JW subtitle extractor

Mabinti wa Otalora: Jenga Imani Inayoweza Kustahimili Majanga

Video Other languages Share text Share link Show times

Nimezaliwa Kolombia.
Nina dada zangu watano.
Nilijifunza kweli nikiwa na umri mdogo
kupitia wazazi wangu.
Tulikuwa na utendaji mwingi wa kiroho.
Baba yangu hakuwa tu katika kweli;
bali alitumia kweli
hizo maishani mwake,
sikuzote alitufundisha kufanya hivyo pia.
Alihakikisha tunasoma andiko la siku
kila siku kabla ya kwenda shuleni.
Hilo lilikuwa muhimu.
Yaani, ni bora tuchelewe shule,
kuliko tukose kusoma andiko la siku.
Ingawa familia yetu ni kubwa,
sikuzote tulienda mikutano pamoja
na kujaza mistari miwili.
Sikuzote aliwajali ndugu na dada.
Alikuwa tayari kuwasaidia.
Yeye na mama
walikuwa wakaribishaji wageni.
Alikuwa anapenda kuwaalika nyumbani
wanafunzi wake wa Biblia,
ndugu na dada,
na angeingia jikoni na kufunga mlango,
aweke muziki,
na kuwapikia chakula kizuri.
Alipanga mambo
ili yawe yenye kufurahisha,
alipenda binti zake wafurahie maisha,
na hasa familia nzima ikiwa pamoja.
Alimpa kila mmoja wetu mahitaji yake
na pia yale yaliyotufurahisha.
Baba
alitupeleka matembezi mwisho-juma
baada ya mikutano
na pia baada ya mahubiri.
Alikuwa mtu wa pekee sana
na baba mzuri.
Ninakumbuka vizuri
siku hiyo, sisi tulikuwa ndani ya nyumba.
Alikuwa amerudi.
Alipokuwa akiegesha gari,
wanaume fulani walimfuata
na kumtisha.
Mama alikuwepo.
Walikuwa na
bunduki kubwa
na walimwambia
atoke kwenye gari
ili wamteke.
Tulisikia makelele.
Tulishtuka sana,
basi tukakimbia nje.
Basi tulipotoka nje, tulimwona baba
akiwa amelala chini,
watu hao walikuwa wamempiga risasi.
Walimwacha hapo.
Nilimwinua na kumkumbatia.
Alipelekwa hospitali,
na baada ya saa chache, alikufa.
Maneno yake ya mwisho yalikuwa:
“Yehova,
walinde binti zangu
na kipenzi changu”—
yaani, mama yangu.
Mama yetu,
alikuwa imara.
Alitusaidia
tuwe imara pia.
Aliendelea na ratiba ileile ya kiroho.
Siku moja baada ya kifo cha baba,
kulikuwa na mkutano,
dada yangu Raquel
alikuwa na hotuba.
Na ingawa Raquel alikuwa amepoteza
baba yake siku moja kabla,
alitoa mgao wake siku hiyo.
Na pia juma lililofuata
hatukukosa kusanyiko la mzunguko.
Sote
tuliazimia kufuata mfano
ambao baba
alituwekea.
Ingawa maisha hayakuwa rahisi,
tulimpa Yehova nafasi ya kwanza,
katika maamuzi yote tuliyofanya.
Tulipotaka kufanya uamuzi,
kwanza, tulimfikiria Yehova
na pia jinsi baba alivyokuwa
mshikamanifu kwake.
Niliendelea na maisha
kana kwamba yuko hai,
na kuhakikisha sisi sote tuko katika kweli.
Mwanzoni, nilisali:
“Ninaomba ‘amani . . .
inayozidi uelewaji wote.’”
Na sasa
ninapokabili hali ngumu,
ninamwambia Yehova:
“Naomba
niendelee kuwa na amani.
Usiruhusu jaribu hili lininyime amani.”
Kisha Yehova mwenyewe huniimarisha.
Ninawapenda sana dada zangu.
Nami ninawaheshimu sana
kwa sababu wamekuwa
kama mama kwangu.
Watatu kati yao bado wanaishi Kolombia,
kwa hiyo tunawasiliana mara kwa mara
kupitia simu au Zoom.
Hivyo, wanaweza kujua
pia Mama anaendeleaje.
Baadhi ya ndugu zetu
ambao si Mashahidi
walitaka kuwachukua baadhi ya dada zangu
ili kuwalea mpaka watakapokuwa wakubwa.
Lakini hatukutaka kutenganishwa
kwa sababu tulijua
ikiwa baba angekuwepo
asingefurahishwa na hilo.
Alitaka tumtumikie Yehova
na kuingia ulimwengu mpya pamoja.
Hatukutaka kuziachilia jitihada zake
zote alizofanya maishani mwake
ziende na maji
kwa sababu tu hayupo pamoja nasi.
Baba alinifundisha mambo mengi
madogomadogo katika uumbaji
kumhusu Yehova,
naam,
ambayo yaliniwekea msingi wa
kumpenda Yehova.
Ingawa sikuelewa,
wakati huo,
kwamba mambo hayo
yangenisaidia kukua kiroho.
Hivyo huwa najiambia,
“Baba yangu aliniacha
kwa Baba mwingine,
ambaye ni Yehova.”
Na hilo limenisaidia nijisikie vizuri.
Maneno ya mwisho ya
baba
yalikuwa,
“Mke wangu, binti zangu, Yehova.”
Hivyo, ninatazamia
kwa hamu kumwambia:
“Ona! Hawa hapa.
Sote tuko hapa.”
Tumefika hapa!
Umetulea vizuri.