JW subtitle extractor

Hermanus van Selm: Yehova Anatuhakikishia Baraka za Wakati Ujao (Ufu. 21:4-6)

Video Other languages Share text Share link Show times

Maelezo ya leo
yametaja baraka za Mungu
kwa wale watakaoishi katika
Paradiso inayokuja.
Tungependa kuchunguza maswali haya:
Yehova aliahidi baraka zipi?
Na kwa nini tunaweza kuwa na
uhakika kwamba zitatimia?
Kwanza, Yehova aliahidi nini?
Jibu linapatikana katika mstari wa Biblia
ulioonyeshwa mwishoni
mwa maelezo
katika Andiko la leo.
Sisi sote tunaupenda sana mstari huu.
Ni Ufunuo 21:4.
Mstari huo unasema:
“[Mungu] atafuta kila chozi
kutoka katika macho yao,
na kifo hakitakuwapo tena,
wala maombolezo
wala kilio
wala maumivu hayatakuwapo tena.
Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”
Baada ya kuwasomea
watu ahadi hii maridadi,
hasa wale tunaokutana
nao katika huduma,
mara nyingi wengi husema,
“Maneno haya hayawezi kutimia sasa.”
Ni kweli, kwamba Yehova alipomwongoza
Yohana aandike ahadi hii
kuhusu Paradiso,
Yehova alijua kwamba sisi
leo tungetumia maneno haya
katika kazi yetu ya kuhubiri.
Na bila shaka, Yehova alijua
ingekuwa vigumu sana kwa
watu wengi kuamini ahadi hii.
Basi hilo
linatuleta kwenye swali letu la pili:
Kwa nini tunaweza kuwa na
uhakika kamili kwamba
ahadi hizi zitatimia?
Yehova
hakutupatia tu ahadi yenyewe,
bali pia alitupatia sababu
kwa nini tunaweza kuiamini ahadi hiyo.
Basi, ni sababu zipi
ambazo Yehova alitoa
ambazo tunaweza kuwaeleza wengine
na kuwasaidia
waone kwamba ahadi
za Mungu ni kweli?
Sababu zenyewe zinapatikana katika
sura hiyohiyo ya Biblia
mstari wa 5 na 6.
Mistari hiyo inasema:
“Na Yule aliyeketi kwenye
kiti cha ufalme akasema:
‘Tazama!
Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’
Pia anasema:
‘Andika,
kwa maana maneno haya ni
ya uaminifu na ya kweli.’
Naye akaniambia:
‘Yametimia!
Mimi ndiye Alfa
na Omega,
mwanzo
na mwisho.’”
Kwa nini andiko hili la Biblia
linaimarisha imani yetu
katika ahadi za Mungu?
Kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu
kinasema hivi,
kinapoelezea mstari wa 5 na wa 6:
“Ni kana kwamba Yehova mwenyewe
alikuwa akitia saini ya dhamana,
au title didi katika
baraka hizi za wakati ujao
kwa ajili ya aina ya
binadamu yenye uaminifu.”
Hivyo, ahadi ya Mungu
inatajwa kwenye mstari wa 4.
Halafu,
kwenye mstari wa 5,
tunapata saini ya Yehova,
kwa njia ya mfano,
ili kutoa uhakikisho kwamba
ahadi yake ni ya kweli.
Basi, acheni tuchunguze
kwa uangalifu zaidi
maneno yanayotajwa kwenye
mstari wa 5.
Mstari huu unaanza kwa utangulizi:
“Yule aliyeketi kwenye
kiti cha ufalme akasema.”
Kwa nini sentensi hiyo ni ya kipekee?
Inatoa utangulizi
wa pindi moja
kati ya pindi tatu tu
katika kitabu chote cha Ufunuo
ambapo Yehova mwenyewe alizungumza
katika maono aliyopewa Yohana.
Basi, ukweli wa kwamba
uhakika huu unatolewa,
si na malaika mwenye nguvu,
wala si hata na Yesu aliyefufuliwa,
bali na Yehova mwenyewe
unatuhakikishia kwamba maneno yanayofuata
ni ya kuaminika.
Kwa nini tunasema hivyo?
Fikiria ulinganisho huo.
Tangazo zito sana linapohitaji kutolewa
iwe ni hapa Betheli
au kwenye kutaniko,
mzee
anayeheshimiwa sana na
familia ya Betheli
au
anayeheshimiwa na kutaniko
anaweza kuchaguliwa kutoa tangazo hilo.
Kwa nini?
Kwa sababu kuaminika kwa tangazo hilo
kunaongezea uzito
na sifa ya uaminifu wa mzee huyo
ambaye amepewa mgawo
wa kutoa tangazo hilo.
Vivyo hivyo, sifa ya Yehova
akiwa “Mungu ambaye
hawezi kusema uongo”
inafanya uhakikisho tunaosoma
kwenye mstari wa 5
uwe wenye kutegemeka kabisa.
Sehemu ya kwanza ya
uhakikisho huu inasema nini?
Yehova alisema:
“Tazama!
Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.”
Ona neno hilo,
“ninafanya.”
Kwa kuwa Yehova anazungumzia
mambo ya wakati ujao,
kwa nini hakusema:
“Nitafanya”?
Kwa sababu,
kwa Yehova,
ahadi hiyo ni hakika kabisa
kwamba itatimia
hivi kwamba anazungumzia
mabadiliko hayo
kana kwamba tayari yanatukia.
Ndiyo sababu anasema:
“Ninafanya,”
si
“Nitafanya.”
Tuone sehemu inayofuata
ya maneno hayo,
“Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.”
Kwenye Ufunuo sura ya 21,
maneno “ninafanya vitu vyote kuwa vipya”
yanarejelea mambo mawili
ambayo Yehova atafanya.
Tunaweza kuyafafanua kuwa
kubadili
na kurudisha upya.
Kwenye mstari wa 1,
tunasoma kuhusu kubadili:
“Mbingu ya kwanza
na dunia ya kwanza
zilikuwa zimepitilia mbali.”
Hapa, jambo ambalo Yehova anafanya
ni kuondoa kabisa vitu vya awali.
Atabadili mbingu ya sasa
na dunia ya sasa na
kuleta “mbingu mpya
na dunia mpya”—
yaani, aina mpya ya serikali
na jamii mpya
ya wanadamu.
Hata hivyo,
kwenye mstari wa 5,
anapozungumza kuhusu Paradiso,
Yehova hazungumzii kuhusu kubadili,
bali kuhusu kurudisha upya.
Kitabu kimoja cha Biblia
kinaonyesha kwamba ‘Yehova hakusema:
“Ninafanya vyote
viwe vitu vipya.”
Bali Mungu alisema:
“Ninafanya vitu vyote
kuwa vipya.”’
Kwa hiyo Mungu atafanya vitu vyote
vilivyopo viwe vipya
kwa kuvirudisha
viwe vikamilifu tena.
Ni nini kingine
kinachohakikishwa na Yehova?
Angalia sehemu ya mwisho ya mstari wa 5:
“Andika, kwa maana maneno haya
ni ya uaminifu na ya kweli.”
Yehova alimwamuru Yohana
kwa neno moja:
andika.
Yehova alimwambia Yohana
kwa nini anapaswa kuandika:
“[Maneno ya Mungu]
ni ya uaminifu na ya kweli.”
Bila shaka, tunaweza kuamini
maneno ya Mungu
kwa sababu ni sahihi
na yanategemeka.
Sisi leo, tunatii kwamba
Yohana alitii amri hiyo ya kuandika,
kwa sababu tunaweza kusoma na
kujifunza kitabu cha Ufunuo.
Sehemu inayofuata ya
uhakikisho wa Yehova ni nini?
Ona mstari wa 6:
“Yametimia!”—
yaani, sasa ni mambo halisi.
Yehova anazungumza na Yohana
kana kwamba mambo yote
yaliyotajwa kwenye mstari wa 4
tayari yametokea.
Na inafaa kwamba alisema hivyo,
kwa sababu hakuna kinachoweza
kumzuia Yehova kutimiza kusudi lake.
Maneno hayo yenye kusadikisha
yanatajwa pia katika sehemu inayofuata
ya uhakikisho wa Yehova:
“Mimi ndiye Alfa
na Omega.”
Kama tulivyotaja mapema,
katika kitabu cha Ufunuo,
Yehova mwenyewe alizungumza mara tatu
katika maono aliyompa Yohana.
Mara ya kwanza ni kwenye
Ufunuo 1:8,
21:5,
22:13.
Jambo lenye kupendeza,
kwenye kila moja ya pindi hizo,
Yehova alisema maneno yaleyale:
“Mimi ndiye Alfa
na Omega.”
Alfa
ni herufi ya kwanza katika
alfabeti ya Kigiriki,
na Omega ndiyo ya mwisho.
Kwa nini Yehova anajipatia
jina hilo la cheo?
Alfa
ndiyo inayoanza kwenye alfabeti,
nayo Omega inakamilisha alfabeti.
Vivyo hivyo,
Yehova anapoanza jambo fulani,
atahakikisha kwamba
analikamilisha kwa mafanikio.
Kwa mfano,
pale mwanzo,
kwenye bustani ya Edeni,
Yehova alisema kwamba kusudi lake
si kwamba tuwe watu wakamilifu
bali pia
wazao wakamilifu wa
Adamu na Hawa
wangeijaza dunia
na kuifanya yote iwe paradiso.
Ni kana kwamba,
wakati huo Yehova alisema:
“Alfa.”
Isitoshe, kama inavyosemwa
kwenye Mwanzo 2:3,
kufikia mwisho wa siku ya
pumziko ya Mungu,
kusudi lake la awali
kwa dunia na wanadamu
litakuwa limetimia.
Kufikia mwisho wa miaka elfu moja,
wazao wakamilifu wa Adamu na Hawa
wataimiliki dunia iliyo paradiso
kama tu Yehova alivyokuwa amesema.
Wakati huo, ni kana kwamba
Yehova atasema:
“Omega.”
Kwa hiyo, kwa kumalizia,
tunawezaje kuwahakikishia watu
ambao wana shaka
kuhusu ahadi
kwamba Paradiso itakuwa halisi?
Tunaweza kuwaambia mambo matatu
ambayo ni sehemu ya
uhakikisho wa Yehova.
Kwanza,
Yehova mwenyewe ametoa ahadi.
Naye ana hekima
na anatamani jambo hilo litimie.
Pili,
kutimia kwa ahadi yake
ni hakika sana
hivi kwamba kwa maoni Yehova,
ni kana kwamba tayari imetimia.
Tatu,
Yehova anapoanza kufanya jambo fulani,
lazima alikamilishe hadi mwisho.
Na kumbuka kwamba,
kila wakati tunapowaeleza watu
uhakikisho huo wenye sehemu tatu,
tunaimarisha imani yetu
katika ahadi za Yehova.
Kwa hiyo wakati ujao utakaposoma
Ufunuo 21:4,
halafu mtu akwambie,
“Sioni maneno haya yakitimia,”
tutafanya nini?
Soma mstari wa 5 na wa 6,
na uonyeshe jinsi Yehova
alivyotoa uhakikisho wa ahadi yake
kwa kutia
saini yake mwenyewe.