JW subtitle extractor

Gary Breaux: Kusimulia Hadithi Ni Mbinu Nzuri Sana ya Ufundishaji (1 Yohana 5:19)

Video Other languages Share text Share link Show times

Maelezo ya Mnara wa Mlinzi leo
yanataja jambo hili waziwazi:
yanasema
Shetani hutumia sinema
na vipindi vya televisheni
kueneza njia yake ya kufikiri.
Wazo hilo tu
linatosha kumfanya yeyote
anayempenda Yehova
afikiri kwa makini kabla ya
kutazama televisheni
au kutumia kompyuta.
Kuhusiana na mbinu hiyo
ambayo Shetani hutumia
kueneza njia yake ya kufikiri
Mnara huo ulisema
Anaelewa kwamba
mbali na kutuburudisha
masimulizi ya hadithi
hutufundisha
jinsi ya kufikiri
kuhisi, na kutenda.
Kwa hiyo
tunapochagua burudani
tunahitaji kukumbuka kwamba
masimulizi ya Shetani
yamekuwa na madhara
makubwa sana
kwa watu wengi
kwa miaka mingi.
Tunaweza kuona matokeo
tunapochunguza Isaya 55
Tusome andiko hilo.
55:7.
Inasema “Mtu mwovu na
aiache njia yake
Na mtu mbaya mawazo yake.”
Kwa hiyo, mtu
anayefundishwa na Shetani
njia yake ya kufikiri itaathiriwa
na mwishowe
atabadilika na kuwa mtu mwovu
na mtu mbaya.
Mstari wa 8 na
9 unaonyesha kwamba
mawazo ya mtu asiye mkamilifu
yanatofautiana sana
na mawazo ya Yehova Mungu.
Ona mistari hiyo inavyosema:
Mstari wa 8
“Kwa maana mawazo yangu
si mawazo yenu,
Na njia zenu si njia zangu,
asema Yehova.”
Kwa maana kama mbingu zilivyo
juu kuliko dunia,
Ndivyo njia zangu zilivyo juu
kuliko njia zenu
Na mawazo yangu
kuliko mawazo yenu.
Kwa hiyo ingawa mistari hii
inazungumzia
kuhusu mtu mwovu
na mtu mbaya
mwanzoni hakuwa mwovu
au mtu mbaya
alikuwa tu mtu asiye mkamilifu.
Hivyo
kuna jambo lililomsukuma na
kumfanya kuwa
mtu mbaya na mwovu.
Alibadilika kwa sababu alifundishwa
na Shetani Ibilisi.
Sisi sote leo
si wakamilifu.
Basi tunawezaje kudumisha
njia ya Yehova
ya kufikiri ili tusigeuke
na kuwa watu wabaya na waovu?
Ni kweli kwamba Yehova
pia anatumia masimulizi
ili kutusaidia
tupatanishe njia yetu ya
kufikiri na njia yake.
Kwa mfano,
Biblia ina mifano mingi ya watu
mifano mizuri
na mifano mibaya.
Biblia inataja mifano
na masimulizi mengi
yanayotugusa mioyo
yanayotusaidia kuelewa
kanuni zenye thamani
na Sheria za Biblia
zinazotusaidia
kufanya maamuzi mazuri
ili njia zetu
zipatane na njia za Yehova.
Tutoe mfano.
Biblia yote inakazia
sifa ya Yehova ya kusamehe.
Tuone jambo hilo.
Tusome kitabu cha Kutoka 34
tusome mstari wa 7.
Kumbuka kwamba tunafundishwa
kuhusu jinsi Yehova anavyosamehe.
Unasema hivi:
“Ninawatendea maelfu kwa
upendo mshikamanifu,
ninasamehe makosa
na uovu na dhambi.”
Huo ndio utu wa
Yehova wa kusamehe.
Na pia tunaposoma kitabu
cha Isaya 1:18
ona jinsi anavyotusaidia
kupata picha ya jambo hilo.
Isaya 1:18.
Anasema “Sasa, njooni,
na tunyooshe mambo kati yetu,”
asema Yehova.
Ingawa dhambi zenu ni
kama rangi nyekundu,
Zitafanywa kuwa nyeupe
kama theluji;
Ingawa ni nyekundu kama
kitambaa chekundu,
Zitakuwa kama sufu.”
Hapa tena
tunajifunza jinsi Yehova
anavyosamehe.
Ili kugusa mioyo yetu
na kuelewa kwa kina jambo hilo
anatumia simulizi fulani.
Yesu ndiye aliyetoa simulizi hilo.
Na linapatikana
katika Luka 15
kumhusu mwana mpotevu.
Hatutalisoma simulizi hilo lote
lakini tutaanza kwa
kusimulia mistari michache.
Kwa mfano mstari wa 11
mtu fulani alikuwa na wana wawili.
Mstari wa 12 mwana mdogo
anachukua urithi wake
na mstari wa 13 anasafiri
na kwenda nchi ya mbali
anatumia vibaya mali yake.
Kisha 15 na 16 akawa maskini
mstari wa 17 akarudiwa na fahamu
na kurudi kwa baba yake.
Mstari wa 20
unaonyesha
“baba yake akamwona
na kumsikitikia,
akakimbia, akamkumbatia
na kumbusu kwa wororo.”
Basi Yehova anatufundisha
somo gani
kupitia simulizi hili?
Kwanza kabisa
Yehova anatamani sana
kutoa msamaha.
Huo ndio utu wake.
Na kama baba huyo
tunatambua kwamba
watenda dhambi wanaweza
kupoteza fursa walizokuwa nazo.
Lakini hatukati tamaa
kwamba mtenda dhambi atarudi.
Nasi tutamkaribisha
kwa uchangamfu
atakapomrudia Yehova Mungu.
Watenda dhambi
wanaweza kubadilika
na kujiunga tena
kwenye familia ya Yehova.
Na mwishowe
tumejifunza huenda
watenda dhambi
wakakata tamaa kabisa
kabla ya kurudiwa
tena na fahamu.
Bila shaka,
hayo ni masomo muhimu
yanayotusaidia kuelewa
kufikiri kwa Yehova
na kupatanisha
njia yetu ya kufikiri isiyo kamilifu
na njia yake.
Na nimetumia mfano huo
kwa sababu
Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inatumia
maneno 350 hivi
kuelezea simulizi hilo.
Lakini imetumia maneno
10 hivi kuelezea dhambi
za mwana mpotevu.
Ukitazama mstari wa
13 unasema
aliishi maisha ya anasa.
Kisha 30
unataja habari za ziada
kwamba alitumia mali yake
na makahaba.
Basi hili ni simulizi linalotaja
makosa yaliyofanywa lakini
halikazii fikira makosa hayo
kuyatukuza au kuyafanya
kuwa yenye kusisimua.
Badala yake linatusaidia
kumkaribia Yehova Mungu
na kuelewa utu wake wa kusamehe.
Hilo ndilo kusudi la simulizi hili.
Wazia jinsi ambavyo Shetani
angepotosha simulizi hilo
kumhusu mwana mpotevu.
Je, angemfanya baba
huyo aonekane kuwa mkali
na shupavu?
Je, angetokeza
picha ya mwana
huyo aliyeasi
kwamba alikandamizwa
na kunyimwa uhuru
akiwa nyumbani?
Je, angetumia lugha chafu
na isiyo na heshima
katika simulizi hilo?
Unafikiri angetumia muda gani
kuelezea mambo mapotovu
katika simulizi hilo?
Na aliporudi nyumbani,
je, angeonyesha mwana
huyo ametubu?
Au je, angeonyesha
baba amelegeza msimamo
kuelekea makosa
ya mwana wake?
Je, angeonyesha mwana huyo
akirudi nyumbani
na mmoja wa wanawake
aliokuwa nao?
Kwa kweli masimulizi ya Shetani
ukiyachunguza kwa undani
utatambua sikuzote
yana uchafu na uwongo.
Masimulizi yake
ni habari zile zile zinazojirudia
zinazohusu uasi
ukatili,
na uasherati.
Ni simulizi lilelile
linalorudiwa tena
na tena
lenye wahusika tofauti.
Lakini masimulizi ya Yehova
tunapoyasoma
tunatambua jambo
jipya kila wakati.
Isitoshe tunapoyatafakari
na kuchunguza kwa undani
masimulizi hayo yanakuwa
mapya kila wakati.
Inaonekana kila tunaposoma
masimulizi hayo
tunajifunza jambo fulani
kumhusu Yehova
tunaloweza kutumia maishani.
Basi tunapofanya maamuzi
kuhusu burudani
tunahitaji kutafakari jambo hili
‘Ninafundishwa na nani?
Je, burudani hiyo itaniburudisha
na kunisaidia kuwa mtu bora zaidi?
Au inawezekana itadhoofisha
imani yangu kwa Yehova Mungu?
Ikiwa ndivyo
itakuwa jambo la hekima
kuiepuka.
Katika mfumo huu
tunahitaji kuwa waangalifu
kuhusu burudani tunazochagua.
Acheni tufundishwe na Yehova
ili tufikiri
tuhisi
na kuona mambo kama anavyoyaona
tunapotazamia kwa hamu
wakati ambapo burudani
pekee itakayokuwepo
itakuwa salama
na yenye kujenga.