00:00:01
Nimezaliwa Kolombia.00:00:02
00:00:02
Nina dada zangu watano.00:00:04
00:00:05
Nilijifunza kweli nikiwa na umri mdogo00:00:07
00:00:08
kupitia wazazi wangu.00:00:09
00:00:09
Tulikuwa na utendaji mwingi wa kiroho.00:00:11
00:00:12
Baba yangu hakuwa tu katika kweli;00:00:14
00:00:14
bali alitumia kweli00:00:15
00:00:15
hizo maishani mwake,00:00:17
00:00:17
sikuzote alitufundisha kufanya hivyo pia.00:00:20
00:00:22
Alihakikisha tunasoma andiko la siku00:00:24
00:00:24
kila siku kabla ya kwenda shuleni.00:00:26
00:00:26
Hilo lilikuwa muhimu.00:00:28
00:00:28
Yaani, ni bora tuchelewe shule,00:00:30
00:00:31
kuliko tukose kusoma andiko la siku.00:00:33
00:00:34
Ingawa familia yetu ni kubwa,00:00:35
00:00:35
sikuzote tulienda mikutano pamoja00:00:37
00:00:38
na kujaza mistari miwili.00:00:39
00:00:41
Sikuzote aliwajali ndugu na dada.00:00:43
00:00:44
Alikuwa tayari kuwasaidia.00:00:46
00:00:46
Yeye na mama00:00:47
00:00:47
walikuwa wakaribishaji wageni.00:00:49
00:00:50
Alikuwa anapenda kuwaalika nyumbani00:00:52
00:00:52
wanafunzi wake wa Biblia,00:00:54
00:00:55
ndugu na dada,00:00:56
00:00:56
na angeingia jikoni na kufunga mlango,00:00:58
00:00:58
aweke muziki,00:00:59
00:01:00
na kuwapikia chakula kizuri.00:01:02
00:01:02
Alipanga mambo00:01:03
00:01:03
ili yawe yenye kufurahisha,00:01:05
00:01:05
alipenda binti zake wafurahie maisha,00:01:08
00:01:08
na hasa familia nzima ikiwa pamoja.00:01:11
00:01:11
Alimpa kila mmoja wetu mahitaji yake00:01:13
00:01:14
na pia yale yaliyotufurahisha.00:01:15
00:01:17
Baba00:01:18
00:01:19
alitupeleka matembezi mwisho-juma00:01:22
00:01:22
baada ya mikutano00:01:24
00:01:24
na pia baada ya mahubiri.00:01:25
00:01:25
Alikuwa mtu wa pekee sana00:01:27
00:01:27
na baba mzuri.00:01:29
00:01:32
Ninakumbuka vizuri00:01:34
00:01:34
siku hiyo, sisi tulikuwa ndani ya nyumba.00:01:36
00:01:36
Alikuwa amerudi.00:01:38
00:01:38
Alipokuwa akiegesha gari,00:01:40
00:01:40
wanaume fulani walimfuata00:01:41
00:01:41
na kumtisha.00:01:43
00:01:43
Mama alikuwepo.00:01:44
00:01:44
Walikuwa na00:01:46
00:01:47
bunduki kubwa00:01:48
00:01:48
na walimwambia00:01:49
00:01:49
atoke kwenye gari00:01:51
00:01:51
ili wamteke.00:01:52
00:01:52
Tulisikia makelele.00:01:54
00:01:54
Tulishtuka sana,00:01:56
00:01:56
basi tukakimbia nje.00:01:58
00:01:59
Basi tulipotoka nje, tulimwona baba00:02:01
00:02:02
akiwa amelala chini,00:02:03
00:02:04
watu hao walikuwa wamempiga risasi.00:02:08
00:02:08
Walimwacha hapo.00:02:09
00:02:15
Nilimwinua na kumkumbatia.00:02:17
00:02:20
Alipelekwa hospitali,00:02:22
00:02:22
na baada ya saa chache, alikufa.00:02:24
00:02:27
Maneno yake ya mwisho yalikuwa:00:02:29
00:02:30
“Yehova,00:02:31
00:02:31
walinde binti zangu00:02:32
00:02:33
na kipenzi changu”—00:02:34
00:02:34
yaani, mama yangu.00:02:36
00:02:44
Mama yetu,00:02:45
00:02:45
alikuwa imara.00:02:46
00:02:46
Alitusaidia00:02:48
00:02:48
tuwe imara pia.00:02:49
00:02:49
Aliendelea na ratiba ileile ya kiroho.00:02:53
00:02:53
Siku moja baada ya kifo cha baba,00:02:55
00:02:55
kulikuwa na mkutano,00:02:56
00:02:57
dada yangu Raquel00:02:58
00:02:58
alikuwa na hotuba.00:02:59
00:02:59
Na ingawa Raquel alikuwa amepoteza00:03:01
00:03:01
baba yake siku moja kabla,00:03:03
00:03:03
alitoa mgao wake siku hiyo.00:03:05
00:03:06
Na pia juma lililofuata00:03:07
00:03:07
hatukukosa kusanyiko la mzunguko.00:03:09
00:03:10
Sote00:03:10
00:03:10
tuliazimia kufuata mfano00:03:12
00:03:13
ambao baba00:03:14
00:03:14
alituwekea.00:03:15
00:03:16
Ingawa maisha hayakuwa rahisi,00:03:18
00:03:20
tulimpa Yehova nafasi ya kwanza,00:03:22
00:03:23
katika maamuzi yote tuliyofanya.00:03:25
00:03:25
Tulipotaka kufanya uamuzi,00:03:27
00:03:27
kwanza, tulimfikiria Yehova00:03:29
00:03:29
na pia jinsi baba alivyokuwa00:03:31
00:03:31
mshikamanifu kwake.00:03:32
00:03:33
Niliendelea na maisha00:03:35
00:03:35
kana kwamba yuko hai,00:03:37
00:03:38
na kuhakikisha sisi sote tuko katika kweli.00:03:41
00:03:42
Mwanzoni, nilisali:00:03:43
00:03:43
“Ninaomba ‘amani . . .00:03:44
00:03:44
inayozidi uelewaji wote.’”00:03:46
00:03:47
Na sasa00:03:48
00:03:48
ninapokabili hali ngumu,00:03:50
00:03:50
ninamwambia Yehova:00:03:52
00:03:52
“Naomba00:03:53
00:03:53
niendelee kuwa na amani.00:03:54
00:03:54
Usiruhusu jaribu hili lininyime amani.”00:03:57
00:03:57
Kisha Yehova mwenyewe huniimarisha.00:04:00
00:04:01
Ninawapenda sana dada zangu.00:04:04
00:04:04
Nami ninawaheshimu sana00:04:06
00:04:06
kwa sababu wamekuwa00:04:07
00:04:07
kama mama kwangu.00:04:08
00:04:08
Watatu kati yao bado wanaishi Kolombia,00:04:10
00:04:11
kwa hiyo tunawasiliana mara kwa mara00:04:13
00:04:13
kupitia simu au Zoom.00:04:15
00:04:16
Hivyo, wanaweza kujua00:04:17
00:04:17
pia Mama anaendeleaje.00:04:18
00:04:20
Baadhi ya ndugu zetu00:04:20
00:04:20
ambao si Mashahidi00:04:22
00:04:22
walitaka kuwachukua baadhi ya dada zangu00:04:24
00:04:25
ili kuwalea mpaka watakapokuwa wakubwa.00:04:27
00:04:28
Lakini hatukutaka kutenganishwa00:04:30
00:04:30
kwa sababu tulijua00:04:31
00:04:32
ikiwa baba angekuwepo00:04:33
00:04:33
asingefurahishwa na hilo.00:04:34
00:04:35
Alitaka tumtumikie Yehova00:04:37
00:04:37
na kuingia ulimwengu mpya pamoja.00:04:39
00:04:39
Hatukutaka kuziachilia jitihada zake00:04:41
00:04:41
zote alizofanya maishani mwake00:04:43
00:04:44
ziende na maji00:04:45
00:04:45
kwa sababu tu hayupo pamoja nasi.00:04:48
00:04:48
Baba alinifundisha mambo mengi00:04:50
00:04:50
madogomadogo katika uumbaji00:04:52
00:04:52
kumhusu Yehova,00:04:54
00:04:55
naam,00:04:55
00:04:56
ambayo yaliniwekea msingi wa00:04:57
00:04:57
kumpenda Yehova.00:04:58
00:04:59
Ingawa sikuelewa,00:05:00
00:05:02
wakati huo,00:05:03
00:05:03
kwamba mambo hayo00:05:04
00:05:04
yangenisaidia kukua kiroho.00:05:06
00:05:07
Hivyo huwa najiambia,00:05:08
00:05:09
“Baba yangu aliniacha00:05:10
00:05:10
kwa Baba mwingine,00:05:12
00:05:12
ambaye ni Yehova.”00:05:14
00:05:14
Na hilo limenisaidia nijisikie vizuri.00:05:17
00:05:19
Maneno ya mwisho ya00:05:21
00:05:21
baba00:05:22
00:05:23
yalikuwa,00:05:24
00:05:25
“Mke wangu, binti zangu, Yehova.”00:05:28
00:05:28
Hivyo, ninatazamia00:05:30
00:05:30
kwa hamu kumwambia:00:05:31
00:05:31
“Ona! Hawa hapa.00:05:33
00:05:33
Sote tuko hapa.”00:05:34
00:05:35
Tumefika hapa!00:05:36
00:05:37
Umetulea vizuri.00:05:38
Mabinti wa Otalora: Jenga Imani Inayoweza Kustahimili Majanga
-
Mabinti wa Otalora: Jenga Imani Inayoweza Kustahimili Majanga
Nimezaliwa Kolombia.
Nina dada zangu watano.
Nilijifunza kweli nikiwa na umri mdogo
kupitia wazazi wangu.
Tulikuwa na utendaji mwingi wa kiroho.
Baba yangu hakuwa tu katika kweli;
bali alitumia kweli
hizo maishani mwake,
sikuzote alitufundisha kufanya hivyo pia.
Alihakikisha tunasoma andiko la siku
kila siku kabla ya kwenda shuleni.
Hilo lilikuwa muhimu.
Yaani, ni bora tuchelewe shule,
kuliko tukose kusoma andiko la siku.
Ingawa familia yetu ni kubwa,
sikuzote tulienda mikutano pamoja
na kujaza mistari miwili.
Sikuzote aliwajali ndugu na dada.
Alikuwa tayari kuwasaidia.
Yeye na mama
walikuwa wakaribishaji wageni.
Alikuwa anapenda kuwaalika nyumbani
wanafunzi wake wa Biblia,
ndugu na dada,
na angeingia jikoni na kufunga mlango,
aweke muziki,
na kuwapikia chakula kizuri.
Alipanga mambo
ili yawe yenye kufurahisha,
alipenda binti zake wafurahie maisha,
na hasa familia nzima ikiwa pamoja.
Alimpa kila mmoja wetu mahitaji yake
na pia yale yaliyotufurahisha.
Baba
alitupeleka matembezi mwisho-juma
baada ya mikutano
na pia baada ya mahubiri.
Alikuwa mtu wa pekee sana
na baba mzuri.
Ninakumbuka vizuri
siku hiyo, sisi tulikuwa ndani ya nyumba.
Alikuwa amerudi.
Alipokuwa akiegesha gari,
wanaume fulani walimfuata
na kumtisha.
Mama alikuwepo.
Walikuwa na
bunduki kubwa
na walimwambia
atoke kwenye gari
ili wamteke.
Tulisikia makelele.
Tulishtuka sana,
basi tukakimbia nje.
Basi tulipotoka nje, tulimwona baba
akiwa amelala chini,
watu hao walikuwa wamempiga risasi.
Walimwacha hapo.
Nilimwinua na kumkumbatia.
Alipelekwa hospitali,
na baada ya saa chache, alikufa.
Maneno yake ya mwisho yalikuwa:
“Yehova,
walinde binti zangu
na kipenzi changu”—
yaani, mama yangu.
Mama yetu,
alikuwa imara.
Alitusaidia
tuwe imara pia.
Aliendelea na ratiba ileile ya kiroho.
Siku moja baada ya kifo cha baba,
kulikuwa na mkutano,
dada yangu Raquel
alikuwa na hotuba.
Na ingawa Raquel alikuwa amepoteza
baba yake siku moja kabla,
alitoa mgao wake siku hiyo.
Na pia juma lililofuata
hatukukosa kusanyiko la mzunguko.
Sote
tuliazimia kufuata mfano
ambao baba
alituwekea.
Ingawa maisha hayakuwa rahisi,
tulimpa Yehova nafasi ya kwanza,
katika maamuzi yote tuliyofanya.
Tulipotaka kufanya uamuzi,
kwanza, tulimfikiria Yehova
na pia jinsi baba alivyokuwa
mshikamanifu kwake.
Niliendelea na maisha
kana kwamba yuko hai,
na kuhakikisha sisi sote tuko katika kweli.
Mwanzoni, nilisali:
“Ninaomba ‘amani . . .
inayozidi uelewaji wote.’”
Na sasa
ninapokabili hali ngumu,
ninamwambia Yehova:
“Naomba
niendelee kuwa na amani.
Usiruhusu jaribu hili lininyime amani.”
Kisha Yehova mwenyewe huniimarisha.
Ninawapenda sana dada zangu.
Nami ninawaheshimu sana
kwa sababu wamekuwa
kama mama kwangu.
Watatu kati yao bado wanaishi Kolombia,
kwa hiyo tunawasiliana mara kwa mara
kupitia simu au Zoom.
Hivyo, wanaweza kujua
pia Mama anaendeleaje.
Baadhi ya ndugu zetu
ambao si Mashahidi
walitaka kuwachukua baadhi ya dada zangu
ili kuwalea mpaka watakapokuwa wakubwa.
Lakini hatukutaka kutenganishwa
kwa sababu tulijua
ikiwa baba angekuwepo
asingefurahishwa na hilo.
Alitaka tumtumikie Yehova
na kuingia ulimwengu mpya pamoja.
Hatukutaka kuziachilia jitihada zake
zote alizofanya maishani mwake
ziende na maji
kwa sababu tu hayupo pamoja nasi.
Baba alinifundisha mambo mengi
madogomadogo katika uumbaji
kumhusu Yehova,
naam,
ambayo yaliniwekea msingi wa
kumpenda Yehova.
Ingawa sikuelewa,
wakati huo,
kwamba mambo hayo
yangenisaidia kukua kiroho.
Hivyo huwa najiambia,
“Baba yangu aliniacha
kwa Baba mwingine,
ambaye ni Yehova.”
Na hilo limenisaidia nijisikie vizuri.
Maneno ya mwisho ya
baba
yalikuwa,
“Mke wangu, binti zangu, Yehova.”
Hivyo, ninatazamia
kwa hamu kumwambia:
“Ona! Hawa hapa.
Sote tuko hapa.”
Tumefika hapa!
Umetulea vizuri.
-