JW subtitle extractor

Betty Georges: Sikuzote Utii Hutokeza Mafanikio (1 Waf. 2:3)

Video Other languages Share text Share link Show times

Acheni tuchunguze pamoja
muktadha wa Andiko la leo,
na kutokana na muktadha huo,
tutaweza kupata kanuni muhimu.
Basi, acheni tusome pamoja
1 Wafalme
sura ya 1,
mstari wa
(samahani) 1 Wafalme sura ya 2,
tunaona kikao katika mstari wa 1—
1 Wafalme 2:1:
“Daudi alipokaribia kufa,
alimpa Sulemani
mwanawe maagizo haya.”
Kwa hiyo,
haya ni maneno ya
mwisho ya Daudi,
mistari wa 2,
Andiko la leo:
“Uwe imara
na ujithibitishe kuwa mwanamume.”
Ona sasa mstari wa 3,
hapa tunapata kanuni muhimu.
Daudi anaendelea kusema:
“Ni lazima
utimize wajibu wako
kwa Yehova Mungu wako
kwa kutembea
katika njia zake
na kwa kushika
maagizo yake.”
Acheni sisi tuishie hapo.
Ikiwa tungetoa muhtasari
wa maneno ya Daudi
kufikia hapo
kwa kutumia neno moja,
tungetumia lipi?
Utii.
Kwa hiyo, ikiwa
Sulemani angekuwa mtiifu,
matokeo yangekuwa nini?
Sehemu ya mwisho ya mstari wa 3.
Daudi anasema: “Ndipo
[matokeo ya utii yangekuwa]
utakapofanikiwa
katika kila jambo unalofanya
na kila mahali unapogeuka.”
Maneno yenye nguvu.
Basi hii ndiyo kanuni muhimu kwetu:
Sikuzote
kutii
hutokeza mafanikio,
kama ilivyokuwa kwa Sulemani.
Maadamu angetii,
angefanikiwa.
Sasa tuitumie kanuni hiyo
katika maisha ya Danieli,
tuone jinsi
alivyotumia
kanuni hiyo
maishani mwake na akafanikiwa.
Basi, tafadhali, acheni tufungue
Danieli sura ya 1.
Tuone jinsi kanuni hii
inavyotumika Danieli
alipofika kule Babiloni.
Tutaona pia jinsi ambavyo
matendo ya Danieli
wakati huo
yanavyopatana na utendaji wa HLC
ulimwenguni pote.
Danieli sura ya 1,
tuone kanuni hiyo tena.
Katika mstari wa 8,
ona jinsi Danieli
alivyoazimia kumtii Yehova.
Danieli 1:8:
“Lakini Danieil aliazimia moyoni mwake
kwamba hatajichafua
kuwa vyakula bora vya mfalme.”
Kwa nini
Danieli hakutaka
kula vyakula bora vya mfalme?
Labda
kwa sababu nyama hiyo
haikuwa imetolewa
damu kwa njia inayofaa.
Hivyo, Daniel alitaka kutii
sheria ya Mungu kuhusu damu.
Hivyo kwetu pia.
Tumeazimia
kutii sheria ya Mungu
kuhusu damu.
Lakini ili Danieli aazimie hivyo,
alitambua angehitaji msaada.
Kwa hiyo alifanya nini?
Mstari unaendelea kusema:
“Basi
akamwomba ofisa mkuu
wa makao ya mfalme
ruhusa ya kutojichafua
kwa njia hiyo.”
Ndivyo ilivyo leo pia.
Ili tutii sheria ya Mungu
kuhusu damu,
tunahitaji msaada
kutoka kwa madaktari ambao wanaweza
na walio tayari
kuheshimu
msimamo wetu kuhusu damu.
Mstari huu umesema
‘[Danieli] alimwomba ofisa
mkuu wa makao ya mfalme.’
Unafikiri aliomba mara moja?
Inapendeza, kwamba toleo letu
la awali linasema
“akazidi” kuomba—
hakuomba mara moja.
Ndivyo ilivyo leo pia.
Kwa sababu ya jitihada
za kuendelea za HLC
za kutafuta na kusitawisha
uhusiano na madaktari,
mpango huo umefanikiwa sana.
Daniel pia alifanikiwa.
Ona mstari wa 9,
ambapo tunasoma.
Tunasoma hivi:
“Na Mungu wa kweli
akamfanya
ofisa mkuu wa makao ya mfalme
amtendee Danieli kwa fadhili
[au amwonyeshe Danieli kibali]
na rehema.”
Danieli alifanikiwa,
ndivyo pia
kwa sababu ya jitihada za
miaka mingi za HLC
ulimwenguni pote,
sasa tuna zaidi ya
madaktari 100,000 ulimwenguni pote
ambao
wako tayari kuwatibu
Mashahidi wa Yehova wakiheshimu
msimamo wao kuhusu damu.
Hata hivyo, ona mstari wa 10.
Kulikuwa na badiliko fulani,
mstari wa 10 unasema:
“Lakini ofisa mkuu wa makao
ya mfalme akamwambia Danieli:
‘Ninamwogopa bwana wangu mfalme.’”
Alibadili maoni, akabadili msimamo wake,
hilo hutupata pia leo.
Nyakati nyingine madaktari
wanaweza kusita
kumtibu mgonjwa ambaye ni Shahidi.
Kwa nini?
Labda kwa sababu hawana uzoefu,
au hawana vifaa,
au labda tu wanataka kufuata sheria
zilizowekwa na waajiri wao.
Ilikuwa hivyo pia na yule
ofisa mkuu wa makao ya mfalme,
hakutaka kukiuka agizo la mfalme.
Je, Danieli alikata tamaa na kusema
‘Yehova, nimefanya nilichoweza,
lakini
sasa nifanyeje?’
Hakukata tamaa.
Angalia tafadhali, mstari wa 11
unasema: “Lakini Danieli akamwambia
mtu aliyeteuliwa
na ofisa mkuu wa makao
ya mfalme ili kumtunza.”
Alizungumza na mtu mwingine.
Vivyo hivyo leo,
washiriki wa HLC
hawaridhiki tu kuwa na
madaktari wachache
ambao wanaheshimu msimamo wetu.
Wanaendelea kutafuta
madaktari ambao
wako tayari
kututibu na kuheshimu
sheria ya Yehova.
Matokeo yalikuwa nini?
Mstari wa 12,
Ona kile ambacho Danieli
anamwambia yule aliyeteuliwa kumtunza.
Inasema: “Tafadhali, tujaribu
sisi watumishi wako
kwa siku kumi.”
Hapa, Daniel anafanya onyesho
mbele ya huyu mtunzaji,
anamwambia:
‘Kuna njia nyingi.
Je, tunaweza kujaribu njia hii tofauti?’
Ndivyo pia na HLC.
Je, tunaweza kujaribu kitu tofauti
mbali na damu, njia mbadala?
Matokea yalikuwa nini?
Mstari wa 13,
yule mtunzaji
alikubali,
hivyo basi,
akawajaribu kwa siku kumi.
Ndivyo ilivyo leo,
washiriki wa HLC
wanafanya maonyesho.
Na hata katika miaka
ya hivi karibuni,
tengenezo limeandaa
maonyesho mapya ya PowerPoint
kwa ajili ya HLC
ili watumie katika maonyesho.
Na basi tungependa
kuwaonyesha kurasa tatu za
kwanza za maonyesho hayo.
Ukurasa huu wa 1
ni wa kuwaonyesha madaktari
tungependa kushirikiana nao.
“Tungependa kuepuka mabishano.
Lengo letu ni kuonyesha ushirikiano.”
Ukurasa wa 2,
unaonyesha kwamba pindi fulani,
Mashahidi na madaktari
wanaweza kuonekana kuwa
wana misimamo tofauti.
Lakini lengo la maonyesho haya,
na mpango wa HLC
ni kutengeneza daraja
(kama ukurasa unaofuata unavyoonyesha)
ili kujaribu kuwaleta pamoja madaktari
na wagonjwa ambao ni Mashahidi.
Na tunaweza kusema kwamba
maonyesho haya
yamekuwa na mafanikio
makubwa kwa HLC.
Asanteni kwa picha.
Na
katika eneo la
ofisi ya tawi ya Marekani,
katika mwaka uliopita,
maonyesho 3,600
yamefanywa Marekani tu,
mbele ya madaktari kuwaonyesha
njia mbadala
inayoweza kutumiwa
ili kuwatibu wagonjwa Mashahidi.
Kwa hiyo tumeona
kanuni hiyo, jinsi iliyotumiwa
katika kisa cha Danieli.
Alitii,
naye Yehova akabariki utii wake.
Ndivyo ilivyo leo.
Yehova amebariki utii wetu
wa kujiepusha na damu.
Kupitia mpango wa HLC,
jitihada zao
zimekuwa na matokeo makubwa sana,
tumepata madaktari ambao wako
tayari kushughulikia mahitaji yetu.
Basi,
swali kwako na kwangu:
Tunawezaje kuunga mkono
mpango huu mzuri, unaofanya kazi,
na wenye upendo
ambayo Yehova ameandaa?
Mambo mawili.
Kwanza, tungependa kufuata mwongozo
ambao Baraza Linaloongoza limeandaa
(unakumbuka
miaka miwili iliyopita,
tangazo lilitolewa
Januari 2023,
tulitiwa moyo)
tuwasiliane na HLC
mapema iwezekanavyo
tunapokabili hali ya kitiba,
hata ikiwa hatufikiri
swala la damu litahusika,
ni afadhali
wakihusishwa
mapema.
Na tunafurahi kuona kwamba
ndugu na dada ulimwenguni pote
wanafuata mwongozo huo.
Na matokeo
ni kwamba idadi ya hali za dharura
zimeshuka.
Na inagusa moyo sana kuona hilo.
Tunaokoa uhai.
Tunaokoa uhai.
Na ni hivyo, hasa inapowahusu
akina dada wajawazito,
na unapofikiria kuhusu dada mjamzito,
si uhai mmoja unaohusika,
ni watu wawili.
Basi kuwasiliana mapema na HLC
kumetokezea matokeo mazuri.
Kisa kimoja kilitokea barani Afrika.
Dada mmoja, mjamzito,
na mume wake waliwasiliana na HLC.
Waliunganishwa na daktari mmoja
ambaye anaonyesha ushirikiano.
Miezi mitatu ya kwanza ilienda sawa.
Kufikia mwezi wa sita,
pia alikuwa sawa.
Lakini baada ya hapo,
dada akaanza kuwa na matatizo,
wakawasiliana na daktari.
Lakini alikuwa ameenda likizo,
lakini akakatiza likizo yake,
ili aje tu kumsaidia dada yetu.
Na daktari huyo akasema,
“Ni vizuri kwamba uliwasiliana nami
kwa sababu uhai wako
na wa mtoto wako
ulikuwa hatarini.
Basi, inagusa moyo kuona kwamba
kutii mwongozo huu unaotolewa
na tengenezo la Yehova
unatokeza matokeo mazuri.
Kwa hiyo (1)
Tunaungaje mkono?
Wasiliana na HLC mapema iwezekanavyo.
Na tungependa kuwatia moyo
ndugu na dada kutanikoni wafanye hivyo.
Jambo la (2)
Tusali kwa ajili ya ndugu hao
na familia zao.
Unafikiri tungehitaji
kumlipa mtu pesa ngapi
awe tayari kutuhudumia
saa 24 kila siku?
Hivyo ndivyo ndugu
wa HLC wanavyofanya.
Basi, tungependa kumshukuru sana Yehova,
ndugu hawa, na familia zao,
kwa sababu ya roho
yao ya kujidhabihu,
kwa kutusaidia tutii sheria
ya Mungu kuhusu damu,
jambo ambalo limetokeza matokeo mazuri!
Tuliona Danieli akitumia kanuni hii.
Alitii,
akapata baraka.
Leo tunatii,
tunafuata mwongozo wa Yehova,
sheria ya yake,
nasi pia tunabarikiwa.
Basi, acheni
tukumbuke kanuni hii:
Sikuzote
utii
hutokeza mafanikio.