JW subtitle extractor

Robert Luccioni: “Msisahau Kuwakaribisha Wageni” (Ebr. 13:2)

Video Other languages Share text Share link Show times

Andiko letu la leo linazungumzia
ukaribishaji wageni.
Na tunajua, ukaribishaji wageni unahusisha,
kuwaonyesha wengine ukarimu.
Na kuna jambo fulani muhimu limetajwa
kwenye maelezo ya andiko la leo.
“Kuonyesha ukaribishaji wageni ni mojawapo
ya dawa bora sana ya kushinda upweke.”
Umewahi kuwa mpweke,
mpweke kabisa?
Upweke unaweza kuumiza sana.
Kama tujuavyo inawezekana kuwa mpweke
hata ingawa tumezungukwa na watu.
Mwandishi mmoja alisema: “Kuwa peke yako si kubaya,
lakini kuwa mpweke ni kubaya sana.”
Mwingine alifafanua upweke ni “sawa na kunyeshewa mvua
huku mawingu yakiendelea kutanda.”
Dada mmoja alilinganisha upweke na
“kuzama kwenye kisima kirefu.”
Kadiri unavyozama
ndivyo hali inavyokuwa mbaya zaidi
Basi ni nini kitakachoweza kutusaidia kukabiliana
na upweke kabla hali kuwa mbaya?
Yaani ni nini kitakachotusaidia
kuondoa mawingu hayo
au kupanda kisima hicho?
Kama andiko letu la leo linavyosema,
ukaribishaji wageni, ukarimu, kutoa
ni mojawapo ya dawa bora za upweke.
Acheni tuone kanuni tatu za Biblia
zinazoonyesha kwa nini jambo hilo ni muhimu,
na tutaona kwa nini ni la kweli.
Tuanze na Matendo 20:35.
Tusome andiko hilo
Matendo 20:35
tutaona ahadi yetu ya kwanza.
Hapo inasema: “Nimewaonyesha ninyi katika mambo yote kwamba
kwa kufanya kazi kwa bidii hivyo, ni lazima mwasaidie walio dhaifu,
na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, aliposema:
‘Kuna furaha zaidi katika kutoa
kuliko ilivyo katika kupokea.’”
Jambo la kwanza ni rahisi yaani kutoa
hutupatia furaha.
Hapa mtume Paulo alikuwa akimnukuu Yesu.
Na tunaona Yesu hakusema kwamba
tunatoa tunapokuwa na furaha
au tunatoa kwa sababu tuna furaha.
Anasema tuna furaha
kwa kuwa tunatoa.
Na hilo ni muhimu kwa kuwa linatueleza kwamba
hata tunapojilazimisha kutoa,
hata kama hatujisikii kutoa tutapata furaha.
Leo watafiti hata wamethibitisha kwamba
maneno hayo ya Yesu kuwa ni ya kweli.
Hata wanasema huenda kutoa
kukatokeza kemikali za endofini katika ubongo
zinazotupatia uradhi na utulivu.
Jambo la kwanza ni kutoa
hutupatia furaha.
Ili kujua ahadi ya pili,
tusoma Waebrania 13:16.
Waebrania 13:16
inasema: “Zaidi ya hayo, msisahau kutenda mema na kushiriki vitu vyenu
pamoja na wengine, kwa maana
Mungu hupendezwa na dhabihu kama hizo.”
Jambo kuu la pili ni kutoa
hutusaidia kuwa na uhusiano wa pekee na Yehova.
Yehova anapendezwa sana tunapowakaribisha
au kuwaonyesha ukarimu wengine.
Na hilo linamsukuma kufanya nini?
Tunaweza kukumbuka maneno ya Paulo
kwenye Wafilipi 4:18, 19.
Hapo analipongeza
kutaniko la Filipi kwa kumsaidia
Paulo kwa ukarimu.
Hivyo, Paulo aliwajibu kwa kuwaambia
‘Yehova angewajazia kikamili
kulingana na uhitaji wao.’
Hivyo kutoa hutusaidia kuwa na
uhusiano wa pekee na Yehova.
Tunakuwa wenye thamani kwa Yehova,
na ameahidi atatosheleza mahitaji yetu yote,
kutia ndani ya kihisia.
Huenda tukajiuliza: “Ngoja kwanza,
ni kweli ninapotoa au kuwa mkarimu,
ninapata furaha kwa muda,
lakini baadaye ninakuwa tena mpweke.
Je, hilo linamaanisha kwamba
kanuni hii hainuhusu?”
La.
Fikiria maneno ambayo Yesu aliyasema
kwenye Mathayo 6:25, 33.
Unakumbuka Yesu alisema:
‘Acheni kuhangaikia uhai wenu kuhusu kile mtakachokula
na kunywa kwa sababu Yehova atatupatia
kile tunachohitaji tunapokihitaji.’
Je, hilo linamaanisha kwamba ikiwa tuna njaa
au tunapitia hali ngumu na Yehova ametupatia kitu fulani
ametimiza mahitaji yetu
je, hatutahisi njaa tena?
La.
Baadaye au siku inayofuata tutakuwa na njaa.
Jambo kuu ni kwamba Yehova atatupatia
kile tunachohitaji kwa wakati tunapokihitaji.
Hata mahitaji yetu ya kihisia.
Yehova hasemi kwamba hatutakuwa wapweke kamwe
au kuhisi mkazo au kushuka moyo,
bali anatuhakikishia tukiwa wakarimu au
wakaribishaji wageni atahakikisha tunapata kile tunachohitaji ili
tuwe na furaha na maisha yenye kusudi.
Hiyo ni ahadi ya pili.
Kutoa utusaidia kuwa na uhusiano wa pekee na Yehova,
naye atatosheleza mahitaji yetu.
Jambo la tatu linapatikana
kwenye Luka 6:38
Luka 6:38.
Kanuni na ahadi hii ni kwamba
Yehova atahakikisha sikuzote tunapata
kuliko kile tulichotoa.
Inasema: “Muwe na mazoea ya kuwapa watu, nanyi mtapewa.
Watawamwagia kwenye mfuko wa nguo zenu kipimo kizuri,
kilichoshindiliwa, kilichotikiswa, na kufurika.
Kwa maana kwa kipimo mnachowapimia watu,
ndicho watakachowapimia.”
Hivyo sikuzote Yehova anahakikisha
tunapata zaidi ya kile tunachotoa.
Na tunaamini andiko hilo.
Lakini wakati fulani
tunaweza tukahisi tumetoa sana
tumetoa kutanikoni, katika familia,
na katika hali mbalimbali.
Tumeendelea tu kutoa
lakini hatujapata kitu chochote.
Tufanye nini?
Je, andiko limesema uwongo?
La, Yesu alijua hilo lingetokea.
Ona maneno aliyotumia hapa.
Alisema: “Muwe na mazoea ya kuwapa watu,
nanyi mtapewa”—watu,
si lazima wale tunaowapatia vitu.
Kwa kipimo mtakachowapimia watu,
ndicho wao watakachowapimia pia.
Jambo kuu ni nini?
Jambo kuu ni kwamba Yehova anatuahidi
ikiwa tuna mazoea ya kutoa,
kuwaimarisha ndugu zetu,
tukiwa wakaribishaji wageni,
Yehova atahakikisha
kwa njia moja au nyingine, tunapokea baraka,
nguvu, na kitia moyo cha kuendelea.
Je, hilo linawezekana?
Ndiyo, na ningependa kuwasimulia jambo lililoonwa
kuhusu dada tutakayemwita Lydia.
Lydia alikuwa dada mseja
na painia wa kawaida.
Ingawa kuna siku alivunjika moyo
kama inavyotokea kwetu sote,
Lydia alijulikana kuwa dada mkarimu
na mkaribishaji wageni
alikuwa na kawaida ya kufanya
tafrija nyumbani kwake.
Angewaalika wote waliohudhuria kikao cha utumishi
kwa ajili ya kiamsha kinywa
kabla ya kuanza utumishi.
Au angepanga matembezi ya pekee
kwa ajili ya watu wenye umri mkubwa.
Kisha Lydia aligunduliwa kuwa na kansa,
na hali hiyo ilimuathiri sana.
Baadaye alihitaji kufanyiwa upasuaji.
Kisha Lydia alipata mshuko moyo mkubwa sana
kiasi kwamba wazee, kutaniko,
na hata marafiki zake walijiuliza
watafanya nini ili wamsaidie.
Katika ziara moja, wazee wawili waliomtembelea,
walisoma pamoja naye Luka 6:38,
andiko ambalo tumechunguza.
Na walimkumbusha jinsi ukarimu wake,
ukaribishaji wageni ulivyomletea furaha.
Na alikubali hilo ni kweli, lakini akasema:
“Sipendi kuwa na watu tena.
Sipendi kuwa karibu na watu.”
Kwa fadhili akina ndugu hao walimpa mtihani
asali na ajilazimishe kutoa
angalau kwa miezi michache
ili aone hali itakuwaje.
Jambo la kushangaza alifanya hivyo.
Ilikuwa ni kana kwamba mawingu yaliondoka
na Lydia wa zamani alirudi tena.
Lilitokea miaka mingi iliyopita.
Ingawa kuna siku ambazo anavunjika
moyo kama sisi sote.
Sasa Lydia ni mtumishi wa Yehova
mwenye furaha na matokeo.
Tunajifunza nini?
Ukaribishaji wageni, ukarimu, na kuwapa wengine
ni mojawapo ya dawa bora zaidi
za upweke na kushuka moyo.
Yehova anaahidi tukitoa tutapata
Kuna simulizi zuri litakalotukumbusha kwamba,
hatuwezi kumpa Yehova “mengi”
kuliko yale atakayotupatia.
Tunaona simulizi hilo katika
kitabu cha 2 Mambo ya Nyakati 25.
Tusome 2 Mambo ya Nyakati 25,
kuanzia mstari wa 5 unazungumzia mfalme Amazia.
Ana miaka 25 na ni mfalme wa Yuda,
na huu ni wakati anakabili vita
na watu wa Edomu.
Mstari wa 5 unasema
akawakusanya pamoja watu wa Yuda
na kuchagua “mashujaa 300,000
waliozoezwa kwa ajili ya utumishi wa kijeshi.”
Akahisi hao hawatoshi.
Angalia mstari wa 6,
alikodi wanajeshi 100,000
kutoka kwa Israeli “kwa talanta 100 za fedha.”
Mstari wa 7,
“mtu fulani wa Mungu wa kweli” anakuja na kusema kwamba
warudishe wale wanajeshi 100,000
kwa sababu ‘Mungu hayuko pamoja nao’
nenda na wanajeshi 300,000 ulionao
nami nitakuwa nawe.
Ukiangalia 2 Mambo ya Nyakati 25:9
sehemu ya kwanza—mfalme akauliza:
‘Vipi kuhusu pesa nilizolipa?’
Hizo zilikuwa pesa nyingi sana.
Kulingana na Nyongeza B14,
talanta hizo 100 za fedha
huenda zikawa sawa na dola
milioni 1.5 za Marekani.
Mfalme alitumia pesa nyingi
kuwakodi wanajeshi hao.
Lakini nabii anamwambia warudishe.
Maneno yanayofuata yanaimarisha
sana na tungependa kuyahusisha
na mazungumzo yetu.
Ona sehemu ya mwisho ya mstari wa 9,
unasema: “Mtu wa Mungu wa kweli akamjibu:
“Yehova anaweza kukupa
nyingi zaidi kuliko hizo.’”
Usiogope.
Yehova anaweza kukupa mengi zaidi.
Huwezi kumpa “mengi” kuliko anayokupa.
Kulingana na mazungumzo yetu, Yehova anatuahidi
tukiwa wakaribishaji wageni, tukiwa wakarimu,
tukitoa, tutakuwa na furaha;
anatuhakikishia atatupatia mahitaji yetu yote,
hata mahitaji ya kihisia na atawachochea wengine
watupatie vingi zaidi
kuliko tunavyoweza kutoa.
Na tuazimie kuwa na kawaida ya kutoa,
kuwa wakaribishaji wageni,
na kuwa wakarimu.
Na kila mara tunapofanya hivyo,
tutayasukuma mawingu mbali sana
na tutapokea zaidi ya kile tunachotoa.