JW subtitle extractor

Kutounga Mkono Upande Wowote Katika Mawazo na Matendo

Video Other languages Share text Share link Show times

“Wao si sehemu ya ulimwengu.”
Yohana 17:16.
“Tunapaswa kudumisha
msimamo wetu wa Kikristo
ili tuwe raia washikamanifu
wa Ufalme wa Mungu.
Vinginevyo,
tungewezaje kuwa na dhamiri safi
tunapowahubiria watu habari njema
kwamba Ufalme wa Mungu pekee
ndio unaoweza kusuluhisha
matatizo ya wanadamu?”
Sasa wanafunzi tuangalie video.
Dan, na Jordan,
mnaweza kufunga pazia tafadhali?
Katika kazi ya vikundi vyenu,
mtaeleza sera mnazofikiri kwamba
serikali za ulimwengu
zinapaswa kuzifuata.
Kumbukeni,
ninyi vijana, yaani, kila mmoja wenu,
ndiye anayepaswa kuchukua hatua
ili kusuluhisha matatizo yanayotishia
kuharibu sayari yetu.
Hatutaki vita, tunataka amani
Hatutaki vita, tunataka amani
Hatutaki vita, tunataka amani
Vita vikitokea,
watatuchukua mimi na
wewe twende tukapigane.
Uko tayari kuwaambia,
‘La, hatutaenda?’
Hatutaki vita
Lakini nina wasiwasi na uchaguzi,
hasa kwa kizazi chenu.
Unafikiri ni nani
atashinda uchaguzi huu?
Aaah, tunaamini kwamba
Eeeh .
Umeuliza swali zuri sana.
Tukiwa Mashahidi wa Yehova,
tunaamini kwamba Ufalme wa Mungu
ndio utakaoleta suluhisho kwa
matatizo yote tunayokabili.
Kwa mfano, .
Ni elfu 3,000, tafadhali.
Asante.
Karibu, unahitaji nini?
Unajua, hii sera mpya ya serikali
nafikiri itafanikiwa.
La hasha.
Kwa sera hizo,
tutafilisika baada
ya miaka mitatu tu.
Lakini ikifanikiwa,
watu watatajirika.
Itawatajirisha matajiri tu.
Wamenichosha.
Kila kiongozi anaahidi hivyo
Tunakaribisha jopo la wataalamu
kuzungumzia jambo hili,
mnafikiri, chama cha upinzani
kinaweza kushinda?
Je, watatimiza ahadi zao
kwa watu wenye kipato cha chini?
Na tunaweza kutarajia mabadiliko gani
kuhusiana na utumishi
wa lazima wa kijeshi?
Natumaini ungependa kujua.
Acha tuanze kuzungumza na
John McGarthy, waziri wa elimu.
Utimilifu wangu ukijaribiwa,
ningependa kuwa
mtimilifu kwa Yehova.
Lakini matokeo ya mambo haya
yataniathiri mimi
familia yangu,
na malengo yangu.
Ninawezaje kutounga
mkono upande wowote
kutoka moyoni?
Yohana 17
Mstari wa 14
“Nimewapa neno lako,
lakini ulimwengu umewachukia,
kwa sababu wao si
sehemu ya ulimwengu,
kama vile ambavyo mimi
si sehemu ya ulimwengu.
Sikuombi uwatoe ulimwenguni,
bali uwalinde kwa
sababu ya yule mwovu.
Wao si sehemu ya ulimwengu,
kama vile ambavyo mimi
si sehemu ya ulimwengu.
Watakase kupitia ile kweli;
neno lako ni kweli.
Kama ulivyonituma ulimwenguni,
mimi pia nimewatuma ulimwenguni.
Nami ninajitakasa kwa ajili yao,
ili wao pia watakaswe kupitia ile kweli.”
Si sehemu ya ulimwengu,
kama Yesu,
katika mawazo na matendo.
Haya mambo mazuri
yatatokea maishani mwetu?
Ndiyo!
Kuna andiko fulani
ambalo limenisaidia
kuwa na uhakika huo.
Mathayo 24:33.
Yesu alisema:
“Vivyo hivyo,
ninyi pia mtakapoona
mambo yote hayo,
jueni kwamba yuko
karibu milangoni.”