JW subtitle extractor

Je, Ulimwengu Uliumbwa?

Video Other languages Share text Share link Show times

Ulimwengu ni mkubwa sana
na ni wenye kustaajabisha.
Dunia na uhai uliomo
ni wenye kutatanisha.
Vitu vyote hivyo vilitokea wapi?
Kitabu cha Biblia cha Mwanzo
kinasema kwamba kuna Muumba.
Lakini mara nyingi
simulizi hilo halieleweki vizuri
na hata wengine wanafikiri ni hekaya.
Je, tunaweza kuamini
kile ambacho Biblia inasema
kuhusu chanzo cha ulimwengu?
Wanasayansi wanakadiria
kwamba ulimwengu
ulitokea miaka bilioni 14 iliyopita.
Hilo linamaanisha kwamba
ulimwengu una mwanzo,
kutia ndani dunia.
Biblia inaunga mkono jambo hilo.
Mwanzo 1:1 inasema:
“Hapo mwanzo Mungu
aliziumba mbingu na dunia.”
Simulizi hilo halisemi ulimwengu
ulitokea lini au jinsi gani.
Badala yake, linazingatia mfuatano wa
jinsi vitu vilivyotokezwa duniani
wakati wa vipindi sita,
ambavyo Biblia inaita siku.
Je, siku hizo sita
zilikuwa na urefu wa saa 24
kama wengi wanavyoamini?
Hapana.
Neno la Kiebrania “siku”
linalotumiwa katika Biblia
linaweza kurejelea
vipindi vyenye urefu mbalimbali.
Hata kitabu cha Mwanzo
kinajumlisha siku zote sita
za uumbaji kuwa siku moja
“siku ambayo Yehova Mungu
aliumba dunia na mbingu.
Kila “siku” inayotajwa
kwenye Mwanzo sura ya 1
lazima iwe iliendelea kwa muda mrefu sana.
Pia, ni muhimu kuzingatia njia ambayo
mwandikaji wa simulizi hilo
anavyofafanua vipindi hivyo vya uumbaji.
Mwandikaji anavifafanua
kwa kutegemea maoni ya mtu aliye duniani.
Ikiwa mtu angalikuwapo
angaliona mambo fulani
yaliyoanza kutendeka katika kipindi kimoja
na yakaendelea kutokea hata
katika vipindi vilivyofuata.
Kwanza,
nuru ilianza kupenya angani na kutokeza
vipindi vya mchana na usiku.
Dunia ilifunikwa na maji,
na mvuke ulijaa hewani.
Mawingu mazito yalipanda kutoka
kwenye maji yaliyofunika dunia
na kufanyiza anga kubwa.
Kisha
maji yakapungua na nchi kavu ikatokea,
halafu mimea ya kwanza ikatokea.
Anga lilizidi kuwa safi
hivi kwamba jua na mwezi zikaonekana.
Halafu, Mungu akaumba viumbe wa majini
na viumbe wanaoruka angani.
Katika kipindi cha mwisho
Mungu aliumba wanyama wa ardhini
na wanadamu.
Kupatana na simulizi la Mwanzo,
Biblia inasema:
“Bila shaka, kila nyumba hujengwa
na mtu fulani,
lakini yule aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.”
Biblia haitaji mambo hususa ya kisayansi,
lakini simulizi lake la uumbaji
linapatana na akili.
Pia, Biblia inatupatia
majibu yanayopatana na akili
kuhusu maswali mengine muhimu.
Je, sayari yetu ina kusudi?
Ni nini kusudi la uhai?
Ni nini kitakachotokea wakati ujao?
Ili upate majibu ya Biblia,
nenda kwenye jw.org®
au ujaze ombi lililo kwenye mtandao
na mmoja wa Mashahidi wa Yehova
atakutembelea wakati
na mahali panapokufaa.