaendelea kutumikia
nikiwa hapa Betheli.
Nilikuwa na afya nzuri sana,
sikuwa na ugonjwa wowote.
Siku moja nilihisi maumivu kichwani,
maumivu makali sana,
nilishindwa kuona vizuri
Tulienda kumwona daktari wa Betheli,
akatuambia tumwone mtaalamu,
na mtaalamu akatuambia ana uvimbe
hatari kwenye ubongo
uitwao glyoblastoma.
Alhamisi iliyofuata
alifanyiwa upuasuaji.
Baada ya upasuaji,
alifanyiwa matibabu ya mionzi na kemikali.
Baada ya mwaka mmoja
alifanyiwa upasuaji mwingine.
Na sasa anaendelea na aina ya nne
ya matibabu ya kemikali.
Tangu alipoanza kuumwa,
jambo gumu zaidi limekuwa
kumwona mume wangu
akinitegemea mimi na watu
wengine ili wamfanyie mambo.
Sikutaka watu wengine
watuone kwa njia hii.
Akina ndugu na dada
walitusaidia sana.
Ndugu mmoja aliposikia
nitafanyiwa upasuaji,
alinisomea andiko,
tukasali pamoja
--sitasahau jambo alilofanya.
Nilihitaji sana kutiwa moyo.
Pia, mke wangu hunitia moyo sana,
kwa kunisaidia kujiandaa
kwa ajili ya mikutano.
Tunaposhiriki katika utumishi,
ninapata nafasi ya kuwasaidia watu.
Pia kuzungumza nao
na kuwatia moyo.
Kwenye mgawo wangu wa Betheli,
katika Idara ya Utumishi,
ndugu mmoja au wawili huja
na kuzungumzia jambo tunaloshughulikia.
Jambo hilo hunipa shangwe sana.
Ninashukuru sana kwamba
hata ninaweza kusaidia kwa njia ndogo.
Unyenyekevu wake
umefanya hali iwe rahisi kwangu.
Imani yangu imeimarika,
na nitaendelea kufanya hivi
nikimtumikia Yehova,
hadi ulimwengu mpya au
hali zibadilike.
Ni wazi kwamba Sara na Scott
walikuwa wamesitawisha
uhusiano wa karibu
pamoja na Yehova.
Na Sara alimuunga mkono Scott.
Je, umetambua zawadi waliyopata
kutoka kwa Yehova?
Scott alisema
akina ndugu walimsaidia sana.
alikumbuka sala na andiko hususa
ambalo alisomewa kabla ya upasuaji.
Ndugu vijana walimsaidia
katika mgawo wake.
Yeye mwenyewe alisema
hilo lilimletea shangwe nyingi
shangwe licha ya dhiki.
Namna gani wewe?
Ni zawadi gani kutoka kwa Yehova
inayokuimarisha
unapokabiliana na majaribu au dhiki zako?
Ni uhusiano wako na Yehova,
ni undugu wetu,
tumaini lako
au zawadi nyingine kutoka kwa Mungu?
Ikiwa unakabiliana na dhiki,
kumbuka,
ni kama Yehova anatuangalia
kwenye televisheni,
na anaona maumivu
yaliyo katika moyo wetu.
Anatuambia
“Usiwe na wasiwasi,
mambo yatakuwa sawa.”
Licha ya maumivu
licha ya dhiki,
acheni tukumbuke maneno haya ya
Waroma 8:37,39
“katika mambo haya yote
tunatoka tukiwa tumeshinda kabisa
kupitia yule aliyetupenda.”
Mstari wa 39
hakuna chochote
hakuna dhiki
itakayoweza kututenga
na upendo wa Mungu
ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Uwe na shangwe
licha ya dhiki.
Sasa ni pendeleo langu
kumkaribisha ndugu Samwel Herd
wa Baraza Linaloongoza
anapotoa hotuba yenye kichwa,
“Tunaweza kuwa na shangwe
licha ya taabu”
Umewahi kupatwa na taabu?
Kama hujawahi kupata,
basi wewe sio binadamu.
Kwa sababu
wanadamu hupatwa
na aina fulani ya taabu,
katika maisha yao mafupi
kwenye mfumo huu.
Taabu ni nini?
Baadhi ya watu husema ni
mahangaiko mengi,
huzuni,
na wengine husema ni maumivu.
Ni nini ambacho husababisha taabu?
Kuna mambo kadhaa.
Mojawapo ya sababu kuu
ni kufiwa na mwenzi wa ndoa.
Sababu ya pili ni,
kupata majeraha au ugonjwa fulani.
Au kupoteza kazi.
Nitaitunzaje familia yangu,
mke wangu na watoto wangu?
Kisha kuna sababu
nyingine muhimu sana.
Kushindwa kushiriki kikamili
katika kazi ya kuhubiri
kuhusu Ufalme.
Hayo ni baadhi ya mambo
yanayosababisha taabu.
Na bila shaka
kuna sababu nyingine nyingi.
Lakini sasa
ungehisije
kama ungepatwa
na taabu ya aina fulani?
Je, ungelemewa na
hisia na kuhuzunika?
Au utashuka moyo,
wengine husema hivyo.
“Hivi ndivyo ninavyohisi.”
Wengine husema:
“Nimeshuka moyo, hata sijui,
nimelemewa kabisa,
nimeishiwa nguvu,
niko hoi,
natamani niondoke
niwe peke yangu
nilie.”
Wengi wetu huhisi hivyo.
Je, kweli
tunaweza kuwa na shangwe
licha ya taabu?
Tunajua inawezekana kwa sababu
kuna mifano katika Biblia.
Biblia ina mifano mingi.
Tutazungumzia
mfano mmoja au miwili,
tuanze na Paulo.
Paulo,
alikuwa na shangwe
licha ya kuwa na taabu.
Licha ya hisia alizokuwa nazo,
alifaulu kupata shangwe.
Tafadhali chukua Biblia yako
ufungue andiko la Wakorintho ya pili.
Tusome pamoja Wakorintho ya pili
sura ya saba mstari wa tano.
Andiko hilo linasema:
Kwa kweli, tulipofika Makedonia,
miili yetu haikupata kitulizo,
bali tuliendelea kutaabishwa
katika kila njia
nje kulikuwa na mapigano
na ndani woga.
Naam, nje kulikuwa na mapigano
na ndani woga.
Alikabili hali ngumu.
Licha ya hali hizo,
Paulo alikuwa na shangwe.
Alikabiliana na hali gani?
Hapo awali Paulo alitarajia
kukutana na Tito huko Troa.
Hakuwa amepata habari zozote kutoka kwa Tito.
Alimhangaikia.
Hakujua alikuwa akiendeleaje.
Je, alikuwa anakabiliana
na hali ngumu
pamoja na akina ndugu na dada katika
kutaniko la Korintho?
Alimhangaikia rafiki yake
alitaka kujua.
Sisi pia tungehisi hivyo,
Ikiwa kwa muda fulani
hatungepata habari kutoka
kwa rafiki yetu.
Inaonekana kwamba
alipatwa na wasiwasi mwingi sana
hivi kwamba akafikia
hatua ya kushuka moyo.
Alijiuliza:
“Nitaendelea kumsubiri Tito
mpaka lini?”
Hakusubiri kwa muda mrefu.
Mwishowe, Tito
alijiunga naye huko Makedonia.
Hilo lilimfariji Paulo.
Na aliposikia ripoti nzuri
kutoka kwa Tito
kuhusu akina ndugu na dada katika
kutaniko la Korintho,
Paulo alishangilia hata zaidi.
Kulingana na Wakorintho
ya pili sura ya 7
mstari wa sita na saba.
Basi alisaidiwa na ndugu yake.
Sisi pia tunapaswa kutafuta
msaada wa akina ndugu.
Na Yehova anatumia
ndugu na dada zetu
kutupatia msaada
wowote tunaohitaji.
Na tuna hakika ndugu zetu
watakuwa tayari kutusaidia
licha ya hali yoyote
na hivyo tudumishe shangwe.
Huenda tukakabili taabu
kwa sababu ya kuvunjika moyo.
Na sisi sote,
kwa kawaida tunakabili
hali hizo maishani
mara kwa mara.
Kuna mambo mengi
yanayoweza kutuvunja moyo.
Fikiria jambo tulilotaja.
Kufiwa na mtu unayempenda.
Labda mwenzi wa ndoa anapokufa.
Mmeishi pamoja kwa miaka mingi.
Na kama Yehova alivyosema
katika bustani ya Edeni
hao wawili watakuwa
mwili mmoja.
Na unajua hali iilikuwa
hivyo kati yako
na mume wako au mke
wako ambaye amekufa.
Unaanza kupatwa na
hisia za kushuka moyo
labda unahuzunika,
una majonzi
una uchungu
unasononeka
na kukosa shangwe.
Lakini kumbuka kwamba
kuna zawadi tatu ambazo zinaweza
kutusaidia kuwa na shangwe
Licha ya majaribu yoyote
tunayoweza kukabili.
Zawadi ya kwanza
ni uhusiano wetu
pamoja na Yehova.
Daudi alikuwa na
uhusiano mzuri na Yehova.
Katika kitabu cha
1 Samweli sura ya 30.
Ningependa kutaja
mambo machache
katika mistari kadhaa
ya sura hiyo.
Kitabu cha kwanza cha
Samweli sura ya 30
tutaanza na mstari wa kwanza.
Majeshi yake mwenyewe
yalipotaka kumuua Daudi
kwa sababu Waamaleki
walikuwa wameliteketeza jiji
na kuwachukua wake zao
na watoto wao mateka
kutia ndani
wake wawili wa Daudi,
kulingana na simulizi hilo
Daudi alitaabika sana.
Ona jambo linalotajwa
mwishoni mwa mstari wa 6.
Kwamba Daudi
alijitia nguvu
kwa msaada wa
Yehova Mungu wake.
Na hicho ndicho chanzo
cha nguvu zetu pia.
Tunapata nguvu kutoka
kwa Yehova Mungu wetu.
Atatusaidia na kutufariji.
Yeye ndiye Mungu wa faraja,
kama Neno lake Biblia
linavyosema.
Basi zawadi ya kwanza
ni uhusiano wetu na Yehova.
Zawadi ya pili,
ni undugu wetu.
Kwa kweli tunatiwa moyo sana na undugu wetu.
Kumbuka Zaburi ya 133.
Ambayo mwanzoni kabisa inaanza kwa kusema:
“Tazama! Jinsi ilivyo vema
na jinsi inavyopendeza
ndugu kukaa pamoja kwa umoja!”
Tunajua maneno hayo ni ya kweli kabisa.
Lakini pia tunajua kwamba
Shetani anatumia mbinu
ya kutufunga gerezani
ili kututenganisha na
ndugu na dada zetu.
Anaweza kufanya tufungwe.
Lakini hata tukifungwa gerezani,
bado tunaweza kupata ushirika.
Tunawezaja kufanya
hivyo tukiwa gerezani
na ndugu zetu wako mbali nasi?
Ni kupitia kumbukumbu.
Unaweza kuchukua daftari
na picha zilizo katika
kumbukumbu lako.
Naam, kumbukumbu lako.
Sio daftari halisi
bali kumbukumbu zilizo
katika ubongo wako.
Na utafakari mabaki ya
chakula cha kiroho.
Yaani, kumbukumbu.
Naam, kumbukumbu nzuri
inaweza kutuimarisha na
kutupatia shangwe.
Kwa wale walio na umri mkubwa
kama mimi mnajua jambo hili.
Mnajua kwamba watu
waliozeeka hufanya hivyo mara nyingi.
Hatuna nguvu za kufanya
mambo mengi.
Kumbukumbu hutupatia shangwe.
Tunapata shangwe moyoni.
Sasa jambo la tatu ni
tumaini letu.
Tuna tumaini la kumtumikia Yehova
chini ya hali zenye uadilifu, milele.
Milele.
Kwa kuendelea.
Bila mwisho.
Kwa kuendelea na
kuendelea na kuendelea.
Kwa mfano, unapotazama
juu angani
huwezi kuona mwanzo
wala mwisho.
Hiyo ndiyo maana ya milele.
Utakuwepo sikuzote.
Utakuwa na fursa ya
kuwa na shangwe, milele.
Unapotazama video ifuatayo
jaribu kutambua
ni zawadi gani
iliyowasaidia ndugu
na dada zetu
kuwa na shangwe
licha ya taabu.
Tangu tulipofunga ndoa
tulijua kwamba siku moja
tutapata watoto.
Hivyo nilipopata uja uzito
tulifurahi sana.
Mke wangu Becky aliponiambia
kwamba ana uja uzito,
kwa kweli nilifurahi sana.
Papo hapo nilijihisi kama baba.
Tukaanza kufanya mipango
mara moja.
Tukajawa na hisia za upendo,
upendo mwingi.
Siku moja Becky alikuwa anaumwa,
rafiki yetu akatuambia
“Nendeni mkamwone daktari.”
Walipomchunguza mtoto kwa kompyuta,
daktari aliporudi akatuambia
hawakuona mapigo ya moyo.
Huo ulikuwa wakati
mgumu sana kwangu.
Ah! kilikuwa kipindi
kigumu sana kwangu.
Kwa sababu ndoto,
matumaini, na matayarisho
yote tuliyofanya
ghafla hayapo tena.
Moyo wangu ulikuwa umejaa hisia
nyingi na upendo
kwa ajili ya mtoto
lakini sasa nilijihisi mtupu.
Nilihisi maumivu makali.
Nilibaki na huzuni nyingi sana.
Hatukujua la kufanya.
Ilikuwa siku ya mkutano
basi tulitamani kwenda.
Na tulitaka kuhudhuria
kwa sababu tulijua hatungefanikiwa
kwa nguvu zetu wenyewe.
Tulimhitaji Yehova.
Watu walipojua kwamba
tumempoteza mtoto wetu,
wengi wao
walinisimulia mambo
ambayo wamepitia
na hilo lilitufanya tusijihisi wapweke.
Lakini Yehova ametupatia
marafiki wazuri sana.
Marafiki ambao wameshikamana nasi
kwa ukaribu kuliko ndugu.
Wanaotambua tunapokuwa na hali ngumu.
Walisali,
walitembea pamoja nasi
na kutusikiliza.
Ninajua huu ni msaada
kutoka kwa Yehova.
Inachukua muda ili kurudia
shangwe tuliyokuwa nayo.
Katika funzo langu la kibinafsi,
nilipata andiko ambalo lilinisaidia sana.
Zaburi 139
linalosema kwamba hakuna mahali
ambapo Yehova hawezi kufika.
Hakuna giza linaloweza kumzuia,
na tulisi tuko katika giza kama hilo.
Kutafakari andiko hilo
kulinisaidia sana.
Na hatua kwa hatua
nilihisi kwamba Yehova alinisaidia
kuwa na furaha tena.
Tunapopata taabu
Yehova hutusaidia.
Hatuachi bila msaada.
Kwa mfano andiko la
2 Wakorintho sura ya 4.
Linasema:
2 Wakorintho sura ya
4 mstari wa 8.
Mstari wa 8 kutia ndani maelezo ya chini.
Linasema:
Tunakandamizwa katika kila njia,
lakini hatubanwi kupita
kiasi cha kushindwa kusonga;
tunafadhaishwa,
lakini si bila njia ya
kutokea kabisa.
Maelezo ya chini yanasema
tukiwa tumekata tamaa.
Yaani, Yehova hataruhusu
tukate tamaa.
Hebu jiulize:
Ni maandalizi gani kutoka kwa Yehova
yanayokusaidia kupata shangwe
licha ya mkazo wa kiakili
na wa kihisia ambao
huenda unapambana
nao sasa?
Je, ni uhusiano wako
pamoja na Yehova?
Undugu wetu?
Tumaini letu?
Au ni jambo lingine?
Mbali na zawadi hizo
kutoka kwa Yehova
fikiria mapendekezo yafuatayo.
Kula chakula chenye lishe.
Vilevile, pumzika vya kutosha.
Na pia ufanye mazoezi.
Unaweza kuandika
orodha mbili.
Orodha moja ya matatizo
unayoweza kuyatatua.
Na orodha ya pili,
ya matatizo ambayo huwezi
kuyatatua kwa sasa.
Shughulikia orodha ya kwanza
na umwachie Yehova orodha ya pili.
Zungumza na mzee wa kutaniko.
Au labda,
rafiki mkomavu.
Mtu mliye na uhusiano wa karibu.
Au mzazi.
Watu hao wako tayari kutusaidia.
Na wako tayari kushiriki nasi
ujuzi na uelewaji walio nao.
Watafanya hivyo kwa ukarimu.
Tambua kwamba huenda
ukahitaji kumwona daktari
ikiwa una matatizo fulani ya kiakili.
Yesu alisema hivi kwenye Luka 5:31.
“Watu wenye afya
hawahitaji daktari,
lakini wagonjwa wanamhitaji.”
Huo ni uamuzi wa kibinafsi
lakini kuna msingi wa kimaandiko.
Labda unahitaji msaada
kutoka kwa daktari au mtaalamu
aliye na uzoefu wa
kushughulikia hali hiyo.
Uwe na shangwe kwa sababu
una kibali cha Yehova.
Usiwe na shaka hata
kidogo kuhusu jambo hilo.
Ni kweli kwamba
si rahisi kushughulika na
mkazo wa kiakili au kihisia.
Lakini kumbuka
Yehova anaelewa.
Na atakusaidia uendelee kuvumillia.
Na unapoendelea kuvumilia
kwa ushikamanifu
utapata kibali cha Yehova.
Jambo ambalo linatupatia
sababu kubwa
ya kuwa na shangwe.
Kumbuka kwamba Mungu hajakuacha.
Bado una kibali chake
kama ngao kubwa inayokuzunguka
na pia baraka zake.
Basi uwe na shangwe
kutokana na ujuzi huo.
Na uendelee kushangilia
licha ya taabu.
Ndugu Gerrit Lösch
wa Baraza Linaloongoza
atatoa hotuba inayofuata
ya mfululizo huu
yenye kichwa:
Tunaweza Kuwa Wenye Shangwe
Licha ya Mateso.
Tangu mwanzo wa karne ya kwanza,
Wakristo wamekuwa wakiteswa.
Tafadhali fungua andiko la
2 Wakorintho sura ya 11
Paulo alikabili hali hiyo
2 Wakorintho 11:23-25,
andiko hilo linasema hivi:
“Je, wao ni wahudumu wa Kristo?
Ninajibu kama mwendawazimu,
mimi ni mhudumu kwa
njia kubwa hata zaidi:
Nimefanya kazi nyingi zaidi,
nimefungwa gerezani
mara nyingi zaidi,
nimepigwa mara nyingi sana,
na kukaribia kufa mara nyingi.
Mara tano nilipigwa na
Wayahudi viboko 40
kasoro kimoja,
mara tatu nilipigwa kwa fimbo,
mara moja nilipigwa mawe,
mara tatu nilivunjikiwa na meli,
usiku mmoja na mchana mmoja
nimekaa baharini;
Muda mfupi baada ya kutaja
hali hizo alizokabili,
katika sura ya 12, mstari wa 10,
Paulo aliandika hivi:
“Basi ninapendezwa na udhaifu,
na matusi, na nyakati za uhitaji,
na mateso na shida,
kwa ajili ya Kristo.
Kwa maana ninapokuwa dhaifu,
ndipo ninapokuwa na nguvu.”
Bila shaka,
si kwamba Paulo alifurahia kuteseka
badala yake,
alipata shangwe kwa
kufikiria matokeo yake,
yaani, kutakaswa kwa jina la Yehova.
Sasa tusome Wafilipi 1:14,
na kisha tutasoma mstari wa 18.
Mateso hutupatia fursa ya kuona
jinsi Yehova anavyotenda
kwa ajili ya watu wake
na kulitukuza jina lake.
Hilo linaweza kuwa ushahidi mzuri.
Wafilipi 1:14, 18
Paulo aliandika hivi:
“Sasa akina ndugu
wengi katika Bwana
wamekuwa na uhakika
kwa sababu ya vifungo
vyangu vya gereza,
nao wanaonyesha uhodari mwingi
wa kulisema neno la
Mungu bila woga.
Matokeo ni nini?
Ni kwamba katika kila njia,
iwe ni kwa unafiki
au ni kwa ukweli,
Kristo anatangazwa,
nami ninashangilia
kuhusu jambo hilo.
Kwa kweli, nitaendelea
pia kushangilia,”
badala ya kudhoofisha
tumaini letu
na uhusiano wetu
pamoja na Yehova,
Mateso hutuimarisha.
Kwenye maneno yaliyoandikwa
katika Waroma 5:3, 4,
Paulo anaeleza hivi:
‘Na tushangilie katika dhiki,
kwa kuwa uvumilivu huongoza
kwenye hali yenye kukubaliwa,
nayo hali yenye kukubaliwa,
tumaini,
nalo tumaini halikatishi tamaa.’
Ni wazi kwamba tumaini
hutusaidia sana kuvumilia mateso.
Biblia hutumia neno tumaini
katika njia mbalimbali
inataja “tumaini la wokovu,”
yaani, tumaini letu la wakati ujao.
Pia inataja tumaini la
kuoka Har-magedoni,
kuna tumaini la kuishi milele,
katika dunia paradiso.
Na pia tumaini la kuishi mbinguni.
Ni tumaini gani linalotajwa katika
Waroma 5:3, 4?
Ni tumaini la kwenda mbinguni.
Ona muktadha kwenye sura ya 5
mstari wa 2, sehemu ya pili
ya mstari huo inasema:
“na tushangilie, kwa kutegemea
tumaini la utukufu wa Mungu.”
Wakristo wa karne ya kwanza
walikuwa na tumaini
la kuishi mbinguni.
Tumaini lao halikumaanisha kwamba
matatizo ya ulimwengu
yangesuluhishwa
au kwamba wangeponywa magonjwa.
Walikuwa na tumaini
la kuishi mbinguni.
Wakolosai 1:3, inasema:
Siku zote tunamshukuru Mungu,
tunaposali kwa ajili yenu
kwa sababu ya tumaini
mlilowekewa akiba mbinguni.
Tusome andiko la
Waroma 8:20, 21.
Umati mkubwa
wa mashahidi wa Yehova leo.
Wanatumaini kwamba Yehova
atawathawabisha
kuishi katika dunia paradiso.
Paulo alitaja tumaini hilo,
alipoandika maneno hayo
katika Waroma 8:20, 21:
“Kwa maana uumbaji
ulitiishwa chini ya ubatili,
si kwa mapenzi yake wenyewe
bali kupitia yule aliyeutiisha,
kwa msingi wa tumaini
kwamba uumbaji wenyewe pia
utawekwa huru
kutoka katika utumwa wa uharibifu
na kuwa na uhuru wenye utukufu
wa watoto wa Mungu.”
Katika andiko la Waroma 12:12
Paulo aliposema shangilieni
katika tumaini lililo mbele yenu.
Alimaanisha tumaini la kimbingu.
Lakini kondoo wengine pia,
wanaweza kushangilia
katika tumaini lao.
Hivyo, sisi sote
tuna sababu za kushangilia.
Ulimwengu hauna tumaini
Lakini tumaini lako ni hakika.
Ulimwengu unaporomoka,
lakini tumaini lako
liko karibu kutimia.
Tumaini la ulimwengu
huu halina msingi
Tumaini lako linategemea imani.
Tumaini la ulimwengu
hukatisha tamaa,
lakini tumaini lako litafanikiwa.
Kwa kuwa ulimwengu
mpya uko karibu sana,
iwe tuna tumaini la kuishi
mbinguni au duniani.
Tutakuwa na shangwe milele.
Tusome pamoja andiko la Tito 2:13:
“Huku tukingojea tumaini lenye furaha
na kufunuliwa kwenye utukufu
kwa Mungu mkuu
na kwa Mwokozi wetu, Yesu Kristo.”
Pia, Waroma 8:24, 25, linasema:
Tumaini litatusaidia kuvumilia,
pia linasema,
‘Tumaini linaloonekana si tumaini
lakini tukitumainia kile
ambacho hatuoni,
tutaendelea kukisubiri
kwa uvumilivu.’
Tumaini linatofautiana,
tunaweza kuimarishaje
tumaini letu?
Neno tumaini linalotumika hapa,
katika kigiriki ni el·pisʹ,
linalomaanisha,
kutarajia mema.
Paulo anataja Tumaini,
mwishoni mwa orodha yake
baada ya kutaja dhiki, uvumilivu
na hali yenye kukubaliwa.
Ni wazi kwamba hakuwa
anarejelea jinsi tulivyohisi
tulipopokea habari njema,
badala yake, anarejelea
tumaini hakika tunalopata,
baada ya kuvumilia majaribu.
Mkristo anapovumilia majaribu
anapata uhakika kwamba
anakibali cha Mungu.
Uhakika huo,
huimarisha tumaini
alilokuwa nalo.
Kama Paulo, sisi pia
tunaweza kuwa na shangwe
licha ya mateso.
Huenda tukasemwa
au kutendewa vibaya shuleni,
kazini, katika familia
au kazi yetu ya kuhubiri
inapopigwa marufuku.
Katika Mathayo 5:11, 12
Kwenye mahubiri ya mlimani,
Yesu alisema hivi:
“Wenye furaha ni ninyi,
watu wanapowashutumu
na kuwatesa
na kuwasingizia kila aina ya uovu
kwa sababu yangu.
Furahini na kushangilia sana,
kwa kuwa thawabu yenu
ni kubwa mbinguni,
kwa maana hivyo ndivyo
walivyowatesa manabii
waliokuwapo kabla yenu.”
sasa unapotazama
video inayofuata,
ona jambo lililowasaidia
ndugu na dada hawa,
kuendelea kuwa na shangwe,
licha ya kukabili mateso.
Asubuhi moja mapema,
Jeshi la Urusi lilivamia
nyumba yangu,
walinifunga pingu
na kufanya msako katika
nyumba yangu.
Walinipeleka kwenye ofisi za FSB
ili kunihoji.
Siku mbili baadaye,
mahakama iliamua
niwekwe kizuizini.
niliogopa kwa sababu sikujua
ningetendewa jinsi gani gerezani.
Walinitisha kwamba mambo
yangekuwa magumu zaidi,
na walitaka nikubali kosa,
na nitaje majina ya Mashahidi wenzangu.
Na nilimkosa sana mke wangu.
Ilikuwa vigumu sana
kuishi mbali naye.
Kwa miezi miwili
sikuwa hata na Biblia.
niliamua kutengeneza nakala yangu.
Mke wangu aliniletea daftari,
na kila siku niliandika
mistari ya Biblia niliyoikumbuka.
Baada ya kuandika
karibu mistari 500,
nilipata Biblia.
Kwa sababu nilikuwa
na njaa ya kiroho,
niliisoma yote kwa miezi minne.
Wakati huo niliandika barua
kwa mke wangu, marafiki
na kuwatajia mambo niliyojifunza.
Barua nilizopokea kutoka
kwa mke wangu
na marafiki zangu
zilifanya nihisi nikiwa
karibu na ndugu na dada.
Ni kama tulikuwa tumefungwa pamoja.
sikuhisi upweke,
nilihisi ni kama rafiki
walikuwa hapo pamoja nami.
Mtu anapowekwa kizuizini,
anatengwa na jamii.
Lakini huwezi kumtenganisha
mtu huyo na Yehova.
siku nzima
nilisali kwa Yehova mara nyingi,
lakini nilisubiri kwa hamu
wakati wa usiku,
wakati ambapo kila mtu
alikuwa amelala.
Nilipata wakati wa kuongea na
Yehova kwa muda mrefu.
Pindi fulani
nilipokuwa peke yangu
katika chumba cha gereza,
nilitumia vizuri muda huo.
Nilipiga magoti,
nikalia machozi
nilipokuwa nikisali kwa Yehova.
Niliamua kuandika orodha ya
maombi yangu kwenye karatasi,
Kisha nikatia alama
maombi ambayo Yehova alijibu
Nilikuwa na uhakika Yehova yupo
karibu sana nami.
Pia niliimba nyimbo zetu
kimyakimya siku nzima.
Lakini nilipokuwa peke yangu
niliimba kwa sauti yangu yote.
Na nilijaribu kuhubiri
kila nilipopata fursa.
Tulizungumzia mambo mbalimbali
kutia ndani kuwekwa tatuu
na mfalme wa kaskazini.
Mambo niliyoogopa hayakutokea
Nilikaa kizuizini siku 343,
na sikupoteza hata unywele mmoja.
Huo ulikuwa mwaka wa
pekee zaidi maishani mwangu.
Shule iliyonisaidia
kuboresha sifa za kiroho.
Nilijihisi nikiwa karibu sana na Yehova.
Ni pendeleo kubwa kuunga mkono
Enzi kuu ya Yehova kwa njia hiyo.
Nini kinachokusaidia leo
uwe na shangwe?
Licha ya upinzani unaokabili?
ni uhusiano wako pamoja na Yehova,
undugu wetu, tumaini lako
liwe mbinguni au duniani,
yote hayo.
Na tuwe na shangwe katika
Upendo wa Yehova
na ndugu zetu
ikiwa unakabili mateso,
uwe na hakika ndugu zako wote
si ndugu zako katika
kutaniko lenu tu,
bali ulimwenguni kote,
wanasali kwa ajili yako.
Malaika wanakutazama,
na wanafurahi unapoendelea
kuwa mwaminifu,
na kwa njia hiyo
unaweza kuwatia moyo
malaika waaminifu.
Kama Yehova, Yesu na malaika,
ndugu zako pia wanajivunia,
na kuwa na shangwe,
kwa sababu ya uvumilivu,
na imani yako,
licha ya kukabili mateso.
Ndugu, William Turner
msaidizi wa Halmashauri ya Utumishi,
atatoa hotuba inayofuata,
katika mfululizo huu,
Tunaweza kuwa na shangwe
licha ya Njaa.
Unahisije ukikosa mlo mmoja?
au usipokula muda mrefu?
Wengine wanaathirika kihisia,
wanashindwa kukazia fikira,
na hata kushindwa kufikiria vizuri.
Vipi ikiwa,
hatuwezi kufanya lolote?
Hatuwezi kupata chakula
na tunaendelea kuwa na njaa.
Mtume Paulo,
alijipata katika hali kama hiyo
katika huduma yake.
katika 2 Wakorintho 11:27, alisema
‘Alikuwa na njaa na kiu
na kukosa chakula mara nyingi,’
huenda hilo lilitokea alipokuwa
akisafiri katika maeneo
yasiyokuwa na watu au jangwani.
Aliwategemea watu asiowajua
ili kupata chakula kidogo,
au huenda alipata chakula
kwa kufanya kazi katika
maeneo mapya.
Aliishi wakati ambapo kulikuwa
na njaa kali.
Kipindi cha njaa kilidumu
kwa miaka mitatu,
na kusababisha umaskini mkubwa
huko Yudea na Yerusalemu.
Licha ya kukosa chakula
katika kipindi hicho chote
mtume Paulo alidumisha
mtazamo mzuri.
2 Wakorintho 6:10,
anajifafanua yeye na wakristo wenzake
“kama walio na huzuni,
lakini wanaoshangilia sikuzote,”
Paulo alitambua kwamba,
nyakati ngumu zinaweza
kusababisha huzuni na taabu.
Lakini aliwezaje kushangilia?
yaani, kuwa na shangwe moyoni?
Licha ya njaa?
Tutapata jibu
tunaposoma kitabu cha wafilipi.
Tusome Wafilipi 4:11-13,
Paulo anasema,
Sisemi hivyo kwa sababu nina uhitaji,
kwa maana hata hali zangu ziweje
nimejifunza kuridhika.
Ninajua jinsi ya kupungukiwa na chakula,
na jinsi ya kuwa na vitu vingi.
Katika mambo yote na katika hali zote
nimejifunza siri ya jinsi ya kushiba
na jinsi ya kuwa na njaa,
jinsi ya kuwa na wingi
na pia jinsi ya kuishi bila kitu.
Kwa mambo yote
nina nguvu kupitia yule
anayenipa nguvu.’
Kwenye mstari wa 12
Paulo anasema alijifunza siri
ya jinsi ya kushiba
na kuwa na njaa.
siri hii
inahusisha kumtegemea Yehova
atuandalie mahitaji yetu,
na kuridhika
na vitu anavyotupatia.
Paulo alifanya hivyo
alijifunza ustadi wa kazi
ili asiwe mzigo kwa wengine.
Alijishughulisha sana na huduma.
Na alikuwa na vitu
vichache vya kimwili
alithamini msaada wa akina ndugu,
aliwathamini akina ndugu
walipomwandalia mambo aliyohitaji
Paulo alijifunza kutokana
na mambo hayo yote.
Na alipoona mkono wa Yehova
katika maisha yake
alitambua waziwazi kwamba
licha ya hali zozote alizokabili
alipaswa kumtegemea Yehova,
amwandalie mahitaji yake.
Kwenye mstari wa 13,
Yehova alimtegemeza Paulo
alimpa nguvu.
Basi, Paulo alipokabili
hali hizo ngumu.
Bado aliridhika,
alidumisha shangwe yake,
na kuendelea na huduma.
Tunajifunza nini kutokana
na mfano wa Paulo?
Huenda sisi pia tukakabili njaa
kwa sababu mbalimbali.
Kwa mfano,
upungufu wa chakula
labda kwa sababu ya misukosuko
na matatizo ya kiuchumi.
Hali zilizo ulimwenguni
zimefanya wengi wapoteze kazi
kutia ndani ndugu zetu
matatizo ya kiuchumi yanaweza
kufanya tupungukiwe.
Tunaweza kuwa na njaa
kwa sababu ya mateso.
Ndugu zetu walifungwa
katika kambi za mateso za wanazi
Mbinu moja ambayo Shetani aliitumia
ni kuwanyima chakula,
ili avunje utimilifu wao.
Inapohusu malengo ya kiroho,
wale wanaohamia kwenye
maeneo yenye uhitaji
hufanya mabadiliko
lazima wajifunze kuridhika
na vitu vichache.
Basi, katika hali mbalimbali
sote tunaweza kupungukiwa
na chakula
na kupatwa na njaa.
Hilo linaweza kutuletea
mahangaiko
na hata mikazo.
Siri ni nini?
Kumtumaini
na kumtegemea Yehova.
Tunapofanya hivyo
tunapata utulivu
na kushughulika na mahangaiko
ya siku moja tu.
Gharama za maisha zilipopanda
baba mmoja alisema,
kila siku nilimwomba Mungu,
atupe leo mkate wetu wa leo.
ili tuendelee kuishi
Tunapaswa kuonyesha shukrani
kwa mambo ambayo
Yehova anatuandalia,
baba huyo alipoenda
kununua chakula,
anasema pindi moja alikuta chakula
ambacho hawakupenda,
alifanyaje?
anasema, sikukipenda
lakini ni chakula,
basi tulikula chakula hicho.
Na alimshukuru Yehova
kwa kuwaandalia,
huenda hali za sasa zinaturuhusu
kula chakula tunachopenda,
lakini hali zikibadilika
tutafanya mabadiliko?
na kuonyesha uthamini?
tunafurahi kujua kwamba
Mungu wetu anatujali,
nakutupatia vitu tunavyohitaji,
Bila shaka,
tunapaswa kutumia maandalizi
ambayo Yehova anatupatia,
tafadhali tazama video inayofuata
na utambue mambo yaliyomsaidia
dada yetu kuwa na shangwe
licha ya kukabili njaa.
Hapa nchini Venezuela
muda mrefu kabla ya msukosuko,
hakukuwa na matatizo ya uchumi
kama ilivyo leo.
Tulienda dukani na kununua
chakula tulichotaka,
na kulikuwa na amani.
Hali ilianza kuwa mbaya sana kwetu
miaka mitano iliyopita.
Haikuwa rahisi hata kupata chakula,
hata vitu vya msingi.
Tulipohitaji kununua bidhaa fulani
hazikupatikana.
Kuna wazee wawili wa kutaniko
ambao walinitembelea karibu kila siku.
Waliniuliza kiasi cha chakula nilichohitaji.
Nilipokiandaa,
hangaiko langu lilikuwa kuhakikisha
watoto wangu wamekula na wameshiba.
Sikuzote niliwapa chakula kingi.
Ingawa mtoto wangu alikuwa akiniuliza,
“Mama hicho kitakutosha?”
Nilikuwa nikimwambia, “Ndiyo,
nitashiba.”
Kisha angeniambia, “Si kweli.”
Nilifikiri chakula hicho kingenitosha,
lakini mwili wangu ulihitaji
chakula kingi zaidi.
Jumapili moja asubuhi tukiwa mikutanoni,
nilianza kujihisi vibaya.
Nashukuru kwamba binti yangu
alikuwa hapo karibu.
Niliporudiwa na fahamu,
aliniambia, “Mama,
ulizirai mara tatu.”
Nikasema, “Haiwezekani.”
Papo hapo akina ndugu
wakanipeleka hospitali.
Daktari alisema kwamba nilikuwa
nimeathiriwa sana na utapiamlo.
Akina ndugu walifanya mipango ya kunisaidia.
Waliniletea chakula kilichopikwa,
na waliketi kando yangu
mpaka nilipomaliza chakula chote.
Bado sijarudia uzito wa mwili wangu,
kwa sababu nilikuwa mnene zaidi.
Lakini sasa, afya yangu ni nzuri zaidi.
Sikuzote, wazee walinijali.
Hilo lilinitia nguvu,
na sikupoteza shangwe yangu.
Namshukuru sana Yehova.
Ninamshukuru kwa sababu yeye
ndiye anayenitegemeza.
Ananilisha na kunivisha,
na kunipa marafiki wazuri.
Yehova amenipa mambo hayo yote.
Umetambua mambo
yaliyomsaidia dada yetu?
kwanza,
uhusiano wake na Yehova.
Aliona umuhimu wa kumkaribia
na kuhudhuria mikutano
kwa ukawaida
na jambo lingine undugu wetu,
inafariji kuona jinsi
wazee walivyokuwa macho
walimtembelea
na kumpa chakula
yeye na familia yake
na kuhakikisha walishiba.
Ni mambo yale yale
kudumisha uhusiano
Mzuri na Yehova,
msaada kutoka kwa
akina ndugu,
na pia kudumisha tumaini letu,
tutapata shangwe
licha ya kukabili njaa.
tunasadiki kabisa mambo
aliyosema Paulo,
kwenye Wafilipi 4:12
Yehova anaweza,
naye huandaa
mahitaji yetu yote,
katika kila hali.
Tunapokabili njaa
ni jambo la kawaida
kuhangaikia hali yetu,
na ya wale tunaowapenda.
lakini kama tulivyoona,
tunaweza kuwa na shagwe
licha ya kukabili njaa,
siri ni nini?
Tambua siri hiyo,
tungependa kuijua siri hiyo
na Yehova yuko tayari
kutufunulia siri hiyo.
Ni lazima tumtegemee
na tuone jinsi anavyotusaidia
Yehova anafurahi kuwaona
watumishi wake
wakibaki kuwa waaminifu
na wenye shangwe,
wakiwa na hakika
hatawaacha kamwe.
Ndugu Robert Luccioni
msaidizi wa halmashauri ya utangazaji
atatoa hotuba inayofuata
ya mfufululizo huu,
“Tunaweza kuwa na shangwe
licha ya kuwa Uchi.”
Kweli tunaweza kuwa na shangwe
licha ya kukabili majaribu makali?
Kufikia sasa
tumeona jinsi mtume
Paulo alivyodumisha
shangwe yake
licha ya dhiki, taabu,
mateso, na njaa.
Na hilo linawatia moyo kwa sababu
wengi wenu, mmewahi
au sasa mnakabili hali hizo.
Namna gani tunapopoteza
kila kitu,
kwa saabu ya misiba
au misukosuko,
mfano wa Paulo unaweza kutusaidia?
Andiko letu la msingi
Waroma 8:35,
Paulo anasema hata uchi.
Hauwezi kututenganishana upendo wa Kristo.
Na Paulo alikabili hali hiyo pia.
Tafadhali fungua 2 Wakorintho 11:27.
Ona jinsi anavyofafanua majaribu yake.
2 Wakorintho 11:27:
“Kwa kazi ngumu na yenye kutaabisha,
mara nyingi kukosa usingizi usiku,
njaa na kiu,
kukosa chakula mara nyingi, na pia baridi
na kukosa mavazi.”
Au katika uchi
kulingana na maelezo ya chini.
Paulo hakukosa mavazi kwa sababu ya uvivu.
Tunajua hilo kwa sababu maandiko
yanasema kwamba alifanya kazi
kwa bidii ili kupata riziki.
Lakini alipatwa na baridi
na kukosa mavazi.
Kwa sababu ya hali alizokabili
katika huduma yake.
Unakumbuka Paulo alipokuwa
katika ile meli
iliyopigwa na upepo mkali sana
na kuvunjika huko Mediterania?
Ilipokuwa ikivunjika-vunjika
Paulo na wenzake
walijishikilia kwenye vipande vya mbao
na vipande vya meli.
Labda walifika ufuoni na mavazi machache
au bila mavazi.
Kumbuka wakaaji wa Malta
waliwasha moto
kwa ajili ya waokokaji hao.
Pindi nyingine
Paulo alikimbia tu na mavazi aliyokuwa nayo.
Na alipigwa viboko au
kwa mawe na hilo lilichanachana nguo zake.
Kwenye Matendo 16:22
tunasoma kuhusu simulizi la
mahakimu wa raia
ambao baada ya kuyararua mavazi ya Paulo
waliamuru apigwe kwa fimbo
na kisha akatupwa gerezani.
Masimulizi hayo yanatusaidia kuelewa vizuri
maneno ya Paulo
kwenye 1 Wakorintho 4:11.
4:11.
“Mpaka saa hii
tunaendelea kuwa na njaa na kiu
na kukosa mavazi ya kutosha
na kupigwa na kuwa bila makao.”
Licha ya hali hizo
Paulo aliwatia moyo Wakristo wenzake
wafanye nini?
Ona mstari wa 16.
“Kwa hiyo, ninawasihi,
iweni waigaji wangu.”
Aliwatia moyo waige mfano wake
wawe na shangwe licha ya majaribu
kwenye Waroma12:12 anasema:
“Shangilieni katika tumaini . . .
Shirikini pamoja na watakatifu
kulingana na mahitaji yao.”
Paulo alikuwa na shangwe
na aliwasaidia wengine
hata yeye mwenyewe alipokabili
hali ngumu.
Wengi kati ya ndugu na dada zetu wapendwa
wamepatwa na majanga mabaya.
Fikiria mifano michache ya mwaka uliopita.
Matetemeko
huko Albania,
Filipino,
Peurto Riko na kwingineko.
Mafuriko makubwa Kongo,
Hispania, Marekani.
Vimbunga na tufani
huko Bahamas
na Filipino.
Moto mkubwa huko Australia
na Marekani na majanga mengine mengi.
Matokeo ya majanga hayo
na mengine mengi ni kwamba
baadhi yandugu na dada zetu
wamelazimika kukimbia usiku
wakiwa tu na mavazi waliyovaa.
Katika hali fulani
majanga hayo yaliharibu mali zao zote.
Tunaumia sana
tunapopata habari hizo.
Ndugu na dada wapendwa
mnaopatwa na hali hizi
tafadhali kumbukeni kwamba
tunasali kwa ajili yenu.
Lakini licha ya hali hizo
ndugu zetu wanaendelea kuwa na shangwe.
Hilo linawezekanaje?
Unapotazama video ifuatayo,
ona mambo yaliyomsaidia
ndugu na dada huyu,
kuwa na shangwe licha ya kukosa mavazi
kwa kipindi fulani.
Jambo moja kuhusu jiji la New York,
ni kwamba
ni jiji lenye shughuli nyingi sana.
Sisi pia tunaishi hivyo.
Maisha yetu yalikuwa mazuri.
Tulikuwa tunafurahia kufanya upainia,
kufanya kazi,
na kujitahidi kuishi jijini New York.
Jambo moja linalotuhangaisha
ni usalama.
Lazima uwe makini kuhusu mazingira.
Lakini hatukuwahi kuwazia kwamba
siku moja tutakabiliana na kimbunga.
Hilo halikutuhangaisha.
Maonyo yalipotolewa
kulikuwa na mvua na upepo.
Maji yakaanza kuingia kwenye
sehemu ya maegesho
karibu na nyumba yetu.
Hapo ndipo nikatambua kuna hatari.
Tuliondoka bila kubeba chochote.
Huo ulikuwa uharibifu mkubwa sana.
Tulipoteza kila kitu
ndani ya usiku mmoja.
Sikuwaza kamwe kwamba
siku moja maji yangeingia
katika nyumba yetu,
na kuharibu kila kitu,
kutia ndani mali zetu na nguo zetu.
Kwa mara ya kwanza maishani
nilijihisi fukara.
Nilivunjika moyo,
nilibaki nikijiuliza,
Mimi na mke wangu tutafanya nini sasa?
Nakumbuka
tulikuwa na kusanyiko mwisho juma huo
na sikuwa na koti wala tai.
Kwa maoni yangu niliona mavazi kuwa
kitu cha kawaida sana.
Nilikuwa na nguo nyingi.
Akina ndugu na dada walijitolea
kutusaidia katika njia nyingi sana.
Ijumaa kabla ya kusanyiko,
ndugu mmoja alibisha mlango wetu
na kutuletea suti tatu,
na viatu.
Walitununulia mavazi,
sikuamini jambo hilo.
Marafiki hao walitukumbatia
wakatupatia zawadi
Tulikuwa na hakika Yehova
alikuwa akituonyesha upendo.
Tulifanikiwa kuhudhuria kusanyiko
na kufurahia chakula cha kiroho
ingawa tulikuwa katika hali hiyo.
Ingawa tulipoteza mali zetu zote,
bado tuliendelea kupainia,
jambo ambalo tunaendelea
kufanya mpaka leo.
Yehova ametuahidi kwamba,
ikiwa tutaendelea kuutafuta
kwanza Ufalme
atatutimizia mahitaji mengine yote.
Na hicho ndicho chanzo
cha shangwe yangu.
Hata ukikabili matatizo
ya aina gani maishani
hata kufikia hatua ya kubaki uchi
hilo haliwezi kuzuia
au kukomesha uhusiano tulio nao
na Mungu wetu Yehova.
Umetambua jambo lililowasaidia?
Walipoteza kila kitu usiku mmoja
na hawakujua jambo la kufanya.
Ulitambua azimio lao?
Kumbuka alichosema Brian,
‘Hata tukikabili dhiki ya aina gani
hata kufikia kuwa uchi
haitakatiza kamwe
uhusiano wetu na Yehova.’
Walifurahi kupata msaada
kutoka wa ndugu zao.
Walikuwa imara kwa sababu ya tumaini lao.
Tunajifunza nini?
Tunapokabili majaribu
hata majaribu ambayo
yanafanya tupoteze mali zetu
au kupungukiwa na mavazi
tunaweza kudumisha shangwe yetu
kwa sababu ya mambo matatu tuliyotaja.
Kudumisha uhusiano mzuri na Yehova,
kupata msaada kutoka kwa ndugu zetu,
na kudumisha tumaini letu.
Wengi wenu huchukua hatua mara moja
mnaposikia kuhusu uhitaji wa
akina ndugu na dada
na tunathamini sana jambo hilo.
Majanga yanazidi kuongezeka,
yanakuwa mengi na mabaya zaidi
basi uhitaji wa kuwasaidia ndugu zetu
unazidi kuongezeka.
Tunawapongeza
na kuwashukuru kwa msaada wenu.
Baadhi yenu hujitolea kwenda kusaidia
katika maeneo hayo.
Kwa mfano baada ya kimbunga Dorian
kupiga Bahamas
marubani Mashahidi
waliwasafirisha zaidi ya wajitoleaji 700
katika maeneo hayo.
Wengine wenu mnawasaidia
ndugu na dada katika eneo lenu.
Kwa mfano nchini Kongo
ndugu na dada walikimbia kutoka vijijini
wakiwa tu na nguo walizovaa
kwa sababu ya msukosuko.
Wangefanya nini baad ya
kupoteza mali zao zote?
Akina ndugu na dada kutoka
katika makutaniko jirani
ambao hawana vitu vingi
walitoa pesa, chakula,
mavazi na hata nyumba
kwa ajili ya ndugu walioathiriwa.
Huko Bolivia na Venezuela
makutaniko yaligawana chakula
kulingana na maeneo yao.
Fikiria pia jinsi ndugu zetu
wameandaa msaada
wakati huu wa janga la ugonjwa wa Corona.
Wameandaaa chakula, misaada,
kutegemezana kihisia na kiroho.
Makutaniko na familia zimesaidiana.
Na kwa sababu ya roho yenu ya kujidhabihu
na michango yenu
mmekuwa baraka kwa
ndugu na dada zenu ulimwenguni pote.
Jambo hilo limemthibitisha Shetani
kuwa mwongo kabisa.
Kwa nini?
Kumbuka katika Ayubu 1:11
Shetani alimtukana Yehova
na pia sote tunaompenda Yehova
kwa kudai kwamba
tutamwacha Yehova
ikiwa tutakabili majaribu.
Tusome Ayubu 1:11:
“Lakini, ili mambo yabadilike,
nyoosha mkono wako na upige kila kitu alicho nacho,
na kwa hakika atakutukana
mbele za uso wako mwenyewe.”
Shetani alikuwa na hakika kwamba
tukiambiwa tuchague kati ya mali zetu
na kuwa washikamanifu kwa Yehova
tutachagua mali zetu.
Kama tungelazimika kuamua kati ya
mahitaji yetu na kumsaidia mtu mwingine
tungejitanguliza sisi kwanza.
Alisema uwongo.
Anakasirika sana anapoona
mambo yanayoendelea katika
tengenezo la Yehova leo.
Basi tufanye nini?
Endelea kumkasirisha.
Endelea kuwasaidia ndugu na dada zako
wenye uhitaji.
Na hivyo tutapata furaha
na kuwasaidia ndugu zetu
wawe na shangwe.
Basi,
sisi sote na tuazimie
kuendelea kudumisha shangwe yetu
kwa kufanya mambo hayo matatu
kudumisha uhusiano mzuri na Yehova,
kuthamini msaada na
upendo kutoka kwa ndugu zetu
na kutafakari kuhusu tumaini letu
na usisahau kamwe
Tunapoendelea kumtumikia Yehova
kwa uaminifu licha ya kuwa uchi,
licha ya kupoteza mali zetu zote
tunaufurahisha moyo wa Yehova
na hiyo mojawapo ya sababu
kuu ya kuwa na shangwe.
Sasa ndugu Ralph Walls
Msaidizi wa Halmashauri ya Wafanyakazi
atatoa hotuba inayofuata katika mfululizo huu,
Tunaweza Kuwa na Shangwe Licha ya Hatari.
Kichwa cha hotuba hii sio swali.
Badala yake tunazungumzia jambo hakika.
Tunaweza kuwa na shangwe licha ya hatari.
Acheni tuchunguze pamoja mfano wa mtume Paulo.
Alikuwa na shangwe licha ya kukabili hatari.
Na alikabili hatari nyingi katika huduma yake.
Katika mstari mmoja tu anataja hatari nane alizokabili.
Kutia ndani hatari za kutokana na wezi.
Akiwa huko Efeso
huenda alikabiliana na wanyama-mwitu
katika ukumbi wa maonyesho.
Tafadhali fungua andiko la 2 Wakorintho 1:8-11
Inasema:
“Kwa maana hatutaki mkose kujua, akina ndugu,
kuhusu dhiki tuliyopata
katika mkoa wa Asia.”
Aliandika hivyo alipokuwa Ulaya,
huko Makedonia.
Anaongeza hivi:
“Tulikuwa na mkazo mkubwa sana
unaozidi nguvu zetu wenyewe,
hivi kwamba hatukuwa na
uhakika hata kuhusu uhai wetu.
Kwa kweli,
tulihisi kwamba tumepokea hukumu ya kifo.
Ilikuwa hivyo
ili tusijitegemee sisi wenyewe,
bali tumtegemee Mungu
ambaye huwafufua wafu.
Alituokoa kutoka katika hatari kubwa ya kifo
na atatuokoa,
nasi tumeweka tumaini letu kwake
kwamba ataendelea kutuokoa.
Ninyi pia mnaweza kutusaidia
kwa kutoa dua kwa ajili yetu,
ili wengi watoe shukrani kwa ajili yetu
kwa kibali tunachopokea
kwa sababu ya majibu ya sala za wengi.”
Mwaka mmoja hivi mapema
aliandika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho
Pindi hiyo alikuwa Asia,
jiji la Efeso.
Kwenye 1 Wakorintho 15:32:
“Ikiwa kama watu wengine,
nimepigana na wanyama wa mwituni huko Efeso,
hilo lina faida gani kwangu?”
Hilo linaonyesha kwamba huenda
alikabiliana na wanyama-mwitu katika
ukumbi wa maonyesho.
Lakini tumaini lake la ufufuo lilimwimarisha.
Kama alivyosema,
“ilikuwa hivyo ili tusijitegemee sisi wenyewe,
bali tumtegemee Mungu
ambaye huwafufua wafu.”
Pia alitiwa moyo na kuimarishwa na
Wakristo wenzake.
Alisema:
“Ninyi pia mnaweza kutusaidia
kwa kutoa dua kwa ajili yetu,
ili wengi watoe shukrani kwa ajili yetu
kwa kibali tunachopokea
kwa sababu ya majibu ya sala za wengi.”
Kutanikoni
tunafurahia ushirika wa ndugu zetu
wanaotusaidia na kututegemeza
katika njia mbalimbali.
Katika huduma yake,
Paulo na wenzake walikabili
mkazo mkubwa sana,
na hata hawakuwa na uhakika
kuhusu uhai wao.
Paulo alipata wapi msaada na kitia-moyo?
Alitiwa moyo
na kufarijiwa na Wakristo wenzake.
Misiba ya asili na misiba mingine
inapotokea, mara nyingi,
ndugu zetu wanawakuwa wa kwanza kufika
ili kuwatolea msaada wa kimwili na wa kiroho
ndugu zao na pia watu wengine wenye uhitaji.
Wakristo hawapigani na wanyama-mwitu
katika ukumbi wa maonyesho.
Leo, kama Paulo,
tunaweza kuwa na shangwe
licha ya hatari tutakayokabili.
Kila mmoja wetu
anaweza kukabili hatari
kutokana na wezi
au kushambuliwa
wakati wa msukosuko.
Biblia ilitabiri kwamba
katika siku hizi za mwisho
watu wangekuwa “wakali,
wasiopenda wema.”
Unapotazama video inayofuata
ona mambo yaliyosaidia familia moja
kuwa na shangwe licha ya hatari.
Nilizaliwa huko Caracas,
na kuishi eneo linaloitwa Petare.
Huko Petare kuna visa vingi
vya uhalifu na ukatili
Miaka michache iliyopita
dada mmoja painia alikufa
kwa sababu ya kupigwa risasi kimakosa.
Mwanangu alipatwa pia na jambo kama hilo.
Kulikuwa na vurugu kwenye ujirani wetu,
mwanangu alipigwa risasi
kimakosa na kufa papo hapo.
Tulibaki na pengo kubwa.
Niliumia nilipoenda chumbani kwake
na kuona kitanda alichokuwa akilalia.
Na kuona vitu vyake,
viatu,
na nguo alizopenda
--nguo zake na kabati lake.
Nilitokwa na machozi.
Ilikuwa vigumu sana
kushughulika na hali hizo.
Lakini baada ya kutaniko kujua hali hiyo,
papo hapo walianza kunisaidia.
Walitusaidia kushughulikia
mipango yote ya mazishi.
Baada ya kupitia hali hiyo,
niliogopa sana kwenda
kwenye utumishi wa shambani.
Nilihofia uhai wangu
na watu wa familia yangu.
Nilisali kwa Yehova naye akanipa hekima
ili niendelee kuhubiri.
Pindi fulani ninapokuwa peke yangu
nikitafakari na kufikiri
kuhusu mwana wangu,
kumbukumbu hizo hunijia.
Mimi hupatwa na hisia za huzuni,
na ninaanza tena kulia.
Lakini ninapokazia fikira tumaini la ufufuo,
hilo hunisaidia kusonga mbele.
Simulizi moja ninalopenda
na kukumbuka sikuzote ni kuhusu Lazaro.
Hapo Martha anasema,
Ninajua atafufuka siku ya mwisho.
Nami nina uhakika kwamba
Yehova atafanya hivyo.
Ninajua atamfufua,
Yehova atanirudishia mwanangu.
Nilipopatwa na msiba huo,
ni kweli kwamba nilipoteza shangwe yangu.
Lakini baada ya kipindi
cha kuomboleza kupita,
tumaini la ufufuo lilitupatia shangwe.
ni kana kwamba Yehova
anazungumza nami na kuniambia
Uwe mtulivu
endelea,
nawe utapata baraka
Endelea kuwa mwaminifu
na uwe mshikamanifu
nami nitakurudishia mwana wako.
Ni nini kilichowasaidia
kuwa na shangwe licha ya hatari?
Sala,
tumani la ufufuo,
msaada wa akina ndugu,
roho ya Yehova.
Ni msaada gani kutoka kwa Yehova
unaokusaidia kuwa na shangwe
licha ya hatari unazokabili?
Ni uhusiano mzuri pamoja na Yehova,
undugu wetu,
tumaini letu,
au jambo lingine?
Katika siku hizi za mwisho,
ngumu kushughulika nazo,
tunahimizwa kushangilia
katika tumaini la kuokolewa
kutokana na hatari.
Tunatarajia sana
mwisho wa mfumo huu mwovu
kama Habakuki alivyotarajia
mwisho wa uovu.
Tusome Habakuki sura ya kwanza.
Ona mkazo alioupata
kwa sababu ya ukatili,
ugomvi,
na ukandamizaji uliomzunguka.
Aliuliza:
‘Ee Yehova, . . .
Nitaomba msaada kwa sababu ya
ukatili mpaka lini?’
“Kwa nini unanifanya nione mambo mabaya?
Na kwa nini unavumilia ukandamizaji?
Kwa nini uharibifu na ukatili uko mbele yangu?
Na kwa nini ugomvi na mizozo inaongezeka?”
Kwa nini,
kwa nini,
kwa nini,
kwa nini,
mpaka lini?
Ona jambo alilosema
kwenye sura ya pili mstari wa tatu.
“Kwa maana maono hayo
bado yatatimia kwa wakati wake uliowekwa,
nayo yanasonga haraka
kuelekea mwisho wake,
nayo hayatasema uwongo.
Hata yakikawia,
endelea kuyatarajia!
Kwa maana
hakika yatatimia.
Hayatachelewa!”
Kama Habakuki,
tunamtegemea Yehova,
na tuna hakika hivi karibuni
atakomesha ukatili.
Habakuki alichukua hatua ya
kumkaribia Yehova,
rafiki wa karibu na baba.
Hakuhangaishwa tu na hali yake,
wala kutegemea uelewaji wake.
Badala yake alisali kuhusu
hisia na wasiwasi wake.
Alituwekea mfano mzuri.
Ona azimo lake
kwenye sura ya tatu
mstari wa kumi na nane.
Anasema:
“Mimi
nitashangilia katika Yehova;
nitakuwa na shangwe
katika Mungu wa wokovu wangu.
Yehova, msikiaji wa sala,
anatualika tumtegemee
na kumwambia mahangaiko yetu.
Yehova hakumkaripia Habakuki
kwa kutaja mahangaiko yake.
Yaliandikwa!
Ili kuonyesha kwamba ni
jambo la kawaida kupatwa na
hisia kama hizo.
Yehova anataka tumlilie.
Tukifanya hivyo
tutaona jinsi atakavyojibu sala zetu.
Atatukumbatia kwa uchangamfu
na kutuongoza kwa fadhili.
Atatusaidia kuelewa mawazo yake
hata tupatwe na nini.
Sala zetu za kutoka moyoni
ni mojawapo ya njia kuu za
kumtegemea Mungu.
Tuna shangwe kwa sababu tunajua
Yehova anatamani kutukomboa
kutoka kwa hatari zote.
Ndugu David Schaffer,
Msaidizi wa Halmashauri ya Ufundishaji,
atatoa hotuba ya mwisho ya mfululizo huu:
Tunaweza Kuwa na Shangwe
Licha ya Upanga.
Alipofungwa mara ya kwanza
huko Roma kati ya mwaka wa
59-61 WK
Mtume Paulo aliruhusiwa kuishi
katika nyumba aliyokodi,
ingawa alikuwa chini ya ulinzi wa mwanajeshi.
Katika miaka hiyo miwili alimhubiria
kila mtu aliyemtembelea.
Vilevile,
aliandika barua kwa Waefeso,
Wafilipi,
Wakolosai,
Filemoni,
na huenda Waebrania pia.
Kisha Paulo akaachiliwa
kutoka gerezani.
Sasa angeanza tena kazi ya umishonari.
Alimwandikia Timotheo
aliyetumikia huko Efeso
na Tito aliyetumikia huko Krete.
Hata hivyo,
Maliki Nero aliwalaumu Wakristo
kwa kuanzisha moto uliochoma
sehemu kubwa ya Roma.
Mara nyingine tena,
Paulo akajikuta
gerezani tena.
Baada ya kutumikia kwa miaka mingi
akiwa Mkristo mwaminifu,
ulikuwa mwaka wa 65,
alihisije?
Tunapata jibu katika barua yake
ya pili kwa Timotheo.
Aliiandika akiwa gerezani.
Tafadhali fungua
2 Timotheo sura ya 4.
Je, wanaume waliomkamata Paulo
walikuwa na mapanga?
Bila shaka.
Paulo alipoona mapanga hayo
alikumbuka jinsi
Mfalme Herode Agripa
alivomuua Yakobo
ndugu ya Yohana kwa upanga?
Inawezekana.
Lakini katika andiko hili la 2 Timotheo,
Paulo alihisi kwamba
baada ya muda mfupi,
yeye mwenyewe angeuawa.
Pia, tunaona jambo jingine.
Tunaona mambo matatu
yaliyomwimarisha Paulo
alipokaribia kuuawa.
Tusome 2 Timotheo 4:6-8.
“Kwa maana mimi tayari ninamiminwa
kama toleo la kinywaji,
na wakati wangu wa kufunguliwa
umekaribia sana.”
Yaani, kifo chake
na mwishowe angefufuliwa katika
Ufalme wa Kristo mbinguni.
Mstari wa 7:
“Nimepigana pigano zuri,
nimekimbia mbio mpaka mwisho,”
Mpaka mwisho! Naam,
Paulo alihisi kwamba
alikuwa akikaribia
kumaliza mbio za maisha yake
kwa ushindi mkubwa.
Anaendelea:
“Nimeishika imani.
Tangu sasa na kuendelea
nimewekewa akiba ya
taji la uadilifu.”
Hapa tunaona tumaini imara la Paulo.
Anasema:
“Ambalo Bwana,
aliye mwamuzi mwadilifu,
atanipa kuwa thawabu
katika siku ile.”
Je, umeona jinsi Paulo alivyokuwa na
uhusiano wa karibu na Yehova?
Maneno yake yanaonyesha
alikuwa na uhakika thabiti kwamba
Mwana wa Mungu angempa tuzo hili.
Kisha Paulo anaendelea kusema:
“Lakini si mimi tu,
bali pia wote ambao wamependa
kufunuliwa kwake.”
Paulo aliwapenda ndugu zake
Wakristo na hakuwasahau.
Kwa njia hiyo Paulo alikuwa na shangwe
ingawa alikabili kifo.
Ndugu zake,
uhusiano wake na Yehova,
tumaini lake,
si kwamba alitamani kufa.
Alitamani kuendelea kumtumikia
Yehova pamoja na ndugu na dada zake.
Lakini alikabili kifo kwa ujasiri.
Na alipata shangwe kwa sababu ya
thawabu ambayo alijua
angepata baadaye.
Sisi pia tunaweza kupata shangwe
tunapokabili kifo.
Jinsi gani?
Tusome tena andiko letu la msingi
Waroma 8:35.
Tungependa kupata majibu ya
maswali mawili ambayo
Paulo anauliza hapa.
“Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo?
Je, ni dhiki au taabu au
mateso au njaa au uchi au
hatari au upanga?”
Ona jibu kwenye mstari wa 38 na 39.
“Kwa maana nimesadiki
kwamba wala kifo
wala uzima wala malaika wala
serikali wala mambo yaliyopo sasa
wala mambo yatakayokuja wala nguvu
wala kimo wala kina wala
uumbaji mwingine wowote
havitaweza”
Ndio kifo hakiwezi
“kututenga
na upendo wa Mungu ulio
katika Kristo Yesu Bwana wetu.”
Kulala katika kifo kwa muda
hakuwezi kuzuia upendo wa Yehova
kwa watumishi wake.
Bado Yehova anampenda Abrahamu,
Isaka, na Yakobo?
Vipi Sara, Rebeka, Ayubu,
Musa, Danieli?
Namna gani waliokufa katika magereza,
kambi za mateso kwa sababu ya
kushikilia imai yao?
Bado Yehova anawapenda,
bila shaka anawapenda.
Bado anawapenda sana
mamia ya ndugu na dada ambao
wamekufa hivi
karibuni kwa sababu ya ugonjwa wa Corona.
Bado anampenda babu yako,
baba yako, dada yako,
wako katika kumbukumbu lake.
Atawarudisha wawe hai tena.
Na akina ndugu,
jambo hili linatusaidia sana
tunapokabili hatari ya kifo
kwa upanga kama Paulo.
Unapotazama video inayofuata,
jaribu kuona msaada kutoka kwa Yehova
uliomsaidia ndugu yetu
Barte Michael Dugbe
kuwa na shangwe
licha ya kukabili hatari
ya kifo.
Hali zinapobadilika,
mambo yanapokuwa mabaya
maishani mwako,
jambo pekee unalobaki nalo
ni uhusiano wako
pamoja na Yehova.
Jina langu ni Baite Michael Dugbe
nilizaliwa Monrovia, Liberia mwaka 1980.
Maisha yalikuwa mazuri
huko Monrovia kabla ya vita.
Wazazi wetu walitupenda.
Tulikuwa na nyumba nzuri
na tulisoma shule nzuri.
Nilipokuwa na miaka tisa,
mambo yalibadilika ghafla.
Tulisikia kwamba waasi
walitaka kupindua serikali.
Habari hizo zilifanya watu
waingiwe na hofu;
Biashara zilianza kufungwa,
huduma mbalimbali zikakatizwa,
hakukuwa na umeme,
maji, yaani, kila kitu.
kwa miaka michache iliyofuata
hali zilizidi kuwa mbaya.
Kisha mwaka wa 1996,
mambo yakaharibika kabisa.
Waasi waliingia jijini,
visa vya uporaji viliongezeka,
na kulikuwa na milio ya risasi,
waasi wangewatendea kikatili
watu ambao wangekataa
kuwaunga mkono.
Katika hali kama hiyo,
una hofu na wasiwasi mwingi.
Unapopatwa na hofu nyingi,
njia nzuri ya kukabiliana
na hali hiyo ni sala,
kusali kwa Yehova
na kumwomba kihususa
akusaidie kujua
jambo la kufanya.
Vita vilipozidi kuongezeka
na kufikia karibu na eneo letu,
hali haikuwa salama
tulilazimika kukimbia
na kwenda kwenye ofisi ya tawi.
Akina ndugu walituonyesha upendo,
walitujali na walitutunza
vizuri sana.
Walihakikisha tunaendelea
na ratiba yetu ya kiroho.
Ninapokumbuka kipindi hicho
ninashukuru kwamba
bado niko hai.
Kuna mambo mawili
ambayo yalitusaidia,
kwanza,
uhusiano wetu pamoja na Yehova.
Hilo ndilo jambo pekee
ambalo haliwezi kubadilika.
Lakini pia,
msaada wa akina ndugu
na dada ulitusaidia.
katika pindi hizo za taabu,
ndipo unapotambua umuhimu
wa kuwa sehemu ya
undugu wetu wa Kikristo
ninapata shangwe nyingi
sana hapa Betheli
kwenye mgawo wangu
katika Idara ya Sauti na Video.
Ninawapenda akina ndugu na dada
ninaofanya kazi pamoja nao.
Na ninamshukuru Yehova
kwamba bado niko hai,
na ninaweza kuendelea
kumtumikia kila siku.
Video hiyo inatukumbusha
kwamba maisha katika mfumo huu
ni mafupi sana.
Umetambua jambo lililomsaidia
ndugu Dugbe
kuwa na shangwe licha ya kukabili kifo?
Ni uhusiano wake na Yehova,
na ndugu zake Wakristo walimsaidia
kudumisha tumaini lake.
Kupitia kujifunza kwa ukawaida,
mikutano, na kuhubiri.
Je, baadhi yetu tutalazimika
kufa kwa sababu ya imani yetu
kama Wakristo wengi wa mapema
na kama baadhi ya Mashahidi wa siku zetu?
Ndiyo!
Lazima tukabili matatizo
katika mfumo huu wa mambo.
Na kuna uwezekano mkubwa kwamba
tutakufa kwa sababu ya ugonjwa,
aksidenti, au matatizo mengine
katika siku hizi za mwisho.
Huenda tukafa kabla ya
ulimwengu mpya kufika,
kama wapendwa wetu wengi walivyokufa.
Au huenda tukaokoka
dhiki kuu tukiwa hai.
Vyovyote vile tunapaswa kuazimia
kuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova
mpaka mwisho.
“Yule atakayevumilia mpaka mwisho
ndiye atakayeokolewa.”
Ikiwa tunafikiri kwamba
mwisho utafika tukiwa hai,
huenda tukashindwa kubaki tukiwa waaminifu
ikiwa tutakabili kifo.
Vivyo hivyo ikiwa tunafikiri kwamba
dhiki kuu haitakuja tukiwa hai
huenda tukashindwa kukabiliana na hali hiyo.
Njia pekee ya kujiandaa kwa ajili ya
hali zozote kati ya hizo,
ni kudumisha hali nzuri ya kiroho
na kuwa macho.
Yesu alisema:
“Endeleeni kukesha kwa sababu
hamjui Bwana wenu atakuja
siku gani.”
Tumenufaika kwa kuchunguza kwa makini
usadikisho thabiti wa mtume Paulo
katika Waroma 8:35
Tumejifunza nini katika mfululizo huu?
Tumeona jinsi Waroma 8:35-39
inavyotuhakikishia hakuna jaribu
linaloweza kumzuia Yehova
aache kutupenda.
Kujua kwamba tuna kibali cha Yehova
na anatupenda
hata tunapokabili majaribu
ni sababu ya kuwa na shangwe.
Licha ya dhiki,
taabu,
mateso, njaa,
kuwa uchi, hatari,
upanga, au kitu chochote.
Basi
endelea kumkaribia yule
anayekupenda sana.
Imarisha uhusiano wako pamoja na Yehova
kupitia funzo la kibinafsi na sala,
hakikishia moyo wako kwamba anakupenda.
Dumisha uhusiano wako wa karibu
pamoja na ndugu na dada zako Wakristo.
Kazia fikira tumaini lako
na utafakari uzima wa kweli ulio mbele yako.
Na mwishowe kumbuka
sala iliyoongozwa na roho
kwenye Wakolosai 1:11.
Akina ndugu
ikiwa tutaendelea kufanya mambo haya
kama Paulo tunaweza kuwa na shangwe
licha ya majaribu yoyote.
Ona maneno haya yenye kutia moyo
kwenye Wakolosai 1:11
“Nanyi mwimarishwe kwa nguvu
zote
kwa uwezo wake wenye utukufu.”
Kuna nguvu kiasi gani katika
uwezo wenye utukufu wa Mungu?
Tunajua kwa sababu Neno lake
limefunua mambo yote ambayo
Yehova ametimiza
na atakayotimiza kupitia roho yake takatifu.
Kani yenye nguvu zaidi.
Na kwa nini atakupatia roho yake?
Si ili uvumilie tu,
au uweze kuvumilia kikamili,
si ili tu uvumilie kikamili kwa subira,
bali kama inavyosema:
‘Ili uvumilie kikamili
kwa subira na shangwe.”
Tukiwa na uhakika huo
tunaweza kuvumilia jaribu lolote
hata liwe gumu kadiri gani
au lidumu kwa muda gani.
Kwa sababu upendo usioshindwa wa
Baba yetu utatusaidia kuwa na shangwe
sikuzote, na kwa umilele wote.