JW subtitle extractor

Samuele Podestà: Sasa Ninachezea Timu Bora

Video Other languages Share text Share link Show times

Nilicheza kwenye Series A
ambayo ndiyo ligi kuu nchini Italia.
Nilichezea
timu ya kitaifa ya vijana,
na hata nilitiwa ndani ndani ya
timu ya Kitaifa ya Wanaume.
Inaridhisha tu kujua kwamba
unajua kazi yako.
Halafu pia kiasi cha pesa nilichopata
kilikuwa kizuri sana.
Baba na mama walikuwa
Mashahidi wa Yehova,
na pia kaka yangu.
Pindi fulani, nilihisi
ni kama nimegawanyika,
hasa wakati ambapo
nilitaka kujifunza kweli.
Niliacha kuiona
kuwa dini ya “familia.”
Baada ya muda,
ni kama kitu kikaanza
kusitawi ndani yangu
ni kama moto,
moto mdogo.
Hatimaye,
nikafikia kujiweka wakfu kwa Yehova
ingawa sikuacha
kucheza mpira wa vikapu.
Lakini ni kama
si eti ni kama,
kwa kweli—sikuwa nikimpa Yehova
kilicho bora,
nguvu zangu zote.
Nilikuwa nikimtumikia Yehova
wakati kazi yangu iliporuhusu
badala ya kumtanguliza Yehova.
Nilitoa udhuru kwamba:
“Ninachofanya ni kazi tu
kama kazi nyingine.
Ndiyo,
inachukua muda wangu mwingi,
lakini ni ya muda mfupi
kwa sababu wachezaji
huwa wanastaafu mapema.”
Kadiri nilivyomkaribia Yehova
ndivyo hisia ya kugawanyika
moyoni mwangu ilivyoongezeka.
Mwangalizi wa mzunguko
katika eneo langu alinisaidia sana.
Nilimfahamu
tangu nilipokuwa mtoto.
Tulipokutana tena,
jambo la kwanza ambalo aliniuliza ni,
“Je, unafurahia kile unachofanya?”
Huenda hilo likaonekana kuwa
swali rahisi,
sivyo?
Lakini swali hilo
lilizama akilini mwangu.
Ninamshukuru sana
yeye na mke wake
kwa muda wote
waliotenda kwa ajili yangu.
Walikuwa na shughuli nyingi sana
lakini hata siku ambayo
hawakuwa wakizunguka,
au jioni
baada ya siku ndefu ya utendaji,
walitenga wakati wa kuwa na mimi.
Baada ya muda
nilihamia miji mingine
na kubadili timu nilizochezea,
kwa hiyo ni kana kwamba
alinikabidhi kwa familia nyingine mbili,
nao walijitoa sana kwa ajili yangu,
wakadhabihu muda wao,
na hakuna wakati ambapo
walinifanya nijihisi vibaya
kwa sababu ya kazi yangu.
Kuhusu maamuzi
yaliyohusu mpira wa vikapu,
hawakuwahi niambia nifanye nini,
mimi nilipaswa kufanya
uamuzi huo mwenyewe,
kuamua ikiwa nitaendelea kucheza
au la.
Ninaweza kusema kwamba
njia yao ya maisha
ndiyo iliyonirekebisha.
Mfano wao,
maisha yao,
mambo waliyotanguliza,
na shangwe waliyokuwa nayo;
hayo ndiyo mambo yaliyonisaidia.
Mfano wao
ulinifundisha mambo mengi sana
kuliko hata maneno yao.
Mfano wao ulinifundisha kile hasa
nilichotaka maishani mwangu.
Nilianza kucheza mpira wa vikapu
mwaka wa 1995
hadi Aprili 2008,
nilipocheza mechi yangu ya mwisho.
Niliamua kwamba
sitacheza tena mpira wa vikapu,
ninashukuru niliamua hivyo.
Nyakati nyingine ninajiambia:
‘Afadhali tu ningefanya
uamuzi huo mapema,
afadhali ningepata ujasiri huo mapema!’
Nilipata pendeleo la kutumikia
nikiwa painia wa kawaida
kwa miaka miwili na nusu,
kisha nikaulizwa
ikiwa ningependa kujaza ombi
la kwenda Betheli.
Na nilishangaa sana,
nilipoalikwa kutumikia
katika ofisi ya tawi ya Italia
na nikatumikia humo kwa miaka mitano.
Miezi michache
baada ya kutoka Betheli,
nilipata pendeleo la kuhudhuria
Shule ya Waeneza-Injili wa Ufalme.
Ilikuwa shule nzuri sana!
Mchezo wa mpira wa vikapu
unapendeza,
unasisimua sana,
ni wenye kuchochea,
lakini si chanzo cha furaha ya kweli.
Ni kweli,
ulimwengu unaweza
ukakupa uradhi wa kadiri fulani,
lakini gharama yake
ni kubwa sana.
Ilinichukua muda mrefu sana
kuelewa jambo hilo.
Lakini kujua kwamba
ninampa Yehova kilicho bora,
kumenileta furaha nyingi.
Naam,
sisi sote tuko kwenye timu,
timu kubwa,
timu ya Yehova.
Ina malengo yenye kusisimua
na ushindi wake
ni hakika.