JW subtitle extractor

Masomo Kutoka kwa Mnara wa Mlinzi—Usiunge Mkono Upande Wowote Katika Ulimwengu Huu Uliogawanyika

Video Other languages Share text Share link Show times

Nikiwa profesa wa fedha,
ninahitaji kuwa na habari kamili.
Na kama Wakristo wote,
ninahitaji kuwa na habari kamili pia.
Ni vigumu kuepuka kuunga
mkono upande wowote.
Ni vigumu sana kwa
sababu tunajua hali zilivyo.
Tangu nilipokuwa mdogo,
nilipenda sana kucheza mpira.
Niliishi katika eneo lenye umaskini,
na mpira ndio uliotufurahisha.
Nilipenda kusoma habari ambazo
mwanahabari fulani aliandika.
Angeandika kuhusu mambo mazuri
na mabaya ya vyama vyote vya kisiasa.
Lakini alipoandika tu kuhusu
mambo mabaya ya chama fulani,
sikufurahishwa na jambo hilo.
Ninaishi katikati ya jiji.
Hapo ndipo maandamano makubwa zaidi
ya kisiasa hufanyiwa.
Watu wanaoishi hapa
wanapenda sana siasa.
Wana msimamo mkali sana.
Na ingawa sikuzote nilijua kwamba lazima
tuepuke kuunga mkono upande wowote,
moyoni niliunga mkono maandamano hayo.
Kwa nje, sikuwa nikiruka-ruka
au kushangilia,
lakini kwa ndani nilikuwa
nikisema: ‘Jamani!
Afadhali tushinde!’
Nilitamani ushindi,
msisimko wa umati,
na fahari ya kuona
timu yangu ikijizolea ushindi
na nishani nyingi.
Nilizoea kujitetea kwa kusema:
“Niliumbwa kwa mfano wa Yehova,
naye ni Mungu wa haki.”
Kilichonisukuma ni hisia
zangu za kupenda haki.
Niliepuka kuunga mkono upande wowote
kupitia matendo yangu,
lakini si hisia zangu.
Mnara wa Aprili 2016
una habari yenye kuvutia kuhusu
kutounga mkono upande wowote.
Hilo linamaanisha kwamba
unaepuka kujiona kuwa
bora kuliko wengine,
“watu wote ni sawa machoni pa Mungu.”
Baada ya kujifunza makala hiyo,
nilitambua kwamba nilihitaji
kufanya mabadiliko;
Hivyo, nilisoma makala hiyo tena.
Nilisali kwa Yehova
nikamwambia kwamba
nilijua kuwa anazungumza nami.
Gazeti hilo lilinigusa sana.
Nakumbuka nikisoma makala hiyo
angalau mara tatu jioni hiyo.
Nilishangaa sana.
Nilitambua kwamba
nilihitaji kufanya mabadiliko makubwa
sana ili nimpendeze Mungu.
Jambo la pili lililotajwa kwenye
makala hiyo lilihusiana na habari
na vyombo vya habari.
Makala hiyo hata ilipendekeza
tupunguze muda tunaotumia
kutazama habari za siasa.
Kuna sentensi nyingine
ambayo ilinigusa sana.
Ilisema:
‘Ingawa hatujiungi na wengine
katika maandamano,
je, moyoni tuko pamoja nao?’
Ndio!
Niliwaunga mkono.
Kuna sentensi kadhaa
kwenye makala hiyo
ambazo ziliandikwa
kihususa kwa ajili yangu.
Nilipoacha kutazama
habari nyingi za kisiasa,
hilo lilinisaidia kuwa na sifa ya
kujizuia nilipozungumza na wengine kazini.
Wafanyakazi wenzangu walipotaja jambo
fulani lililotajwa kwenye habari,
sikuwa na la kuchangia kwa
kuwa sikuwa nimelisikia.
Mfanyakazi mwenzangu angesema:
“Je, uliona mtu fulani alisema hivi
na mtu fulani alitoa maelezo haya?”
Ningesema: “Hapana, sikuona,”
na huo ungekuwa mwisho
wa mazungumzo hayo.
Makala hiyo inataja Waroma 10:12
kwamba Yehova ni ‘Bwana juu yetu sote,
na kwamba hakuna tofauti kati ya
Myahudi na Mgiriki.’
Machoni pa Yehova,
si jambo muhimu ikiwa
nchi yangu imeshinda
au ilikuwa ya mwisho
katika Kombe la Dunia.
Watu wote ni sawa machoni pake.
Nilichukua karatasi ndogo tu
na kuandika mambo manne ya msingi
ambayo makala hiyo ilizungumzia
—mambo manne ya msingi
yatakayotusaidia kuepuka
kuunga mkono upande wowote.
Mimi huiweka kwenye pochi langu;
hivyo ninaweza kuyasoma wakati wowote
nikiwa kazini.
Napenda kutazama mpira;
unachangamsha.
Bado mimi hutazama
mpira kwenye televisheni.
Bado mimi hucheza mpira
pamoja na rafiki zangu hapa Betheli,
lakini nimejitahidi kubadilika.
Pole kwa pole,
nimefaulu kuwa na maoni
yanayofaa kuhusu mpira.
Hilo limenisaidia kuepuka
kuathiriwa na kiburi
na roho ya utaifa.
Makala hii imenifundisha kuepuka
kutoa maoni kuhusu mambo ya kisiasa.
Na lazima hilo litoke
ndani kabisa ya moyo wangu.
Ikiwa nimesadiki kabisa kwamba
Ufalme wa Mungu ndio suluhisho
bora la mambo yote,
itakuwa rahisi kuepuka
kuunga mkono upande wowote.
Lazima niendelee kuwa macho.
Ninafurahia kujifunza makala
za Mnara wa Mlinzi,
hasa zinazozungumzia mambo ya
kutumia kila siku.
Zinanisaidia kuiona Biblia kuwa
kama kioo ili nijirekebishe.
Kutumia ushauri wa makala hizo na
kufanya marekebisho
kumenisaidia kuzungumza kwa usadikisho
kwamba ni Ufalme tu
unaoweza kutatua matatizo ya wanadamu.