JW subtitle extractor

Je, Watu Watateswa Katika Moto wa Mateso?

Video Other languages Share text Share link Show times

Dini nyingi zinafundisha kwamba
Mungu huwatupa waovu
katika moto wa mateso baada ya kufa
zikitarajia kwamba hofu ya kuteketezwa
itawazuia watu kutenda mabaya.
Je, kweli Mungu huwaadhibu watu
baada ya wao kufa?
Biblia inatuhakikishia kwamba
wafu hawana fahamu
na hawajui jambo lolote kamwe.
Ikiwa wafu hawana fahamu
hawawezi kuteseka.
Je, hilo linamaanisha Mungu
hawaadhibu waovu kamwe?
Hapana.
Mungu aliwaeleza wazazi wetu wa kwanza
jinsi ambavyo wangeadhibiwa
ikiwa wangemwasi.
Lakini Mungu hakusema chochote
kuhusu moto wa mateso.
Alimwambia Adamu
“hakika utakufa.”
Baada ya kufukuzwa kutoka
kwenye bustani ya Edeni,
hilo ndilo jambo lililowapata Adamu
na Hawa waliokuwa waovu.
Walikufa wakawa mavumbi.
Biblia inaonyesha kwamba mtu anapokufa
hawajibiki tena kwa ajili ya makosa
aliyofanya alipokuwa hai
kwa sababu “yule ambaye amekufa
ameondolewa hatia ya dhambi yake.”
Lakini kuna sababu nyingine muhimu zaidi
kwa nini moto wa mateso
hauwezi hata kuwepo.
Biblia inatuambia:
“Mungu ni upendo.”
Je, Mungu mwenye upendo anaweza
kuamuru waovu wateswe,
si kwa dakika chache
bali milele na milele?
Fikiria jambo hili:
katika nyakati za Biblia
Mungu alishutumu zoea la
kuwadhabihu watoto katika moto
kwa ajili ya miungu ya uwongo.
Alisema kwamba tendo la ukatili kama hilo
hata halikuingia moyoni mwake.
Sisi tunachukia wazo lenye ukatili kama hilo
kwa sababu tumeumbwa
kwa mfano wa Mungu
mwenye upendo na mwenye rehema.
Ni wazi kwamba hatuhitaji
kuwa na wasiwasi
kwamba wapendwa wetu waliokufa
huenda wakawa wanateswa mahali fulani.
Bilia inatuambia kwamba
wamepumzika.
Lakini kwa nini watu wema wanakufa?
Wanapatwa na nini wanapokufa?
Kuna tumaini gani kwa
wapendwa wetu waliokufa?
Ili ujifunze mengi zaidi
tembelea tovuti ya jw.org
na utafute habari hizo
au ujaze ombi kwenye mtandao
na mmoja wa Mashahidi wa Yehova
atawasiliana nawe.