JW subtitle extractor

Maisha Yangu ya Utineja—Ninawezaje Kupinga Kishawishi cha Kufanya Ngono Kabla ya Ndoa?

Video Other languages Share text Share link Show times

Kila siku shuleni,
wanafunzi wenzangu walizungumza
kuhusu ngono.
Wangezungumza kuhusu
marafiki zao wa kike, wa kiume,
mambo waliyofanya pamoja mwishojuma,
na mambo waliyofanya
Walijua kwamba mimi ni Shahidi wa Yehova,
na kwamba siwezi kufanya ngono
kabla ya ndoa.
Lakini bado walinishinikiza.
Wavulana
wangenisogelea karibu sana
na wakati mwingine hata wangejaribu
kunigusa au kunishika.
Siku moja,
msichana fulani darasani aliniambia
nimguse kwa njia isiyofaa.
Bila shaka, nilikataa.
Lakini msichana huyo
alianza kunitukana.
Alisema nina kasoro,
na kwamba huenda mimi ni shoga.
Walifanya hivyo kama mchezo,
waliendelea kunilazimisha
ili nifanye mambo mapotovu pamoja nao.
Na kwa kuwa sikukubali
kufanya walichotaka
waliona kama mzaha au utani.
Walianza kunilazimisha
nimguse msichana.
Wanafunzi wawili walikuwa
nyuma yangu wakinisukuma.
Walikuwa wamenishika mikono
pande zote mbili
na kunisukuma ili nimguse.
Nilitambua nilipaswa kuondoka.
Kwa kuwa nilikuwa Shahidi wa Yehova
tayari nilikuwa tofauti sana
na wanafunzi wenzangu.
Lakini pia nilikuwa mwenye haya sana.
Wakati mwingine
nilitamani kuwa kama wao
ili waache kunikazia fikira sana.
Nilitambua hilo halingemfurahisha
Yehova ikiwa ningeufuata umati,
na kufanya mambo ambayo
wengine walifanya.
Mara moja nilisali kimyakimya na
kusema, ‘Tafadhali Yehova nisaidie.’
Papo hapo nikamfikiria Yosefu.
Alifanikiwa kumkimbia mke wa Potifa
na alifanya hivyo kwa sababu
aliazimia kumfurahisha Yehova.
Nilitambua nilipaswa kufanya hivyo.
Hivyo, mara moja nilikimbia
na kutoka darasani.
Funzo la kibinafsi
lilikuwa muhimu sana.
Lilinisaidia kumwona Yehova
akiwa halisi.
Kadiri nilimwona kuwa halisi,
ndivyo nilivyoogopa
kumhuzunisha na kumkasirisha.
Kuwa na uhusiano huo pamoja naye
na kumtegemea
kulinisaidia sana kushinda
hali hiyo ya kutaka kuwa kama wao
na kufanya mambo waliyofanya.
Haikuwa rahisi kumkataa msichana huyo.
Lakini nilijua ndilo jambo linalofaa.
Muda mfupi kabla ya tukio hilo,
nyanya yangu alinitayarisha.
Alinitafutia makala za
Mnara wa Mlinzi
zilizozungumzia jinsi ya
kukabiliana na vishawishi.
Ingawa mazungumzo hayo yaliaibisha
lakini kwa kweli yalinisaidia
kuendelea kuwa imara kiroho
na kupinga kishawishi hicho.
Sikuzote, wazazi wangu
waliniambia nitende kwa hekima.
Yaani,
nifikirie jinsi ambavyo tendo hilo
lingeniathiri wakati ujao
na jinsi ambavyo lingeathiri
uhusiano wangu na Yehova,
na marafiki na familia yangu.
Kwa kweli,
nilifikiria sana jambo hilo wakati huo.
Unachohitaji tu ni
kumtumaini Yehova
kwa sababu unapofanya hivyo,
kila kitu kitakuwa sawa.
Chapisho lililonisaidia sana ni kitabu
Vijana Huuliza, buku la 2, sura ya 5.
“Kwa Nini Uendelee Kuwa Bikira?”
Kitabu hicho kilinisaidia sana.
Niliposoma kuhusu vijana wenzangu
ulimwenguni pote wanaokabiliana
na kishawishi hicho hicho
nilifarijika sana.
Na nikahisi kwamba siko peke yangu.
Ninamshukuru sana Yehova na
tengenezo lake kwa sababu
ya upendo
ambao wanatuonyesha sisi vijana.
Wanatusaidia tusijihisi peke yetu
na kutusaidia tukabiliane
na hali hizo ngumu.
Kitabu Vijana Huuliza, buku la 2,
sura ya 14
“Naweza Kujilinda Jinsi Gani Shuleni?”
kilinisaidia sana kuwa
thabiti nilipokuwa shule
na kuwa mshikamanifu
ili nimfurahishe Yehova.
Ninamshukuru sana Yehova
kwa kunisaidia kukumbuka maandiko
kama vile 1 Wakorintho 6:18
linalosema ‘ukimbieni uasherati.’
Na ninafurahi kusema, niliukimbia.
Kinachonifurahisha zaidi
ni kujua nilimfurahisha Yehova
na hiyo ndiyo hisia bora zaidi.