JW subtitle extractor

Mark Sanderson: Nafasi za Kumtukuza Yehova Shambani

Video Other languages Share text Share link Show times

Miaka 140 iliyopita,
mwaka wa 1884
Zion’s Watch Tower
and Tract Society.
iliandikishwa kisheria.
Najua wengi hapa
wana ndevu nyeupe
lakini sidhani ikiwa yeyote
alikuwepo wakati huo.
Nafurahi kujua hivyo.
Ilikuwa kama Zekaria
sura ya 4 mstari
wa 10 inavyosema
yaani ilikuwa “siku
inayoanza kwa mambo madogo,”
mambo machache sana.
Lakini Yehova ametimiza nini
katika shamba?
Baada ya miaka 140.
Leo kuna zaidi ya
watu 9,000,000
ambao wanahubiri habari njema
katika nchi 240.
Wakiitumia machapisho katika
lugha zaidi ya 1000.
Je, akina ndugu,
hatuchochewi kumtukuza Yehova
kwa mambo aliyotimiza?
Lakini tulifikaje tulipo?
Na ni nini ambacho
kimechangia sana
katika upanuzi wa
ulimwenguni pote
ambao umeonekana
katika tengenezo la Yehova?
Na sasa kuna nafasi zipi
zinazopatikana shambani
kwa ajili ya vijana wetu?
Tafadhali tazama.
Unapofikiria kuhusu mmishonari,
huenda unamfikiria mtu
mwenye umri mkubwa
ambaye amekuwa akihubiri
kwa miaka mingi.
Lakini ukweli ni kwamba
wengi wao walikuwa
vijana walipoanza.
Kwa kweli
katika miaka ya 1940
asilimia 30 ya wamishonari
waliotumwa kutoka Gileadi
hawakuwa wamefikisha
umri wa miaka 24.
Walikuwa vijana,
wenye nguvu,
wachangamfu,
na walikuwa tayari
kupokea migao
popote ulimwenguni
na walitimiza mengi.
Kwa mfano,
mwaka wa 1943,
tulikuwa tukihubiri
katika nchi 54.
Na idadi ya wahubiri
bado ilikuwa ndogo.
Yehova alibariki kazi yao
hivi kwamba,
katika miaka mitano tu,
idadi ya wahubiri
ulimwenguni pote iliongezeka
mara mbili.
Kufikia 1953
ilikuwa imeongezeka
mara mbili tena.
na tengenezo lilikuwa
likihubiri katika nchi 143.
Mlipuko huo wa ukuzi
ndani ya miaka 10
uliweka msingi wa
Tengenezo la Yehova
kukua kufikia ulivyo leo.
Zaidi ya watu 8,000,000
walio katika nchi 239
wanawafikia mabilioni
kwa habari njema.
Wamishonari vijana
wametimiza moja kwa moja
maneno ya Yesu Kristo.
Wanahubiri “habari
njema ya Ufalme”
“kuwa ushahidi
kwa mataifa yote.”
Lakini miaka 80 imepita,
kwa hiyo
huenda ukawa unajiuliza:
“Je, bado leo
kuna uhitaji wa wamishonari?”
Mambo hakika yanaonyesha nini?
Tunaona ukuzi mkubwa
na uwezekano wa kuona
ukuzi mkubwa hata zaidi.
Kumekuwa na matokeo gani
katika mwaka wa
utumishi uliopita
Msumbiji
kulikuwa na kelele kipya
cha wahudhuriaji wa ukumbusho.
Watu 400,000 walihudhuria.
Hiyo ni mara nne
ya idadi ya wahubiri
nchini humo.
Angola
kulikuwa na wastani wa
wamisionari 900 wapya
kila mwezi.
Samahani ni wahubiri.
Hao ni wengi sana.
Ofisi ya tawi ya Congo
ilikuwa na wastani wa
wahubiri wapya 1300
kila mwezi.
Na nchini Filipino
kwa wastani
watu 1000 walibatizwa
kila mwezi.
Ndugu na dada
katika nchi hizo
ambako kuna ukuzi mkubwa,
kuna uhitaji mkubwa
wa wamishonari wapya.
Lakini kuna uhitaji
katika nchi nyingine pia.
Nchi nyingi zina
wamishonari ambao wametumikia
kwa muda mrefu
na wamefanya kazi nzuri.
Hata hivyo,
wengi kati ya
ndugu hao waaminifu
sasa wamekufa.
Wengine wamelazimika
kuondoka katika migawo yao.
Labda ili wakawatunze
watu wa ukoo
au ambao wana matatizo
yao wenyewe ya afya.
Kwa hiyo swali ni hili,
Je, bado tuna uhitaji
wa wamishonari leo?
Jibu ni bila shaka ndiyo.
Kuna kazi kubwa sana
inayohitaji kufanywa
ulimwenguni kote
katika utumishi wa umishonari.
Na vijana wachangamfu
na wenye bidii
wanatumwa kila mwaka
wakatumikie wakiwa wamishonari.
Kwa mfano, hivi karibuni
idara ya utumishi
ilituma wamishonari wapya
36 kule Madagaska
na 10 kule Latvia.
Wamishonari hao
wanahisije kuhusu pendeleo
la utumishi walilokabidhiwa?
Acheni tuone.
Uhitaji mkubwa wa kuhubiri
nchini Madagaska
sasa hivi ni kuzoeza wapya.
Tuna wahubiri wengi wapya
ambao hata bado hajabatizwa
ambao wanaongoza mafunzo
ya Biblia yenye maendeleo.
Kwa hiyo tuna
furaha sana kupokea
wamishonari wengi wapya.
Halmashauri yetu ya tawi
iliposikia tutapokea
wamishonari wapya kwenda Latvia,
tulifurahi sana.
Tulitumikia kwa miaka mitatu
tukiwa mapainia wa pekee.
Kisha tukapokea barua hiyo.
Nilijiuliza: “Latvia?
Kweli tunajua chochote
kuhusu Latvia?”
Nilitetemeka sana.
Halafu nikajiambia:
“Inasisimua sana!”
Kwangu bado ni kama ndoto.
Na nyakati nyingine
namwuliza Franzi:
“Je, kweli ni halisi?”
Mimi nilikuwa nikitarajia
labda nitatumwa Afrika.
Lakini jibu likawa:
“Hapana.
Utapigwa na theluji maridadi.”
Tulihisi hao wamishonari
wakichochea mambo shambani.
Msisimko wao
unasukuma kazi mbele.
Sasa wahubiri wengi zaidi
ni watendaji katika huduma.
Na roho ya upania inaongezeka.
Nilihisi baraka za Yehova
katika mgawo wetu.
Na hasa watoto
kutanikoni kwetu
wanapokumbatia, unahisi
ni kama upo nyumbani
na hata hufikirii
kuhusu matatizo ya lugha.
Ninapenda mgawo wangu wa umishonari
kwa sababu umefanya macho yangu
yafunguke na kuona kitu maridadi.
Utumishi kwa kweli unapendeza sana.
Kuwa mmishonari
ni jambo la pekee
lakini kwa upande mwingine,
ni maisha
ya kawaida ya Mkristo.
Kwa sababu unakazia fikira
kuhubiri na kufurahia maisha.
Ni sawa kuwa na wasiwasi,
kuwa na shaka,
lakini mpe Yehova nafasi.
Kuwa mmishonari
ndilo jambo kubwa zaidi
limetokea maishani mwangu.
Mgawo wangu umeimarisha
hali yangu ya kiroho
kwa sababu sasa
siogopi migawo migumu.
Nakubaliana na hilo.
Kwa hiyo tunahitaji
vijana wengi zaidi
wa kushiriki
utumishi wa umishonari.
Swali basi ni
unawezaje kuwa mmishonari?
Hatua ya kwanza ni
kuchukua utumishi
wa wakati wote
kisha baada ya kushiriki
utumishi wa wakati wote
kwa miaka miwili,
unahitaji kufanya nini?
Unahitaji kujaza ombi
la kwenda kwenye
Shule ya Waeneza Injili wa Ufalme.
SKE ndio mlango wa kuingia
utumishi wa umishonari.
Unahitaji pia kuwa na
roho ya Isaya aliposema:
“Mimi hapa! Nitume mimi!”
Uwe tayari kwenda popote
ambapo tengenezwa litakutuma.
Baada ya kuhitimu SKE,
unaweza kupokea mgawo
wa kuwa painia wa pekee
wa muda katika
eneo la nchi yako.
Ili upate uzoefu
na ukifanya vizuri
katika mgawo huo,
unaweza kupata mgawo
wa kutumikia
ukiwa mmishonari
katika nchi nyingine.
Utumishi wa umishonari
ni nafasi yenye
kusisimua ya kuwapelekea
habari njema watu wenye
mioyo minyoofu
mahali pengine ulimwenguni.
Tunahitaji vijana ambao
wangependa kwenda
kuwafanya watu wa mataifa
yote kuwa wanafunzi.
Basi,
unahitaji kuwa na umri gani
ili ujaze ombi
la Shule ya
Waeneza Injili wa Ufalme?
Tuna furaha kubwa
kutangaza leo
kwamba Baraza Linaloongoza
limeamua kwamba
ndugu na dada vijana
wenye umri wa miaka 21
au zaidi
sasa wanaweza
kujaza ombi la
kwenda SKE.
Je, hilo halipendezi sana?
Lakini sasa hivi
wengi wenu vijana mnatumikia
katika maeneo yenye uhitaji,
labda hata katika
nchi nyingine.
Hongereni sana.
Lakini, tunawatia moyo sasa,
mjaze ombi la kwenda
Shule ya Waeneza
Injili wa Ufalme.
Tunajua hilo litawezesha
tengenezo kuona kwamba
wewe unafaa zaidi
kutumiwa wapi,
katika shamba la ulimwenguni.
Ndugu na dada vijana,
tafadhali chukueni nafasi hii
yenye kupendeza sana.
Lakini vipi kuhusu sisi
ambao tuna umri mkubwa?
Tunaweza kufanya nini
ili kuwasaidia
hawa vijana wetu?
Acheni tuwe wakarimu
katika kuwazoeza
na kushiriki nao
uzoefu wetu.
Acheni tuwasaidie
wakue na tuwatie moyo
wafikie
mapendeleo haya yote
ambayo yako mbele yao
ya kumtukuza Yehova.
Mimi nilipokuwa na miaka 19 tu
ndugu mmoja alinialika
nihudhurie
mkutano wa kila mwaka
kwa mara ya kwanza.
Ulikuwa wa pekee.
Ilikuwa tunasherehekea
miaka 100
ya WatchTower
Bible and Tract Society
huko Pittsburgh, Pennsylvania.
Nilisisimka sana.
Nilifikiri nimekufa
na kwenda mbinguni.
Sikuweza kuamini.
Eti ndugu huyo
alinialika mimi
nikiwa kijana hivyo.
Lakini sijasahau
kitia moyo nilichopata
katika tukio hilo
na ninakumbuka kufikia leo.
Ndugu na dada,
ninyi mtafanya nini?
Wewe utafanya nini
kumtia moyo
kijana amtukuze Yehova?
Bila shaka Yehova atakubariki
ukitafuta njia
za kufanya hivyo.
Kazi ya kuhubiri
inahitaji kufanywa
kwa uharaka zaidi.
Tafadhali tusome Waroma
sura ya 10.
Waroma sura ya 10,
mstari wa 13.
Inasema: “Kwa maana
‘kila mtu anayeliitia
jina la Yehova ataokolewa.’
Hata hivyo,
watawezaje kumwitia
ikiwa hawajamwamini?
Nao watamwaminije
yule ambaye hawajamsikia?
Nao watasikiaje
bila mtu wa kuhubiri?
Nao watahubirije
isipokuwa wawe wametumwa?
Kama ilivyoandikwa:
‘Jinsi inavyopendeza
miguu ya wale wanaotangaza
habari njema.
ya mambo mema!’”
Tunahitaji vijana
kama mstari wa 15
unavyosema
‘watumwe’ wakahubiri habari njema.
Tunahitaji vijana watumikie
wakiwa mapainia,
mapainia wa pekee,
na wamishonari.
Tunahitaji watume maombi
kwa ajili ya
Shule ya Waeneza
Injili wa Ufalme.
Yehova ametimiza kazi kubwa
katika miaka hii 140
ambayo imepita.
Amebariki siku inayoanza
kwa mambo madogo.
Lakini ndugu na dada,
kazi bado haijakwisha.
Je, mnakubaliana na hilo?
Kuna nafasi nyingi nzuri
kwa ajili ya vijana wetu.
Kwa hiyo vijana
ninyi mtafanya nini?
Sasa mnaweza kuomba
kutumikia Betheli
na utumishi wa ujenzi
mkiwa na miaka 18.
Mnaweza kuomba kwenda
Shule ya Waeneza Injili
wa Ufalme mkiwa na
umri wa miaka 21.
Jiwekeni mikononi mwa Yehova.
Jionyesheni kwamba
mko tayari,
hamtawahi kujutia hilo.
Na sisi wenye umri mkubwa
na tufanye yote tunayoweza
kuwatia moyo na kuwazoeza
vijana wetu.
Naam,
kama Ndugu Losch alivyosema
acheni ‘tuendelee kung’arisha
vioo vyetu.’
Na tuendelee kutafuta
njia za kupanua
huduma yetu
na kumtukuza Mungu wetu
mwenye kupendeza sana
Yehova.