JW subtitle extractor

Dale and Nadja Bode: Yehova Alitusaidia Kulea Watoto Tisa Jijini Alaska

Video Other languages Share text Share link Show times

Tulikuwa tunatumikia katika
mji mdogo huko Alberta,
na kisha tulianza kupata watoto.
Tulipohamia Craig
tulikuwa na watoto wanne.
Kwa sasa tuna watoto tisa.
Kulea watoto wanaompenda
Yehova ni daraka
na kwa hiyo ukiwa mzazi
unapaswa kutafuta kwanza Ufalme,
kuwawekea mfano mzuri,
kuhudhuria mikutano
na kushiriki utumishi kwa ukawaida.
Tuliamini kwamba tulihitaji
kumpenda Yehova kwanza
ili tuwe mfano mzuri
kwa watoto wetu.
Wazazi walitusaidia
kutambua kwamba
kumtumikia Yehova
kutafanya tuwe na furaha.
Wazazi wetu walitufundisha
kutafuta kwanza Ufalme
si kwa maneno tu
bali hasa kwa matendo.
Si rahisi kulea watoto tisa.
Ukiwa na watoto wengi,
huenda ukahisi, hiyo ni sababu
ya kutohudhuria mikutano.
Ni vigumu sana
kulea watoto tisa.
Kuna wakati mama
alikuwa akikaa kwenye kiti
na ukimwangalia
unaona amechoka sana.
Ninakumbuka siku moja
ilikuwa siku ya mikutano lakini
nilikuwa nimechoka sana.
Nilifikiria andiko la Isaya 40,
ambalo linasema kwamba
“wale wanaomtumaini Yehova
watapata nguvu tena.”
Hivyo, nilitambua kwamba
Yehova anataka niende mikutanoni.
Atanipatia nguvu ili niweze kuhudhuria.
Kwa hiyo, nilisali na kujitayarisha.
Si rahisi.
Andiko la Waebrania linatuhimiza
tusiache kamwe “kukutana pamoja.”
Sikuzote baba alitukumbusha
maneno hayo.
Kuna wakati tulisafiri
kwa muda wa saa mbili hivi,
ili tuweze kufika mkutanoni
kwa sababu kilikuwa ni kipindi
cha baridi kali.
Tulirudi nyumbani usiku sana;
watoto wote walikuwa wamechoka
na hata sisi pia.
Kwa kuwa wazazi wetu
walithamini sana mikutano,
nilitambua kwamba
sipaswi kuipuuza.
Wazazi wetu walisisitiza sana
tushiriki kwa ukawaida
katika utumishi wa shambani
kama tu tunavyohudhuria
mikutano kwa ukawaida.
Tulifanya hivyo.
Hatungekataa kwenda kuhubiri.
Tulipoamka Jumamosi asubuhi,
tulijiandaa kwa ajili ya kwenda kuhubiri.
Hatungekaa tu kwenye gari
tukiwasubiri wazazi.
Tulijua kwamba tulienda
ili tuhubiri.
Tangu tukiwa wadogo,
tuliiga mfano wa wazazi wetu
wa kupendezwa na wengine.
Kwa sababu hiyo,
tulifurahia kwenda kuhubiri.
Nilienda utumishi nikiwa na kusudi.
Nilikuwa na ziara za kurudia.
Nilijitayarisha mapema
na hivyo nilijua habari
nitakayozungumzia.
Tulipokuwa tukihubiri,
tulihitaji kupumzika
mara kwa mara
kwa ajili ya watoto
na sisi wenyewe.
Tulikuwa na usawaziko
na tulibadilika kulingana na hali
ili watoto wetu wafurahie utumishi.
Ninafikiria andiko la Methali 22:6
ambalo linasema
“Mzoeze mvulana njia anayopaswa kuifuata.”
Walituzoeza kwa kutanguliza
utumishi wa Yehova
badala ya vitu vya kimwili.
Yehova alitusaidia kuwa
wazazi bora kadiri tuwezavyo.
Nyakati fulani tulikosea,
lakini sikuzote nilijua kwamba
Yehova ndiye Mzazi bora.
Hivyo, tukiwafundisha
wampende Yehova,
yeye atawasaidia
waendelee kumkaribia.
Tulifanikiwa tukiwa familia
kwa sababu tulimruhusu Yehova
aongoze maisha yetu.
Watoto wetu wote
wanaendelea kumtumikia Yehova.
Jambo hilo linatupa shangwe sana
na nina uhakika kwamba
linamfurahisha Yehova.