JW subtitle extractor

Je, Mungu Anakubali Sanamu Zitumiwe Katika Ibada?

Video Other languages Share text Share link Show times

Tangu zamani
Wanadamu wametaka kujihisi
wako karibu na Mungu.
Hiyo ni tamaa nzuri.
Biblia inasema kwamba
‘tukimtafuta Mungu’
kwa kweli ‘tunaweza kumpata’
na ‘kumkaribia.’
Hata hivyo,
Mungu hawezi kuonekana.
Kwa hiyo, tutajihisije tuko karibu
na Mungu ambaye hatuwezi kumwona.
Je, ingefaa kuabudu
vitu vilivyotengenezwa
ili kujihisi tuko karibu na Mungu?
Watu fulani hutumia sanamu katika ibada.
Wengine hutumia picha,
na mifano mingine ya kidini
katika ibada yao.
Lakini je, inawezekana kwamba
wale ambao wanajaribu
kumkaribia Mungu kwa njia hiyo
wanasogea mbali zaidi naye?
Fikiria kile ambacho Biblia inasema kilitokea
wakati ambapo Waisraeli wa kale
walitengeneza sanamu ya ndama
na wakajaribu kuitumia kumwabudu Mungu
kisha wakafanya sherehe na kuiita
“sherehe kwa ajili ya Yehova”
Mungu wa Biblia.
Je, Mungu alikubali aina hiyo ya ibada?
Hapana.
Alisema kwamba alichukizwa
na kile ambacho walikuwa wamefanya.
Fikiria hili:
Badala ya kuwasaidia kumkaribia Mungu
sanamu hiyo iliwasogeza mbali zaidi naye.
Kwa kweli, tofauti na
watawala wengine wa kale ambao
mara nyingi walionwa kuwa miungu
na ambao waliagiza
sanamu zao zitengenezwe.
Yule “Mfalme mkuu” juu ya wote
Yehova Mungu
aliwaambia watu wake wasitengeneze
wala wasitumie sanamu katika ibada.
Alisema:
“Usijitengenezee sanamu ya kuchongwa
. . . Usiviinamie . . .
mimi,
. . . ni Mungu ninayetaka
watu waniabudu mimi peke yangu.”
Karne nyingi baadaye,
amri hiyo pia ilitumika kwa wafuasi wa Yesu
Mtume Yohana aliwaandikia
Wakristo wa mapema akisema:
“Jiepusheni na sanamu.”
Mungu anaeleza kwa nini
hakuna anayepaswa
kutumia sanamu kumwabudu.
“Simpi yeyote utukufu wangu,
wala kuzipa sanamu
za kuchongwa sifa yangu.”
Anawaalika watu wamkaribie yeye kibinafsi
na wasali kwake moja kwa moja
bila kutumia sanamu.
Je, kweli ni vibaya kutumia
sanamu, picha, au mifano
kama njia ya kutusaidia tu katika ibada?
Tunawezaje kujihisi karibu na Mungu
ikiwa hatuwezi kumwona?
Ili ujifunze mengi zaidi
tafuta habari hizi kwenye jw.org
au ujaze ombi kwenye mtandao
na mmoja wa Mashahidi wa Yehova
atakutembelea
wakati na mahali panapokufaa.