JW subtitle extractor

Geoffrey W. Jackson: Waige Wanawake Wenye Imani Yenye Nguvu!—Maria Mama ya Yesu

Video Other languages Share text Share link Show times

Yehova alimchagua Maria
aliyekuwa kijana
atimize mgawo mgumu.
Ulikuwa mgawo wa pekee.
Uliohitaji imani yenye nguvu.
Alipaswa kumtunza na kumlea
mwana mzaliwa-pekee
wa Mungu,
Yesu Kristo.
Hilo lilikuwa pendeleo
la pekee sana.
Lakini Maria alihitaji
kuwa na imani
yenye nguvu sana.
Si tu
kwa sababu hili lilikuwa
jukumu zito sana.
Ambalo angehitaji
kushughulikia kwa
miaka kadhaa
lakini mwanzoni
kabla ya Maria
kukubali mgawo huu
alikuwa na wasiwasi fulani
jambo moja ambalo
bila shaka lilimhangaisha
jinsi ambavyo
wengine wangeitikia.
Marafiki, majirani,
watu wa ukoo,
na bila shaka pia
mchumba wake, Yosefu.
Kwa sababu
malaika hakumwambia
wewe usijali
nitaenda niwajulishe
watu wote wanaohusika
kuhusu kitakachotokea
ili wasikasirike.
Kwa hiyo ulikuwa
mgawo mgumu
na mzito sana
kwa Maria kutimiza.
Je, unaweza kuwazia
jinsi alivyoshughulikia
hali hiyo?
Ili kutusaidia kuwazia
acheni tuzazame
video hii fupi.
Nilikuwa nimechumbiwa
na Yosefu.
Tulifikiri tungekuwa na
maisha rahisi,
yenye utulivu.
Lakini ghafla,
mambo yalibadilika.
Najua kwamba
wakati mwingine Mungu
hutuomba tufanye jambo gumu,
lakini hili
lilikuwa gumu sana.
Jambo tulilodhani
hatungeweza kutimiza,
lakini nilikuwa
na uhakika kwamba
Yehova angenisaidia.
Ikiwa tungekuwa
washikamanifu Kwake
na kufanya yote tuwezayo
kumtunza Mwana
wake mpendwa,
Yeye angekuwa
mshikamanifu kwetu
na kututimizia mahitaji yetu.
Unapofikiria kuhusu
hali ya Maria
alichotaka tu
ni kuwa na maisha
matulivu na ya kawaida
lakini ghafla
kila kitu kilibadilika.
Na huenda ilionekana
kwamba haiwezekani
kwa upande wake
kukubali mgawo huo.
Lakini alitendaje?
Tafadhali chukueni
Biblia zenu
na tufungue
Luka 1:38
Luka 1:38
Hapa tunaona
jinsi Maria alivyoitikia:
“Tazama!
Kijakazi wa Yehova!
Na itendeke kwangu
kulingana na tangazo lako.”
Naam,
akiwa na imani kamili
na unyenyekevu
alikubali mgawo
huo mgumu.
Alijua kwamba Yehova
angekuwa pamoja naye
na kwamba angemsaidia.
Lakini ni nini
kilichompa Maria
imani yenye nguvu vile?
Tunapata wazo fulani hapa
tunapotazama chini kidogo
kwenye mstari wa 46
Luka 1:46
hatutasoma mstari
wenyewe hasa
lakini tutachunguza
habari za utafiti
kwenye Biblia ya Kiingereza.
Hapa inasema
maneno ya sifa
ambayo Maria alisema
katika mstari wa 46-55
yana zaidi ya marejeo 20
yaliyotolewa
moja kwa moja
au yanayogusia habari iliyo
kwenye Maandiko
ya Kiebrania.
Maneno ya Maria
yanaonyesha kwamba
alikuwa na hali
nzuri ya kiroho
na ujuzi wa Maandiko.
Yanaonyesha kuwa alikuwa na
roho ya uthamini.
“Maneno yake pia
yanaonyesha
kina cha imani yake
alipozungumza kumhusu Yehova
kuwa anawashusha
wenye kiburi na wenye nguvu
na kuwasaidia
walio chini na masikini
wanaotaka kumtumikia.”
Naam,
imani ya Maria
ilitegemea ujuzi wake
wa Neno la Mungu,
Maandiko Matakatifu
yaliyopatikana.
Lakini inaonekana kwamba
hakuwa na
nakala yake mwenyewe
ya Maandiko hayo Matakatifu.
Bali
aliweka katika
kumbukumbu yake
Maandiko aliyosikia
yakisomwa kwenye sinagogi.
Inastaajabisha sivyo?
Kwa hiyo moyo wa Maria
ulijaa mambo hayo yote
kutoka kwenye
Maandiko ya Kiebrania
hivi kwamba
alipoanza kumsifu Yehova
katika mazungumzo
ya kawaida.
Maneno yote hayo yalibubujika
kwa sababu alikuwa
ameyaweka moyoni mwake.
Naam,
Maria alikuwa na imani
yenye nguvu
iliyotegemea Maandiko Matakatifu
na hilo ndilo lilimfanya astahili
kwa ajili ya mgawo huo.
Namna gani sisi?
Tunaweza kuigaje
imani hiyo yenye nguvu
ambayo Maria alikuwa nayo?
Tunapotazama video ifuatayo
ona kwamba ingawa
migawo yetu inaweza
kuwa tofauti
sisi pia
tunahitaji kuwa na
imani yenye nguvu.
Waliponiambia
kwa mara ya kwanza
nisimamie idara
katika kusanyiko la kimataifa?
Nilifikiri wamekosea.
Yaanii, mimi
niliona kana kwamba
lilikuwa jukumu
kubwa sana kwangu.
Lakini
ninakumbuka nilihisi
vivyo hivyo
miaka mingi iliyopita
nilipoombwa kutumikia
katika Halmashauri ya
Kutoa Msaada,
na nilipotumikia katika
Halmashauri ya Uhusiano
na Hospitali,
kwa kweli,
nimekuwa nikihisi hivi
kila mara ninapopata mgawo
kutoka kwa Yehova.
Lakini nimejifunza kwamba
Yuko tayari
kutusaidia siku zote.
Kwa hiyo,
Yehova anaponiomba
kufanya jambo
linaloonekana kuwa gumu,
najikumbusha kwamba
napaswa kusali,
kubaki nikiwa mshikamanifu,
na kuwa na imani kwamba
atatimiza mahitaji yangu.
Je, ulimsikitia
huyo ndugu kijana?
Huenda unaweza kuelewa
jinsi alivyohisi aliposema,
“Waliponiambia kuhusu
mgawo wangu
nilifikiri wamekosea.”
Bila shaka, huenda sisi pia
tumewahi kufikiri hivyo, sivyo?
Lakini ni nini kilichomsaidia?
Alikumbuka jinsi Yehova
alivyokuwa amemsaidia
alipokabili hali kama hiyo
wakati uliopita.
uliona jinsi alivyo kumbuka
pindi ambayo
aliisaidia
katika Halmashauri ya
Kutoa Msaada
na akiwa amesimama hapo
akiwa kijana
ndugu hao wote
wote wanamtazama
atoe mwongozo.
Hilo lilimtisha sana.
Halafu vipi pindi
ili nyingine alipopaswa
kuzungumza
akiwa mshiriki wa HLC?
Ulimwona akiwa
ameketi pale nje
halafu yule mwanamke
akamwomba aingie ndani
na hakuonekana
kuwa mwenye urafiki.
Na pia madaktari
waliokuwemo hawakuonekana
kuwa wenye urafiki.
Kwa hiyo migawo kama hiyo
inaweza kuwa
yenye kuogopesha.
Lakini ndugu huyu
kijana alisemaje?
Alisema mambo yaliyomsaidia
ni kusali,
kuwa mshikamanifu,
na kuwa na imani.
Naam,
kama Maria
sisi pia tunaweza
kuwa na imani yenye nguvu
inayompendeza Yehova.
Tunahitaji
kuonyesha unyenyekevu
na kuwa na uhakika kamili
katika Yehova.
Aina hiyo ya uhakika
ndiyo inazungumziwa
kwenye andiko la Zaburi.
Fungua Biblia yako
kwenye Zaburi 56:3, 4
Zaburi 56:3, 4
“Ninapoogopa,
ninakutumaini wewe.
Katika Mungu
ninayelisifu neno lake
katika Mungu
ninaweka tumaini langu;
siogopi.
Mwanadamu ambaye ni duni tu
atanifanya nini?
Naam,
kama mtunga-zaburi
na kama Maria
tunaweza kuwa na
uhakika kamili
katika Yehova.
Naam, acheni
tuonyeshe imani yenye nguvu
tunapopata migawo migumu,
tukimtumaini Yehova,
na tukijua
kwamba atatubariki
kama alivyombariki Maria.
Sehemu inayofuata
ya mfululizo huu
itashughulikiwa na
Ndugu Leonard Myers,
msaidizi wa Halmashauri
ya Uandikaji.
Kichwa cha hotuba yake ni
“Waige Wanawake
Wenye Imani Yenye Nguvu—
Mwanamke Mfoinike.”