JW subtitle extractor

Historia Yetu Hatua kwa Hatua—Makusanyiko

Video Other languages Share text Share link Show times

Hamjambo Ndugu na Dada?
Tunafurahi kukusanyika pamoja
kwa ajili ya programu hii
ya kiroho!
Mashahidi wa Yehova
wanapenda kuhudhuria makusanyiko
ili kujifunza,
kuabudu na kuimba pamoja.
Lakini makusanyiko makubwa kama hayo
yenye makumi ya maelfu ya watu
hayakuwa sehemu ya ibada yetu.
Yalianzaje?
Tutapata jibu katika sehemu hii
ya Historia Yetu Hatua kwa Hatua.
Kusanyiko kubwa la kwanza
la Mashahidi wa Yehova,
lilifanyika maelefu ya miaka iliyopita
Musa alipowakusanya Waisraeli
chini ya Mlima Sinai
ili kujifunza kutoka kwa Yehova.
Baada ya hapo,
Waisraeli walihudhuria sherehe tatu
kila mwaka.
Na kama ilivyo katika makusanyiko yetu leo.
pindi hizo
watu wa makabila tofauti
walikuja kumsifu Mungu
wakiwa familia moja kubwa.
Katika siku zetu,
makusanyiko ya kwanza
yalianza mwishoni
mwa miaka ya 1880.
Yalikuwa tofauti sana
na makusanyiko ya leo.
Yalihudhuriwa na mamia kadhaa
tu ya watu
basi yalikuwa mikutano mikubwa
ambayo wanafunzi wa Biblia
walifanya ili kuadhimisha pamoja
Mlo wa Jioni wa Bwana.
Na mikutano hiyo yote
ilifanywa Allegheny, Pennsylvania, Marekani.
Lakini
kulikuwa na badiliko kubwa
mwaka wa 1893
maonyesho ya Chicago World’s Fair yalipoanza.
Yalihudhuriwa na mamilioni ya watu.
Wakati huo,
gari-moshi za kwenda Chicago
zilikuwa zimepunguza nauli,
kwa hiyo,
Wanafunzi wa Biblia
waliona ni fursa nzuri
ya kuwaalika akinandugu na dada
kwenye kusanyiko la siku tano.
Watu 360 hivi walihudhuria
idadi ndogo sana
ikilinganishwa na makusanyiko
yetu ya leo.
Lakini,
makusanyiko hayo
yaliwasaidia Wanafunzi wa Biblia
kuona kwamba
kukutana na waabudu wenzao
kutoka maeneo mengine
kunaimarisha sana.
Hatimaye,
makusanyiko yalianza kufanywa kila mwaka.
Baadhi ya makusanyiko
yalifanywa nje au kwenye mahema,
kama kusanyiko la 1908
lililofanyika Put-in-Bay,
karibu na Ziwa Erie, Ohio.
Kusanyiko hili
lilifanyika kwa siku kumi!
Lilikuwa kusanyiko kubwa zaidi
kufanywa kufikia wakati huo,
inakadiriwa kwamba
watu 3500 na zaidi
walilihudhuria.
Ndugu na dada,
wazee kwa vijana,
walipata nafasi ya kuburudishwa kiroho,
kutumia wakati pamoja,
kucheka pamoja,
kula pamoja,
kujenga urafika,
na kusitawisha upendo.
Baada ya muda,
ulimwengu ulikumbwa na madhara
ya vita vya kwanza vya Ulimwengu
na pia homa ya Kihispania
ya 1918 iliyowaua watu
milioni 50 hivi.
Lakini watu wa Mungu
walisonga mbele.
Umoja wetu na upendo wetu
ulionekana hata zaidi
mwaka 1919,
huko Cedar Point, Ohio.
Hilo ndilo kusanyiko la kwanza
kubwa kufanyika
baada ya Ndugu Rutherford
na wenzake kuachiliwa
kutoka gerezani.
Wanafunzi wa Biblia
walisisimka sana
walipokutana kwa usalama
kwa hivyo waliendelea kumiminika
hivi kwamba ililazimu
kufanya program nje.
Kulikuwa na wahudhuriaje 7,000 hivi.
Miaka mitatu baadaye,
mwaka wa 1922,
kulikuwa na kusanyiko
lililosisimua hata zaidi
huko Cedar Point
kwa wastani
watu 10,000
walihudhuria kila siku.
Watu wa Mungu walitiwa moyo
kuhubiri zaidi.
Kadiri miaka ilivyosonga
makusanyiko yaliwaimarisha sana
watu wa Mungu,
kama kusanyiko lile lisilosahaulika
la Columbus, Ohio, mwaka wa 1931.
Hebu wazia
unaingia katika ukumbi wa Fair Grounds,
na kuna wahudhuriaji 15,000
na ukumbi umejaa kabisa.
Programu yako ya Kiingereza
ina herufi mbili kubwa:
JW.
Katika siku mbili za kwanzaza kusanyiko,
wote wanajaribu kukisia maana,
wengine wanasema:
Just Watch
au Just Wait.
Hatimaye,
Ndugu Rutherford anapanda jukwaani.
Mwishoni mwa hotuba yeke,
anatoa azimio hili:
“Twataka kujulikana
na kuitwa kwa jina hili,
Jehovah’s witnesses
yaani,
Mashahidi wa Yehova.”
Katika miaka ya 1940,
Vita vya Pili viliharibu nchi nyingi
na kuleta mgawanyiko
lakini Mashahidi
waliendelea kuongezeka
na a kuwa na umoja.
Mwaka wa 1946,
walikutana Cleveland, Ohio,
kwa ajili ya Kusanyiko la Kitheokrasi
lenye kichwa
“Mataifa Yenye Furaha”
kichwa hicho kilifaa sana.
Lilikuwa kusanyiko halisi la kimataifa
lenye wajumbe 55,000
waliotoka mataifa 33.
Wengine hata walilala
ndani ya mahema
au magari makubwa..
Kipindi hicho
ilikuwa kawaida kuona
majiji ya mahema kusanyikoni.
Familia yetu ya kiroho
iliendelea kukua
na kufikia miaka ya 1950
makusanyiko yalikuwa yakifanywa
katika sehemu mbalimbali ulimwenguni
hata katika mataifa maskini.
Mfano mzuri
wa jinsi makusanyiko ya kimataifa
yalivyoendelea kubadilika
ni kusanyiko kubwa la 1958
la Mapenzi ya Mungu
lililofanyika katika jiji la New York,
lilihudhuriwa na watu zaidi ya 250,000
kutoka katika mataifa 123.
Hili ndilo kusanyiko kubwa zaidi
kufanyika katika jiji moja,
watu walijaa kabisa
katika uwanja wa Yankee
na kwenye Polo Grounds
zilizokuwa karibu.
Mambo yaliyowaunganisha watu wa Mungu
kwenye makusanyiko kama haya
si idadi kubwa tu
bali mambo ya kiroho
kama vile hotuba motomoto,
mifululizo yenye kujenga,
machapisho mapya
na kuanzia miaka ya 1960,
drama za Biblia zilizoigizwa jukwaani.
Zawadi hizo zilizotoka kwa Yehova,
pamoja na shangwe
ya kupata marafiki wapya
na kuonana na marafiki wa zamani
kunafanya makusanyiko
yawe baraka kubwa .
Lakini haikuwa rahisi pindi nyingine.
Nchini Georgia,
ambako Mashahidi walikabili upinzani mkali,
akina ndugu walikuwa
wamepanga kufanya
Kusanyiko la Wilaya
la 2006, lenye kichwa
“Ukombozi Unakaribia!”
katika ukumbi wa Tbilisi Philharmonic.
Lakini wasimamizi wa ukumbi huo
walivunja makubaliano
wiki moja kabla ya kusanyiko!
Siku chache kabla ya kusanyiko,
kikundi kikubwa
cha ndugu na dada wenye bidii
waligeuza mashamba mawili
kuwa uwanja wa kusanyiko,
walivuna viazi
vilivyokuwa katika mashamba hayo,
wakatengeneza jukwaa
na mabenchi
na kuweka mfumo wa sauti.
Wakati wa kuanza kusanyiko ulipofika,
kila kitu kilikuwa tayari
na watu zaidi ya 17,000
walihudhuria kwenye uwanja huo,
na wengine walisikiliza kupitia simu.
Kusanyiko lilienda vizuri,
na wahudhuriaji walifurahi sana,
walipopata baraka nyingine
ambayo hawakutarajia!
Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
katika Kigeorgia
hilo liliwafanya wajihisi
wakiwa sehemu ya familia
ya ulimwenguni pote.
Katika miaka ya karibuni,
makusanyiko ya pekee
na makusanyiko ya kimataifa
yamefanywa katika sehemu mbalimbali
ulimwenguni pote.
Na tuliposhindwa kuhudhuria ana kwa ana,
tulifanya makusanyiko kupitia mtandao!
Kutoka Poland hadi Korea,
kutoka Australia hadi Afrika Kusini,
siku zote
makusanyiko yamekuwa pindi zenye shangwe
zinazowatia moyo watu wa Mungu.
Makusanyiko yanatuchochea
na kututia moyo,
yanatuunganisha
na ndugu na dada zetu,
na jambo muhimu zaidi,
yanatuleta karibu na Yehova.