JW subtitle extractor

Mark Noumair: Tunaweza Kuvumilia Kama Ayubu (Rom. 15:4)

Video Other languages Share text Share link Show times

Leo, tutapenda kujifunza somo
kutokana na kitabu cha Ayubu.
Na somo ndilo hili:
Licha ya kwamba Mungu
amemruhusu
“Ibilisi kuwa mtawala wa ulimwengu,”
kitabu cha Ayubu kinatupa uhakika
kwamba Yehova
ndiye mwenye mamlaka kuu.
Nasi tunapokuwa na uhakika
kwamba ana mamlaka kuu,
tunaweza kuvumilia.
Kwa kweli, Yehova anarejelewa
kuwa Mweza-Yote mara 32
katika kitabu cha Ayubu
mara nyingi kuliko
vitabu vingine vyote vya Biblia.
Biblia haituelezi tu
kuhusu simulizi la Ayubu
inatueleza pia
kuhusu mambo ambayo
“hayakuonekana,”
ambayo mwanadamu hawezi kuona.
Yanayotendeka mbinguni
na kutufundisha masomo muhimu
kuhusu ukuu wa Yehova.
Tuchunguze kwa undani
fungua Biblia yako
kwenye Ayubu sura 1.
Ayubu sura ya 1
tuanze kusoma mstari wa 6
“Basi siku ilifika
ambayo wana wa Mungu wa kweli
waliingia na kusimama mbele za Yehova,
Shetani pia akaingia kati yao.”
Shetani alikuwepo hapo kwa sababu tu
ya kuruhusiwa na Yehova.
Yehova alimvumilia Shetani
ili suala fulani kuu liweze kutatuliwa.
Lakini tunahitaji kukumbuka kwamba
Yehova akiwa mwenye enzi kuu
ya ulimwengu wote
hakutishwa na uwepo wa Shetani
Yehova aliendelea kuwa na mamlaka
ndie aliyekuwa akiongoza mambo
na mamlaka yake kuu haikuwa hatarini,
kama tunavyoona
katika mstari unaofuata wa 7
“Ndipo Yehova akamuuliza Shetani:
Umetoka wapi?
Yehova ndiye anayeongoza mazungumzo.
Yehova anauliza maswali.
Shetani ndiye anayejibu.
Anadhibiti mambo.
Na Yehova alijua jibu la swali hilo,
Umetoka wapi?
Lakini kwa kumruhusu
Shetani azungumze,
alimpa Ibilisi nafasi ya
kuwafunulia wengine wote
jambo ambalo tayari Yehova alijua
kwamba alikuwa akizurura duniani
na hakuwa na nia nzuri.
Sasa tusome mstari wa 8
tuone Yehova anafanya nini.
Anaendelea kudhibiti mambo
na anaanza kumminya Shetani,
mistari wa 8:
“Yehova akamwambia shetani:
‘Je, umemwona mtumishi wangu Ayubu?’”
au kama maelezo ya chini yanavyosema:
Je, “umeuweka moyo wako juu ya” Ayubu?
Anamlazimisha shetani ajifunue.
Anajua kinachoendelea
lakini Shetani kama mwoga
hata hakuwa ameanza
kuzungumza kumuhusu Ayubu.
Yehova ndiye aliyeanzisha dai hilo,
akijua kwamba Shetani
alikuwa akifikiria jambo hilo muda wote.
hapa tunamwona Yehova
akisoma mawazo ya ndani kabisa
ya moyo wa Shetani.
Ni kama anasema tu: ‘Yafichue.
Fichua.’
Na basi akafichua.
katika mstari wa 10,
“Shetani anasema:
‘Umeweka ukuta wa ulinzi
kumzunguka yeye
na umebariki kazi ya mikono yake.’
Ni kweli
na huwezi kufanya chochote.
ukweli wa kwamba Shetani
hangeweza kuondoa
ukuta huo wa ulinzi
unatuonyesha kwamba yeye ni duni
na Yehova ni Mkuu.
Na kwa kweli Yehova ana haki
ya kulinda maslahi ya watumishi wake,
naye hutumia nguvu zake
kufanya hivyo.
Katika bustani ya Edeni
Adamu na hawa walipotenda dhambi,
Yehova alifanya nini?
Alichukua hatua mara moja
kulinda bustani hiyo
aliweka makerubi wawili
walinde mti wa uzima.
Shetani asingeweza
kufanya chochote kuhusu hilo.
Na wakati wa gharika ya siku za Noa,
aliwafagilia mbali wanefili.
Raia wa kidunia wa Shetani
na Shetani asingeweza kuzuia hilo,
hilo linakazia tena
ukuu wa Yehova Mungu.
Basi katika sura ya 1:11,
Shetani sasa anasema:
“Nyoosha mkono wako
upige kila kitu alichonacho.”
Eti Shetani anamtaka Yehova
anyooshe mkono wake ampige Ayubu?
Yehova hawezi kufanya hivyo.
Yehova anadumisha mamlaka yake
na hawezi kujishusha
eti kuwe na mjadala.
Hakubali kupewa maagizo na Ibilisi,
wala hawaumizi watu wake.
Lakini anamruhusu Shetani
amjaribu Ayubu kwa kiwango fulani.
Tunaona hilo katika
mstari wa 12.
Lakini ona jinsi ambavyo
Yehova anavyodumisha ukuu wake.
Mstari wa 12
anamruhusu Shetani amtese Ayubu
kwa kiwango fulani lakini anasema
“Ila tu usimguse mwanamume huyo!”
Hilo linaonyesha
alimwekea Shetani mipaka fulani,
na Shetani alitii
kuonyesha wazi kwamba
mamlaka yake ina mipaka hususa.
Yehova anaonyesha wazi
mamlaka ya Shetani ni ya uwongo,
hana nguvu.
Na jambo ambalo Shetani
anatamani zaidi
ndilo hatawahi kulipata kamwe,
na hilo ni
siku zote hapa duniani
kutakuwa na mtu anayeshikamana
na ibada ya kweli.
Basi katika sura ya 1,
hapo tumeona,
Shetani anathibitika kuwa duni
na mamlaka Yehova ni ya wazi
na sasa katika sura ya 2,
tunaona sehemu ya pili au
kusanyiko lingine
na kwenye mstari wa 1,
Shetani anahudhuria tena
lakini ona tena mstari wa 6,
anapotaka kwa mara nyingine
kumshtaki Ayubu
kuwa yeye si mshikamanifu.
Katika mstari wa 6, Yehova anasema:
“Tazama! yumo mkononi mwako!
Ila tu usiondoe uhai wake!”
Kwa mara nyingine tena
Shetani anatambua hana nguvu.
Yehova anamwekea mipaka,
naye analazimika kufuata.
Alifuata sheria.
Hilo tena linaonyesha
Yehova ni Mweza-Yote
na hilo ndilo jambo kuu
la mazungumzo haya.
Tunaweza kuvumilia
kwa sababu tunajua kwamba
Yehova ndiye mwenye nguvu zote.
Sasa ona mamlaka kamili
kwenye sura ya 42,
mstari wa 10,
42:10.
Jaribu la Ayubu liliisha
baada ya miezi michache,
aliteseka
labda kwa karibu mwaka mmoja,
kisha jaribu likaisha.
Lakini
ona kinachotokea kwenye mstari wa 10:
Baada ya Ayubu kusali
kwa ajili ya rafiki zake,
Yehova akamwondolea Ayubu dhiki.
au akauondoa utekwa wake
kama maelezo ya chini yanavyosema.
Kwa hiyo, kwa mara nyingine tena
tunaona hapa Yehova
mara tu jaribu hilo
lipotimiza kusudi lake lilipotatuliwa
Yehova alisema imetosha!
akapiga nyundo chini kesi kwisha.
Halafu mara moja
Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote
akachukua hatua mara moja
kurudisha hali ilivyokuwa.
Alikuwa akimdhibiti Shetani
muda wote huo.
Kwa nini hilo ni muhimu?
kwa sababu kwa mara nyingine tena
kuelewa ukuu wa Yehova
kunatupatia uhakika
kwamba hataruhusu mfumo huu
uendelee kwa muda mrefu
kuliko inavyohitajika.
Kwa hiyo, tuunganishe mawazo yote
kupatana na Waroma 15:4.
Haya ndiyo mambo
ambayo yanatuimarisha tuvumilie
na yanatukumbusha majaribu yetu
hayatapita kiwango
tunachoweza kuvumilia.
Haya ndio mambo
yanayotukumbusha kwamba Yehova
ndiye mwenye udhibiti
na chochote anachoruhusu
kinapatana na kusudi lake
na kwamba Shetani
ni mtawala bandia tu.
Haya ndio mambo
ambayo yanatuthibitishia kwamba
Baba yetu wa mbinguni anatamani
kugeuza hali yetu ya utekwa.
Naam! Haya ndiyo mambo
‘yaliyoandikwa ili kutufundisha.’