JW subtitle extractor

Utumishi wa Betheli—Sehemu Muhimu ya "Lolote Mnalofanya"

Video Other languages Share text Share link Show times

Kulingana na Isaya 60:17
Yehova alisema:
“Badala ya shaba
nitaleta dhahabu,
na badala ya chuma nitaleta fedha.”
Kwa kutumia maneno hayo,
Yehova aliahidi kwamba ubora wa
sehemu ya kidunia ya tengenezo lake
ungeongezeka hatua kwa hatua.
Kadiri ambavyo miaka imepita
ameboresha jinsi tunavyofanya
kazi yake kutia ndani
kazi muhimu sana
inayofanywa Betheli.
Kazi hii ya maana sana
inayofanywa Betheli inatimiza
mambo mawili muhimu:
inahakikisha chakula cha kiroho
kinapatikana kwa watu wengi iwezekanavyo
na inategemeza kazi ya kuhubiri
ulimwenguni pote.
Baraza Linaloongoza linaporekebisha
kazi zinazofanywa Betheli,
lengo limekuwa kuunga mkono mambo hayo.
Kadiri ambavyo miaka imepita
tumefanya marekebisho katika mbinu za
uchapishaji, matumizi ya teknolojia,
na mbinu za ujenzi,
na tukarahisisha jinsi kazi
inavyosimamiwa katika ofisi fulani za tawi,
kutaja machache tu.
Familia ya Betheli ulimwenguni pote
imeunga mkono mabadiliko hayo
kupatana na himizo linalopatikana
kwenye Wakolosai 3:23:
“Lolote mnalofanya,
lifanyeni kwa nafsi yote kama kwa Yehova,
na si kwa wanadamu.”
Wengi wametumikia Betheli
kwa miaka mingi sana
na wamejionea mabadiliko hayo
moja kwa moja.
Kama Yehova, tunawathamini sana
wale wanaojitoa kwa hiari
kwa ajili ya utumishi mtakatifu.
Wana roho ile ile kama ya nabii Isaya
ambaye alisema:
“Mimi hapa! Nitume mimi!”
Ulimwenguni pote,
idadi ya ndugu vijana
wanaoomba kutumikia Betheli inaongezeka.
Wakati huo huo sikuzote
kuna uhitaji wa ndugu na dada
waliozoezwa na wakomavu kiroho
kutumikia shambani.
Baada ya kupitia upya mahitaji ya Betheli
na ya shamba la ulimwenguni pote,
Baraza Linaloongoza limeamua kufanya
mabadiliko kuhusu maoni yetu
ya utumishi wa Betheli.
Kuanzia sasa,
utumishi wa Betheli hautaonwa
tena kuwa mgao ambao
mtu anatumikia maisha yote.
Betheli itaendelea kuwa sehemu
ambapo watu wanakuja
kumtumikia Yehova kwa bidii
na kupokea mazoezi yanayoweza
kutumiwa na tengenezo lake.
Hata hivyo, sasa mkazo utakuwa
kwa ndugu na dada kutumia
mazoezi hayo shambani
au popote ambapo tengenezo
la Yehova linawahitaji zaidi.
Ili hilo liwezekane,
tunafurahi kuwajulisha kuhusu
mabadiliko fulani ambayo
yatakuwa yakifanywa hapa Betheli.
Kwanza,
tutakuwa na kawaida ya kuhamisha
wafanyakazi kutoka shambani
kuja Betheli
na kutoka Betheli
kwenda shambani.
Kama tulivyotaja awali,
kutumikiwa Betheli hakutaonwa tena
kuwa mgao wa kudumu.
Kwa hiyo ingawa sikuzote
kutakuwa na uhitaji wa wenye umri mkubwa
wenye uzoefu wa kuzoeza
kizazi kinachofuata cha Wanabetheli,
wengi wanaokuja Betheli
watatumikia kwa muda
wapate mazoezi, wajipatie uzoefu muhimu,
wazoeze wengine,
kisha wakatumie mazoezi hayo shambani.
Kutakuwa na pindi zilizoamuliwa
mapema katika utumishi wa Mwanabetheli
ambapo tutachanganua mazoezi ambayo
tayari amepata, yanafaa kutumiwa wapi.
Kuna faida gani kwa tengenezo
kuhamisha wafanyakazi hivyo?
Tunakualika usikilize tafadhali
mahojiano yafuatayo.
Mazoezi hapa Betheli
pamoja na mgao wangu
yamenifundisha kuwa na busara.
Kufanya kazi na ndugu na dada
wakomavu ambao wana uzoefu na
ambao wanamtegemea Yehova,
ni jambo ambalo lilinisaidia
nikiwa mzee mpya kutanikoni,
kujifunza jinsi ya kuendelea kumtegemea
Yehova katika mgao wangu.
Na pia ukanisaidia kuona jinsi ya
kuwasaidia ndugu na dada wengine
kama tu nilipokuwa Betheli.
Mwanzoni tulipopewa mgao mpya
tulianza kusoma vitabu vya Injili tena
kuanzia mwanzo.
Na kwa kweli hicho ndicho nilichohitaji.
Kusikia maneno hayo yakikazia
kwamba Yehova anatupenda
na kwamba mabadiliko hayo
yalikuwa tu sehemu ya kile
ambacho tengenezo linahitaji na
kwa kushirikiana na mabadiliko hayo,
tungeendelea kuwa na baraka za
Yehova hata katika mgao wetu mpya.
Unapokuwa Betheli unapata nafasi ya
kukutana na watu wengi sana.
Unaanzisha urafiki na watu ambao
mnafanya kazi nao,
kuna wageni wengi wanaokuja kutembea,
na kwa njia hiyo unaweza kujionea
tengenezwa kwa ujumla kuliko
ikiwa ungekaa tu kutanikoni.
Na kwa njia hiyo unathamini
ya kwamba una familia kubwa,
undugu wa ulimwenguni pote.
Sasa ninaweza kuwasimulia
ndugu na dada katika kutaniko langu jipya,
kuhusu mambo, nilijionea,
na kuwachochea waone kwamba
hata wao wenyewe wanaweza
kufanya mengi zaidi
kwa ajili ya Yehova.
Kuna tengenezo kubwa sana
nyuma yetu ambalo linatutegemeza.
Na huo ni wonyesho wa
upendo wa Yehova kwamba anatujali.
Na basi tunaweza kuwaeleza wengine
mambo yote hayo mazuri
ambayo tumejionea.
Kama mifano hiyo inavyoonyesha wazi,
hata ikiwa Betheli si mgao wa maisha,
ni mgao unaobadili maisha.
Je, hilo linamaanisha kwamba
kila mtu ambaye sasa yuko Betheli,
hatimaye lazima atahamishiwa shambani?
Hapana.
Sikuzote kutakuwa na uhitaji
wa kuwa na wenye umri
mkubwa na vijana pia.
Kama Methali 20:29 inavyosema:
“Utukufu wa vijana ni nguvu zao,
na fahari ya wazee ni mvi zao.”
Mnara wa Mlinzi la Machi 15, 1993
lilizungumzia mstari huo:
“Nguvu za ujana
zinapounganishwa na ujuzi na hekima
ya miaka, muunganisho wenye nguvu
sana unafanyizwa.
Maneno haya yamethibitika kuwa
kweli hapa Betheli.
Hali ya kiroho yenye kina
na makumi ya miaka ya uzoefu ya
wenye umri mkubwa ni muhimu.
Lakini huenda ukajiuliza,
‘Ikiwa kutakuwa na
uhamisho wa kawaida Betheli,
akina ndugu watafauluje kuendelea
kutimiza kazi muhimu inayofanywa huko?’
Hilo linatuleta kwenye badiliko la pili.
Mkazo mkubwa sasa utawekwa
kwenye kuharakisha mazoezi.
Tunataka kuwasaidia ndugu na dada
wapate ustadi unaohitajika kutumikia
katika migao mbalimbali upesi zaidi.
Mazoezi hayo yanatia ndani
kuwakabidhi ndugu vijana
mapendeleo ya usimamizi mapema.
Ndugu wenye umri mkubwa
watawasaidia na kuwazoeza vijana
wakiwasaidia kuchukua majukumu
ya usimamizi na ya uangalizi Betheli.
Mazoezi haya yatawasaidia wawe
na thamani Betheli.
Yatawaandaa watumiwe kujazia mahitaji
ya wakati ujao ya tengenezo.
Na yatajenga ndani yao sifa
na ustadi ambao
utakuwa muhimu sana
katika ulimwengu mpya.
Ofisi za tawi zimenufaikaje
tayari kwa kutumia miongozo hii?
Tafadhali sikiliza kwa makini
maelezo yafuatayo.
Kasi na ubora wa mazoezi
inaendelea kuboreshwa.
Badala ya kumzoeza kila mtu
kwa njia ile ile
tunachochewa kufikiria vizuri zaidi
kuhusu utu wa mtu,
uwezo wake, na ustadi wa kila ndugu.
Na pia kuchunguza ni wapi
anahitaji msaada.
Kwa hiyo badala tu ya kuzoeza
kwa ujumla, mazoezi yanakuwa na lengo.
Na basi tunaweka msingi wa
mtu kufanikiwa.
Nilipokuwa kijana,
sidhani nilipata mazoezi mengi.
Nilipata migao lakini sikupata mazoezi.
Tengenezo linakua.
Kwa hiyo mazoezi ni muhimu.
Na inapendeza kuona yakiharakishwa
ili kazi itimizwe.
Tengenezo linanufaika sana
kwa kuwazoeza na kuwakabidhi
ndugu vijana mapendeleo.
Tumeona kwamba akina ndugu vijana
wanaleta nguvu na mawazo mapya.
Wakati huo huo wenye umri mkubwa
wakiwapa hekima na uzoefu.
Unapounganishwa mambo hayo,
hivyo ndivyo tengenezo linaweza
kuendelea kukua na kukabiliana
na changamoto mpya.
Badiliko muhimu la tatu,
litahusu jinsi tunavyowaratibu
wajitoleaji wengi sana
ambao wako tayari kupanua
utumishi wao wa Kitheokrasi.
Tutakazia zaidi kuwatumia
kwa hekima na kwa njia inayofaa
wajitoleaji wanaoishi nyumbani
na pia wanaofanyia kazi wakiwa
nyumbani na pia wa muda.
Hilo linamaanisha kuamua
ni watu wangapi wanaofaa
kuwa Betheli ili wengi zaidi
waweze kutumia nguvu zao
katika kazi muhimu sana ya kuhubiri.
Kuna faida nyingi sana za kufanya hivyo.
Fikiria mifano ifuatayo.
Imekuwa wazi kwamba utumishi wa Betheli
hautegemei uko wapi.
Ni aina ya utumishi,
utumishi mtakatifu ambao unaweza
kutolewa mtu akiwa popote duniani.
Nilienda Betheli nilipokuwa na miaka 19.
nikakaa huko kwa muda nikatoka,
nikafunga ndoa, nikawa na familia,
na sasa miaka kadhaa baadaye,
ninatumikia tena Betheli.
Ninafanyia kazi nikiwa nyumbani.
Si kila siku. Lakini ninaendelea
kuona manufaa ya kazi hiyo
na jinsi inavyoboresha.
Ninaendelea kupata mazoezi
ni kama ninachungulia dirishani
na kuona jinsi Yehova
anavyoongoza tengenezo lake.
Lazima tunyumbulike.
Tunaacha kuzingatia mambo
kama vile ratiba au
mahali ambapo mtu yupo.
Na basi tunakuwa wabunifu
na hivyo tunatokea mbinu
zinazoweza kumsaidia mtu
anayefanyia kazi nyumbani
atusaidie kazi hapa.
Unaweza kuwa unaishi katika eneo
ambapo muda unatofautiana
lakini wanakuhusisha katika mazungumzo.
Na hivyo wanakufanya unajihisi unaaminiwa.
Wewe ni sehemu ya timu.
Mara nyingi hatuwezi kuchagua timu yetu,
lakini Yehova anaandaa ndugu na dada
wenye kupendeza sana.
Wenye ustadi mwingi, wanaotusaidia.
Tunapofungua akili zetu kuona njia mbali mbali
za kutimiza kazi yetu
tumegundua kwamba tunaweza kupunguza
idadi ya wafanyakazi Betheli
na bado tufanye kazi yenye ubora wa
hali ya juu katika idara yetu.
Ikiwa unafanya kazi ya muda Betheli
ni muhimu sana kwa kutaniko lako
kuelewa jinsi hilo linavyoathiri ratiba yako.
Tayari tumekuwa tukifanya kazi na
ofisi za tawi ulimwenguni pote ili
kutekeleza mabadiliko haya hatua kwa hatua.
Na tayari tumejionea matokeo mazuri sana.
Washiriki wa Halmashauri za Tawi
wameona kuna idadi kubwa zaidi
ya nafasi kwa ajili ya ndugu na dada
kupokea mazoezi Betheli.
Vivyo hivyo mbinu hii mpya
imewasisimua na kuwachochea vijana
ya kufikia mapendeleo na kupanua
utumishi wao wa Kitheokrasi.
Mbali na hilo,
Halmashauri za Tawi zinaripoti kwamba
wale ambao wamepelekwa shambani
wanatimiza mengi sana katika kazi
ya kuhubiri ulimwenguni pote.
Wengi wamepanua utumishi wao
na wakawa tayari kusaidia
mahali ambapo kuna mahitaji ya pekee.
Kwa mfano, katika utendaji wa
usanifu-majengo na ujenzi,
Halmashauri za Uhusiano na Hospitali,
na mahubiri ya hadharani
katika miji mikubwa.
Wengine wamehamia katika maeneo
ambako kuna uhitaji mkubwa wa
wahubiri wa Ufalme,
wakahudhuria Shule ya Waeneza-injili
wa Ufalme, na mengi zaidi.
Mabadiliko haya matatu yatawasaidia
ndugu na dada wengi zaidi kunufaika
kutokana na mazoezi na uzoefu
unaopatwa kupitia utumishi wa Betheli.
Halafu wao wanaweza kutumia
mazoezi hayo kuendeleza
masilahi ya Ufalme.
Waefeso 4:16 inafafanua
jinsi mwili Wakristo unavyounganishwa
na kushirikiana na unafanya kazi vizuri
kwa sababu ya utendaji kazi
wa kila kiungo.
Tunatumaini kwamba
mabadiliko haya yatatusaidia
sisi sote kuendelea kufanya kazi
pamoja kwa ushirikiano
na kuendelea kujitiisha
kwa ukichwa wa Kristo
kwa roho ya upendo.
Ndugu vijana tunawahimiza
msali na kufikiria
ikiwa sasa ndio wakati wa kufikia
na kuanza utumishi wa Betheli.
Wakati wa hotuba ya kuweka wakfu
jengo jipya katika Betheli ya Brooklyn
mwaka wa 1960,
Ndugu Frederick Franz,
aliyekuwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza,
alifafanua Betheli kuwa taasisi bora zaidi
ya elimu duniani pote.
Zaidi ya miaka 65 baadaye,
bado tunakubaliana kabisa
na maneno hayo.
Kutumikia Betheli
ni nafasi ya pekee ya kupokea
mazoezi yenye thamani
mazoezi ambayo yatakusaidia wewe
na tengenezo kwa miaka mingi ijayo,
na hata katika ulimwengu mpya.
Wazazi, wasaidieni watoto wenu
wajiwekee mradi wa kutumikia Betheli
ili waweze kujipatia
mazoezi hayo yenye thamani.
Hiyo ni njia moja ya kuwasaidia
wamtumikie Yehova kwa bidii
katika lolote wanalofanya.
Kwa wale ambao tayari wameanza
kufanyia kazi nje ya Betheli,
tafadhali hakikishweni kwamba
tunawapenda na kuwathamini.
Mambo mnayojionea Betheli ni zawadi
mwe wakarimu kwa kuwagawia
wengine zawadi hiyo.
Watie moyo ndugu na dada zako
wamtumikie Yehova kwa moyo wote
katika lolote wanalofanya
ili wao pia wajionee baraka
ambazo umefurahia.
Mfano wako mzuri
utadumu mioyoni mwao.
Wale unaowatia moyo
hawatawahi sahau upendo unaoonyesha.
Kupatana na Isaya 60:17,
tuna uhakika kwamba Yehova
ataendelea kuboresha mipango inayofanywa
hapa Betheli ili kushughulikia
mahitaji ya tengenezo lake.
Pia tuna uhakika kwamba
upendo na ujitoaji wetu kwa Yehova
na tengenezo lake utatuchochea sote
tumtumikie Yehova kwa moyo wote
katika lolote tunalofanya
sasa na hata wakati ujao.