JW subtitle extractor

David Schafer: Msimamo wa Kikristo wa Kutounga Mkono Upande Wowote—Unamaanisha Nini, Kwa Nini Tunaamua Kufanya Hivyo?

Video Other languages Share text Share link Show times

Kichwa cha mwezi huu ni
“Msimamo wa Kikristo wa Kutounga
Mkono Upande Wowote
—Unamaanisha Nini?
Kwa Nini Tunaamua Kufanya Hivyo?”
Una maoni gani?
Una msimamo gani?
Je, mtu mmoja anaweza kukomesha ukosefu wa haki?
Tunaposikia watu wakizungumzia siasa,
huenda mwanzoni tukafikiri wanazungumzia dhana fulani tu;
lakini mpendwa wetu anapotendewa isivyo haki,
tunaathiriwa kibinafsi.
Tunajua kwamba watu wataendelea
kuwa na maoni tofauti ya kisiasa.
Ufunuo sura ya 8 hadi 13
ilitabiri kwamba katika siku za mwisho,
watu wangependezwa sana na serikali
na wangeshinikizwa kuchukua msimamo.
Kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza,
Ninatendaje watu wanapozungumzia
kuhusu suluhisho la ukosefu wa haki?
Tukiwa Wakristo tungependa kuiga mfano wa Kristo.
Yesu alikuwa na uwezo mkubwa wa
kukabiliana na ukosefu wa haki.
Aliwasikitikia sana watu.
Aliwalisha wenye njaa,
aliwaponya wagonjwa,
aliwafufua wafu,
na kuwachochea watu kwa maneno yake.
Mambo hayo yote yangemfanya awe
na ushawishi mkubwa wa kisiasa.
Kwa kweli alikuwa na nafasi ya kufanya hivyo.
Shetani alitaka kumpa “falme zote za dunia inayokaliwa”
kwa kubadilishana na tendo moja la ibada.
Lakini Yesu alikataa.
Hata hivyo, hakusema Shetani hana
uwezo wa kutoa mamlaka hiyo.
Baadaye, Wayahudi walijaribu
kumfanya Yesu awe mfalme,
lakini alikataa katakata.
Pindi nyingine,
mtu fulani alimuuliza kama ni halali
kulipa kodi kwa serikali ya Roma.
Yesu hakuunga mkono upande wowote.
Alikataa kuwa mtawala wa kidunia,
kiongozi wa taifa,
au mwanaharakati wa kisiasa.
Je, inamaanisha Yesu hakujali?
kwamba hakuwa na maoni yoyote?
La hasha!
Yesu aliwajali sana watu kuliko tunavyoweza kuelewa.
Kwa kutowabagua watu,
Yesu alionyesha maana halisi ya haki.
Hata hivyo, alikazia fikira kuwafundisha watu kuhusu Ufalme wa Mungu,
ambao ungeondoa ukosefu wote wa haki.
Basi Yesu alisema tunapaswa kuwa na mtazamo
gani kuelekea serikali za kibinadamu?
Tunajifunza kutokana na jibu la Yesu
kuhusu kulipa kodi ya serikali ya Roma
kama tunavyosoma kwenye Marko 12:15-17:
“‘Nileteeni dinari niitazame.’
Wakaleta dinari moja, akawauliza:
‘Sura hii na maandishi haya ni ya nani?’
Wakajibu: ‘Ni ya Kaisari.’
Ndipo Yesu akasema:
‘Mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari,
na Mungu vitu vya Mungu.’”
Vitu vya Kaisari ni nini?
Kwenye Waroma Waroma 13:1-7,
mtume Paulo anataja kodi,
ushuru,
woga,
na heshima.
Vilevile, ona kwamba Yesu alisema
“mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari.”
Hilo linamaanisha nini?
Kwamba Kaisari,
yaani, mamlaka iliyokuwa ikitawala wakati huo
ilikuwa imetengeneza vitu vyenye thamani
—kama vile sarafu.
Kwa hiyo, Kaisari alikuwa na haki ya
kuomba arudishiwe baadhi ya sarafu hizo.
Hilo liliiwezesha serikali kuendelea
kutoa huduma muhimu.
Yesu alitambua jambo hilo.
Kwa upande mwingine,
mali zetu zenye thamani zaidi ni zawadi
tunazopokea kutoka kwa Mungu
—kwa mfano moyo wetu,
uhai wetu,
akili yetu,
na nguvu zetu.
Hatuwezi kumpa Kaisari vitu hivyo
kwa sababu si Kaisari aliyetupatia vitu hivyo.
Tunampatia Mungu vitu hivyo tunapojiweka
wakfu kwake na kumpenda.
Lakini kuhusu upendo wetu kwa Mungu,
Yesu alisema hivi kwenye Marko 12:30:
“Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote
na kwa nafsi yako yote
na kwa akili yako yote
na kwa nguvu zako zote.”
Basi tunampa Mungu upendo kamili
—kila kiungo cha mwili,
hakuna sehemu ya mwili,
utendaji,
uwezo,
au tamaa yoyote inayobaki.
Wale wanaompenda Mungu wana mtazamo kama wa Yesu,
ambaye Yehova amemchagua awe Mfalme.
Lakini wanafunzi wa Yesu
wangeuteteaje Ufalme wake ikiwa
watu wangeupinga?
Tunapata jibu kupitia mambo yaliyotokea usiku
wa mwisho wa maisha ya Yesu duniani.
Kumbuka kwamba kwenye Mathayo sura ya 26
“umati mkubwa [wenye] mapanga na marungu”
ulipokuja kumkamata Yesu,
Petro “a[li]uchomoa upanga wake,
akampiga mtumwa wa kuhani mkuu na kumkata sikio.”
Yohana anasema kwamba jina la mtumwa
huyo lilikuwa Malko.
Luka anaongezea kwamba Yesu aligusa
sikio la mtu huyo na kumponya.
Wazia jambo hilo!
Yesu hakuwakasirikia watu hao waliotaka kumkamata.
Isitoshe, kulingana na Mathayo 26:52,
Yesu alimwambia Petro:
“Rudisha upanga wako mahali pake,
kwa maana wote wanaochukua upanga
wataangamia kwa upanga.”
Kwa nini Yesu hakufurahishwa na kitendo cha Petro?
Alichochewa na sababu ileile
iliyomfanya aepuke siasa.
Yesu alieleza jambo hilo baadaye alipokuwa
mbele ya Pontio Pilato usiku huo.
Tunasoma hivi kwenye Yohana 18:36:
“Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.”
Naam, kwa kuwa Ufalme wa Yesu
hautokani na wanadamu,
hauhitaji ulinzi wa kibinadamu.
Tunawezaje kuwa na hakika Yesu alimaanisha hivyo?
Tazama kwa makini sehemu inayobaki ya Yohana 18:36:
“Kama Ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu,
watumishi wangu wangenipigania ili nisitiwe
mikononi mwa Wayahudi.
Lakini, kama ilivyo, Ufalme wangu
hautoki katika chanzo hiki.”
Basi, tukiwa Wakristo tuna msimaamo gani kuhusu siasa?
Hatuungi mkono upande wowote.
Mara nyingi watu hawaelewi mtazamo huo.
Baadhi yao wanafikiri kwamba kwa sababu
hatuungi mkono serikali moja ya kibinadamu
basi tunaunga mkono serikali nyingine ya kibinadamu.
Miaka ya 1950, katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,
wenye mamlaka walisingizia kwamba
Mashahidi wa Yehova walikuwa Wakomunisti.
Lakini miaka ya 1970,
nchi ya Kongo ilipokubali utawala wa Kikomunisti,
serikali hiyo mpya ilikasirishwa nasi kwa sababu hatukuwa Wakomunisti!
Leo, kwa karibu miaka 30,
Mashahidi wa Yehova wametambuliwa
kisheria katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Ingawa baadhi ya watu wanaona msimamo
wetu wa kutounga mkono kuwa ni kutojali,
wengine wanafikiri sisi ni wapinzani.
Acheni tuzungumzie maoni hayo mawili.
Kwanza kuna tofauti kubwa kati ya msimamo wa Kikristo
wa kutounga mkono siasa na kutojali.
Kutojali
ni “kutopendezwa na jambo wala kuhangaishwa nalo.”
Kwa kweli tunapendezwa na watu,
na tunajali hisia zao.
Kama Yesu,
tunajaribu kuwapunguzia watu mateso yao
kwa kuwasaidia kwa njia halisi
huku tukiwafundisha kuhusu Ufalme pekee
unaoweza kuondoa kabisa ukosefu wa haki.
Tunapowafundisha watu kwa kutumia Neno la Mungu,
tunajitahidi kubadili mioyo yao,
si mashirika ya kisiasa.
Tunaamini mtazamo huo unafaa kwa sababu
matatizo yanayowakabili wanadamu
si ya kisiasa bali yanahusu maadili.
Lakini kwa nini tunaweza kusema kwamba
Mashahidi wa Yehova si wapinzani,
bali wanatoa msaada?
Tunafuata sheria kwa makini,
tunaunga mkono jamii kupitia kazi ya kujitolea
au kwa kushiriki utumishi wa kiraia katika maeneo
yaliyo na mpango huo,
na tunalipa kodi.
Ni kweli kwamba hatupigii kura
vyama vya kisiasa wala wagombeaji,
na hatuvurugi uchaguzi wala kuwaingilia
wale wanaoamua kupiga kura.
Ni kweli kwamba hatupendekezi sera za kisiasa,
hatufanyi kampeni,
hatugombei cheo cha kisiasa,
na hatuwaingilii wenye mamlaka
au kudharau sera zao,
wala hatufanyi maandamao ya
kuleta mabadiliko ya kisiasa.
Ni kweli kwamba hatusalimu bendera,
na hatuwezi kuchoma bendera
au kuitemea mate,
au kudharau nchi inayowakilishwa na bendera hiyo
—hata katika nchi ambazo mambo
hayo hayajakatazwa kisheria.
Ni kweli kwamba hatuimbi nyimbo za taifa,
na hatuwazuii wengine wasiimbe,
wala hatujaribu kuonyesha kila mtu kwamba hatuimbi;
tunaepuka tu kushiriki.
Ni kweli kwamba hatuui watu vitani,
wala hatuwashambulii nyumbani kwao.
Basi ingawa hatuungi mkono upande wowote kisiasa,
hatupingi msimamo wowote wa kisiasa
—hata moyoni mwetu.
Hiyo ndiyo maana ya kutounga mkono upande wowote.
Hatujihusishi na siasa.
Lakini,
namna gani matakwa ya serikali
yakipingana na amri za Yesu?
Biblia inatoa kanuni kuhusu hilo.
Labda unafikiria jambo linalotajwa
kwenye Matendo 5:28, 29
—kwamba “Lazima tumtii Mungu kuwa
mtawala badala ya wanadamu”?
Hilo halimaanishi kwamba tunadharau serikali,
badala yake, tunamheshimu sana Mungu.
Serikali ikituamuru tufanye jambo
ambalo Mungu anakataza
au ikituamuru tusifanye jambo ambalo
Mungu anataka tufanye,
basi tutachagua kumtii Mungu.
Huenda mtu akasema,
‘Katika hali fulani, uamuzi huo
unaweza kutuletea matatizo.’
Yesu alitabiri ingekuwa hivyo kwenye Mathayo 24:9,
aliposema:
“Mtachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.”
Kwenye Ufunuo 2:10,
Yesu alitaja kihususa kwamba baadhi ya
wanafunzi wake wangetupwa gerezani
—sio sisi sote bali baadhi yetu.
Basi hatutavunjika moyo ikiwa hatutatupwa gerezani,
wala hatutavunjika moyo tukifungwa gerezani.
Tunawakumbuka maelfu ya ndugu na dada zetu
ambao wamefungwa gerezani
kwa sababu ya msimamo wao wa Kikristo
wa kutounga mkono upande wowote.
Tunawapenda sana.
Tunasali kwa ajili yao.
Tunajua kwamba Yehova anawapenda.
Uvumilivu wao chini ya majaribu
ni ushindi kwetu sote.
Jinsi gani?
Paulo aliandikia hivi kutaniko la Efeso:
“Ninawaomba msife moyo kwa sababu ya dhiki
zangu kwa ajili yenu,
kwa maana zinamaanisha utukufu kwenu.”
Paulo alipoandika maneno hayo
alikuwa katika kifungo cha nyumbani huko Roma.
Ni kwa njia gani dhiki za Paulo zilimaanisha
“utukufu” kwa Waefeso?
Ni kwa sababu uvumilivu wake katika
kuhudumu licha ya majaribu
ulionyesha kutaniko hilo kwamba mapendeleo
waliyokuwa nayo wakiwa Wakristo
yalikuwa muhimu zaidi.
Ikiwa Paulo angekata tamaa,
hilo lingemaanisha nini?
Kwamba imani yao, huduma yao,
na tumaini lao katika Ufalme wa Mungu
hayakuwa mambo yenye thamani yoyote.
Badala yake,
uvumilivu wa Paulo ulionyesha thamani ya Ukristo.
Ulionyesha kwamba tunapaswa kujidhabihu chochote
ili kuendelea kuwa waaminifu.
Vivyo hivyo,
uvumilivu wa ndugu na dada zetu wapendwa walio gerezani
unathibitisha kwamba tumaini lao liko hai
na kwamba Ufalme wanaotangaza ni halisi.
Wao ni wajumbe,
si wa serikali za kibinadamu,
bali wa Ufalme wa mbinguni
—Ufalme ambao utawapatia
thawabu ya uzima wa milele
katika ulimwengu usio na vita.