JW subtitle extractor

Geoffrey W. Jackson: Tunajua Nini Kuhusu Hukumu za Yehova za Wakati Ujao?

Video Other languages Share text Share link Show times

Kwa hiyo tumejifunza
jambo gani kufikia sasa?
Nina hakika kwamba
tulielewa jambo kuu.
Tumekumbushwa kumfikiria
Baba yetu mwenye upendo
wa mbinguni Yehova
kuwa Mwamuzi mwenye
rehema wa dunia yote,
pamoja na Mwana wake, Yesu Kristo.
Naam, tunaweza kuwatumaini
kwamba watatoa hukumu zinazofaa.
Tunajua kwamba Yehova na Yesu
wanaweza kusoma mioyo.
Na tunajua kwamba wana
rekodi ndefu
ya kuishi kupatana
na viwango vya haki
ambavyo Yehova ameweka.
Basi,
vipi kuhusu
hukumu za wakati ujao
wakati wa
dhiki kuu?
Je, kuna jambo lolote
katika uelewaji wetu
ambalo tunaweza kurekebisha?
Kabla ya kuanza kuzungumzia hilo,
acheni tuwe wazi kabisa.
Katika miaka kadhaa ambayo imepita,
tumefanya mabadiliko mbalimbali
kuhusu matukio wakati wa dhiki kuu.
Na ikiwa umekuwa katika
kweli kwa miaka kadhaa
huenda ikawa vigumu
wakati mwingine kukumbuka,
zamani tulikuwa tunaamini hivi
au sasa ndio tunaamini hivi?
Basi ili kutusaidia kupata wazo
kuhusu matukio mbalimbali
ambayo yatatokea wakati
wa dhiki kuu,
acheni tutazame video hii
fupi ya pitio.
Ni tukio gani litakaloashiria
mwanzo wa dhiki kuu?
Ni kuangamizwa
kwa Babiloni Mkubwa.
Huu ndio wakati ambapo
mamlaka za kisiasa
zitageukia miliki
ya ulimwenguni pote
ya dini ya uwongo
na kuonyesha
jinsi wanavyomchukia
kahaba huyo wa mfano.
Hilo litaongoza
kwenye kuangamizwa
kwa mashirika yote
ya dini za uwongo.
Ni tukio gani litakaloashiria
mwisho wa dhiki kuu?
Ni vita vya Har-Magedoni.
Hiyo ndio itakayokuwa
sehemu ya mwisho
ya dhiki kuu.
Yesu pamoja na wale
144,000 waliofufuliwa
na mamilioni ya malaika,
watapigana na wote
wanaompinga Yehova,
Ufalme wake,
na watu wake hapa duniani.
Hiyo ndiyo itakayokuwa vita
ya sikukuu ya Mungu Mweza Yote.
Sasa kwa kuwa tunajua mwanzo
na mwisho wa dhiki kuu,
acheni tujiulize maswali kadhaa.
Kipindi hicho kitakuwa
kirefu kadiri gani
kuanzia mwanzo hadi mwisho?
Jibu ni
hatujui.
Tunajua kwamba
matukio mengi yametabiriwa
yatatukia wakati wa kipindi hicho
lakini huenda matukio hayo yote
yakatokea katika
kipindi kifupi cha wakati.
Hata hivyo,
acheni tukazie fikira
matukio machache
ambayo yatatokea
mwishoni mwa dhiki kuu.
Shambulizi la Gogu wa Magogu
litatokea wakati gani?
Halitatokea mwanzoni
mwa dhiki kuu
bali kuelekea mwisho
wa kipindi hicho cha wakati.
Shambulizi hilo
dhidi ya watu wa Mungu
litakalofanywa na
muungano wa mataifa
litaongoza moja kwa moja
kwenye vita vya Har-Magedoni.
Kwa hiyo shambulizi la Gogu
litakuwa kabla tu
ya vita vya Har-Magedoni.
Mabaki ya watiwa mafuta
watakusanywa lini
na kupelekwa mbinguni?
Kitabu cha Biblia cha Ezekieli
kinaonyesha kwamba
Gogu wa Magogu
atakapoanza shambulizi lake,
baadhi ya watiwa mafuta
bado watakuwepo duniani.
Hata hivyo,
Ufunuo 17:14 inatuambia
Yesu atakapopigana na mataifa
atakuja ‘pamoja na walioitwa
waliochaguliwa’
yaani, wale 144,000
wote wakiwa wamefufuliwa.
Kwa hiyo kukusanywa kwa mwisho
kwa waliochaguliwa
lazima kutatokea
baada ya kuanza kwa
shambulizi la Gogu wa Magogu
lakini kabla ya vita vya Har-Magedoni.
Hilo linamaanisha kwamba
watiwa mafuta watakusanywa
na kupelekwa mbinguni
kuelekea mwishoni mwa dhiki kuu,
na si mwanzoni.
Kuhukumiwa kwa mwisho
kwa kondoo na mbuzi
kutatokea wakati gani?
Ingawa hatuwezi kusema
kwa uhakika kabisa
kuhusu mfuatano wa matukio,
inaonekana kwamba
hukumu ya mwisho
inatokea mwishoni mwa dhiki kuu,
si mwanzoni.
Huu ndio wakati ambapo
“Mwana wa binadamu atakapokuja
katika utukufu wake
pamoja na malaika wote.”
Bila shaka kuna matukio
mengine mengi
ambayo yametabiriwa kutokea
wakati wa kipindi hicho.
Lakini kwa sasa
acheni tuzungumzie tu
matukio hayo machache
ambayo yote yatatokea kabla tu
ya Har-Magedoni kuanza.
Tunajifunza nini kutokana nayo?
Kwanza,
Yesu atawahukumu kondoo na mbuzi
na pia kuwaangamiza waovu
mwishoni mwa dhiki kuu.
Pili, baadhi ya watiwa mafuta
bado watakuwepo duniani
hadi kufikia mwanzoni mwa
shambulizi la Gogu wa Magogu
karibu na mwishoni mwa dhiki kuu.
Tatu,
kuhukumiwa kwa kondoo na mbuzi
kutategemea mambo
waliyowatendea ndugu za Kristo
hata wakati wa dhiki kuu.
Kwa hiyo hilo ni pitio
la mambo ambayo tayari tunaamini.
Ikiwa ulikuwa unaandika ukasema
(“eh hilo ni jambo jipya”),
uwe mwangalifu
unawaambia nini wengine?
Kwa hiyo mambo hayo ya msingi
(tunapoangalia mambo ambayo
yatatokea kuelekea
mwishoni mwa dhiki kuu,
mambo hayo) yanaathirije
uelewaji wetu
kuhusu hukumu za Yehova
ambazo zitatekelezwa na
Yesu Kristo?
Tunajua kwamba kadiri
tunapokaribia dhiki kuu
ndivyo uelewaji wetu
kuhusu mambo yatakayotokea
utakavyokuwa.
Naam,
uelewaji wetu unarekebishwa
kwa wakati unaofaa
na pia kwa njia
ambayo itatuwezesha
kuvumilia dhiki kuu
na pia kuendelea kuwa waaminifu
na wenye furaha
katika kipindi hicho.
Kwa hiyo sasa tutakachofanya
ni kuchunguza maswali manne
yenye kupendeza sana.
Na inaonekana
nina muda wa kutosha.
Swali la kwanza ni hili.
Dhiki kuu itakapoanza
(tayari tuliona pale kwenye chati
itaanza na kuharibiwa
kwa Babiloni Mkubwa,
basi mara itakapoanza),
je, nafasi itapatikana
kwa ajili ya wasioamini
kujiunga nasi
kumtumikia Yehova?
Je, nafasi itapatikana?
Uelewaji wetu ulikuwa nini?
Tulisema,
“Hapana,
hakutakuwa na nafasi ya watu
kujiunga nasi wakati huo.”
Kwa nini tulisema hivyo?
Kwa sababu kimsingi
tuliona simulizi kuhusu Gharika
kuwa mfano
au ufananisho wa kinabii.
Na tulifikiri
kwa sababu mlango wa safina
ulifungwa
kabla ya Gharika kuanza
hilo liliashiria
kwamba mlango ungefungwa
baada ya dhiki kuu kuanza.
Ni kweli kwamba Yesu Kristo
alilinganisha kipindi cha Noa
na kuwapo kwake
akiwa
Mfalme anayetawala.
Lakini ona kwamba
hakuna lolote linaloonyesha
kwamba Yesu alisema simulizi hilo
lilikuwa ufananisho wa kinabii,
na pia hakutaja chochote
kuhusiana na mlango
wa nafasi ya
kumtumikia Yehova kufungwa.
Kwa hiyo acheni tufikirie
swali hilo tena.
Dhiki kuu itakapoanza,
je, nafasi ya kuanza
kumtumikia Yehova itapatikana?
Ili kujibu swali hilo
ukitazama chati hii
kumbuka kwamba
kuhukumiwa kwa kondoo na mbuzi,
hukumu ya mwisho
inatokea wakati gani?
Si mwanzoni
bali karibu na mwisho wa dhiki kuu.
Kwa hiyo tufikirie baadhi
ya watu tunaowafahamu
labda ni watu wetu wa ukoo
wasioamini,
au watu waliotengwa na ushirika,
au wengine waliosikia
ujumbe na wakajifunza.
Je, baadhi yao
baada ya kujionea
kuangamizwa kwa Babiloni Mkubwa
wanaweza
kujiambia kwamba
Mashahidi wa Yehova
walikuwa sahihi wakati wote?
Je, wanaweza
kuchukua msimamo wa
upande wa kweli?
Kwa kweli,
ikiwa wangebadili mioyo yao
na kujiunga nasi,
je, sisi tungekwazika?
Hatuwezi kusema kwa uthabiti.
Lakini
hatutaki pia kuwa kama Yona
na kusema:
“Mlango umefungwa.
Hapana.
Mh-mh,
mh-mh,
hapana.
Mh-mh.”
Kwa kweli tunahitaji
kukumbuka visa vingine
katika Maandiko
vinavyotusaidia kuelewa
jinsi Yehova
akiwa Mwamuzi mwenye rehema
alivyoshughulika
na watu nyakati za kale.
Kwa mfano,
wafikirie Waisraeli
walipoondoka Misri.
Tafadhali fungua Biblia yako
kwenye Kutoka
sura ya 12.
Kutoka sura ya 12
na tutasoma sehemu ya kwanza
ya mstari wa 38.
Mstari huu unafafanua Kutoka.
Na Kutoka 12:38 inasema:
“Pia, kundi kubwa lenye
mchanganyiko wa watu
lilienda pamoja nao.”
Na pale unaona
kuna maelezo ya chini.
Yanasema nini?
“Yaani,
kundi kubwa lenye mchanganyiko
wa watu ambao
hawakuwa Waisraeli
kutia ndani
Wamisri.”
Kwa hiyo,
ni nini kilichotokea?
Wakati ambapo yale Mapigo Kumi
yalikuja dhidi ya Wamisri,
ni wazi kwamba baadhi ya Wamisri
walianza kuona
tofauti kati ya Yehova
na miungu ya uwongo
waliyoabudu.
Kwa hiyo wakati wa
kufanya uamuzi ulipofika
na Waisraeli walikuwa
wakiondoka Misri,
baadhi ya Wamisri hao
walijiunga na Waisraeli.
Hilo ni jambo lenye kupendeza,
sivyo?
Lakini kweli,
huenda tukawa tunajiambia:
‘Ndiyo,
ninaelewa,
kwa nini tulisema
tulichosema awali,
lakini je,
ni kweli kwamba
wote hawa ambao
tumejifunza nao
(huenda baadhi yao)
wakawa na nafasi
ya kujiunga nasi
baada ya Babiloni Mkubwa
kuangamizwa?
Hiyo ni haki kweli?
Eti mtu anatubu dakika ya mwisho.’
Lakini tukifanya hivyo
je, tutakuwa tunamwiga
“Mwamuzi wa dunia yote”
ambaye ni mwenye rehema?
Kwa kweli hatupaswi kushangaa
ikiwa jambo hilo litatokea,
sivyo?
Na unapofikiria
tulipotazama ile chati ya wakati,
tuliona kwamba hilo
litatokea muda fulani
kabla ya hukumu ya mwisho.
Kwa hiyo mtu
yeyote atakayesimama
upande wa Yehova mapema
wakati wa dhiki kuu
bado atapatwa na shambulizi
la Gogu wa Magogu,
na hicho kitakuwa
kipindi kigumu sana.
Basi tunahitaji kukumbuka nini
kuhusiana na jambo hili?
Kama ilivyokuwa
katika karne ya kwanza,
mwaka wa 66 W.K.,
ulikuwa wakati
wa kufanya uamuzi
na wengi sana
waliamua kuondoka
kutoka Yerusalemu wakati huo.
Walifanya uamuzi wao
kwa kutegemea
kile walichopata kujua
na kusikia.
Basi kwa njia hiyo pia
kazi yetu ya kuhubiri leo
ni muhimu sana.
Tuone kile ambacho
Mtume Paulo alisema
kama ilivyoandikwa
katika kitabu cha Waroma.
Waroma sura ya 10
mstari wa 13 na wa 14.
Tunaposoma mistari hii,
fikiria muktadha wa mambo ambayo
tunazungumzia
wakati Babiloni Mkubwa
atakapoangamizwa.
Kwa hiyo kabla ya wakati huo
ona mstari wa 13 unavyosema:
“Kwa maana ‘kila mtu anayeliitia
jina la Yehova
ataokolewa.’
Hata hivyo,
watawezaje kumwitia
ikiwa hawajamwamini?
Nao watamwaminije
yule ambaye hawajamsikia?
Nao watasikiaje
bila mtu wa kuhubiri?”
Je, unaona kwa nini
kazi yetu ya kuhubiri
ni ya haraka na
muhimu sana leo?
Naam, watu wengi wanapata
nafasi ya kufanya uamuzi
sasa hivi.
Lakini je, inawezekana
kwamba baada ya dhiki kuu kuanza,
wengi ambao walikuwa
wamesikia ujumbe
ambao Mashahidi wa
Yehova wanahubiri
wakapata nafasi
ya kufanya uamuzi unaofaa
wakati huu?
Kwa mara nyingine,
hatuwezi kusema kwa uhakika
lakini tunatumaini sana
kwamba mambo yatakuwa hivyo.
Sasa tunapozungumzia hili,
acheni tuzungumzie pia suala nyeti.
Tunamaanisha nini?
Unajua baadhi yetu
nyakati zilizopita (hatutataja majina,
baadhi yetu) tumesema:
“Unajua mtu wangu wa ukoo
ambaye si mwamini,
afadhali afe kabla ya dhiki kuu kuanza.”
Ahaa!
Tunajua mmekuwa mkisema nini.
Tulisema:
“Huenda akifa
kabla ya dhiki kuu kuanza
labda atapata nafasi ya kufufuliwa.
Lakini akifa wakati huo . . .
Mh-mh.”
Lakini acheni tufikirie jambo hili.
Je, wokovu wa milele
wa mtu unategemea
wakati anapokufa?
Au je, unategemea
hali yake ya moyoni?
Kwa kweli,
Mwamuzi wa dunia yote
mwenye rehema
anajua hali yake ya moyoni.
Na kwa kweli,
tunawazia nini
tunapouliza swali hilo?
Je tunamwazia Yehova
akimwambia Yesu:
“Unamwona mtu huyu.
Huyu mtu anapaswa kufa milele.
Lakini
sasa ona amekufa
kabla ya dhiki kuu.
Ah!
Sasa lazima tumfufue.”
Jamani kweli?
Yehova ni Mwamuzi mwadilifu
na mwenye rehema.
Anajua mioyo ya watu.
Hatuwezi kumpumbaza.
Hilo ndilo lilikuwa swali la kwanza
najua lilikuwa lenye kupendeza,
sivyo?
Lilikuwa mara dhiki kuu inapoanza,
je, nafasi ya kuanza
kumtumikia Yehova inaondolewa?
Na jibu ni
tunahitaji tusubiri tuone.
Lakini kulingana na Maandiko,
kuna uwezekano kwamba
baadhi watachukua msimamo
upande wa kweli.
Swali la pili:
Kuhubiriwa kwa
habari njema ya Ufalme
kutakwisha wakati gani?
Swali zuri.
Jambo la kwanza la kukumbuka
ni kwamba habari njema
ni njema kwetu
na kwa wale wanaoamua kuikubali.
Lakini kama Zaburi ya 2
inavyoonyesha
kwa wengine ulimwenguni
haijawahi kuwa habari njema.
Basi,
Mathayo 24:14 inatuambia nini?
Inatuambia
‘habari njema itahubiriwa,’
na “ndipo
ule mwisho
utakapokuja.”
Tuangalie tena
mfuatano wa wakati.
“Mwisho” unaotajwa hapo
ni nini?
Ni sehemu ya mwisho
ya dhiki kuu.
Hilo linamaanisha kwamba
wakati wa dhiki kuu,
bado habari njema
ya Ufalme itahubiriwa.
Na bado ni habari njema kwetu
lakini si
kwa wengine ulimwenguni.
Hiyo habari njema
itaendelea kuwa
na ujumbe mkali
kadiri wakati unavyosonga,
na kuwalazimisha watu
kufanya uamuzi
watasimama upande gani,
kuamua ikiwa wanaukubali
Ufalme au la.
Je, hiyo sio sababu ya ziada
kwa nini hatupaswi kushangaa
kwamba baadhi
watachukua msimamo
upande wa kweli
hata wakati ambapo
dhiki kuu inaendelea?
Swali la tatu:
Wote watakaokufa
wakati wa dhiki kuu,
je, watapatwa na kifo cha milele
na wasiwahi tena kufufuliwa?
Kwa kweli tunaweza
kusema kwamba
mbuzi hawatafufuliwa,
sivyo?
Kwa sababu
“watakatiliwa mbali milele”
kulingana na kile ambacho
Yesu alisema.
Na Wathesalonike ya Pili
sura ya 1
inataja kuhusu
“adhabu ya uharibifu wa milele”
ambayo watapata.
Lakini hilo linazungumza
kuhusu wakati gani?
Acheni tutazame chati yetu tena.
Unaona
hilo linarejelea wakati
ambapo Yesu atakuja
pamoja na watakatifu wake.
Kwa hiyo, tunapotazama chati hii
ya mfuatano wa wakati
inatuambia nini?
Kwamba hilo linatokea
katika sehemu ya mwisho kabisa
ya dhiki kuu.
Wakati ambapo watu watahukumiwa
kuwa mbuzi.
Wakati huo
watu hao watahukumiwa
kuwa mbuzi.
Lakini maswali mengine
yanayojitokeza hapa.
Hawa ambao wanahukumiwa
kuwa mbuzi
(watakaopata uharibifu wa milele)
ni wazi kwamba
wamepata nafasi ya kutosha
(nafasi kamili)
ya kuukubali au kuukataa Ufalme.
Lakini vipi
kuhusu wale
wa kabla tu
ya hukumu hiyo ya mwisho?
Yaani,
dhiki kuu inaanza
na hatujui itaendelea
kwa muda gani,
lakini kila siku inayopita
kuna watu ambao
bila shaka watakufa.
Je, unatambua kwamba
ulimwenguni pote
kila siku
watu 150,000 wanakufa,
iwe ni kwa sababu za kiasili,
vita,
magonjwa,
na kadhalika?
Basi vipi kuhusu watu hao?
Si eti wameuawa na Yehova
kwamba wamepewa adhabu.
Tunahitaji kujikumbusha nini?
Hakimu wetu mwenye rehema
anajua nani anapaswa kufufuliwa
na nani hapaswi kufufuliwa.
Kwa hiyo hatupaswi kusema
kwa uthabiti kabisa
kuhusu watakaokufa wakati huo.
Tunajua kwamba Yehova na Yesu
watafanya jambo linalofaa.
Sasa
swali lingine la mwisho
lenye kupendeza:
Je, wale wote watakaokuwa hai
wakati wa dhiki kuu
watakuwa na nafasi kamili
ya kujiamulia
ikiwa watasimama
upande wa Ufalme au la?
Wewe ungejibuje?
Usijibu kwa sauti.
Jibu rahisi ni:
Sisi
hatujui,
na hatuhitaji kujua
kwa sababu sisi sio waamuzi.
Hiyo si kazi yetu.
Lakini huenda ndani yako
labda unajiambia:
‘Kwa nini hatujui?
Mimi sikuzote nimeamini
wakati huo
mambo kwisha.’
Lakini kwa kweli
kama tulivyotaja tayari,
kila siku watu 150,000 wanakufa,
lakini watoto 350,000
wanazaliwa kila siku.
Kwa hiyo hata ikiwa dhiki kuu
ingekuwa na urefu wa
siku chache tu,
kila siku kungekuwa
na watoto wengi zaidi
wanaozaliwa.
Na vipi kuhusu yale
maeneo ambako
habari njema haijafika kikamili,
labda katika nchi
ambapo kazi yetu
imewekewa vizuizi?
Huenda tukajiuliza,
‘Je, kweli tutaweza
kumhubiria kila mtu?’
Mathayo 10:23,
ukiisoma baadaye,
inatuonyesha
huenda hatutaweza.
Kwa hiyo hapa kuna swali
lenye kupendeza.
Je, ni jambo linalopatana
na akili
kwetu kusema kwamba
Yehova na Yesu
wanawahukumu mamilioni ya watu
moja kwa moja kuwa mbuzi
hata ingawa hawajapata
nafasi kamili
ya kufanya uamuzi?
Ni swali lenye kupendeza.
Ikiwa hawajapata nafasi
nao wafe wakati huo,
je, inawezekana kwamba
watafufuliwa wakiwa
miongoni mwa watu
wasio waadilifu?
Jibu ni nini?
Kwa kweli sisi hatujui.
Hatuwezi kusema kwa uthabiti
na hatupaswi kufanya hivyo
kwa sababu hatujui.
Badala yake,
acheni tufarijiwe na
kile ambacho tunajua
na tunajua nini.
Tunajua kwamba
Yehova na Yesu ni wenye rehema
na kwamba sikuzote
watafanya uamuzi bora.
Na
Ezekieli 33:11
inasema nini?
‘Yehova hafurahishwi
na kifo cha mwovu.’
Anataka watu waovu wabadilike.
na tunajua
kwamba Yehova na Yesu
watamhukumu kila mtu
kwa njia yenye usawaziko,
ya uadilifu,
na yenye rehema.
Huenda sasa ukawa unajiambia:
‘Hayo ni mambo mengi
sana kukumbuka.’
Huenda labda umechoka
kuandika mambo makuu.
Usiwe na hofu
makala ya Mnara wa Mlinzi
hivi karibuni
itatupatia habari zote
kuhusiana na jambo hili,
isubiri kwa hamu.
Lakini kwa sasa tunahitaji
kuendelea kufanya nini?
Tunahitaji kuendelea kuhubiri ujumbe
kwa watu wengi iwezekanavyo.
Hatujui ni matokeo
gani yatakayopatikana
kwa kufanya hivyo.
na tunapoendelea kuhubiri,
kumbuka,
mwachie Yehova na Yesu
kazi ya kuhukumu!
Siku zote wao
watafanya uamuzi bora
wenye rehema na wa haki.
Tunaweza kuwa na uhakika
kamili kuhusu hilo!