JW subtitle extractor

M. Stephen Lett: Usimruhusu Kamwe Shetani Akutishe (Kum. 1:17)

Video Other languages Share text Share link Show times

Kichwa cha mazungumzo yangu ni
“Usimruhusu Kamwe Shetani
Akuogopeshe.”
Kuogopesha kunamaanisha
kujaribu kumfanya mtu afanye
au asifanye jambo fulani
kwa kumnyanyasa,
kumshambulia,
au kumtisha
na bila shaka
Shetani ni Mungu
anayewaogopesha watu.
Na hivyo ndivyo anavyofanya
watu watende jinsi anavyotaka.
Kwa upande mwingine
sikuzote Yehova hutuchochea kwa upendo.
Neno “kuogopesha”
linapatikana mara mbili
katika Biblia
yenye maelezo ya utafiti.
Na neno msiogopeshwe
linapatikana mara moja
kwenye maandishi ya Biblia yetu
kwenye Kumbukumbu la Torati 1:17,
ambapo waamuzi ambao
wangemsaidia Musa
waliamriwa:
‘Msiogopeshwe na wanadamu.
Hampaswi kuhukumu
kwa upendeleo.’
Ingawa maneno hayo
hayatumiwi mara nyingi katika Biblia,
wazo hilo
linapatikana mara nyingi.
Fikiria mifano michache,
mfikirie Goliathi
ambaye alikuwa na urefu wa mita 2.9
na alijaribu kumtisha kijana Daudi.
Unakumbuka jambo alilomwambia
kwenye Samweli cha kwanza sura ya 17 alimwambia:
“Nikaribie tu,
nyama yako
nitawapa ndege wa angani
na wanyama wa mwituni.”
‘Nikaribie tu, mvulana mdogo,
nami nitawalisha fisi na mwewe
maiti yako.
Kwa kweli
alimtisha sana.
Namna gani Rabshake
ambaye alijaribu kuwatisha Wayahudi
kuzungumza Kiebrania vizuri
kwa sauti kubwa
katika siku za Hezekia
au Sanbalati na Tobia
waliojaribu kumdhihaki Nehemia
na Wayahudi
kwa sababu ya kujenga ukuta?
Au mfano mwingine
ulio katika maelezo ya Mnara wa Mlinzi
ya andiko la leo,
Nebukadneza alipojaribu kuwatisha
wale Waebrania watatu
ili waabudu sanamu.
Alifanyaje hivyo?
Danieli 3:1 inasema kwamba
alijenga sanamu
kubwa sana
urefu wa mita 27.4 hivi
na upana wa mita 2.7,
na sanamu hiyo kubwa
ilikuwa yenye kuogopesha sana.
Kisha
kulingana na mstari wa 2
akakusanya kundi kubwa la watu:
“maliwali,
wasimamizi,
magavana,
washauri”
kundi lenye kuogopesha kweli.
Kisha kwenye mstari wa 4-6,
akaamuru tangazo hili litolewe kwa sauti kubwa:
‘Mtakaposikia sauti ya pembe,
zumari, zeze .
. mnaamriwa kwamba
lazima mwanguke chini
na kuabudu sanamu hii.
Na mtu ambaye hatafanya hivyo
atatupwa mara moja
katika tanuru
lenye moto mkali.
Hilo liliogopesha sana
lakini
wale Waebrania watatu
hawakuogopa chochote.
Lakini kama tulivyosema
Shetani
bado anajaribu kuwaogopesha watu leo.
‘Usipokubali kuongezewa damu mwilini
kwa hakika utakufa.’
‘Usipokubali kazi hii
(kazi ambayo itaathiri hali yako ya kiroho),
familia yako italala njaa.’
‘Vuta hii sigara,
unaogopa
kwani wewe ni mwoga kama kuku?’
‘Kwa nini usianzishe urafiki na msichana huyu
anayekupenda darasani?
Je, wewe ni shoga?’
Leo,
Shetani anatumia
mbinu ya kuwaogopesha watu.
Petro ya kwanza 5:8 inasema kwamba
Ibilisi “anatembea huku na huku
kama simba anayenguruma.”
Na mara nyingi
ananguruma
kwa njia inayokusudiwa kutuogopesha.
Kama vile
mngurumo halisi wa simba
kulingana na kitabu cha Insight,
mngurumo huo
umekusudiwa kuwafanya wanyama wanaofugwa,
wakanyagane
na kutoka ndani
ya zizi lenye ulinzi.
Tufikirie swali hili:
ni masomo gani ambayo tunaweza kujifunza
kutoka kwa Waebrania hao watatu
yatakayotusaidia tusikubali kamwe
Shetani atuogopeshe?
Yafuatayo ni masomo machache.
Kwanza:
usiache kamwe kumtumaini Yehova
kwa moyo wako wote,
licha ya mingurumo ya Ibilisi.
Tufungue Danieli sura ya 3,
ona jinsi walivyomtumaini kabisa Yehova
licha ya kukabili hali hiyo
yenye kuogopesha
sura ya 3, mstari wa 16:
“Shadraki, Meshaki, na Abednego
wakamjibu mfalme:
“Ee Nebukadneza,
hatuhitaji kukujibu kuhusiana na jambo hili.
Ikiwa ni lazima iwe hivyo,
Mungu wetu tunayemtumikia
anaweza kutuokoa
kutoka katika tanuru hilo lenye moto mkali,
Ee mfalme,
na kutuokoa kutoka mikononi mwako.
Lakini hata asipotuokoa,
Ee mfalme,
ujue kwamba
hatutaiabudu miungu yako
wala kuabudu sanamu ya dhahabu
uliyosimamisha.”
Kwa kweli walimtumaini Yehova.
Kuna somo lingine pia:
Roho takatifu
itatusaidia kuendelea kuwa watulivu
na kuepuka kushtuka,
na kuwajibu kwa njia nzuri
wale wanaotutesa.
Unapofikiria jambo ambalo tumesoma
kwa kweli walikuwa watulivu,
kwa kweli
walitoa jibu zuri sana
ni wazi kwamba
roho takatifu
ilikuwa ikiwaongoza
kwa njia kubwa sana.
Na tunaahidiwa kwamba
itakuwa hivyo kwetu pia.
Kwenye Luka 12:11, 12,
Yesu alisema:
“Mtakapopelekwa mbele ya makusanyiko
ya watu wote,
maofisa wa serikali,
na mamlaka,
msihangaike kuhusu jambo mtakalosema,
saa hiyohiyo
roho takatifu itawafundisha
mambo mnayopaswa kusema.”
Hili ni somo lingine:
Yehova anaweza kutumia
malaika zake wenye nguvu
ili kutukomboa
kutoka kwenye hali
yenye kuogopesha.
Katika kisa cha wale Waebrania watatu,
waliokolewa kimuujiza.
Mfalme alipotazama ndani ya tanuru hilo,
badala ya kuona wanaume watatu
waliofungwa wakiteketezwa,
aliona wanne
wakitembea wakiwa huru.
Ni wazi kwamba
wa nne alikuwa malaika.
Walipotolewa ndani ya tanuru hilo,
Danieli 3:27 inasema kwamba
hata hawakuwa
na “harufu ya moto.”
Hakuna hata unywele mmoja
uliokuwa umeungua.
Unapoenda katika nyumba
ya mtu ambaye anavuta sigara,
wewe pia
utakuwa na harufu ya sigara.
Kuhusu kuunguza nywele,
ni rahisi sana kwa nywele kuungua.
Wakati fulani uliopita
nilijaribu kuwasha jiko la gesi
kwa kutumia kiberiti.
Lakini nilichelewa
kuwasha kiberiti.
Moto mkubwa ukawaka
na kuchoma nywele kwenye mkono wangu.
Lakini Waebrania hao
hawakuungua unywele hata mmoja,
wala hawakuwa na harufu ya moshi.
Leo, hatutarajii kwamba
malaika wa Yehova
watatuokoa kimuujiza.
Lakini Yehova
anaweza kuwatumia malaika
kutusaidia
tunapokabiliana na hali fulani.
Na hivyo, unapata kazi
ili kuiandalia familia yetu.
Au tunapata daktari mwenye ushirikiano
ambaye anaheshimu msimamo wetu
kuhusu damu,
hiyo ni mifano michache.
Au huenda akawatumia malaika
kutuimarisha
tuendelee kuwa waaminifu
tunapokabili jaribu gumu.
Hili ni somo lingine tunalojifunza.
Imani thabiti
kuhusu ufufuo
inaweza kutuimarisha
kwa njia kubwa,
hata tunapotishiwa kuuawa.
Bila shaka,
Waebrania hao watatu
walijua maneno
ya Ayubu 14:13,
ambapo Ayubu
alimwomba Yehova
amfiche kaburini,
ampimie wakati,
kisha amkumbuke,
amfufue.
Inawezekana kwamba
walifahamu kuhusu ufufuo
ulifanywa na Eliya na Elisha.
Hawakujua kwamba
watakombolewa kimuujiza,
lakini walijua kwamba
wangefufuliwa
ikiwa wangeendelea kuwa watimilifu.
Hivyo, ndivyo ilivyo kwetu leo.
Na imani hiyo thabiti katika ufufuo,
unapofikiria jambo hilo,
humwondolea Shetani
nguvu zake
za kutuogopesha
hata tunapokabili kifo.
Tunaweza kusema kwamba
tumaini hilo
litatusaidia kuendelea kuwa waaminifu.
Tunapata pia somo lingine:
tunaposimama imara
na kutoogopeshwa
tunawatolea ushahidi wenye nguvu
wale wanaotutazama.
Unakumbuka alichosema mfalme
walipotoka kwenye tanuru
bila madhara?
Alisema:
“Na asifiwe Mungu wa Shadraki,
Meshaki, na Abednego, .
. kwa maana
hakuna Mungu mwingine yeyote
anayeweza kuokoa kama huyu.”
Ikiwa Nebukadneza
na watazamaji wengine wa Babiloni
watafufuliwa
wakiwa sehemu ya wasio waadilifu,
wanaotajwa kwenye Matendo 24:15,
tukio hilo litawasaidia
kumkaribia Yehova,
na kuunga mkono upande wake.
Katika ulimwengu mpya.
Pia fikiria
wale wanaume waliowatupa
ndani ya tanuru la moto,
na wakafa kwa kufanya hivyo.
Ikiwa watafufuliwa
wataambiwa kuhusu
mambo yaliyotokea baada ya wao kufa.
Na bila shaka,
jambo hilo litawasaidia kumkaribia Yehova zaidi,
katika ulimwengu mpya.
Hivyo ndivyo ilivyo pia leo.
Tunaposimama imara
bila kuogopeshwa
tunatoa ushahidi wenye nguvu.
Na kuna wengi ambao leo wamejifunza kweli
kwa sababu ya ushahidi kama huo.
Tumezungumzia masomo matano
kuhusu kutoogopeshwa,
ambayo tunaweza kujifunza
kutokana na Waebrania hao watatu.
Kwa muhtasari:
usiache kamwe kumtumaini Yehova,
licha ya mingurumo ya Ibilisi.
Pili:
Roho takatifu itatusaidia
kuendelea kuwa watulivu
kuepuka kushtuka,
na kujibu kwa njia nzuri.
Tatu Yehova anaweza kutumia malaika wake
kwa njia mbalimbali
ili kutuokoa
kutoka kwenye hali zenye kuogopesha.
Na nne:
Tumaini la ufufuo
litatuimarisha
ili tusiogopeshwe
hata ikiwa,
tutakabili kifo.
Na tano:
tunaposimama imara kabisa bila kuogopeshwa,
tunawatolea ushahidi mkubwa
wale wanaotutazama.
Basi, acheni sisi sote
kama Waebrania hao watatu,
tuazimie
kwamba hatutamruhusu kamwe
Shetani
atuogopeshe.