JW subtitle extractor

Maisha Yangu ya Utineja—Biblia Inawezaje Kunisaidia?

Video Other languages Share text Share link Show times

Nilizaliwa na kulelewa
katika kweli hivyo
nilijifunza Biblia,
nilihudhuria mikutano
na kwenda utumishi
pamoja na wazazi wangu
Kwa kuwa nililelewa
katika kweli
nilijua kwamba
kuishi kulingana na
viwango vya Biblia
ndilo jambo bora
wazazi walikuwa na bidii sana
kwenye mambo ya kiroho
ninapokumbuka mambo hayo
ninatambua kwamba sikutaka tu
kuwavunja moyo wazazi wangu
Viwango vya Biblia si mzigo
na wala si vigumu kuvifuata
Kwa kweli tukifanya kile
ambacho Biblia inasema
tunanufaika sana
lakini pindi fulani nilitamani
kujua maisha yangu
yangekuwaje ikiwa
nisingekuwa kwenye kweli
nilifurahia sana kuwa na
wanafunzi wenzangu shuleni
Nilifurahia kuwa shuleni
nilikuwa na mahusiano mazuri
na wanafunzi wenzangu
na hata walimu
walinipenda pia
hivyo maisha yalikuwa
mazuri sana
sikuzote wazazi wangu
waliniambia nisiwe
na urafiki wa karibu sana
na wanafunzi wenzangu
lakini mimi niliwaona
kuwa watu wazuri
na wenye tabia nzuri
hivyo, sikuelewa kwa
nini wazazi wangu
walikuwa na wasiwasi sana
wanafunzi wengi shuleni
kwetu walikwenda kanisani
na hata walimu wetu
walipenda mambo ya dini
Siku moja jambo
fulani lilitokea shuleni
ambalo lilifanya
wanafunzi wote wajue
kwamba mimi ni
Shahidi wa Yehova
Nilijua kwamba
baadhi ya wanafunzi
wasingefurahia kujua kwamba
mimi ni Shahidi wa Yehova
lakini sikutegemea
wangebadilika haraka hivyo
Nilianza kutumia
muda mwingi zaidi
na wanafunzi wenzangu
lakini baada ya muda
nilitambua kwamba maisha
yetu yalitofautiana sana
wangezungumzia
maeneo waliyotembelea
na vitu walivyonunua
mwisho-juma
lakini kwa upande wangu
nilifanya tu mambo ya kiroho
nilihisi kwamba sifurahii
maisha kama wao
nilijihisi mpweke na
nimetengwa na wengine
nilijua kwamba
kanuni za Biblia
ni sahihi na zina manufaa
lakini hali hiyo ilipotokea,
nilianza kuwa na mashaka
nilianza kuhisi sikuwa wa
kisasa kama rafiki zangu
kwa hiyo walipoanza kuzungumzia
malengo yao maishani
niliaibika kuzungumzia
malengo yangu
Hivyo nilianza kufikiria
ninawezaje kutenda
kwa njia inayofaa?
nilipata msaada
nilipowaambia wazazi wangu
kuhusu hali ninayopitia
tulizungumzia jambo hilo
katika ibada ya familia
tulisoma Mathayo 5:11
Wenye furaha ni ninyi,
watu wanapowashutumu
na kuwatesa
na kuwasingizia
kila aina ya uovu
kwa sababu yangu
Lakini mnawezaje kuwa
na furaha mnapoteswa?
niliwaza lakini sasa sina furaha
mama yangu alinisomea Marko 8:38
niliguswa sana na
sehemu ya andiko iliyosema
ikiwa tutamwonea
aibu Yesu Kristo
yeye pia atatuonea aibu
nilitambua kwamba niliaibika
kujitambulisha kuwa Shahidi
Mambo hayo
yalipokuwa yakitokea
ndugu mmoja alitoa
hotuba kutanikoni
na akasoma Mathayo 19:29
Hapo inasema:
kila mtu ambaye ameacha
jambo muhimu kwake
kwa ajili ya Yehova
atapata mara 100 zaidi
Hivyo niliamua kuacha mambo
niliyoona kuwa ni muhimu
ili nijionee matokeo
na baraka nitakazopata
wakati huo wazazi wangu
walinitia moyo nianzishe urafiki
na ndugu na dada ambao
wanashiriki katika aina
mbalimbali za utumishi
wa wakati wote
ili nisikie mambo waliyojionea
Hilo lilinisaidia kuamua
jambo nitakalofanya maishani
Jambo moja ninalofurahia
kuhusiana na uamuzi wangu
ni kukutanana na
ndugu na dada wengi
ambao mwanzoni
sikuwafahamu
nilitambua kwamba
kuna watu wengi
wenye mawazo na
malengo kama yangu
hao ndio waliokuwa
marafiki wangu wa kweli
siku nyingine
wanafunzi wenzangu
walipoanza kuzungumza
malengo yao
niliweza kuwaeleza
kwa ujasiri kuhusu
malengo yangu
ninawashukuru sana wazazi
kwa kunisaidia kuwa na ujasiri
Nilijionea kwamba sikuzote
Yehova hutimiza ahadi zake
ninapofikiria hilo
ninatambua kwamba Yehova
ametimiza ahadi yake
kwa kunibariki mara 100 zaidi
kwa sababu niliamua kuishi
kulingana na kanuni za Biblia
sasa nina furaha sana
na nina uhakika kwamba
ikiwa nitafuata mafundisho ya Biblia
ninapofanya maamuzi
sikuzote nitapata
matokeo mazuri