JW subtitle extractor

Domenic Alessia: Kupata Tumaini Licha ya Kuwa na Ugonjwa wa Akili

Video Other languages Share text Share link Show times

Maisha yangu ya utotoni
yalikuwa ya kawaida tu.
Nilikuwa na wazazi wazuri
lakini nilihisi ninahitaji
kitu fulani ambacho
kilikuwa kinakosekana.
Sikuwa na furaha.
Nilipokuwa mdogo,
muziki ulinivutia sana.
Niliimba kwenye kwaya
na kushiriki mashindano mengi.
Nilipoimba nilifurahi watu waliponishangilia.
Nilianza kufikiri kwamba
ikiwa sitakuwa mwimbaji maarufu,
sitakuwa mtu mwenye furaha.
Kadiri nilivyoendelea kukua
nilihisi huzuni zaidi na zaidi.
Nilienda kumwona daktari
na nikagundulika nina ugonjwa
wa kushuka moyo sana.
Baada ya hapo,
nilifanya kila kitu kwa ajili ya muziki.
Nilikuwa na masomo ya kuimba.
Mwalimu wangu alinishauri
nijiunge na Chuo cha Sanaa cha Victoria.
Nilisisimka sana kupata
nafasi ya kuimba katika
majumba madogo ya maonyesho.
Na hivyo nilitunukiwa
Diploma katika Opera.
Hata baada ya hayo yote
bado nilihisi nimekosa kitu fulani.
Nilikuwa nimejisadikishia
akilini mwangu kwamba
ikiwa nitakuwa mashuhuri
nitakuwa na furaha.
Wakati huo huo
lilikubaliwa kujiunga na
Opera Australia.
Hilo ni jambo kubwa sana.
Nilizunguka sehemu mbalimbali
za dunia kama vile
Uswisi, Ugiriki, na Hong Kong.
Nikapata ugonjwa wa OCD
ambao ulinifanya nishindwe
kudhibiti mawazo na misukumo.
Akili yangu haikuwa imetulia.
Nilipenda kuimba
lakini wakati huo huo
nilikuwa nikitafuta kitu kingine
ambacho sikujua ni nini.
Hilo lilinilemea sana.
Niliacha opera.
Niliacha kila kitu.
Nilikaa tu nyumbani
nikila na kunywa ili nisife.
Sikuwa na kusudi la maisha.
Nilijiona sifai.
Niliacha kufanya kila kitu
nilichopenda kufanya kwa
miaka 10 hivi.
Mashahidi wa Yehova
walituletea magazeti kwa miaka mingi.
Niliyasoma.
Na niliona yalianza kunisaidia.
Nilikuwa mdogo baba alipojifunza
Biblia kwa mara ya kwanza.
Alinieleza tunaweza kuishi milele
na kwamba Yehova
ni Mungu anayetupenda.
Ilikuwa kama ni jambo
nililohitaji kujua
lakini sikutambua
uhitaji huo mara moja.
Ghafla tu siku moja
nilipokuwa nimeketi chumbani kwangu
nikajiambia, ‘Dom, unahitaji
kwenda kwenye mikutano.’
Nilijua Jumba la Ufalme lilipo
lakini nilikuwa mzito
sikupata ujasiri wa kwenda.
Hivyo nikasali kwa Yehova,
“Tafadhali usiruhusu ugonjwa
wangu wa akili
unizuia kufanya maendeleo ya kiroho.”
Muda mfupi baada ya hapo,
Ammm, nikaenda tu.
Na hapo ndipo nilipojiuliza:
‘Nilikuwa wapi?
Kwa nini nilikuwa ninasita?’
Na kadiri nilivyoenda kwenye mkutano
ndivyo nilivyozidi kupata afueni.
Nilibatizwa mwaka 2020.
Hiyo ndio siku bora
zaidi maishani mwangu.
Tangu nikiwa mdogo,
nilijua kuna kitu kinakosekana.
Sasa najua kitu hicho
ni kweli na pia
urafiki wangu pamoja na Yehova.
Ugonjwa wangu wa OCD
haunisumbui sana.
Hata nikiwa na siku mbaya
na kuhisi nimelemewa
ninapokumbuka nina ndugu na dada
wanaonipenda kutanikoni,
na jambo muhimu hata zaidi
Yehova ananipenda,
hilo linanisaidia kupata utulivu.
Ninapohubiri ninawafikiria
wengine zaidi kuliko kujifikiria
mwenyewe pamoja na matatizo yangu.
Dawa na ushauri nasaha hunisaidia.
Dawa hunisaidia kupata utulivu
zinasaidia tu kwa njia hiyo.
Lakini haziwezi kunipa tumaini
la kuwa na afya njema wakati ujao.
Sikuwahi kuwazia ningeweza
kuwa na furaha niliyo nayo sasa.
Laiti ningemwomba Yehova
msaada mapema zaidi
badala ya kujitafutia furaha mwenyewe.
Na sasa kwa mara ya kwanza
ninafurahia kikweli kuimba.