JW subtitle extractor

Je, Mungu Ni Halisi?

Video Other languages Share text Share link Show times

Watu wengi huhisi kuamini kwamba Mungu
yupo ni kuwa na imani isiyo na msingi.
Wanasema wanaweza kuamini
mambo wanayoona tu.
Mara nyingi wanachoona ni
wanadamu wakiteseka.
Hawawezi kumuona Mungu.
Kwa hiyo wanauliza,
ikiwa Mungu ni halisi kwa nini watu
wazuri wanapatwa na mambo mabaya?
Je, kuamini kwamba Mungu yupo
kunamaanisha kwamba mtu
ni mpumbavu au anaweza
kudanganywa kwa urahisi?
Kwenye Waebrania kumi na moja
moja Biblia inasema,
Imani ni uthibitisho ulio wazi wa
mambo halisi ambayo hayaonekani.
Uthibitisho ulio wazi kwamba Mungu yupo,
unatuzunguka kila mahali.
Tunaweza kuona uthibitisho fulani?
Na huenda mwingine
usionekane kwa macho.
Kwa mfano, jua letu hutokeza
miale ya urujuani.
Tunalindwaje kutokana na madhara
ya miale hiyo?
Dunia ina ngao ya kutulinda.
Ni utando wa gesi ya ozoni inayochuja miale
yenye mnururisho wenye madhara.
Mnururisho huo unapoongezeka
utando huo hutanuka.
Inapatana na akili kuuliza,
je, mifumo ya dunia na mambo ya asili
tunayoona ilibuniwa na mtu fulani mwenye akili?
Kwenye Waebrania tatu nne,
Biblia inasema hivi:
“Kila nyumba hujengwa na mtu fulani.
Lakini yule aliyevijenga vitu
vyote ni Mungu.”
Kunapokuwa na ubuni,
Lazima kuwe na mbuni.
Hilo linapatana na akili.
Je, hukubali kwamba wazo hilo
la msingi linaihusu dunia yetu?
Huenda ukakubali kwamba Mungu yupo.
Lakini huenda ukajiuliza
basi kwa nini tunateseka?
Ukiona nyumba inayobomoka,
Je, utafikia mkataa kwamba haikujengwa
na mtu au kuna wazo lingine linalopatana na akili?
Kwa nini ukatae kwamba Mungu yupo
kwa sababu tunateseka?
Badala ya kufanya hivyo,
tafuta majibu ya maswali yako
kuhusu kuteseka.
Ili ujifunze mengi zaidi kuhusu
kile ambacho Biblia inasema
kuhusu hili na habari nyingine
nyingi tembelea jw.org