JW subtitle extractor

Kujitolea kwa Ajili ya Utumishi wa Betheli

Video Other languages Share text Share link Show times

Inatia moyo sana kuona mamilioni
wakichukua msimamo upande
wa ibada ya kweli!
Na maelfu ya watu wanajiunga
nasi kila juma.
Yehova anaharakisha
kazi ya kuwakusanya,
na hilo hutufanya tuwe na furaha sana.
Lakini ni nani watakaofanya kazi
ya kuchapisha Biblia,
machapisho ya Biblia,
kutayarisha rekodi za kusikiliza na video
ambazo hutuimarisha kiroho
na kutusaidia kutimiza kazi yetu
ya kuhubiri Ufalme na kufundisha?
Betheli ni mahali pa pekee.
Ni mahali ambapo Wakristo wakomavu
humtolea Yehova utumishi mtakatifu
wakishirikiana kwa ukaribu
na baadhi ya Wakristo watiwa mafuta.
Wanashughulikia mahitaji
ya ndugu ulimwenguni pote
na kutegemeza kazi ya kuhubiri.
Familia ya Betheli ni kikundi
cha watumishi wa Yehova
waliojiweka wakfu na kubatizwa,
wanaoishi na kufanya kazi pamoja.
Hivyo, wanajionea kwa njia ya pekee
utimizo wa Zaburi 133:1 inayosema:
“Tazama! Jinsi ilivyo vema
na jinsi inavyopendeza
ndugu kukaa pamoja kwa umoja!”
Tunafurahi sana kuona wengi
wamepanua utumishi wao kwa Yehova
kwa kuwa tayari kujiunga na utumishi
huo wa pekee wa Betheli
Je, umefikiria kutumikia Betheli?
Kujitolea kwa ajili ya
utumishi wa Betheli
ni kama kubisha mlango
unaotuongoza kupata mapendeleo
mengine mengi ya utumishi.
Bila shaka, ili kutumikia Betheli,
unahitaji roho ya kujidhabihu
na kuwa tayari kutumikia mahali
popote penye uhitaji.
Huo ndio mtazamo aliokuwa
nao nabii Isaya
kama unavyoonyeshwa katika Isaya 6:8:
“Kisha nikasikia sauti ya Yehova ikiuliza:
‘Nimtume nani,
na ni nani atakayeenda kwa ajili yetu?’
Nami nikasema: ‘Mimi hapa!
Nitume mimi!’”
Isaya alipotambua kwamba kuna nafasi
ya kufanya mengi katika utumishi wa Yehova,
alifurahi kujitolea,
ingawa hakujua kihususa
mgawo ambao angepewa.
Isaya aliridhika kujua kwamba mwaliko huo
wa kutumikia kwa njia ya pekee
ulitoka kwa Yehova,
naye alitaka kujitolea.
Roho hiyo ndiyo inayoonyeshwa
na washiriki wa familia ya
Betheli ulimwenguni pote.
Ni nini hasa kinachowachochea
wengi watumikie Betheli?
Upendo kwa Yehova unatuchochea
kutanguliza masilahi ya Ufalme
badala ya masilahi yetu.
Kama kitabu Wapiga-Mbiu
ukurasa wa 295 kinavyosema:
“Hiyo si kazi ambayo wao hujipatia
umashuhuri wa kibinafsi
au mali za kimwili.
Tamaa yao ni kumheshimu Yehova,
na wanaridhika na upaji wanaopewa
kama vile chakula, malazi,
na rudishio la fedha la kiasi
kwa ajili ya matumizi ya kibinafsi.”
Kuna thawabu zozote za kutumikia
kwa njia hii ya pekee?
Wale ambao wamejitoa kwa hiari
katika utumishi wa Betheli
wamepata baraka nyingi.
Upendo na umoja uliopo hapa
hauwezi kulinganishwa
na kitu chochote.
Si kama kampuni za kilimwengu,
kwa sababu hapa unaweza
kufanya kazi
na marafiki wako kila siku.
Unahisi watu wote hapa
wana mtazamo uleule,
wana malengo yanayofanana,
na wanategemezana.
Unaweza kupangiwa ufanye
kazi ambayo hujawahi kuifanya,
lakini kuna ndugu na dada wengi
wenye uzoefu ambao wanaijua,
nao wanaweza
kukusaidia sana kuielewa.
Tunaburudishwa sana
tunapochunguza andiko la siku,
Funzo la Mnara wa Mlinzi
la familia ya Betheli,
au kusikiliza maelezo yanayofaa
na yenye thamani ya ndugu na dada zetu.
Unahisi kwamba kwa kweli
wanampenda Yehova,
na maelezo yao yanakufanya
umpende Yehova zaidi.
Hapa Betheli, tuna Mwajiri
bora zaidi, yaani, Yehova.
Hakuna mwajiri mwenye shukrani
na ufikirio kama yeye,
hivyo kwa sababu unampenda Yehova,
unafurahia kumtumikia kwa moyo wote.
Ninasisimuka sana
ninapofikiria kazi zote
zinazotimizwa Betheli
kutokeza machapisho na kuyasafirisha,
kuandaa video za makusanyiko,
na kutafsiri katika lugha nyingi.
Hata niwe ninafanya kazi gani hapa,
kujua kwamba
ninawategemeza ndugu za Kristo
kunanifanya nihisi vizuri sana.
Hivyo, kijana anahitaji kufanya nini
ili astahili kutumikia Betheli?
Wazazi wangu walinifundisha
nikazie uangalifu mambo ya kiroho.
Hivyo, wakati wa likizo
na kadiri nilivyokua,
maisha yetu yalihusisha sana kuhubiri
pamoja na kushiriki
utendaji wa kiroho.
Hilo lilisaidia familia yetu
ikazie uangalifu mambo ya kiroho
na kunisaidia kukazia
uangalifu malengo niliyotaka kufikia.
Ninapenda sana kusoma,
siku moja Baba aliniambia,
“Kwa nini usisome Biblia?”
Ingawa ni jambo linalotazamiwa,
lakini kufikia wakati huo,
sikuwahi kusoma Biblia yote
kuanzia Mwanzo hadi Ufunuo.
Hivyo, nilipomaliza kusoma Biblia yote,
njia yangu ya kufikiri ilibadilika
na ilinithibitishia
kwamba hii ndiyo kweli.
Hicho ndicho kilichonisaidia
kuzingatia uhusiano wangu na Yehova,
na hiyo ilikuwa hatua ya kwanza
ya kufikia mapendeleo
na malengo ya kiroho niliyojiwekea.
Kutanikoni, nilifanya kazi
ya kugawa magazeti,
kusaidia katika mfumo wa sauti,
na kupanga utaratibu wa jukwaa
wakati wa mikutano.
Na mapendeleo hayo yalinisaidia
kuwa na mazoea
mazuri ya kufanya kazi
na kulinipa nafasi ya kufanya
mengi zaidi kwa Yehova.
Wazee walikuwa wakihubiri
pamoja nami mara nyingi.
Nilipokuwa nahisi kwamba
‘Siwezi kuendelea’
au ‘Haya ni mambo mengi sana’
au ‘Nimelemewa sana’
au ‘Sitaweza kamwe kufikia lengo hili,’
mzee fulani alinionyesha andiko
ambalo Yehova alimtia
moyo Yoshua awe jasiri;
na ushauri huo ulikuwa na
matokeo mazuri sana kwangu
hivi kwamba niliweza kuwa jasiri
kuendelea kufuatilia lengo
langu la kutumikia Betheli.
Nilipotembelea Betheli,
niliona kwamba walikuwa
watu wa kawaida kama mimi
lakini wenye sifa nyingi sana nzuri
ambazo nilitaka kuiga,
walikuwa wakarimu
sana na wenye urafiki.
Hilo lilinichochea hata zaidi
kujitahidi kufikia lengo langu
ili niwe kama wao.
Ili kutumikia Betheli
kuna matakwa unayohitaji kutimiza.
Unapaswa kumpenda sana Yehova
na tengenezo lake,
jambo linaloonyeshwa kwa kuishi
kulingana na viwango vya Biblia.
Unapaswa kujulikana
kuwa na sifa nzuri
ya kuwa mtu wa kiroho.
Unapaswa kuheshimu viwango
vya maadili vya Yehova,
kuepuka uchafu na maadili mapotovu.
Unapaswa kuwa na dhamiri
safi mbele za Yehova
na amani ya akili
kwa sababu hujawaficha
wazee habari zozote.
Unapaswa kuwa mfano mzuri
katika mavazi na mapambo,
kutia ndani muda unaostarehe,
unapaswa kuonekana
kuwa mhudumu Mkristo.
Wanabetheli hawapaswi
kufuata mitindo,
kuvaa mavazi yaliyopita kiasi,
au yanayotuhusianisha na
mwenendo usiofaa ulimwenguni.
Mwanabetheli hapaswi kusoma, kusikiliza,
au kutazama vitu ambavyo
havimfai Mkristo.
Vitu hivyo vinatia ndani ponografia,
muziki usiofaa,
au burudani yoyote inayohusisha
maadili mapotovu,
kuwasiliana na roho waovu, au jeuri.
Wanaoomba kutumikia Betheli
wanapaswa kuwa na umri wa miaka
kati ya 19 na 35.
Pindi fulani, Betheli inawaalika
watu wenye umri wa miaka zaidi ya 35
ambao wana ustadi
wa pekee unaohitajika,
kama vile wataalamu wa kiteknolojia
au matibabu, watafsiri,
au wataalamu wa ujenzi
kama vile mafundi-bomba, umeme,
wataalamu wa kutengeneza mashine kubwa,
au maseremala.
Wote wenye uwezo na ustadi
wa kufanya kazi hizo
wanaalikwa wajaze fomu.
Kwa sababu ya ratiba yenye
mambo mengi ya Betheli,
unapaswa kuwa na afya nzuri
ya kiakili na kihisia,
unapaswa kuwa na nguvu,
na uwezo wa kufanya kazi
kwa saa nyingi.
Unapaswa kujua kusoma, kuandika,
na kuzungumza lugha kuu
inayotumiwa katika eneo
la ofisi yenu ya tawi.
Hilo litafanya iwe rahisi
kuwasiliana vizuri na wengine
wanaotumikia Betheli,
kupata mazoezi unayohitaji,
na kufanya kazi kwa usalama ukiwa Betheli.
Wanaoalikwa Betheli
wanakubali kufanya kazi
kwa muda usiopungua mwaka mmoja,
wakati huo wanapata mazoezi
yatakayowasaidia kuendelea
kutumikia Betheli.
Inapohusu ustadi wa kazi,
hatupendekezi mtu apate
elimu ya chuo kikuu
akiwa na wazo kwamba
kufanya hivyo
kutaboresha uwezekano
wa kuitwa Betheli.
Njia bora ya kujitayarisha kwa ajili ya
utumishi wa Betheli ni kuwa painia.
Wanaohitajika hasa ni ndugu waseja.
Hata hivyo, wengine
wenye sifa za kustahili,
kutia ndani akina dada,
wanatiwa moyo wajaze fomu
ya kutumikia wakiwa
wajitoleaji wa muda.
Kutumikia Betheli ukiwa
mjitoleaji wa muda
kunaweza kufungua nafasi nyingine
za kupanua utumishi
wako kwa Yehova.
Ikiwa ungependa kujaza
fomu ya kutumikia Betheli,
unahitaji kumwomba mshiriki wa
Halmashauri ya Utumishi
ya Kutaniko fomu gani?
Kwa kuwa kuna aina mbili za
maombi unayoweza kujaza,
sali na ufikirie hali
zako kwa uangalifu.
Baada ya hapo, amua
ni fomu gani utakayojaza,
ama Ombi la Kuwa Mjitoleaji (A-19),
ambayo inaweza kujazwa
na wale ambao
wangependa kutumikia
kwa muda mfupi
kama vile kwa juma moja
au kwa miezi kadhaa.
Au unaweza kuamua kujaza fomu ya
Ombi la Kuwa Mshiriki wa Kikundi
cha Ulimwenguni Pote
cha Watumishi wa Pekee wa Wakati
wote cha Mashahidi wa Yehova (A-8).
Fomu hii ni kwa ajili ya wale
wanaopenda kutumikia kwa muda mrefu
kama vile kwa mwaka mmoja au zaidi.
Ikiwa Halmashauri ya Tawi
inaamua kwamba wanakuhitaji,
itaamua eneo ambalo utatumikia,
ama Betheli ama labda
katika mgawo wa ujenzi.
Kutuma fomu yako ya maombi
kunaweza kufungua nafasi
za kumtumikia Yehova
na tengenezo lake katika njia mbalimbali.
Kwa kweli, si kila mtu anayetamani
kutumikia Betheli
ambaye hali zake zinamruhusu
kujiunga na utumishi huo.
Lakini, tunaweza kuwatia moyo
wale ambao hali zao zinawaruhusu.
Wazazi, igeni mfano wa wazazi
waliomwogopa Mungu
kama vile Hana na Elkana,
ambao walimtoa kwa hiari mtoto wao
ili amtumikie Yehova katika
utumishi wa pekee.
Endelea kuwatia moyo watoto wako
wafikie lengo la kutumikia Betheli,
na uwachochee wawe na tamaa ya
utumishi wa wakati wote
kupitia mfano na maneno yako.
Ikiwezekana, fanya mipango
ya kuwatembeza
kwenye makao makuu
yaliyoko New York, Marekani,
au Betheli iliyo katika eneo lenu.
Matembezi hayo
yatawasaidia vijana
kujionea kazi zinazofanywa Betheli
ambazo zinategemeza
masilahi ya Ufalme.
Wazee, wasaidieni vijana walio
katika makutaniko yenu
wanaoweza kupanua
utumishi wao kwa Yehova
ili waweze kustahili kutumikia Betheli.
Yehova anaendelea kuwatafuta
wale walio tayari kukubali mwaliko
wa kupanua utumishi wao.
Kama katika siku za Isaya,
Yehova aliuliza hivi:
“Nimtume nani, na ni nani
atakayeenda kwa ajili yetu?”
Je, utajibu kama
alivyojibu nabii Isaya:
“Mimi hapa!
Nitume mimi!”?
Tunakutia moyo ufanye
maendeleo ya kiroho
na umtumikie Yehova
kwa nafsi yote.
Baada ya muda huenda
ukastahili kutumikia Betheli
au katika utumishi mwingine
wa pekee ambao utakupa nafasi
ya kutumia kwa ukamili zaidi
afya na nguvu ulizopewa na Yehova,
kwa ajili ya utukufu Wake.
Uwe na uhakika kwamba tunakupenda
kwa sababu ya
roho ya utayari unayoonyesha
unapoendelea kujitahidi kupanua
utumishi wako kwa Yehova