JW subtitle extractor

Izak Marais: Maneno Yako na Yawe Yenye Neema Sikuzote (Kol. 4:6)

Video Other languages Share text Share link Show times

Andiko letu la leo
Wakolosai 4:6
linatuonyesha
jinsi tunavyopaswa kuzungumza.
Linasema:
“Maneno yenu
na yawe yenye neema sikuzote,
yaliyokolezwa chumvi.”
Tutazungumzia maswali matatu.
Kwanza,
maneno yenye neema
yanamaanisha nini?
Pili,
Kwa nini
maneno yenye neema
ni muhimu sana?
Na tatu,
Tunawezaje kujifunza
kuzungumza kwa neema?
Basi, swali la kwanza
(maneno yenye neema ni nini?),
neno
“neema”
lina maana ya pekee.
Mtume Paulo
alitumia neno hilo la Kigiriki
zaidi ya mara miamoja
katika maandishi yake.
Kwa nini neno hili
ni la pekee sana?
Neno hili
pia linatafsiriwa kuwa
“fadhili zisizostahiliwa,”
na katika visa fulani
linatafsiriwa kuwa
“zawadi
ya fadhili.”
Katika andiko la leo
tunaweza kusema,
‘Siku zote
maneno yenu na yawe
zawadi ya fadhili.’
Tunaweza kulinganisha wazo hilo
na maneno ya Paulo
katika Waefeso sura ya 4.
Sehemu ya pili
ya Waefeso 4:29,
inasema hivi:
“Neno jema
kwa ajili ya kujenga
kulingana na uhitaji,
ili liwanufaishe
wale wanaolisikia.”
Lakini sasa ona
sehemu ya kwanza ya mstari huo
inavyosema:
“Neno lililooza
lisitoke
kinywani
mwenu.”
Hilo linatokeza
picha fulani akilini.
Labda
ulikuwa umehifadhi chakula kwenye friji
lakini chakula hicho
kikaharibika.
Huenda kikaonekana kiko sawa
lakini unapofungua chombo
kilicho na chakula hicho
na kupigwa na uvundo
unaotoka humo,
unageuka kando upesi,
unafunika chombo hicho,
na kutupa chakula hicho mara moja.
Wazia kuhusu
mazungumzo uliyokuwa nayo
pamoja na rafiki wa karibu.
Unatarajia kusikia
jambo zuri
lenye kujenga kutoka kwake,
lakini anasema
maneno ya kuchambua,
yenye kuchukiza,
yasiyofaa
kumhusu mtu fulani,
au kuhusu mpango fulani.
Inavunja moyo sana!
Uvundo huo ni wenye kulemea,
lakini huwezi kumtendea
kama vile ambavyo ungetendea kile chombo
chenye chakula kilichooza,
lasivyo,
huenda akasema mambo mabaya kukuhusu.
Basi unafanyaje?
Unafunika taratibu
mazungumzo hayo,
na kuyatupilia mbali.
Kwa kweli
nina hakika kwamba,
sisi sote
tumewahi kuhusika
katika mazungumzo kama hayo.
Sasa
tuzungumzie jambo la pili.
Kwa nini
ni muhimu sana
kusema
maneno yenye neema?
Fikiria maneno
yaliyo kwenye kitabu cha Yakobo sura ya 3.
tutasoma mstari wa 6,
Yakobo 3:6:
“Ulimi pia
ni moto.
Kati ya viungo vya mwili wetu,
ulimi
unawakilisha
ulimwengu wa ukosefu wa uadilifu,
kwa maana
unautia mwili wote unajisi
na kuwasha moto
maisha yote
nao huwashwa moto
na Gehena.”
Basi, nani ‘anastahili Gehena’?
Ni wale wanaotumia vibaya ulimi wao.
Yesu alisema pia
maneno kama hayo.
Fikiria maneno aliyosema
kwenye andiko la Mathayo,
Mathayo sura ya 12,
kwenye mstari wa 36,
Yesu anasema hivi:
36
Ninawaambia kwamba
katika Siku ya Hukumu
watu
watatoa hesabu
kuhusu kila neno lisilofaa
wanalosema.”
Huenda tukajiuliza,
Je, Yehova hatuhukumu
kulingana na mtu
tuliye kwa ndani?’
Ni kweli!
Ona jinsi mstari wa 34 unavyosema:
sehemu ya pili ya mstari wa 34
“Kwa maana
kinywa husema
mambo yaliyojaa
moyoni.”
Ingawa huenda ikaonekana
mtu anasema mambo
bila kufikiri,
ukweli ni kwamba
mambo hayo
yanatoka
moyoni.
Na Yehova
humhukumu mtu
kwa kutegemea jinsi alivyo kwa ndani
na jinsi maneno yake
yanavyowaathiri wengine.
Bila shaka,
Yehova anatuwekea mfano maridadi sana
wa kusema maneno yenye fadhili
na neema.
Ona mfano huu
kwenye kitabu cha Zekaria.
Zekaria sura ya 1.
Hapa kwenye Zekaria sura ya 1,
malaika wa Yehova
anazungumza na Yehova,
malaika huyo
anahangaishwa sana na jambo fulani,
kwa sababu inaonekana kwamba
wapinzani
wanajaribu kuwazuia Wayahudi
ili waache ibada safi.
Anasema hivi kwenye mstari wa 12:
“Ee Yehova wa majeshi,
utaendelea hadi lini
kukataa kuwaonyesha rehema
wakaaji wa Yerusalemu
na wa majiji ya Yuda,
ambao umewakasirikia
kwa miaka hii 70?”
Ona
mstari wa 13
“Yehova akamjibu
kwa maneno ya fadhili
na yenye kufariji
malaika huyo
aliyekuwa akizungumza nami.”
Simulizi hilo
halitaji maneno ya Yehova
lakini tunajua
Yehova ni mwenye neema
na fadhili.
Tuzungumzie swali letu la tatu:
Tunawezaje
kujifunza
kuwa wenye neema
au kusema maneno yenye neema?
Tungependa kuzungumzia kanuni mbili,
kwa sababu
hili ni jambo muhimu sana.
Kanuni ya kwanza
ambayo tungependa kukazia
ni kwenye Waefeso sura ya 5:1,
Waefeso 5:1.
Andiko hilo linasema:
“Kwa hiyo,
iweni waigaji wa Mungu,
kama
watoto
wapendwa.”
Tunajua kwamba
Watoto
huwa wanawaiga wazazi wao.
Watoto
wanaona jambo hilo
kuwa lenye kufurahisha.
Kufanya jambo fulani
kwa ajili ya wazazi wao.
Unaweza kumwona msichana mdogo
akimpa mama yake zawadi.
Huenda
hiyo si zawadi bora kabisa,
lakini kwa mama yake
ni zawadi nzuri.
Hiyo ni zawadi bora kwa mama yake
kwa nini?
Ni kwa sababu anamwiga mama yake.
Inawezekana kwamba
alimwona mama yake
akiwaonyesha watu wengine ukarimu.
Na hilo linamfanya
ajihisi vizuri sana.
Ndivyo ilivyo na Yehova.
Sisi tunapomwiga Yehova
tunafanya
moyo wake
ushangilie
Kanuni inayohusika hapa
ni kuonyesha shukrani.
Hakuna jambo
linaloweza kutusaidia kuwa wenye uthamini zadi
kuliko kuonyesha
shukrani,
kusema
asante.
Basi, mshukuru Yehova,
kwa kila jambo analotufanyia
kila siku.
Yehova anatufanyia mambo mengi sana.
Huenda tusijue
baadhi ya mambo hayo.
Lakini ikiwa tunamshukuru
kila wakati,
kila siku kukumbuka kumshukuru
kwa ajili ya mambo tunayoona akitufanyia,
hilo litakuza moyoni mwetu
hisia za shukrani kumwelekea Yehova
na tutampenda Yehova.
Na kadiri tunavyozidi kumpenda Yehova,
ndivyo tutakavyokuwa
na mwelekeo wa kumwiga.
Hatuhitaji kuhisi kwamba hatufai,
na kujiambia
“Haiwezekani kwangu
kumwiga Yehova.”
Hapana!
Jambo pekee tunalohitaji kuwa nalo
ni moyo
uliojaa shukrani.
Kanuni ya pili
ambayo tungependa kukazia leo,
inapatikana katika andiko letu la leo,
ambalo linasema
maneno yetu yanapaswa
“kukolezwa
chumvi.”
Katika nyakati za Biblia
hakukuwa
na friji.
Basi
ili kuhifadhi chakula,
walikuwa
wakiongeza chumvi.
Wakikihifadhi kwa kutumia chumvi
ili kuhakikisha kwamba
chakula hicho hakiharibiki.
Maneno yetu
maneno yetu yenye neema
yanapaswa
kulinda
heshima ya watu wengine;
yanapaswa kulinda urafiki
na upendo ambao
utadumu
milele.
Maneno hayo
tunayosema
yatatoka
katika moyo wenye shukrani.
Kazia fikira sifa nzuri
za watu wengine
na useme
mambo yanayofaa
ili kuwatia moyo waendelee
kufanya mambo mazuri.
Na tunasema mambo mazuri
kuhusu wale tunaowapenda, sivyo?
Basi, kwa kumalizia,
hata tuwe tunakabilina na hali gani,
au tunahisije,
sikuzote na tuwe wenye neema.
Hatuwezi kukosea kwamwe,
kwa kutenda mema
na kuwa wenye fadhili.
Usife moyo.
Na uwe na lengo
la kufuata maneno ya Zaburi 19:14:
“Maneno
ya kinywa changu
na kutafakari
kwa moyo wangu
Na yakupendeze wewe,
Ee Yehova,
Mwamba wangu
na Mkombozi wangu.”